Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
mkuu mbona asaiv binadamu tunaelekea kufanana?Kichuguu Mkuu, ningependakujua kwa mawazo au uhakika wako kuwa baada ya miaka hiyo ya mamilioni ​hao makaburu wa Afrika ya Kusini watakuwa weusi na Negros wa Marekani na Latin Amerika watakuwa weupe? Unadhani au una hakika kuwa genetics inaweza kuathiriwa na climate baada ya mamilioni ya miaka?
Uko sahihi, lakini nadhani Mhindi atabaki kuwa Mhindi na Golo atabaki kuwa Golo kama hawa hawakuchanganya damu, isipokuwa kama walivyosema wengine kuwa hadi ipite mamilioni ya miaka.mkuu mbona asaiv binadamu tunaelekea kufanana?
Swaali zuri sana;
Kwanza fahamu kuwa kuna mbilikimo wa aina mbili: mbilikimo wa asili (pygmy) na mbilikimo wa ugonjwa (dwarf). Wale wa kongo ni mbilikiko wa asili kwa maana ya kuwa maumbile yao ni asili yao na yanatokana na mazingira yao ya asili. Umbilikimo wa aina hii ni hereditary kwa maana ya kuwa huzaliwa na mbilikimo pia. Ni kama ambavyo maumbile ya asili ya waachina yalivyo tofauti na maumbile ya asili ya wazungu, na pia wachina huzaliwa na wachina tu.
Kuna mbilikimo wa aina nyingine ambao wanapata matatizo ya mwili kushindwa kutengeneza hormones zinazohitajika mwili kukua, na hivyo kubaki na umbo la kitoto maisha yao yote; hawa wanajulikana kama drwafs. Mbilikimo wa aina hii huweza kutokea katika familia yoyote ile, wazazi wawili warefu wanaweza kuzaa mbilikimo wa aina ya dwarf.
Theories zinazonyesha kuwa evolutionary process iliyosababisha waafrika wakawa na ngozi nyeusi kutokana na mazingira ya joto la tropical, ndiyo pia iliyosababisha watu waliokuwa wakiishi kwenye misitu mizito kama vile Kongo kuwa wafupi kwa vile miili yao ilikuwa inakosa mwanga wa jua kutengeneza vitamin D; kwa hiyo miili yao ikawa haiwezi ku-absrob calcium ya kutosha, jambo liliosababisha wawe na mifupa midogo na hivyo kuwa na miili midogo. Misitu ya Kongo ndiyo yenye mbilikimo wengi wa aina hiyo ikifuatiwa na misitu ya Amazon huko Brazili. Kuna sehemu nyingine za dunia kama Papua New Guinea na Australia ambako pia kuna mbilikimo waliotokana na misitu mikubwa iliyokuweko maeneo hayo.
wapare na wasambaa nani wafupi zaid?Na wapare vipi? Ni milima au misitu inawafanya wawe ma-shorties?
Mkuu umeshusha shule nzuri sana, sina zaidi nasubiri mengi zaidi kuhusiana na mada hii.Vipi, bado kuna watu wako interested na discussion hii? Iliibuka sana wakati nikiwa nakwenda kwenye mkutano, nikaomba ikatishwe hadi nikimaliza mkutano ule. Nimekuwa nakuta notifications nyingi sana kwenye account yangu zinazohusu thread hii, je bado wachangiaji wenye interest zaidi ya nilivyokwisha andika huko nyuma?
Hivi Kichuguu,
ni kweli kabisa unaamini theory ya evolution?Wale watu weusi kule Australia na black indian unataka kuniambia hali ya hewa ya kule inafanana na ya Africa? Ni kwanini nchi moja kunakuwa na watu wenye ngozi za rangi mbili tofauti?
Kuna nadharia nyingine inadai watu wa asili ya bara hili sio weusi ni aina ya watu wanaofanana na waarabu, sijui unaifahamu nadharia hiyo?
Sielewi iwapo unakataa maelezo niliyotoa hapo juu au unapinga theory ya evolution. Maelezo niliyotoa hapo juu yana ushahidi wa kutosha kuwa watu wa sehemu zote zenye asili ya mistu mikubwa (rainforests) kama vile Congo, Amazon, Quuensland, na papua new Guinea ni mbilikimo. Sababu yake halisi ni hiyo, mifupa hujengwa kwa calcium ambayo mwili wako utaiabsorb tu iwapo una Vitamin D ya kutosha. Na vitamin D hutokana na mwanga wa kutosha. Process hii inajijenga pole pole kwa muda mrefu san (evolution).
Kuhusu Theory ya evolution sijui nikueleze vipi iwapo huiamini. Kumbuka kuwa theory hiyo inatumia muda wa mamilioni ya miaka siyo miaka elfu moja tu. Kama umepiga shule ya kutosha kuhusu mabadiliko ya muudo wa dunia, utajua kuwa Africa, South America, Australasia na India zilikuwa ni bara moja kwenye maeneo ya tropical. Kwa hiyo watu weusi unaowaona huko wote wana asili ya tropical. Soma theory ya Pangaea kwa makini halafu ufuatilie theories za Plate Tectonics, baadaye uchunguze tena namna matetemeko ya dunia yanavyotokea leo ndipo uangalie tena ukaribu wa sehemu zote unazoona leo zina asili ya watu weusi. Uhamiaji uliotokea baada ya ugunduzi wa vyombo vya kusafuiria ndio uliosababisha watu hawa kuchanganyikana; hakukuwa na mtu mweupe kusini ya ikweta. Uhamiaji huo umetokea miaka isyozidi 2000 zilizopita, kipindi ambacho si kifupi sana katika process ya evolution.
biashara ya utumwa ilisababisha watu weusi kusambaa duniani kote kwani ndio walionekana wana nguvu ya kufanya kazi kwa muda mrefu bila kuchoka na kuhimili magonjwa yaliyokuwa wanaweza kuwaua watu wengine wakiwemo wahindi wekundu. Baada ya biashara ya utumwa kukomeshwa watu weusi waliokuwa wameshikiliwa kama watumwa waliachiwa wakaanza kuishi kama watu huru, wakaoa na kuzaa,
hii ilitokana na kukosekana kwa taarifa za kutosha watu hao walichukuliwa katika nchi gani Afrika ili warudishwe. ndio maana marekani ilijaribu kuwarudisha wachache tu na ikawamwaga Liberia, ndio maana hadi leo bendera ya Liberia iko sawa na ya marekani/inafanana sana. unakumbuka na jina la makao makuu ya Liberia yanaitwaje? weusi walipokuwa wanazaliana na damu nyeupe waliendelea kutokea weusi wa aina mbalimbali, na ndio maana mabara mengi yana watu weusi au wanaofanana na weusi katika baadhi ya maeneo walipoishi watu weusi
Tz ukienda kondoa dodoma na Manyara mbulu utaona kuna weusi lakini wanafanana nywele zao na kwa sehemu ya ngozi yao na waarabu n.k.
Genetic changes is not a few centuries process but rather takes millions of years. Pale SA makaburu hawana hata 500 yrs hivyo haitegemewi wawe wamebadilika kijetiki kwa kiwango cha kubadilika rangi ya ngozi n.k..... Kumbuka kuwa kuna makaburu Afrika ya Kusini wanaoishi kule kwa karne nyingi na bado hawajabadilika rangi kwa kuishi katika tropikali.