Kwanini Mungu na Shetani wasimalize tofauti zao?

Kwanini Mungu na Shetani wasimalize tofauti zao?

Kama huamini universe imetokea kwa Chance ina maana kuna Designer na kama kuna Designer mtaje ama Explain zaidi.
Did I say that ?!!!

Nimekwambia hata ukichukua test tube ukazitoa kila kitu ndani (kwa macho yako ukadhani umecreate nothing) ukaseal hizo test-tube na kuzipeleka sehemu tofauti usishangae baada ya muda kwa vifaa vyako ambavyo mwanzo hukuweza kuona kitu ukakuta life form humo ndani and that will have nothing to do with a designer its just chance and happenstances...
 
Chochote anacho kifanya Mungu ni chema. Ingawa kwa macho yetu ya nyama tunaweza kulaumu hapa na pale.
Mwanadamu ndiyo kiumbe pekee aliye pendwa sana na Mungu hadi akamuumba kwa mfano wake na kumpatika kila hitaji lake.
Nina uhakika tungejua kuonge kama kina simba, au Virus au Bacteria na wenyewe kama wana Bible yao wangesema haya haya kwamba Mungu katupenda sasa sisi bacteria hadi katupa uweze wa ku-regenerate kwa kasi sana...

Au kipindi kile hivi vitabu vinaletwa wanawake ndio wangekuwa na nguvu wala ubavu uliotumika kumtengeneza Eva usingekuwa wa Adam bali vice versa...

Ukiangalia kwa jicho la tatu throughout generations Imani imekuwa ikitumika kama justification wa baadhi ya kufanya mambo yanayowanufaisha... Mfano kuheshimu mamlaka, Taifa Teule n.k.
 
Swali lako ni fikirishi! Ngoja nijaribu hivi.
Kwenye spritual life, Kuna timing mkuu.Hata wewe ukifa kabla hujatubu dhambi zako,hauna tena chance ya ku-negotiate(japo kuna baadhi ya dini zinasema inawezekana kumuombea marehemu toba,sijui maandiko wanayotumia).Ila kwa jinsi ya maandiko matakatifu (biblia takatifu) usipoweza kutengeneza mahusiano yako na Mungu ungali hai,hakuna chance tena ya kufanya hivyo mara baada ya kufa . So it is too late kwa Shetani kuomba toba.kitendo cha shetani kufukuzwa,ilikuwa ni spritual death kwa shetani.Ndiyo maana anachosubiri ni hukumu tuu.

Pia tukumbuke kwamba Mungu na Shetani hizi ni Kingdom mbili tofauti zenye mamlaka kamili(Ijapokuwa Mungu ni mkuu) bado shetani anweza fanya copies ya mambo ya Mungu kudanganya watu.Again,fahamu mpaka sasa Shetani mwenyewe anajiona hana kile cha kumfanya aombe msamaha kwa sababu ana mamlaka kiasi anaona mambo yake yako on-track na pia ana watu wafuasi kibao nyuma yake.So akiweka chini siraha watu wake watabaki wapi by now? ikiwa tuu kuiunganisha simba na yanga kuwa yanga ni ngumu kuliko hili,au angalia kinachoendelea sasa Urusi na Ukrane kama haiko rahisi kwa ukrane kuachia nchi si zaidi sana kwa shetani?.Au ulikuwa unamanisha Mungu aseme sawa bwana shetani,mimi nimeamua kuwa chini yako sasa?

Mwisho kabisa,Mungu ametoa uhuru wa kuchagua unachoona kinafaa,ila ametoa angalizo juu ya mwisho wa kila njia utakayoamua kuiendea.

Ubarikiwe
Nice explanation according to your faith...

Kwahio kwa imani yako huko kwenye mamlaka ya Shetani huo moto atakuwa anatoa Mungu au Shetani ndio atakuwa anatoa kibano kwa wadau wengine..., yaani ile pain itakuwa sawa kwa wote au itakuwa everyman / woman for himself / herself au mkikutana wadau mliokuwa mnafanya ujambazi wote huku kitaa mtaendeleza crew yenu ?

Pili huko Peponi kutakuwa na nini ? Ni nini kitafanyika sababu kama kila kitu kipo na hakuna cha kufanya kuna tofauti gani na ma-pre-programmed robots ?
 
