Kwanini Puza wa Tambaza alijiua?

Kwanini Puza wa Tambaza alijiua?

Mimi nilikuwa nasikia sifa zake tu nilipokuwa Azania. Alikuwa anawatembelea mabesti wake pale Azania wakijiita Barcelona lkn zaidi ya usela, hawakuwahi kufanya jambo lolote la ajabu shuleni kwetu Azania zaidi ya utoro wa kawaida wa watukutu kutoingia darasani kwa kujichinbia vichakani.

Kilichokuwa kibanisikitisha kwenye lile kundi kulikuwa na dada mmoja akisoma Zanaki akiitwa Herieth ambaye alikuwa akishinda pake Azania kwa boyfriend wake aitwaye Gift ambaye alikuwa member wa group la kina Puza liitwalo Barcelona. Sijui yule dada aliishia wapi na upuuzi wao maana mwaka aliojinyonga Puza mimi nilikuwa namaliza F 4.

Vv
 
Hii Thread inaeza kutukumbusha wana Tambaza wa 80's and 90's au wanasekondary wa miaka hiyo kama azania, zanaki, Jangwani, hasa wakati wa mabasi ya wanafunzi, au yale ya mashirika kuja kutubeba bure,,,,,,long time,,let be connected...

Puza akiwa form 1 mm form III (Ztwo) 1990. alikuja darasan kwetu ambako kulikuwa watemi kadhaa..duh aliingia gafla na kuchimba mkwara kinoma..then akatoka na wapame wake...duh tukabak tunapiga meza na kutukana huyu form I anajiamini nini mikakati ya kumfuata ikapangwa lakin nan akamfunge paka kengele....ilikuwaa kaz..ikiishia hewani..

Anex anachukua msosi atakavyo...!! Ila tulilaumu sana kwa kujiua kikike sana....niliudhuria mazishi japo nilkuwa nimemaliza shule nikitokeaa home kwa mfuga mbwa....Tambaza my school

R.I.P Puza

Mkuu ulikuwa F3 session A au B? Ulikuwa darasa gani? Mimi nilikuwa session B lebo nyekundu, F1 hadi F2 nilikuwa darasa N, nilipoingia F3 nilikuwa R (commerce).

Vv
 
Kwa wale watoto wa Tambaza 1990 to 1993 mtakuwa mnakumbuka jamaa wakuitwa Puza.Huyu alikuwa ni miongoni mwa watukutu mashuhuri wa Tambaza..Mwaka 1992 Puza alijiua kwa kujinyonga nyumbani kwao maeneo ya Riverside...Mpaka Leo bado haijajulikana nini sasa kilimsukuma Puza hadi kupelekea kujinyonga ingawa watu wengi wanasema alijinyonga kwa sababu alikuwa anakabiliwa na kesi nyingi nzito . Za mauaji tatu na kati ya hizo tatu tukio la mwisho inasemekana alimuua denti wa Zanaki kwa kipigo Kikali so akawa anatafutwa na polisi.Mdau wewe unajua vipi kuhusu kujinyonga kwa huyu jamaa

Ni kweli Marehemu Omary au Omario a.k.a Puza alijiua ila naomba nikusahihishe kidogo ni kwamba hakujiulia Riverside na wala alikuwa haishi Riverside bali alikuwa ni ' Mtoto ' wa Magomeni na hata Msiba wake ulikuwa hapo hapo Magomeni. Leo mnamwogopa Scorpion wakati Puza alikuwa akiyafanya makubwa na ya hatari zaidi yake na Masela wote wa Dar enzi hizo walikuwa ' wanaufyata ' kwake ila na yeye Marehemu Puza na ujanja wake wote alikuwa akisikia tu Marehemu Nkama Sharp yule Police ' mbabe ' na ' mtemi ' kuliko Police wote wa kipindi hicho au miaka hiyo anakuja tu alikuwa anatoka ' nduki ' kujificha. Puza alikuwa akipanda tu ' Daladala ' Makondakta walikuwa wakianza kukusanya nauli siti za mbele yake tu na kama akikaa siti ya mbele basi Makondakta walikuwa wakianza kukusanya nauli zao siti za kuanzia nyuma yake tu huku wakimtolea ' tabasamu ' la kumnunia kimoyo moyo. R.I.P Omary Puza na Nkama Sharp.
 
