Kwanini Tanzania haikupata waandishi vitabu maarufu yaani "African Writers"?

Kwanini Tanzania haikupata waandishi vitabu maarufu yaani "African Writers"?

Pia yumo Ishmael MBISE. Huyu kwa sasa ni Profesa wa Literature, Chuo Kikuu Tumaini Makumira. Aliandika: Blood on Our Land. Waandishi wa Kazi za Fasihi wako WENGI tu. Pamoja na Shaaban Robert, wapo pia: Kezilahabi, Semzaba, Aldni Mutembei, Mulokozi, Angoro Anduru, Kaigarula, Penina Muhando-Mlama, Ebrahim Hussein, Richard Mabala, Profesa Mbogo, Julius Nyerere, Gabriel Ruhumbika, Amandina Lihamba, Balisidya, Ndulute, nk. Wengi wa hawa waliandika kazi zao za Fasihi kwa lugha ya Kiswahili.
Ieleweke pia kuwa Africa Writers' Series, ni kampuni la uchapishaji wa kazi za Fasihi za Kiafrika (zilizoandikwa na Waafrika) kuhusu Afrika. Lugha ya uchapishaji ni Kiingereza. Kwa maana hii, kukosa kuchapisha kazi ya Fasihi katika AWS, haimaanishi Watanzania Hawajabobea katika kazi za Fasihi. Kwa waliosoma Fasihi shule za sekondari na vyuo, wamesoma kazi nyingi tu za fasihi zilizotayarishwa na Watanzania.

Mimi ndiye niliyeanzisha thread hii hivyo kama ni suala la kumaanisha mimi ndiye mmiliki wa maana niliyotaka muone.

Nimesoma hadi vya mepelezi Willy Gamba lakini huwezi kufananisha popularity ya KUFA NA KUPONA cha Musiba na JAMES HADLEY CHESS.

Mimi ninaongelea popularity. Kama ni kazi za sanii basi hata bibi yangu mzaa mama alituhadithia hadithi nyingi za kabila lao.
 
Usipojua jambo uliza ufundishwe. Nyerere hajawahi kuandika kitabu kiitwacho "Mabepari wa Venice". Tofautisha kati ya kuandika kitabu na kutafsiri kitabu, tena hichohicho cha "Merchant of Venice" cha wazungu unaotudanganya huwahusudu.
Mkuu soma vizuri mwishoni nimeeleza nimemtaja pia William Shakespears

Hoja inajenga povu linabomoa
 
T
Tujenge utamaduni wa kusoma kazi za nyumbani zipo nyingi sana

Mimi siwezi kuwa mteja wako kwa sababu tu nimezaliwa na wewe taifa moja. Hatutakaa kusoma kazi za nyumbani kama hazivutii wakati dunia imejazana kazi za tele zinavutia. Shindana na dunia. Fanya kazi nzuri nitagombania vitabu vyako.

Lakini ukiandika vitabu vya kujipendekeza kwa viongozi wako nitaacha vyako nitakimbilia vya nje.
 
Mkuu soma vizuri mwishoni nimeeleza nimemtaja pia William Shakespears

Hoja inajenga povu linabomoa

Julius Nyerere and all Tanzanian's, is not among the renown African Writers champion, which is the basis of my thread.

Sikueleza thread ya mtu kukopi na kutafsiri, tena unatupa tafsiri mbovu kwa maana ya kwamba Nyerere aliwachukia wafanyabiashara na akawapa jina mabepari wakati Shylock alikuwa merchant mzuri tu na kizuri ni kwamba system ilimdhibiti kupitia akina Bassanio, Portia etc.
 
Mimi siwezi kuwa mteja wako kwa sababu tu nimezaliwa na wewe taifa moja. Hatutakaa kusoma kazi za nyumbani kama hazivutii wakati dunia imejazana kazi za tele zinavutia. Shindana na dunia. Fanya kazi nzuri nitagombania vitabu vyako.

Lakini ukiandika vitabu vya kujipendekeza kwa viongozi wako nitaacha vyako nitakimbilia vya nje.
Mm si mwandishi ni msomaji kama wew hata kazi za nje pia nasoma si mbaguzi
 
T
Tujenge utamaduni wa kusoma kazi za nyumbani zipo nyingi sana

Tuna uhuru wa kuchagua kusoma vitabu vyovyote vya taifa lolote. Shindana na waandishi bora duniani hata hao tu "African Writers" ili kitabu chako kigombaniw
Nchi ya kusadikika............?


Endelea na huohuo uswahili wenu, siku moja natarajia kuleta opinion kwamba JF kuwe na windo kwa kiingereza tu. Ili kupunguza kejeli za watu wa Lumbumba na Ufipa, maana if you talk the queen tongu, Lumbumba and Ufipa turns dumb.
 
1: Nigeria kulikuwa na Wole Soyinka, Chinua Achebe.
2: Kenya kulikuwa na mtu kama Ngugi wa Thiongo.
3: Uganda kulikuwa na Okot P'Bitek.

Wote hawa waliitwa African writers na vitabu vyao vilisomwa kwenye "english literature" katika nchi nyingi.

