Kwanini Puza wa Tambaza alijiua?

Kwanini Puza wa Tambaza alijiua?

Kwa wale watoto wa Tambaza 1990 to 1993 mtakuwa mnakumbuka jamaa wakuitwa Puza.Huyu alikuwa ni miongoni mwa watukutu mashuhuri wa Tambaza..Mwaka 1992 Puza alijiua kwa kujinyonga nyumbani kwao maeneo ya Riverside...Mpaka Leo bado haijajulikana nini sasa kilimsukuma Puza hadi kupelekea kujinyonga ingawa watu wengi wanasema alijinyonga kwa sababu alikuwa anakabiliwa na kesi nyingi nzito . Za mauaji tatu na kati ya hizo tatu tukio la mwisho inasemekana alimuua denti wa Zanaki kwa kipigo Kikali so akawa anatafutwa na polisi.Mdau wewe unajua vipi kuhusu kujinyonga kwa huyu jamaa
Kila mtu akileta mambo ya shuleni kwake hapa itakuwa shida,hayo jadili na tambaza wenzio wa huo mwaka tena ktk wasap group kama halipo unda group uwe ADM mjadili kwa kina.
 
Inasemekana PUZA alijiuwa sababu ya wivu wa mapenz
 
Ha ha ha kitambo Sana daah...nakumbuka uuzwaji wa kiwanja cha mpira kutoka Tambaza kwenda muhimbili Primaly..mkaguzi wa Elimu sec Alexzander Ndeki akaja mkutanoni akamwaga data...,namkumbuka,Puza,Sagapower,Vimto..... Makamu WA shule Mr Wajimira,yule mzee aliyekuwa mkuu WA shule jina nimemsahau....baada ya fujo na Azania 1994,form wote tukasimamishwa shule mwaka nzima...mwaka uliofuata tukaperekwa shule za mikoani,...form one yetu ya 1993 ilikuwa na watu wakorofi Sana...
Mimi hapa umenikumbusha Mzee Alexander Ndeki alikuwa mkurugenzi wa elimu nilipoanza kazi ya ualimu baada ya kuhitimu UDSM 1994. Mzee alikuwa very principled. Nilipangiwa kazi kwenye shule ambayo nilifanyia BTP mwaka uliotangulia. Habari za Tambaza zilivuma sana kipindi hicho.
 
Mimi hapa umenikumbusha Mzee Alexander Ndeki alikuwa mkurugenzi wa elimu nilipoanza kazi ya ualimu baada ya kuhitimu UDSM 1994. Mzee alikuwa very principled. Nilipangiwa kazi kwenye shule ambayo nilifanyia BTP mwaka uliotangulia. Habari za Tambaza zilivuma sana kipindi hicho.
Kaka shikamoo
 
Familia ya kina Puza hii ni familia ya Kinyakyusa Puza,Ulimboko ( Uli ) na Aliko


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
miaka hiyo azania na tambaza vijana walikua machachari na akili zao zilikua machachari ila sasa azania na tambaza zimepoa na vijana akili zao zimekua baridiii, matokeo yao yanatuumiza sana tuliosona ktk shule hizi huko nyuma
dah kweli kbs..sikuhizi vimekuwa visengevisenge,hawawezi ubabe wa kimwili wala kiakili..facken
 
Duh! Mkuu umenikumbusha huyu jamaa jinsi alivyokuwa anawadhibiti makondakta wa daladala waliokuwa wanatunyanyasa madent wa miaka ile, maanake jamaa alikuwa na mbavu na walikuwa wanamhanya hasa, niliwahi kushuhudia moja ya valangati zake pale Ubungo minazi ambapo ndipo palipokuja kuwa kituo cha Ubungo (wakati huo kituo cha Ubungo kiko pale Ubungo maji) jamaa aliwadhibiti kondakta na dereva wa daladala moja ikijulikana kwa jina la TORINO huku akitoa onyo kwa wanafunzi wasiingilie kwani atawamudu peke yake, na kweli aliwatuliza makonda wawili na dereva wao. Ila utakuwa umechanganya(?) sidhani kama kifo chake kilikuwa 1992, kama sio mwaka 1990 ilikuwa 1991 nadhani alikuwa kidato cha pili by then, pia umenikumbusha sonda boy bila kumsahau Okelo.
kumhanya, valangati lugha za kibabe wakati huo.
 
Old is gold, Puza ni jina kubwa sana miaka hiyo, kila kijana au mtoto wa miaka hiyo alitamani kuwa pengine asome Tambaza au Azania, tulitamani hivyo kwa kuwa mbali na undava pia walikua wana Akili nzuri darasani.

Habari mbaya kwa vifo vya watu hawa, akina Puza na baadhi wa wasemi wa miaka hiyo, ila Puza nadhani alikua na Nguvu za kuzaliwa, maana ukiangalia wadogo zake kama marehemu Uli na Aliko wate walikua ni Majibaba na chembe chembe za ubabe hazikuisha, wote wame isha kuwa na matukio kadhaa mtaani ila bahati mabaya maisha yao haya kua marefu , Mungu awa laze pema peponi.
Design familia ilikuwa na chembechembe za u primitive. Maana vibaba vitatu vimeondoka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
You are right,shule iliyokuwa inatoa upinzani kidoogo kwa tambaza wakati huo kwa mambo ya fujo ilikuwa kinondoni,ila kwa masomo ilikuwa Azania.Azania walikuwa wazuri kwa O level wakati Tambaza walikuwa wazuri kwa A level,na fujo za Tambaza ilikuwa ni O level Na zaidi form two na form one,na pia watu wa fujo hasa walikuwa wachache ila shule nzima na hasa O level walikuwa na umoja sana ndicho kilikuwa kinawabeba kwenye vurugu,ukimgusa tambaza mmoja ni kama umeigusa shule nzima,A level tambaza walikuwa watulivu sana na wengi wao walikuwa ni wale waliotoka Azania O level Ile Azania ya Mzee Kisamo na Mzee Meja ambayo ukichomekea shati unapewa adhabu,uniform ni kaptula ya kaki na shati bila kuchomekea,hapo one za point saba kwa O level ilikuwa kitu cha kawaida na Tambaza ya Kalumuna na baadae Mushi one za point 3 kwa A level ilikuwa kitu cha kawaida.Dah siku zimekwenda!
Daah jamaa wamekukumbusha mbali .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimesoma uzi wote nilichogundua Mwl lulindi aliwahi nifundisha kibasila mwanzoni wa miaka ya 2000 . Alikua anafundisha civics na utani mwingi japo alikua anaonekana umri umeenda. Ilikua raha sana kipindi chake . Haya wakongwe hongereni RIP puza
 
Nimesoma uzi wote nilichogundua Mwl lulindi aliwahi nifundisha kibasila mwanzoni wa miaka ya 2000 . Alikua anafundisha civics na utani mwingi japo alikua anaonekana umri umeenda. Ilikua raha sana kipindi chake . Haya wakongwe hongereni RIP puza
Lulindi alitufundisha civics Tambaza,nadhani ndio mwaka lilipobadilishwa jina kutoka siasa kwenda civics,baada ya zile fujo walimu wengi walihamishwa,Lulindi akaletwa Kibasila sec.
 
Back
Top Bottom