You are right,shule iliyokuwa inatoa upinzani kidoogo kwa tambaza wakati huo kwa mambo ya fujo ilikuwa kinondoni,ila kwa masomo ilikuwa Azania.Azania walikuwa wazuri kwa O level wakati Tambaza walikuwa wazuri kwa A level,na fujo za Tambaza ilikuwa ni O level Na zaidi form two na form one,na pia watu wa fujo hasa walikuwa wachache ila shule nzima na hasa O level walikuwa na umoja sana ndicho kilikuwa kinawabeba kwenye vurugu,ukimgusa tambaza mmoja ni kama umeigusa shule nzima,A level tambaza walikuwa watulivu sana na wengi wao walikuwa ni wale waliotoka Azania O level Ile Azania ya Mzee Kisamo na Mzee Meja ambayo ukichomekea shati unapewa adhabu,uniform ni kaptula ya kaki na shati bila kuchomekea,hapo one za point saba kwa O level ilikuwa kitu cha kawaida na Tambaza ya Kalumuna na baadae Mushi one za point 3 kwa A level ilikuwa kitu cha kawaida.Dah siku zimekwenda!


You are quite right. Aliyetuletea sheria ya kuchomekea mashati alikuwa Mwalimu Andrew Kwayu aliyekuja kuchukua nafasi ya Mzee Kisamo nadhani 1990, nilikuwa na-enjoy kutochomekea mashati.

Vv
 
Nilikuwa hostel ya Azania miaka ya 91-93 ... A level.... wakati huo tulikuwa wachache sana A level ila O level wengi sana.....na Azania walikuwa wazuri kwenye mpira... ilikuwa Tambaza wakija cheza mechi pale Azania na wakafungwa, ni lazima tuhame hosteli... kama huna ndugu mjini inabidi ukajibanze kwao mshikaji... vijamaa vifupi hivi havijachomekea mashati... vingi lakini vibabe mbaya....kituo cha fire ndo makutano yao kama konda fulani alileta taabu asubuhi... long time

Umenikumbusha kikosi cha Azaboy Footbal. Kina Robert Mwampembwa, Edward Mpandang'ong'o, Cecil/Sisili, Tilla, Sasi .... Dah, Azania my school, the school of gentlemen.

Vv
 
1. Puza hakujinyonga but alikunywa dawa (sifahamu kama kunywa dawa nyingi ni kujinyonga).

2. Jamaa, hakuwa na murder case yoyote, he was mtukutu tu kama ilivyokuwa watukutu wengine pale shule.

3. Kama ulivyosema mwenyewe, hakuna anayefahamu hadi sasa ni sababu zipi zilizopelekea jamaa kujiua kwa kunywa na zile dawa (wengine walidai kuwa alipima akakuta ameathirika hivyo hakupenda kushuhudia yale mathila) - maana aliamka akafagia uwanja na kumwambia mother wake kuwa nasafisha/ fagia uwanja maana kesho rafiki zangu watafika hapa kupiga story and ndio akajiua.

Aisee jamaa umeongea sawa kabisa, kipindi hicho nilikuwa la saba pale muhimbili na bro zangu watatu walikuwa.pale. Na kuna mbabe mwingine alikuwa anaitwa Chino. Haitakuja kutokea shule kama Tambaza Boy.
 
