Kwanini Mawakili wengi binafsi wanashangilia na kukimbilia kusimamia kesi za wanaodaiwa kutukana au kuikosoa Serikali?

Kwanini Mawakili wengi binafsi wanashangilia na kukimbilia kusimamia kesi za wanaodaiwa kutukana au kuikosoa Serikali?

Leo tumeona Polisi wamedai kumkamata mmiliki wa akaunti ya X inayotambulika kwa JINA la Sukunuku; mara tu polisi walipotaka hayo mawakili binafsi wengi wameonyesha nia ya kusimamia kesi hiyo huku baadhi wakiweka wazi kwamba watashinda kesi husika mapema kabisa.

Mmoja wa mawakili ndugu Madeleka ameeleza ugumu wa kesi ya mtandao kwamba ili uthibitishe upotoshaji lazima uonyeshe ukweli jambo ambalo kwenye kesi ambazo uandaliwa kwa hisia za mpelelezi nivigumu kupata ushahidi wa kuishawishi mahakama.

Upande mwingine wanaharakati wanaeleza kwamba pamoja na sheria ya cyber kuwepo ni vigumu kuthibitisha makosa yaliyoainishwa katika sheria hiyo na hivyo kushindwa kesi kwa Jamuhuri ni jambo la kawaida.

Wapo wengine wanaodai kwamba sheria hii ni ngumu kutekelezeka hasa ikizingatiwa kwamba mwana CCM akitoa lugha fulani hazitafsiriwi na jeshi la polisi kama matusi. Mfano anatajwa Nape Nauye kwamba mara kadhaa ametukana mtandaoni lakini hakuna aliyewahi kumkamata. Viongozi waandamizi wa serikali pia utukana lakini hakuna aliyewahi kukamatwa jambo linaloleta tafsiri kwamba sheria hizi zimeundwa kwaajili ya wapinzani na siyo watu wote.

kulingana na mitizamo hii naamini imewafanya mawakili wengi kuona wanaokamatwa wanaonewa na hivyo kujitolea kuwasimamia lakini pia jeshi la Polisi limekuwa halichukulii serious kesi hizi hasa wakitambua kwamba hawatendi haki kwa watu wote bali wanakandamiza kundi flani

Kwa upande wangu naamini hali hii imepelekea wavunjaji wa sheria kuwa na watetezi wengi hasa sheria zinazolinda maslahi ya wanasiasa watawala. Hakuna mwananchi anayechukizwa na watoe matusi kwa sababu wameona watoa matusi nao wana hoja isipokuwa katika kuwasilisha malalamiko yao wanaweka na maeneo ya udhalilishaji na yanayotweza utu.

Way foward: Tukamate kwanza watawala na kuwafungia ili walio nje ya utawala wajifunze. Nazungumza haya nikikumbuka alivyofanyiwa NONDO wa ACT......akahesabika kama gaidi leo anakula meza moja na watawala
Hupendi watu watetewe haki zao? Hupendi uhuru wa mawazo? Unataka kilamtu asifu na kuabudu kama wewe?
Vijana critical wanaohoji hata Hayati Nyerere aliwasifu na vimbelembele wanaojikomba na kujipendekeza alisema wataliua taifa...
 
Ah mimi nilimuelewa sana mbona wapo wengi wanaomcruticize rais na hawajawahi chukuliwa hatu sema ni wanyonge tu ndo wanaoonewa
Kucriticize na kutukana watu ni vitu tofauti, mzee kucriticize raisi kuna tweep anayemfikia MMM maspana? (Huyu yeye atatukana tweeps wengine comments ila sio post yake kuu iwe ya kutukana viongozi) huyu dogo sukununu wanyooshe ipasavyo akirudi uraiani awe na nidhamu kiasi
 
Ni kwa kuwa ni kesi nyepesi sana na ngumu kwa serikali ku-define matusi ninini na kutukana ninini!
NI kesi ngumu sana serikali kushinda labda kwa figisu mahakamani!
 
Leo tumeona Polisi wamedai kumkamata mmiliki wa akaunti ya X inayotambulika kwa JINA la Sukunuku; mara tu polisi walipotaka hayo mawakili binafsi wengi wameonyesha nia ya kusimamia kesi hiyo huku baadhi wakiweka wazi kwamba watashinda kesi husika mapema kabisa.

Mmoja wa mawakili ndugu Madeleka ameeleza ugumu wa kesi ya mtandao kwamba ili uthibitishe upotoshaji lazima uonyeshe ukweli jambo ambalo kwenye kesi ambazo uandaliwa kwa hisia za mpelelezi nivigumu kupata ushahidi wa kuishawishi mahakama.

Upande mwingine wanaharakati wanaeleza kwamba pamoja na sheria ya cyber kuwepo ni vigumu kuthibitisha makosa yaliyoainishwa katika sheria hiyo na hivyo kushindwa kesi kwa Jamuhuri ni jambo la kawaida.

