Kwanini sijawahi kuona ama kusikia mikutano ya dini Masaki, Ostebay ama Posta?

Kwanini sijawahi kuona ama kusikia mikutano ya dini Masaki, Ostebay ama Posta?

Nashangaa hawa hasa watangaza dini wanaochipukia kwanini wote kutwa kujazana miji ya pembezoni mwa mji kwanini mitaa nikiyoitaja hawaendi?
Sijawahi kuona tangazo wala mkusanyiko kule mtu akihuburi injili
Umewahi kusikia mikutano ya siasa maeneo hayo? Je kuna maeneo ya kufanyia mikutano? Je ulikuwa hai au ulikuwa wapi wakati viwanja vya mnazi mmoja vinatumika kwa ajili ya mikutano ya dini?
 
Kwa sababu matajiri tunasubiri kwanza ngamia apite kwenye tundu la sindano Kama mlivyo tuahidi hatuiingii peponi hadi ngamia apite kwenye tundu la sindano

Mtuambie kwanza kama kuwa tajiri ni dhambi au ni chuki zenu tu
 
Kwanin wahubiri wengi wa kiroho wako kinondoni kuliko wilaya ya temeke mfano mbagala tandika ni ngumu sana kukuta makanisa ya kiroho
Yapo mengi sana..sema hujui yanakopatikana tukuelekeze ama una jibu unalotarajia tofauti.

#MaendeleoHayanaChama
 
Nashangaa hawa hasa watangaza dini wanaochipukia kwanini wote kutwa kujazana miji ya pembezoni mwa mji kwanini mitaa nikiyoitaja hawaendi?
Sijawahi kuona tangazo wala mkusanyiko kule mtu akihuburi injili
kule kuna watu wamejaa kiburi cha maisha, watu ambao kwa nje unawaona wamevaa nguo nzuri ila viunoni wame mahirizi, wamejaa machale na wengine majini na misukule wanaishi nayo. watu walioshinda kwa waganga kutafuta vyeo na pesa, wamezipata na wapo kifungoni kutoacha ushirikina kwasababu wakiacha tu shetani anabeba mali zote wanarudi kuishi manzese. jambo hili linawafanya wawe watumwa hadi siku ya kifo chao na wanaelekea moja kwa moja motoni kwa shetani baba yao.

masaki na oysterbay hakuna viwanja vya kuweka mikutano na kule wanakaa watu wenye hadhi/viongozi n.k. ni sawa na uzunguni zozote zile nchini. hao viongozi wengine wa serikali hawataki makelele, ukiweka mkutano tu watapiga tu simu polisi waje wauondoe. ni watu wanaokataa Neema ya Mungu, wanaona kama injili ni mambo ya kipuuzi kumbe katika upuuzi huohuo Mungu anaokoa watu. hao ni watu ambao wanaamini zaidi katika materialism kulili nguvu za Mungu, akiumwa anaamini tu kutibiwa na uzima wake upo kwenye mali zake kwamba zitamsaidia ndio maana hata kungekuwa na uwanja ukaweka mkutano kule wanaweza wasije kwasababu hawana njaa jikoni wala mifukoni, wanaweza kuwa na shida kiafya tu ila sasa hela ya hospitali wanayo, tofauti na ndugu zetu ambao hata hela ya hospitali hana sasa anageukia kwa Mungu. hao wa masaki hawajui tu kwamba hata ukiwa na hela ukakodi madoctor wote duniani wakutibu, uzima wako bado upo mikononi mwa Mungu ambaye ndiye Mungu huyo huyo wa wote. masikini kwa matajiri.

maisha ya duniani tunapita tu, makao yetu ni mbinguni kwa Mungu, whenever you live on this earth, try to figure out where you will spend your eternity. kuna sehemu mbili tu jehanum na uzimani. nafasi ya kuchagua aina ya maisha utakayoishi baada ya kifo ni sasa kabla hujafa, ukishakufa tu ni hukumu hakuna kuokoka hata ukiombewa na mapadre na maaskofu.

Okoka leo, mpe Yesu Maisha yako, atayabadilisha nawe utaupata uzima wa milele hapa duniani na ukifa mbinguni.
 
Nashangaa hawa hasa watangaza dini wanaochipukia kwanini wote kutwa kujazana miji ya pembezoni mwa mji kwanini mitaa nikiyoitaja hawaendi?
Sijawahi kuona tangazo wala mkusanyiko kule mtu akihuburi injili
Umewahi kukutana na fisi au nyoka pale posts dar es salaam au pale mnara wa mashujaa Dodoma?
 
Hizo sehemu ni geti kali halafu kila mtu yupo bize na maisha yake. No changanyikeni kivile
 
Tatizo maeneo ya kufanya hio mikutano katika ukanda huo hakuna, kama masaki uwanja ni masaki mwisho ndio kuna space nako hakuna population, posta utafanyia wap? Gymkhana?.. kwanza posta asilimia kubwa ni maofisi sio makazi ikifika saa 2 usik kweupe hakuna watu wapo wahindi tu 😂😂..
Mim naona shida ni Eneo ndio maana wanafanyia kawe ndio kitovu
 
Nashangaa hawa hasa watangaza dini wanaochipukia, kwanini wote kutwa kujazana miji ya pembezoni mwa mji kwanini mitaa niliyoitaja hawaendi?

Sijawahi kuona tangazo wala mkusanyiko kule mtu akihuburi injili.
Mwamposa aende Masaki sasa
 
Kila kibonde ana mbonde wake aseeee wao. Mbonde wao ni akina mwamposa , nabii bushiri and the like , upo ?
 
Nashangaa hawa hasa watangaza dini wanaochipukia, kwanini wote kutwa kujazana miji ya pembezoni mwa mji kwanini mitaa niliyoitaja hawaendi?

Sijawahi kuona tangazo wala mkusanyiko kule mtu akihuburi injili.
Sasa huyu unaenda kumtabiria kuwa kesho utamiliki gari? Kesho utaitwa kazini? Waliokudhulumu kiwanja chako wanaenda kukirudisha? Sijui kukomboa ardhi na mengne Kama hayo?
Hapana,manabii watabanana nasisi hukuhuku.
 
Mikutano ya injili, mahubiri ya vitisho na makanisa yasiyo na kichwa wala mguu ni kwaajili ya watu masikini.
 
Back
Top Bottom