Kwanini Rais Samia aliamua kujibu hivi kuhusu Katiba Mpya?

Kwanini Rais Samia aliamua kujibu hivi kuhusu Katiba Mpya?

Kikeke: Unaweza kuhakikishia waTz au kutoa ahadi kuwa kabla hujaondoka madarakani Tz itakuwa na Katiba Mpya?
SSH: Kwa nini nihakikishe hilo? Kwa nini unataka nihakikishe hilo?
Kikeke: Kwa sababu watu wanadai kuwa Katiba hii imepitwa na wakati.
SSH: Basi niachie mi na waTz tutaelewana.
Kikeke: Kwa hiyo Katiba itapatikana?
SSH: Si we huishi Tz? Mi na waTz tutaelewana..
Kikeke: WaTz wanasema wanataka Katiba..
SSH: ...wamekwambia wewe?

Chui jike amevurugika duuh, hakuna mwimba mgumu kwa viongozi kama katiba mpya
 
President amejibu ki mipasho sana hilo swali...

Unamuulizaje mwandishi kwamba Walikwambia wewe?, niachie mm na watanzania..?

Bimkubwa angekuwa anaandaliwa majibu,, kuna siku ataaibisha taasisi ya Urais
Ngoja wampambanishe siku na Sakur km hajapigwa maswali akaanza kulia anaonewa kwasabu yeye mwanamke
 
Kwani hapo kafanyaje,kama sio kuidhalilisha!
Kuna kundi Fulani la watu halitakiwi kupewa madaraka makubwa ,wata abuse tu...watu wengine wanataka vitu simple...Ngoma ,michezo...Utamaduni!

Dunia ya sasa imelipa kipaumbele sana hilo Kundi...

Soon hata familia itaongozwa na hilo kundi
 
Maraisi wote tuonawapata sasa ni makosa yaliyofanyika nyuma, ipo siku tutapata raisi mwendawazimu
 
Watanzania wamekuambia wewe😂, Rais wa nchi hajui wewe hao watanzania umekutana nao wapi kama sio UMBEA NA Uchonganishi ... sisi hatutaki katiba mpya MAMA hatukutaki WEWE Tu
 
Kwa hiyo mulitarajia Rais SSH atatemeke kuhojiwa na Salim Kikeke? Our serious kweli?

Personally namuona amefanikiwa sana kwa majibu aliyompa. Kwani Marais wa kutetemekea waandishi wanapatikana wapi duniani?

Nitajie mmojawapo
 
Ila kama raisi katukosea anasema eti

Kwani watanzania wamekwambia wanataka katiba mpya

Ina maana hajui kelele zote hizi
nani kakwambia watanzania wanataka katiba mpya? Iliyopo ndo iliyotuponya na misukosuko ya kiuchuni, kisiasa, kiutamauni, kidini na kiutandawazi..

Katiba tuliyonayo 'is balanced to perfection! 'Wanaotaka kuvuruga nchi hii ni magaidi wa chadema
 
Hata wanaodai Katiba mpya wangekuwa wao madarakani hiyo isingekuwa kipaumbele
Umesema vizuri, ila kuna watu umewahukumu kwa hisia zako tu.

Kama hisia hizo ni kweli, kumbe ni wazi basi tunahitaji Katiba mpya
 
Kwani hujui kwamba wanakudharau kwa sababu wamekuweka madarakani?🐒🐒🐒
 
Katiba mpya itapatikana pale wadau wa maendeleo watakapowabana kama kwenye kesi ya kubumba ya ugaidi
 
Back
Top Bottom