Kwanini Puza wa Tambaza alijiua?

Kwanini Puza wa Tambaza alijiua?

Nikiwa form one Tambaza 1994 nilivuliwa viatu na kunyang'anywa pesa na mwanafunzi aliyefahamika kwa jina la Dictator akiwa na mwenzake aitwaye Bedui.Aliyetoa wazo la kufuta O level Tambaza ashukuriwe maana nilichaguliwa tena Tambaza A level 1998 shule ilikuwa imebadilika.Mabronso na masistadu walikuwa wa kutosha.
Wewe si ulikoswakoswa kupigwa mtama karibu na Azania? Kama nakukumbuka hivi
 
Wakati ule puza ulikuwa tishio kwa migomo,fujo baina ya Shule Na shule .nilikuwa Na mwalimu alikuwa anaitwa otieno ulikuwa Mwl.mkuu musoma alliance kama ulikuwa mkorofi shuleni ulikuwa huwezi kuendelea Na masomo kwani ndiye alikuwa mkuu wa body selection.lakini sidhanii kama ndio ulikuwa sababu zaidi ila kuna makosa nafikiri aliyafanya akawa anatafutwa.
 
.....acha kuua soo kipusti we chocolate!...

Naona umeamua kuja na ID nyingine! Kweli GENTAMYCINE ni homa ya jiji humu JF yaani mpaka ' naogopwa ' na Watu wanaona njia pekee ya kuzima ' moto ' wangu ni kunishambulia kwa ma ID's mbalimbali lakini pamoja na ' mbinu ' zote hizo bado tu nawapelekesheni ' puta ' kwa hii hii ID yangu. Haya hii ID yako nyingine nimeshaijua sasa njoo basi tena na zile mbili zingine Mkuu.
 
miaka hiyo azania na tambaza vijana walikua machachari na akili zao zilikua machachari ila sasa azania na tambaza zimepoa na vijana akili zao zimekua baridiii, matokeo yao yanatuumiza sana tuliosona ktk shule hizi huko nyuma
Siku hizi wanakula sana chips.. Wanakuambia zikaushee
 
Imekuchoma nini? Asilimia kubwa ya hao waliokuwa secondary miaka ya 80 wanapiga kelele kuwa maisha magumu serikali imewaletea umaskini. We jaribu kufuatilia comments zao uone.

Kama ulianza miaka ya 80 ulikuwa secondary na upo humu JF jua we ni maskini. Na hauwezi tena kuwa kama bill gates huu ni muda wetu sisi tuliozaliwa miaka hiyo nyie mkiwa secondary
Dogo unaijua Jf kweli wewe team wema
 
Huo mwaka Hata nilikuwa bado sijazaliwa,
Kwani Huyo Puza Anaingia kwa mnyama
SCORPION ?
runner.png
 
Kwa nini mkuu ? Funguka
Puza Fala,

Mwenyewe ndivyo alivyokuwa akijiita Tambaza na masela wake ndivyo tulivyomuita.

Puza alikuwa na split personality, moja boonge la mtemi halafu nyingine bonge la mtu wa kawaida hivi, kama fala, basi ukimkuta kakaa nyuma kule mesi na machizi kanyong'onyea anasikiliza story ukimwambia "Puza Fala" na yeye utamsikia "niambie kichaa wangu". Hapo kila mtu ana "Nom de Guerra". Jina la vita. Kuna Msoviet, Bedui. Mpalestina. Tyson. Buchiza. Carlos. Bokassa. Abacha. Mkonda, duuh, machizi kibao nawasahau majina wengine.Miaka 26 sasa.

Ila siku moja Puza alijichanganya anga za Herman, form one. Herman alimrusha Puza makata mbele ya darasa sitasahau mpaka leo. Puza alichezea kichapo bila kutegemea halafu ile issue ikawa imeishia pale pale kama haijatokea. Halafu ukimuangalia Herman mwenyewe aliyemchapa Puza kama mtoto mtoto tu hana jina wala mwili.

Nikasema kila mtemi ana mtemi wake.
 
Kipindi hiki wakati kina Puza Wanajivunia ujinga hata mimi nilikuwa O level, ndio kilikuwa kipindi cha kwenda Zenj na passport, kwenda UK bila viza ilikuwa unakata tu ticket unakipa kitu, na walioingia UK kipindi hicho karibu wote sasa hivi wana uraia.
Michongo ya kwenda Marekani ilikuwa kwa summer Camp na Jambo lee kupitia boy scout hakika nimekumbuka zamani.

Kuna walimu waliniwekea bifu za kitoto kisa navaa mokasini za dukani maduka ya samora avenue wao wanavaa bora shoes.

Ila ilinishangaza zaidi kipindi chetu mafisadi walikuwa mafisadi kweli watoto zao walikuwa wanadrive magari kuja nayo shule kuanzia form one mpaka form four.

Kampani yangu ya kutokea mtaani ilikuwa wote wapo Tambaza mimi nilikuwa ni mmoja ya wanafunzi wachache tuliokuwa tunaingia Tambaza na uniform za shule nyingine na tulikuwa powa na msosi wa bure wa shule nilikuwa napiga bila kubaguliwa.

Namkumbuka mshikaji mmoja wanamuita kiuno jina lake nimemsahau alikuwa karibu na kina Saigon wa Diplomats huyu jamaa alikuwa anatisha kwenye kucheza na gari.

Wakati kina Puza wanatamba na usela mavi wao mimi nilijiongeza kwa watoto wa kishuwa tukitoka na mikoko ya madingi zao breki Forodhani secondary school kwa mademu wenye TBS.
Matola kumbe we mtoni kitambo ee
 
Back
Top Bottom