Kwanini Mo Anapata Hasara Simba, Yanga wanapata Faida?

Unalinganisha Yanga na Mo !!

Au unapaswa kuilinganisha Yanga na Simba,, Mo na GSM.

Kilichosomwa na Yanga leo Ni taarifa za klabu ya Yanga si taarifa ya mwekezaji.

Kuna Simba Kama timu halafu Kuna Mo km mwekezaji na hesabu zake.

Hiyo milioni 500 si hela za GSM. Ni hela za timu. GSM anaweza kupata hasara lkn Yanga ikatengeneza faida.

Mwekezaji akipata hasara siyo kwamba timu Ndiyo imepata hasara. Hapana.
 
Halafu watu mna ujinga mwingi Sana halafu hata mkielimishwa mnakaza mafuvu.

Uliona wapi bepari anayewekeza kwa hasara ? Au Uliona wapi bepari anapata hasara halafu akaendelea kuweka hela zake ktk hiyo biashara?

Bepari km Mo hafanyi biashara ya hasara. Ingekua hivyo angekuw alishaachia timu kitambo. Unapata hasara halafu miaka kumi upo umeng'ang'ania.
 
Hiyo ripoti nilipoisikia mimi ngachokaa. Nikisema niinyambue hapa kuna watu watakosa pa kuficha sura zao. Anyway, tumeambiwa tusiwaonee wivu vijana.
 
Tajiri Wao = Kanjanja+ Msanii

Management = Wapigaji

Mashabiki = Makolo
 
Hiyo ripoti yao inatia kichefuchefu. Mhasibu mjanjamjanja, mwanasheria mjanjamjanja, hao GSM ndiyo kabisa.
 
hujaona mahali pa mkopo wa bil 4 plus (hio faida unapataje wakati kuna deni hujatoa bado?[emoji3][emoji3][emoji3])
 
Kitu muhimu angalau uwazi wa mapato na matumizi tumeuona, ni mwanzo mzuri.

Hii itawafunga mdomo wote wanaojifanya kupata hasara wakati makampuni yao yanafaidika pakubwa na brand.
huo mkopo wa 4.8 ni wa nini?

btw, yanga jezi zao zinavotembea vile wamepataje mil 300?
 
taarifa kama hio yanga huwa wanaitoa kila mwaka nadhani,....

tatizo pia ni simba, wale sijui kama huwa wanatoa walau report ya kuzugia kama hio
 
Simba na yanga hazina tofauti na vyama vya siasa, uongo ni mwingi kuliko ukweli, alietoa hiyo taarifa siku sio nyingi atakuja kusema tena yanga ina endeshwa kwa hasara
 
Yani na mikopo imewekwa kwenye mapato ili waseme wanaendasha kwa faida, Yanga imekopa 4.8B, hii ni pesa nyingi sana, Yanga haijapata faida yeyote, ilipata hasara ndo mana ikabidi kukopa ili kuweza kuishi,
Shida ni wamekopa kwa nani? Riba ipoje ?
 
Huo mkopo hapo ndio kuna siri ya upigaji, mkopo wa 4.8bn kutoka kwa taasis yenye ambayo haina history ya kutengeneza faida ni wajanja wameshatanguliza kete, baadae yatasikika maumivu tu. Eng Hersi lazima anahusika na huu upigaji. Taasis ya umma inachukua mkopo mkubwa ambao haujulikana riba yake na mkopaji kafichwa, wenye akili tushanusa kinachokuja.
 
Hata ulaya kamwe huwezi pewa financial statements wanasemaga wamepata faida au hasara kiasi gani
Kuwa unapenda kufuatilia mpira na sio kuwa zwazwa
 
Ni bora huyo aliyesema alichukua mkopo
Wengine kila siku ni kulalamika wamepata hasara
Only auditors ndo anaweza thibitisha huo mkopo ni upigaji na sio wewe uliyekaa nyuma ya keyboard unayeongozwa na hisia na sio uhalisia
 
Hizo assumptions hazipo.

Huwezi kusema Yanga ina mademi ya TRA ikiwa huna vithibitisho.

Report iliyotolewa imejitosheleza, tusipinge pinge hovyo hovyo kwqa ababu ya. Usimba na Uyanga.
Anatumia hisia alafu anataka watu wamuamini
 
Taarifa ya simba waliitoa lini
 
Madeni yote yameorodheshwa ndani ya matumizi acha ujuaji wa kipuuzi
Matusi ya nini kwenye mjadala mzuri kama huu?
Hayo mabishano ya matusi peleka huko FB kwa watoto, hapa tunajenga ili kuweka mambo wazi zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…