Malaika sio mashetani...ushetani ni sifa ya kiumbe muasi kwa Mungu.

Malaika wao wameumbwa wakiwa hawana hiyari, wanatenda yale waliyoamrishwa.
Okay ni sawa kwa Imani yako ila kuna wanaosema / amini kwamba huyu Shetani alikuwa pia Malaika ila hao ni wao, twende na wewe...
Binadamu na Majini wao wana hiyari ya kufanya mema au kufanya maovu ila ndio kumewekwa mafikio ya machaguo yetu...kuwa kuna pepo kwa ajili ya walioamini na kutenda mema na kuna moto kwa ajili ya waliokadhibisha.
okay... ila nina swali hivi unaweza kwenda mbinguni kwa kutenda mema bila kuamini au inabidi uamini pia ? Kama inabidi uamini pia kuna swali hapo chini........
Nafsi zimeshaumbwa kabla ya kuletwa hapa ulimwenguni na Mungu alishazibainishia njia ya kweli ni ipi na akazionya pia juu ya upotovu. Wote mimi na ww tumekiri kuwa hapana mola isipokuwa Mungu mmoja , baada ya hapo Mungu ndio anatupa mtihani kwa kutuleta humu duniani katika vipindi tofauti...
Sasa wale wanaomanini vinginevyo walipata amnesia au wasiokumbuka imekuwaje na Je wanaokufa siku ya kuzaliwa huoni ni kama mtihani huu wamefanya cheating ? (Free Pass to HEAVEN) ?
kuna waliotangulia miaka mingi iliyopita nasi tumefuatia ,tutakufa na wataendelea kuja wengine mpk pale ulimwengu utakapofika tamati kisha tutakwenda kulipwa kwa yale tuliyoyatenda katika siku ya hukumu.
Ngoja kidogo..., hizi habari wewe kuja kuzipata vema na haya mafundisho yalikuwa kabla au baada ya Mtume Muhammad kuja na kuelezea ?!!! Sasa wale waliokuja kabla walijua vipi au waliambiwa na nani kuhusu mapato tuliyoambiwa na Mungu ? (Yaani walijua vipi mafundisho ya Mtume ambaye alikuwa bado hajaja)?
Mungu hapangiwi wala haulizwi kwanini kaumba Moto na Pepo....bali sisi viumbe ndio tugakaokwenda kuulizwa. Mungu ni mfalme na anamiliki kila kitu, unapata wapi authority ya kuhoji God's will?
Mababu zetu wasingehoji walichoambiwa huenda mpaka leo kungekuwa kuna mabwana na sisi watwana kazi yetu ni kuwalamba miguu...
 
twende taratibu, swali weka moja moja, ukienda haraka huto elewa.

Mungu ninaemzungumzia mimi ni Mungu aliye baba wa roho zetu.. muumba wa ulimwengu.

Matendo ya Mitume 17:24-28
[24]Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo, yeye, kwa kuwa ni Bwana wa mbingu na nchi, hakai katika hekalu zilizojengwa kwa mikono;
[25]wala hatumikiwi kwa mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji kitu cho chote; kwa maana ndiye anayewapa wote uzima na pumzi na vitu vyote.
[26]Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao;
[27]ili wamtafute Mungu, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu.
[28]Kwa maana ndani yake yeye tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu.
Na unataka unachoamini wewe kwamba ndio kiwe universal ? Nimekuuliza swali mtenda mema asiyemuamini unayemuamini wewe atakwenda au hataenda mbinguni.., yaani kutokumuani tu unayemuamini ni guarantee ya kuwa doomed ?
 
Huna excuse....Jua kuwa tupo hapa duniani kwa ajili ya mtihani.

Maisha yetu yapo katika mfumo huu!!

Mungu kwa hekima,utashi na mapenzi yale aliamua kutuumba ili atufanyie mtihani! Viumbe vyote vilihudhurishwa mbele yake, akauliza nani yupo tayari kufanyiwa huu mtihani wa kupewa amana!! ?

