#COVID19 Kwanini Rais ameamua kujificha nyuma ya kamati ya Corona? Anaogopa nini kuwambia Watanzania wajiandae na AstraZeneca? Anaogopa nini?

#COVID19 Kwanini Rais ameamua kujificha nyuma ya kamati ya Corona? Anaogopa nini kuwambia Watanzania wajiandae na AstraZeneca? Anaogopa nini?

Sasa hawa wanaosema Jiwe kafa kwa corona wamejuaje? maana unaambiwa fulani kafa kwa corona ila wale watu wa karibu wa marehemu huoni kama wameambukizwa huwaoni hata na mafua sasa hii corona ya bongo ni ya aina gani?
Kwa sasa yeyote anaweza kusema vyovyote.
 
Mkemia aliharibu kwa kuzuia takwimu kuchukuliwa akidai wote wamepona kabisa. Sasa Mama anatoaje maamuzi bila analysis na tafiti ya kitaaluma?

Mwanzoni tulianza vizuri ila walipoingiza siasa wakaharibu kila kitu....
Ni tafiti gani ya kitaaluma iliyowaambia wasishikane mikono kwa sababu ya corona ila barakoa wasivae wala kuepuka mikusanyiko?

Maana tunaona wanasalimiana kwa kutoshikana mikono hilo tunaelewa ni kwa sababu ya corona ila tunaona hawavai barakoa wala kuepuka mikusanyiko,sasa hapo nako kuna ushauri gani wa kitaalamu ambao utakuja na mapendekezo mengine tofauti na watu kuvaa barakoa? sasa nashangaa hata hilo nalo Mama kashindwa kulitangaza ukiachilia na yeye kufanya et tunatetea hadi aambiwe na wataalamu.
 
Mimi na familia yangu tutachoma chanjo Kama kamati itayoundwa ikipendekeza tuchomwe chanjo..siwezi kufuata mambo ya kichawi na kuacha ya sayansi
 
Chanjo lazima Ili kutotengwa kimataifa, mbona mataifa mengine wametumia wewe ulitakaje
Chanjo sio lazima ni hiari ya mtu kudungwa ama kutodungwa,yeye mama anaonekana anataka zilitwe ila sasa asitumie mgongo wa kamati,tunajua hilo ndio lengo lake sasa yeye alete tu asizunguke zunguke zikija watakaochoma watachoma basi tutakuwa tunaelewa na wazungu maisha yaendelee.
 
Naomba kujua mh mollel Ana hali gani? Alikuwa anataminisha mambo hovyo hovyo wakati yeye Ni daktari..
 
Hivyo vifo ndio vinatangazwa sana na ndio vinavyofanya watu waogope corona na kuona ni ugonjwa hatari na ndio maana vinatangazwa sana kuliko wanaoumwa na kupona japo ndio wengi. Sasa kama wenzetu huko wenye huduma bora za afya na kufuata tahadhari zote wengine hadi lockdown ila bado unasikia maelefu ya watu wanakufa kwa siku ndio maana ikaonekana afrika tutaokota maiti barabarani,kuna muda hadi kulitokea ule uvumi wa kwamba hospitali zimezidiwa wagonjwa Tz,ila sasa hivi inaonekana tatizo hatuna takwimu story za maiti barabarani na hospitali kuzidiwa wagonjwa hazipo tena.
Hiyo ni wave mbona huelewi..... Ukisikia third wave ndio iliyopita hapa Tz mwezi december ika peak February. So waliopona ewaa waliokufa walienda na nmeshaeleza humu kwamba Baba yangu mzazi almanusura afe kama sio kumpeleka hospital ya kibeberu baada za serikali kudai "ana homa ya kawaida tu".

Wote tunajua hata influenza za kawaida tu zinawaua wazungu kuliko hata Corona.... So sio jambo jipya kwa mafua hatari kma swine au bird flu kuua sana nchi za magharibi. Otherwise wangekufa wengi zaidi if wasinge weka sheria kma za lockdown au wasingekua na medical facility nzuri.

Tanzania waliugua wengi na sisi pia 5% walifariki tofauti ni kwamba hatutangazi takwimu. Ila mie mtaani tu na ukoo wangu, peers,friends, kulikua na misiba multiple mwezi February. Hili hta ww unafahamu ni WAVE

Kama mngetaka kucompare na wazungu kwanini hujiulizi Ukimwi au malaria inatuua sisi kuliko wao? Ama Miili yetu ina nguvu tu kwenye corona na magonjwa mengine haifui dafu?