Duh! Mkuu umenikumbusha huyu jamaa jinsi alivyokuwa anawadhibiti makondakta wa daladala waliokuwa wanatunyanyasa madent wa miaka ile,manake jamaa alikuwa na mbavu na walikuwa wanamhanya hasa,niliwahi kushuhudia moja ya valangati zake pale ubungo minazi ambapo ndipo palipokuja kuwa kituo cha ubungo (wakati huo kituo cha ubungo kiko pale ubungo maji)jamaa aliwadhibiti kondakta na dereva wa daladala moja ikijulikana kwa jina la TORINO huku akitoa onyo kwa wanafunzi wasiingilie kwani atawamudu peke yake,na kweli aliwatuliza makonda wawili na dereva wao.Ila utakuwa umechanganya(?) sidhani kama kifo chake kilikuwa 1992,kama sio mwaka 1990 ilikuwa 1991 nadhani alikuwa kidato cha pili by then,pia umenikumbusha sonda boy bila kumsahau Okelo.

Sonda boy tumeishi nae kino tu, jamaa alikuwa na mwili kama Wa Tyson.
 
UMENIKUMBUSHA WADOGO ZAKE PUZA WAKINA GWANTWA N'A GWAKI WALIYOKUWA WANAKAA KOTA ZA TANESCO...OPOSITE N'A DRIIVE IN(UBALOZI WA MAREKANI SAHV)

OVA

Gwantwa sijui alipotelea wapi. Alikuwa anatisha sana kwenye kikapu
 
Tatizo lenu ndio hilo mnaukataa ukweli huku mkiendelea kuwa maskini na mawazo mgando. Kuanza upya sio ujinga na kukubali kuwa umekosea ni challenge ambayo inaweza kukusaidia kujijenga. JF ilikuwa home of great thinkers miaka hiyo ya 2007 mpaka 2009 sio sasahivi imekuwa political forum. Wengi wenu mlio humu ni njaa kali mmetumwa na vyama vyenu vya siasa kupiga porojo ili muweze kusaidia maisha yenu. hakuna hata mmoja anayekuja JF sikuhizi jst kuchangia mada au kuleta hoja ambazo zinaweza kuwajenga wengine.

Mfano mzuri ni wewe msem pitia thread hizo mbili ulizofungua na comments zote za nyuma ulizochangia inaonyesha wazi maisha yamekupiga una hela sio za maendeleo bali za kupeleka maisha mbele.

Watu waliokuwa vizuri kiuchumi huwez kuwakuta JF. Humu tumejaa sie vijana na nyie watu wazima ambao maisha yamewapiga. Kuanza upya si ujinga. Saa tatu hii usiku mtu una familia na umri umeenda uko JF kama si kukosa kazi nini?

Jitathmini mkuu.
Jamii forum ni tofauti na social forums zengine za whatsapp au facebook.Wengi wanaotumia JF ni waajiriwa au watumishi wa umma,wenye elimu zao au watu wenye heshima zao.Kama unaona umepotea kwa bahati mbaya unaweza kurudi kwenye groups za whatsapp au facebook.
 
Kwa wale watoto wa Tambaza 1990 to 1993 mtakuwa mnakumbuka jamaa wakuitwa Puza.Huyu alikuwa ni miongoni mwa watukutu mashuhuri wa Tambaza..Mwaka 1992 Puza alijiua kwa kujinyonga nyumbani kwao maeneo ya Riverside...Mpaka Leo bado haijajulikana nini sasa kilimsukuma Puza hadi kupelekea kujinyonga ingawa watu wengi wanasema alijinyonga kwa sababu alikuwa anakabiliwa na kesi nyingi nzito . Za mauaji tatu na kati ya hizo tatu tukio la mwisho inasemekana alimuua denti wa Zanaki kwa kipigo Kikali so akawa anatafutwa na polisi.Mdau wewe unajua vipi kuhusu kujinyonga kwa huyu jamaa


Siku zote damu ya mwanadamu haimwagwi hovyo, ukiua tu basi juwa umejipa laana na usije shangaa unakuja kujiua bila kutaka kwani roho ya marehemu inakudai.
 
miaka hiyo azania na tambaza vijana walikua machachari na akili zao zilikua machachari ila sasa azania na tambaza zimepoa na vijana akili zao zimekua baridiii, matokeo yao yanatuumiza sana tuliosona ktk shule hizi huko nyuma
Na kibaya zaidi zote zmewah kushika mikia hivi karibun ktk matokeo ya kitaifa[emoji20] [emoji20]
 
R.I.P labda angekuja kuwa Scorpion mwingine pengine mungu tunamwitaga fundi.
 