Jua,milima,wanyama,bahari,malaika,mwezi,mbingu,nyota,miti na ardhi vyote vilikataa kuibeba hiyo amana badala yake mwanadamu alikubali kubeba hiyo amana.

Amana yenyewe ni hii kuwa atafanya aliyoamrishwa na ataacha aliyokatazwa kwa maana ya kuwa mtiifu. Viumbe wengine waliogopa kubeba kutokana na uzito wa suala hili ila mwanadamu ali underestimate uzito wa jambo hili akabeba majukumu. Ila aliambiwa kuwa akifaulu kutekeleza hayo atalipwa malipo makubwa ambayo ni Pepo na akishindwa basi ataadhibiwa kwa moto.

Viumbe vingine vilistaajabu kuona kiumbe dhaifu kama binadamu kukubali kubeba mzigo mzito.

Mwandamu yeye alichagua hiyari hivyo viumbe vingine havina hiyari ya kutenda kama mwanadamu.
Okay who am I to argue with your faith........
Nafsi inapoletwa duniani huwa ineletwa kwa ajili ya mtihani hivyo ili kuwe na fair test kila nafsi huanza ikiwa haina kitu kichwani!! Ila humu duniani Mungu tayari ameshatanguliza kuweka uongofu kupitia vitabu vyake vitukufu,mitume na manabii (wa kweli).
Babu yangu mzaa babu yangu mzaa babu yangu ambaye hakukuta hivi vitabu na alikuwapo hata kabla Mtume ambaye kafanya hii habari / knowledge kuwa mainstream hajazaliwa unawemuweka katika kundi gani ?
Hivyo ni jukumu lako mwanadamu kuutafuta ukweli kama vile unavyohangaika kila siku kuutafuta mkate wako.

Mtihani huu una muda maalumu kwa kila mtahiniwa kuna ambao wamepewa muda mrefu na wengine mfupi. Mtoto toka anapozaliwa mpk kufikia baleghe huwa hana dhambi! Ila kalamu inaanza kuandika mema na mabaya yake mara baada tu ya kuwa ameshabaleghe kwa maana sasa anaelewa lipi jema na lipi ovu.
Kwahio watoto wote wanaokufa kabla ya kuwa wakubwa wamepewa free pass yaani wa mtihani wao ambao kule walikubali kubeba huu mzigo mzito wamekuja huku na kukuta kumbe kwao mzigo ni rahisi kuliko ?!!!!

Pili ni kwamba tuliitwa wote kwa wakati mmoja alafu wengine wakawekewa pause wasizaliwe kwanza mpaka hapo baadae au kila sekunde kabla ya mtoto kuzaliwa huwa kuna kundi linaitwa wakiwepo kina sisimizi, miti, michicha, funza n.k. na kuulizwa choice hii ?
 
Let's not forget. Shetani alipoasi, alisababisha ^system disorder^ ulimwenguni kote. I mean, harufu ya dhambi aliyoileta duniani haiwezi kuondolewa tu hivihivi. Lazima ing'olewa ^mizizi, shina, na matawi^ yake yote.
And this was known all along that it would happen as it did happen ?
Na, most importantly, uong'olewaji huo unafanyika katika namna ambayo daima itamwonesha Mungu kwamba ni mwenye haki na upepo.
He has already seen and he knows au unamaanishi nini itamwonesha ? and for whose benefit ?
The ultimate goal now is to eventually eradicate sin completely never ever to resurface again.
But it was known all along ? And who created sin by the way ?
 
Huku tena tunaambiwa shetani alipotupwa duniani, akaja kuanza kukimbizana na mwanamke gani sijui.. mara mwanamke akapewa mabawa ili shetani asimkamate!! Yaani shetani huyuhuyu ambae ametoka kupigana na Mungu, eti akashindwa kumkamata yule mwanamke 😆😆 seriously?

Kuna baadhi ya vitu ukisoma kwenye hivi vitabu yani unaona kabisa ni alfu lela ulela.
Unaweza kuiweka hapa hii story kwa faida ya wengi ? Kwani Shetani yeye hana mabawa ?
 
Ndiyo maana kuna umuhimu mkubwa sana wa kuisoma Biblia na kuielewa vizuri. Maswali yako yote (na zaidi) yanajibiwa humo.