Wapo wengine wanaodai kwamba sheria hii ni ngumu kutekelezeka hasa ikizingatiwa kwamba mwana CCM akitoa lugha fulani hazitafsiriwi na jeshi la polisi kama matusi. Mfano anatajwa Nape Nauye kwamba mara kadhaa ametukana mtandaoni lakini hakuna aliyewahi kumkamata. Viongozi waandamizi wa serikali pia utukana lakini hakuna aliyewahi kukamatwa jambo linaloleta tafsiri kwamba sheria hizi zimeundwa kwaajili ya wapinzani na siyo watu wote.

kulingana na mitizamo hii naamini imewafanya mawakili wengi kuona wanaokamatwa wanaonewa na hivyo kujitolea kuwasimamia lakini pia jeshi la Polisi limekuwa halichukulii serious kesi hizi hasa wakitambua kwamba hawatendi haki kwa watu wote bali wanakandamiza kundi flani

Kwa upande wangu naamini hali hii imepelekea wavunjaji wa sheria kuwa na watetezi wengi hasa sheria zinazolinda maslahi ya wanasiasa watawala. Hakuna mwananchi anayechukizwa na watoe matusi kwa sababu wameona watoa matusi nao wana hoja isipokuwa katika kuwasilisha malalamiko yao wanaweka na maeneo ya udhalilishaji na yanayotweza utu.

Way foward: Tukamate kwanza watawala na kuwafungia ili walio nje ya utawala wajifunze. Nazungumza haya nikikumbuka alivyofanyiwa NONDO wa ACT......akahesabika kama gaidi leo anakula meza moja na watawala
Nilimsikia kamanda Muliro anadai mojawapo ya sababu kubwa ya kumkamata huyo Sukunuku kisa ameandika " Makamba amepanga kumchinja Samia 2025" hapo hata nikimchukua bibi yangu kutoka Namtumbo anayelima tungule kama wakili anashinda kesi asbhi tu.
 
Tanzania mtu akiwa anatukana na kudhalilisha watu,anaonekana shujaa kwa baadhi ya wajinga wanaenda mbali zaidi na kusema ni Uhuru, tunatengeneza kizazi cha ovyo sana kwa kisingizio cha Uhuru. Yaani utukane matusi usingizie uhuru?
Mkuu, alitukanaje? weka "tusi" hapa
 
Shida wakishakukamata hadi waje kutangaza wanakushikilia ni karibu wiki 1 au zaidi ya wiki. Hapo katikati unafanyiwa vitendo visivyo vya kibinadamu. Ukitoka hapo kesi umeshinda lakini utu wako umeshatwezwa unakuwa kama mdude vile. Sasa unapata faida gani au unaona sifa umetetewa na mawakili wengi wakati umeshafanyiwa ukatili wa kutosha? Au unadhani huko behind the scenes hao mawakili wanakuwepo?
 
Talking about Sukununu yule jamaa yuko vizuri sana kwenye critics na sio kwa Gvt tu bali hata kwa tweeps wengine.

Mbaya zaidi anafanyia bullying watu wa X(formerly Twitter) kiasi wanamchoka hasa sana wanawake, wanaume(few of them especially those seeing themselves as superior than others) na watu wa Gvt.

The issue of Sukununu ilichukua sura mpya baada ya kuibuka pande mbili
1. Upande wa sukununu (utetezi)
2. Upande usio wa sukununu (washtaki)

Hata baada ya kuzagaa taarifa kua Sukununu amekamatwa ilizua gumzo why & how mbona wako wengi tu ambao wanatukana tena sana ila hawajawahi kamatwa so why him?

Nape aliwahi sema (yashakum si matusi) m*e**e ila hakuwahi kuchukuliwa hatua hata pia bungeni kuna mbunge aliwahi kusema live sasa kwanini Sukununu tu.

Nadhani hiyo ndo imeleta picha tofauti kwa Advocates kukivalia njuga ili kuepusha uonevu kwa raia wa kawaida.

NO ONE IS ABOVE THE LAW
"NO ONE IS ABOVE THE LAW", the President is.
the Speaker of the National Assembly is.
may be I too!
 
Hawana ueledi,double standard.
Akili ndogo Sana hao.
Ifikie waone aibu,Kwa maana inajulikana mpaka Sasa kuwa ccmB.
So,hawana jipya,tunawazuuuuuum
 
Shida nchi yenyewe inaendeshwa kitapeli, ni kweli ana makosa ila sio makubwa kiasi hicho, na nchi yenyewe ipo kiholela, mfano mdogo waziri wa michezo anasema atakaye enda kuwapokea wapinzani (al ahly na mamelodi) watashughulikiwa kwa kosa lipi? Na kanuni ipi?
Amesema "watashughulikiwa", kwani wewe Lax umeelewaje neno "kushughulikiwa?
 
Shida wakishakukamata hadi waje kutangaza wanakushikilia ni karibu wiki 1 au zaidi ya wiki. Hapo katikati unafanyiwa vitendo visivyo vya kibinadamu. Ukitoka hapo kesi umeshinda lakini utu wako umeshatwezwa unakuwa kama mdude vile. Sasa unapata faida gani au unaona sifa umetetewa na mawakili wengi wakati umeshafanyiwa ukatili wa kutosha? Au unadhani huko behind the scenes hao mawakili wanakuwepo?
Huyi jamaa akitoka sijui kama atatumia tena mitandao

Ova
 
Back
Top Bottom