Ukiangalia list yote ya "African writers" huoni na kujivunia mtanzania hata mmoja. Tujiulize kwa sababu za ukweli, kwa nini Tanzania hatukupata wala mmoja kwenye hao "African writers"?
ijulikane wazi kwamba tanzania ni mojawapo kati ya nchi chache ulimwenguni ambamo wanaharakati, watetezi wa haki, na wasomi walioelimika huishi kwa mashaka makubwa saaaaaana. hivyo ni wazi kwamba ni vigumu kuwa na watu mashuhuri wa kuandika vitabu vye maudhui za kimataifa, kikanda na kimataifa (hofu No. 1)
 
Tuna uhuru wa kuchagua kusoma vitabu vyovyote vya taifa lolote. Shindana na waandishi bora duniani hata hao tu "African Writers" ili kitabu chako kigombaniw



Endelea na huohuo uswahili wenu, siku moja natarajia kuleta opinion kwamba JF kuwe na windo kwa kiingereza tu. Ili kupunguza kejeli za watu wa Lumbumba na Ufipa, maana if you talk the queen tongu, Lumbumba and Ufipa turns dumb.
Huna hoja kijana umeanza kupwaya sasa

Kakojoe ulale mm siyo level yako ..
 
Eilesh lema ni mwandishi mzr sana wa kitanzania...ameandka novel itwayo ...parched erth ...sio lazima wazungu watupangie nn Cha kuandika...wasi wasi wangu ni huu utawala wa unaobeza hata masomo ya lugha kwa kigezo Cha arts ...but tunaweza
 
1: Nigeria kulikuwa na Wole Soyinka, Chinua Achebe.
2: Kenya kulikuwa na mtu kama Ngugi wa Thiongo.
3: Uganda kulikuwa na Okot P'Bitek.

Wote hawa waliitwa African writers na vitabu vyao vilisomwa kwenye "english literature" katika nchi nyingi.

Ukiangalia list yote ya "African writers" huoni na kujivunia mtanzania hata mmoja. Tujiulize kwa sababu za ukweli, kwa nini Tanzania hatukupata wala mmoja kwenye hao "African writers"?
Naona umemsahau Severin R.Ndunguru mwandishi wa vitabu vya fasihi kwa lugha ya kiingereza.
Ameandika vitabu hivi 1.A WREATH OF FR MAYER OF MASASI (kinatumika O level Literature)2.DIVINE PROVIDENCE 3.SPARED
 
Tunao akina [HASHTAG]#Mnyamphala[/HASHTAG] huyu ni mgogo wa Dodoma, ni wandishi wazuri tu ila sasa lugha kwetu baba ndo issue na ni mpaka leo
 
Eilesh lema ni mwandishi mzr sana wa kitanzania...ameandka novel itwayo ...parched erth ...sio lazima wazungu watupangie nn Cha kuandika...wasi wasi wangu ni huu utawala wa unaobeza hata masomo ya lugha kwa kigezo Cha arts ...but tunaweza

Wazungu hawajakupangia. Issue ni kwamba havijulikani kwani kiwango ninachosema. Ukimtaja huyo Eiles Lema mimi ndiyo kwanza namsikia. Lakini "African Writers" library zimejaza vitabu vyao.
 
Naona umemsahau Severin R.Ndunguru mwandishi wa vitabu vya fasihi kwa lugha ya kiingereza.
Ameandika vitabu hivi 1.A WREATH OF FR MAYER OF MASASI (kinatumika O level Literature)2.DIVINE PROVIDENCE 3.SPARED

Sijamsahau. Hata kumjua simjui and to be honest leo ndiyo namsikia.
 
1: Nigeria kulikuwa na Wole Soyinka, Chinua Achebe.
2: Kenya kulikuwa na mtu kama Ngugi wa Thiongo.
3: Uganda kulikuwa na Okot P'Bitek.

Wote hawa waliitwa African writers na vitabu vyao vilisomwa kwenye "english literature" katika nchi nyingi.

Ukiangalia list yote ya "African writers" huoni na kujivunia mtanzania hata mmoja. Tujiulize kwa sababu za ukweli, kwa nini Tanzania hatukupata wala mmoja kwenye hao "African writers"?
Kama ungefanya ka research kidogo ungekutana na vitabu kama Kisima cha Giningi, Kuli, Adili na Nduguze, waandishi na watunzi nguli, Kiu, Kwaheri Ukoloni, kwaheri uhuru, nk ama ungekutana manguli kama SHAABAN Robert, E. Kezirahabi, PENINA Mlama, Mohammed Shafi, Julius Nyerere, Mzee Said Abdullah, nk..
 
Julius Nyerere and all Tanzanian's, is not among the renown African Writers champion, which is the basis of my thread.

Sikueleza thread ya mtu kukopi na kutafsiri, tena unatupa tafsiri mbovu kwa maana ya kwamba Nyerere aliwachukia wafanyabiashara na akawapa jina mabepari wakati Shylock alikuwa merchant mzuri tu na kizuri ni kwamba system ilimdhibiti kupitia akina Bassanio, Portia etc.
'Julius nyerere and all Tanzanians'...so where do you peg yourself! and what have you done to make the indifference??? You are so mouthful blindly pitting yourself against your inner self
 
Naona umemsahau Severin R.Ndunguru mwandishi wa vitabu vya fasihi kwa lugha ya kiingereza.
Ameandika vitabu hivi 1.A WREATH OF FR MAYER OF MASASI (kinatumika O level Literature)2.DIVINE PROVIDENCE 3.SPARED
Umenikumbusha KITABU cha The Mwembechai Killings kilichotungwa na Dr Njozi, lakini serikali ikakipiga stop nchini..
 
Back
Top Bottom