Nimecheka sana ulivyosema kwamba Shetani na jeshi lake walikuwa ^wananunua silaha za maangamizi^! (Russia au Marekani?)🙂
Unajua kitu kinaitwa figure of speech .....
 
Mimi nadhani kuna kitu hakipo sawa kwenye hizi habari za Mungu na shetani.

Kwanza kabisa, iliwezekana vipi kwa shetani (malaika) kumsaliti Mungu? Ni kipi hasa kilichomsukuma shetani kumsaliti Mungu?

Pili, tunaambiwa THELUTHI MOJA ya malaika mbinguni walimuunga shetani mkono!! Yaani katika kila malaika 10, zaidi ya malaika watatu walikua upande wa shetani! Ni kipi hasa ambacho malaika walikerwa na utawala wa Mungu kiasi cha kufikia theluthi yao kuunga mkono upinzani?

Tatu, tunaambiwa shetani alikua na JESHI na kwamba jeshi hilo lilienda vitani kupigana na jeshi la malaika!

a) Ina maana wakati shetani ana organize jeshi lake, wanafanya mazoezi, wananunua silaha za maangamizi, wana plan attacks nk Mungu yeye alikua amekaa tu anawaangalia? Si yeye anaona kila kitu?

b) Vita kati ya malaika wa Mungu na wa shetani ilipiganwa vipi? Wakati hao wote ni roho na tunajua roho haziumii wala hazifi? Silaha gani zilitumika? Ushindi ulipatikanaje?

Nne, tunaambiwa katika vita hiyo, shetani na jeshi lake walichakazwa vibaya sana na kutupwa duniani. Lakini hata hivyo, shetani na Mungu waliendelea kushirikiana katika "projects" mbalimbali, huku wakikutana mara kwa mara kupiga soga, kupanga majaribu nk.

Huku tena tunaambiwa shetani alipotupwa duniani, akaja kuanza kukimbizana na mwanamke gani sijui.. mara mwanamke akapewa mabawa ili shetani asimkamate!! Yaani shetani huyuhuyu ambae ametoka kupigana na Mungu, eti akashindwa kumkamata yule mwanamke 😆😆 seriously?

Kuna baadhi ya vitu ukisoma kwenye hivi vitabu yani unaona kabisa ni alfu lela ulela.
Suala la imani ni tete. Linaweza kua sawa na hadithi ya kuku na yai
 
unaweza kusema vipi Aliyetengeneza hawa hawa hausiki kwenye haya matukio?

Tofauti na mashine ama mfano wa roboti, mwanadamu amepewa uwezo wa kutambua jema na baya. Yeye ni kiumbe anayetambua maadili (moral being).

Mwanadamu ni kiumbe mwenye maarifa anayeweza kutambua athari za maamuzi yake na kufanya yaliyo sahihi (intelligent being).


kwenye free will huwezi kusema mtu kapewa chaguo la kuchagua either shetani au Mungu wakati anaambiwa akichagua shetani atachomwa milele na akichagua mungu ataishi milele kwa raha mustarehe (hio ni intimidation) na chaguo hilo ni la kushinikizwa....

Usichojua ama unachokwepa kutambua ni kwamba Muumbaji ni mwenye maarifa na hekima zaidi kuliko kiumbe.

Maana yake ni kwamba kila kitu chema na bora ambacho mwanadamu angehitaji kinapatikana kwa Muumbaji wake, na uchaguzi mwingine wowote tofauti na huo ni wenye madhara.

Uhuru wa kuchagua ama utashi amepewa mwanadamu (na malaika) kwa sababu Mungu hapendi utii wa kulazimishwa, bali wa hiari, wa upendo.

And How is That......., Kwamba chagua dhambi nikuchome, au nichague mimi nisikuchome !!!!, Pili katika chaguzi zako nimeweka vikwazo ambavyo vitapelekea ugumu wa kunichagua ?

Umeshawahi kujiuliza kwa nini mwanadamu atake kuchagua upande mwingine tofauti na ule wa Muumbaji wake? Kwamba amekoswa au amepungukiwa nini, kwa mfano, wakati vyote vilivyo bora na vyema vinapatikana?