Nilikuwa hostel ya Azania miaka ya 91-93 ... A level.... wakati huo tulikuwa wachache sana A level ila O level wengi sana.....na Azania walikuwa wazuri kwenye mpira... ilikuwa Tambaza wakija cheza mechi pale Azania na wakafungwa, ni lazima tuhame hosteli... kama huna ndugu mjini inabidi ukajibanze kwao mshikaji... vijamaa vifupi hivi havijachomekea mashati... vingi lakini vibabe mbaya....kituo cha fire ndo makutano yao kama konda fulani alileta taabu asubuhi... long time
Hivi unajua umenichekesha kwa sauti! !! Eti vijamaa vifupi hivi havijachomekea mashati... vingi lakini vibabe mbaya..
 
Kwan jf ni kituo cha wahuni na walioshindwa? Je hakuna mada za kitabibu na Afya humu? Habari za malez na ujasiriamali je ? Tatizo letu waafrika tunaangalia umri kwa namba sio kwa kujifunza, waache wazee waendelee kujifunza huku wewe ukifanya jitihada za kuwachafua
Unajuaje! ?Labda angekuja kuwa Putini wetu. huoni alishaanza kuonyesha dalili za kutetea wanyonge! ?
 
RIP Puzza mara ya mwisho nilikuwa nae camp ya skauti 77 nadhani mwaka 1990 nikuwa form three R hapo Tambaza yeye akiwa form one ,alikuwa ni best yangu tunacheza ngumi hapo jengo waliokuwa wanakaa bording form 5 and six ,Apumzike kwa AMANI nimekumbuka mbali sana mzee Kalumuna na second master Mwaipopo, na babu TALIBARI mhindi aliyekuwa anauza juice dukani pale mbele ya stamico
 
Kama alivyojiua john mjema. Kuchanganya cha arusha na cha tabora ni shida.
 
Kipindi hiki wakati kina Puza Wanajivunia ujinga hata mimi nilikuwa O level, ndio kilikuwa kipindi cha kwenda Zenj na passport, kwenda UK bila viza ilikuwa unakata tu ticket unakipa kitu, na walioingia UK kipindi hicho karibu wote sasa hivi wana uraia.
Michongo ya kwenda Marekani ilikuwa kwa summer Camp na Jambo lee kupitia boy scout hakika nimekumbuka zamani.

Kuna walimu waliniwekea bifu za kitoto kisa navaa mokasini za dukani maduka ya samora avenue wao wanavaa bora shoes.

Ila ilinishangaza zaidi kipindi chetu mafisadi walikuwa mafisadi kweli watoto zao walikuwa wanadrive magari kuja nayo shule kuanzia form one mpaka form four.

Kampani yangu ya kutokea mtaani ilikuwa wote wapo Tambaza mimi nilikuwa ni mmoja ya wanafunzi wachache tuliokuwa tunaingia Tambaza na uniform za shule nyingine na tulikuwa powa na msosi wa bure wa shule nilikuwa napiga bila kubaguliwa.

Namkumbuka mshikaji mmoja wanamuita kiuno jina lake nimemsahau alikuwa karibu na kina Saigon wa Diplomats huyu jamaa alikuwa anatisha kwenye kucheza na gari.

Wakati kina Puza wanatamba na usela mavi wao mimi nilijiongeza kwa watoto wa kishuwa tukitoka na mikoko ya madingi zao breki Forodhani secondary school kwa mademu wenye TBS.
 
Back
Top Bottom