Twende kwa hoja
 
Tunasubiri muujiza gani mwingne Watanzania kudhihirisha kwamba Mama alikuwa tofauti na mtangulizi wake!
 
Jifariji ila unasahau alikuwa mwenyekiti mwenza bunge la katiba, alikuwa makamu wa rais na bado yupo ccm utakuja baadae kulalamika usichojua ccm ni ileile ni sawa na chupa mpya mvinyo wa zamani
Ccm ikipata mtu anayetumia akili na sio makalio wala tumbo kufikiri lazima tumuunge mkono huyo mtu. Kwa iyo ni sawa tunavyomuunga mkono mama samia
 
Tunasubiri muujiza gani mwingne Watanzania kudhihirisha kwamba Mama alikuwa tofauti na mtangulizi wake!
We unaisi akili za mtangulizi wake zilikuwa sawa??? Yule si shetani aliyekuwa kwenye umbo la binadamu tu! Sasa kuna shida gani mama kuwa tofauti nae?
 
Wasalaam wana jamvi!

Nimeshangazwa sana na Mh Rais kusema ataunda kamati kuhusu swala la Corona ili baadae tuwe na msimamo kuhusu Corona!

Mimi kwenye hili nimejiuliza maswali hivi ni kweli Tanzania hatukuwa na msimamo kuhusu Corona? Huyu Rais si alikuwa Makamu wa Rais na Rais wake alishasema wazi kuwa Tanzania hakuna Corona na kama ipo ni ndogo sana?

Hii kamati anayounda anataka imwambie nini kipya asichokijua? Anataka aanze kutoa takwimu za Corona sasa anataka kamati imshauri?

Anataka aweke watu Lockdown sasa anataka kamati imshauri?

Anataka kulazimisha watu kuvaa barakoa sasa anataka kama imshauri?

Anataka kupokea chanjo ya Astrazeneca sasa anataka kamati imshauri?

Rais anaogopa nini kusema alikuwa hakubaliani na jinsi mtangulizi wake alivyo kuwa anaikabili Corona? Rais anaogopa nini kusema wamejiandaa kupokea chanjo ya AstraZeneca hivi karibuni?

Sidhani kama Rais anatakiwa kujificha nyuma ya kamati kwenye swala kama hili ambalo liko wazi!

Kuna kitu gani hajui ambacho anataka kamati imwambie?

Kwanini anajificha nyuma ya kamati anashindwa nini kuwambia watanzania wajiandae kudungwa Astrazeneca?

Kama Tanzania hatuna msimamo kwanini yeye havai barakoa? Hajui huo nao ni msimamo? Anataka ashauriwe nini?

Kwanini Tusiamini ana ajenda zake mkononi anataka azipitishe nyuma ya kamati ili watanzania waamini ni msimamo wa kamati kumbe ni msimamo wake?

Wasalaam!
Nia yako unataka kumlinganisha na Magufuli?
 
Unataka tuweke lock down, huo ndio utaalam unaotaka, hao wenye lock down wanakufa wengi zaidi ya Tz sasa nini faida ya lockdown ? SSH ana tatizo, tena ni KUBWA.
Kwani njia pekee ya kupambana na Corona ni lockdown tu? Mbona umeng'ang'ania lockdown, kakuambia ikidhihirika kuwa kweli Corona ipo Tanzania ataweka lockdown? Hiyo ni hofu yako tu na huna sababu ya kujenga hofu kwa kuwa utatuzi utatolewa na wataalamu na bila shaka Mh. Rais atazingatia ushauri huo katika uamuzi wake. Au huna imani na wataalamu wetu?
 
Kumekucha!

Yupo sahihi kabisa kwa sababu ile kamati ya mwanzo iliongozwa na PM Majaliwa na Ummy Mwalimu ilikuwa ni ya kisiasa siyo ya kitaalamu na haijawahi kuvunjwa!

Ndio maana ukaona Jaffo amejiingiza na nyungu zake.
Leo hii mshaanza kumbana Magu kama vile wasaliti walivyo mkana yesu kristu.
 
Back
Top Bottom