Kama mwanadamu asingekuwa na uhuru wa kuchagua (free will), basi asingetenda dhambi. Maana yake ni kwamba angekuwa ameumbwa kama kiroboti fulani kinachofanya vilevile tu kilivyoprogramiwa.
 
And this was known all along that it would happen as it did happen ?
Exactly. God knows the end from the beginning.

He has already seen and he knows au unamaanishi nini itamwonesha ? and for whose benefit ?

Sure! There is nothing hidden from God; He's very well acquainted with every single detailed of anything in the whole universe. He's omniscient Being.

^For whose benefit?^ I mean for people like you who still don't believe and appreciate that God is able, good, and loving.

Even as we speak, God is graciously trying to vindicate His goodness. The Devil, on the other hand, is also trying to deceptively attract our attention and win us to himself.

Ultimately, the game will be up, and God will be fully vindicated. Don't forget that since his fall from heaven, the Devil and his evil angels have been accusing God of all kinds of negative things.

For what could be a better strategy to unsettle your opponent than to heap all blames on them?

But it was known all along ? And who created sin by the way ?

It's true that God foresaw the entrance of sin in the creation of Satan. There was no way He could have created reasonable, intelligent, free moral beings without this potential and inclination on their part to not choose Him (to sin).

Rather that creating robot-like beings, God risked creating individuals endowed with the capacity to choose whatever they wanted to.

This is how much the freedom of choice is so expensive!
 
Naomba u-pause kwa sekunde chache alafu jiulize Mungu anajua kitakachotokea Kama jibu ni ndio nadhani usingeweka baadhi ya maelezo yako hapo chini kama ni hapa Okay tuendelee.

Angejua haya yatafanywa na Majini si angeweza kutengeneza Mwanadamu kabla au sio kwamba aliamua kuumba kiumbe mwingine sema ule muda wa kuumba kiumbe mwingine ulifika

Okay....

Bali Mungu ?
Sijaelewa unachouliza...mwanzo nilikwambia kuwa Mungu ana maamuzi yake , yaani anafanya vile apendavyo wakati wowote ule. Yes uumbaji wa mwanadamu ulikuwepo katika mipangilio au maamuzi yake kabla hata ya kumuumba mwanadamu. Hakuna aliyeyajua haya ila YEYE mwenyewe.
 
Sawa wewe unayemtisha na kumuona duni yeye mwenye mtizamo tofauti na wako huoni kwamba na wewe ni walewale tu, tukiwa na open mind hapa huenda akabadilika akawa kama wewe ukimuonyesha kile unachokiamini wewe kwa mtizamo wake (sio kwa kutumia katiba yako lakini kama the only proof) sababu Katiba yako (Kitabu chako) kwake hakifanyi kazi na hakiamini ukishaamini kitabu hicho basi wewe ni muumini unayehitaji uelewa zaidi
Simlazimishi kuamini ninachokiamini kama vile mchungaji asivyoweza kumlazimisha punda kunywa maji mara baada ya kumfikisha lamboni.

Mimi jukumu langu ni kumuelekeza ila kuamini au kutokuamini ni juu yake ila matokeo ya machaguzi yake atakuja kuyaona baada ya kufa.

Sidhani kama atakuja kusema kuwa Mungu alimsababisha asiamini ili hali alishaletewa kila aina ya ushahidi na akaupuuza ,kuukejeli na kuudharau.


Mwanadamu siku ya hukumu hatakuwa na argument yoyote juu ya Mola wake. Huwezi kumlaumu Mungu kwanini hukuamini ilihali alikuletea kila aina ya ushahidi ili umwamini lakini kwa jeuri na kiburi ulikataa.
 
If that was the case hakuna watu wangejiua ?!!!, Kuna saa na wakati kujiua ni shortcut yaani mpambano wa kitaa unakuwa mgumu zaidi....

Au hujasikia watu kwenye pain wanaomba wapewe sumu wafe!!!
Kujiua kutokana na changamoto za kimaisha ni aina ya mwisho ya kukata tamaa juu ya uwezo wa Mungu katika kukutatulia shida zako. Maisha haya ni mtihani tu hivyo usitegemee kuwa yatakuwa marahisi vile unavyotaka wewe. Ukiwa tajiri kuna mitihani na ukiwa masikini vilevile kuna mitihani yake.
 
Mungu anajua kuwa mtu huyu atachagua "A"

Mpaka hapo "A" ishakuwa ni lazima

Kama "A" ishakuwa lazima maana yake huyo mtu hawezi kuchagua vinginevyo

Kama huyo mru hawezi kuchagua vinginevyo, basi hayuko huru.

Hivyo kila kitendo afanyacho, atafanya akiwa hana uhuru

Ili uhuru uwepo inatakiwa kuwa na multiple options ambazo ni possible

Since "A" haiwezi kuepukika maana yake iko fixed, choice kuwa fixed....hakuna uhuru
Elimu ya Mungu ni pana sana kiasi ukiamua kuitafakari sana kiundani unaweza ukakufuru ikiwa kama huna imani moyoni mwako na kama una imani ndani yako basi inakuzidishia zaidi imani juu ya uwezo wa Mungu.

Mungu anafahamu uhalisia wa nafsi zetu ile kindani ndani. Yaani hata ukifake vipi ki-nje bado yeye anaujua u-ndani wako. Ndio maana mara baada ya watu kuhukumiwa kwenda motoni na kuishi miaka mingi ndani ya moto, watamuomba Mungu kuwa awarudishe tena duniani ili waje kusahihisha makosa yao na wawe watu wema kwa maana watakuwa wameshakoma kwa kuonja uchungu wa adhabu.


Mungu atawajibu kuwaambia kuwa hata kama arawarejesha huku duniani bado watarudia yale yale waliyokuwa wakiyafanya na wataikataa kweli. Hivyo ombi lao halina maana yoyote ile.
 
Kwahio in Short dhambi kubwa kuliko zote kwa Imani yao ni wale wanaoamini Mungu Tofauti na unayemwamini wewe ?

Au sijakupata vema ?


Dhambi kubwa ni kumuamini Mungu tofauti na huyu aliyeumba kila kitu. Ukimfanyia kuwa ana mshirika au washirika unakuwa umemtukana sana .
 
Quran 16:9

And upon Allah is the direction of the
way, and among the various paths are those deviating. And if He willed, He could have guided you all.



"Na ni juu ya Mwenyezi Mungu kuelekeza Njia. Na zipo njia za upotovu. Na angeli penda angeli kuongoeni nyote."


Mungu yeye kazi yake ni kubainisha tu njia Sahihi na Njia zisizo sahihi. Ila jukumu la kufuata wapi mwanadamu unataka uelekee ameliacha kwa mwanadamu mwenyewe.

Mungu angelitaka angelituongoa wote (kama ilivyo kwa malaika ambao hawatendi dhambi) kwa maana tungekuwa waumini ila hakutaka kwa kuwa ametupa free will kuchagua tunachokitaka ila katika kila chagua huwa kuna consequences zake.


Mwanadamu licha ya kuwa ni kiumbe mwenye hoja nyingi sana ukimpa nafasi ajitetee ila siku hiyo ya hukumu hatakuwa na hoja kabisa ila atabaki tu kuilaumu nafsi yake mwenyewe.

Yaani ni mfano wa Mtu mwenye njaa apelekewe chakula izuri mbele yake kisha agome kula kwa utashi wake halafu mwiso wa siku afena njaa kutokana na ukaidi wake ila akija kuulizwa nini kilikufanya usile? Ajibu kuwa aliyemletea chakula alimzuia asile !!

Lazima huyu mtu ataonekana hana hoja maana pindi wakati analetewa chakula hakushikwa mkono wala kuzibwa mdomo asile, ila kwa kiburi na jeuri yake aligoma tu kula kile chakula. Huu ndio mfano wa mwanadamu anayeikataa haki na kuamua kuchagua batili ili aje kulalamika kuwa hakuwa na free will kwasababu tu Mungu anajua matokeo na muishilio wa kila machaguzi yatakayofanywa na matendo ya wanadamu.

Ni jambo la kawaida kujua kuwa usipokula ni lazima utakufa kwa njaa.

Ukimkataa Mungu ni lazima utakwenda kukutana na adhabu.

Ukimkubali Mungu utakwenda kulipwa mema n.k​
 
Back
Top Bottom