Kwanini Tanzania haikupata waandishi vitabu maarufu yaani "African Writers"?

Kwanini Tanzania haikupata waandishi vitabu maarufu yaani "African Writers"?

1: Nigeria kulikuwa na Wole Soyinka, Chinua Achebe.
2: Kenya kulikuwa na mtu kama Ngugi wa Thiongo.
3: Uganda kulikuwa na Okot P'Bitek.

Wote hawa waliitwa African writers na vitabu vyao vilisomwa kwenye "english literature" katika nchi nyingi.

Ukiangalia list yote ya "African writers" huoni na kujivunia mtanzania hata mmoja. Tujiulize kwa sababu za ukweli, kwa nini Tanzania hatukupata wala mmoja kwenye hao "African writers"?
wapo watanzania wengi mf. bernad mapalala,novel yake inatumika mashuleni

Screenshot_2017-10-15-22-23-50.png
 
Ain't necessarily wawe kwenye list ya African writers lakini bado tunao famous world class writers kama :
●Abdulrazak Gurnah (1948– ), novelist and critic
● Mark Behr (1963– ), fiction writer also connected with South Africa
● Prince Kagwema (1931– ), novelist
● Julius Nyerere (1922–1999), politician and writer[Gikandi & Mwangi]
● Chachage
Hawa wote kazi zao zinapatikana na kutumiwa na wanazuoni ktk varsities mbalimbali zinazofunza lugha duniani
 
Ndio utambue hatuna wasomi bali wahitimu.
Zile kelele sijui Mimi shule na vyuo changu kipanga ww chako cha kata ni kujifariji.
Unakumbuka ile zain African challenge, watanzania walikuwa wanafanywa nini..!??
Ilikuwa aibu mkuu.
 
Ain't necessarily wawe kwenye list ya African writers lakini bado tunao famous world class writers kama :
●Abdulrazak Gurnah (1948– ), novelist and critic
● Mark Behr (1963– ), fiction writer also connected with South Africa
● Prince Kagwema (1931– ), novelist
● Julius Nyerere (1922–1999), politician and writer[Gikandi & Mwangi]
● Chachage
Hawa wote kazi zao zinapatikana na kutumiwa na wanazuoni ktk varsities mbalimbali zinazofunza lugha duniani

University ipi unayotudanganya ili kujifuta aibu. Essays on Ujamaa tu ya Nyerere ililetwa tukaisoma secondary lakini nayo haikukidhi kuingia kwenye heshima ya African Writers.

Hao unaowataja unawaju mwenyewe tena kwa ka kufukunyua kwa jasho hata kama kweli vipo. Kubali tatizo kwamba watanzania mlijipendkeza kw akudumisha fikra za fulani na historia sasa inawaumbua.

Hamuonekani hata kwenye vitabu vya bara lenu. Aibu tupu.
 
Aina ya WaTz ni waswahili kwa tabia na matendo!! Na mtu kuwa mswahili kwa tabia ni kasoro. Rais wa awamu ya kwanza angalau alijitahidi, Lakini wa sasa na wale wengine mhhh.
Awamu ya kwanza si ndio ilikichinjia baharini kiingereza? Anyways kiswahili kimesaidia kuliunganisha taifa japo critiques wanasema hatukupaswa kukifuta kiingereza kama lugha ya kufundishia kuanzia elimu ya awali/msingi, maana kiswahili tayari kilikua kinazungumzwa na zaidi ya asilimia 95 ya wa Tz,; kwa hiyo ilikua ni makosa kuondoa msingi wa kiingereza kwa watu wetu
Waandishi kwa maana ya waandishi tunao wengi na mahiri kuanzia riwaya hadi ushairi kwa fasihi ya kiswahili, hao African Writers wanataka kiingereza tu ambayo ni lugha tu. Ndio maana hata kwa Nigeria nchi yenye population kubwa lakini waandishi tuwajuao ni wachache tu, hii ni kwa sababu wapo wengine wengi wazuri hatuwajui sababu wameandika kwa lugha zao za kienyeji
 
Umetaja nchi 3 zenye waandishi mahili kati ya 52, hao wengine vp nao wana mazingira kama yetu?
 
Awamu ya kwanza si ndio ilikichinjia baharini kiingereza? Anyways kiswahili kimesaidia kuliunganisha taifa japo critiques wanasema hatukupaswa kukifuta kiingereza kama lugha ya kufundishia kuanzia elimu ya awali/msingi, maana kiswahili tayari kilikua kinazungumzwa na zaidi ya asilimia 95 ya wa Tz,; kwa hiyo ilikua ni makosa kuondoa msingi wa kiingereza kwa watu wetu
Waandishi kwa maana ya waandishi tunao wengi na mahiri kuanzia riwaya hadi ushairi kwa fasihi ya kiswahili, hao African Writers wanataka kiingereza tu ambayo ni lugha tu. Ndio maana hata kwa Nigeria nchi yenye population kubwa lakini waandishi tuwajuao ni wachache tu, hii ni kwa sababu wapo wengine wengi wazuri hatuwajui sababu wameandika kwa lugha zao za kienyeji
Aksante kwa hoja yako nzuri, lakini mimi nimemgusia Mwl, tu kwa sababu yeye mwenyewe ameandika vitabu!! wengine hawa si wapenzi wa vitabu, Other wise ni vile ulivyosema.
 
1: Nigeria kulikuwa na Wole Soyinka, Chinua Achebe.
2: Kenya kulikuwa na mtu kama Ngugi wa Thiongo.
3: Uganda kulikuwa na Okot P'Bitek.

Wote hawa waliitwa African writers na vitabu vyao vilisomwa kwenye "english literature" katika nchi nyingi.

Ukiangalia list yote ya "African writers" huoni na kujivunia mtanzania hata mmoja. Tujiulize kwa sababu za ukweli, kwa nini Tanzania hatukupata wala mmoja kwenye hao "African writers"?
Usiite "English Literature" bali Literature in English.
 
Shukran ... Nilitaka nimpe jibu hili. Watanzania tunajishusha mno, mpaka tunatia huruma.
Bado thread hii itaendelea kwa comments za kujiponda na kujibeza, na wanetu watakua hivyohivyo watu wa kujibeza.
Nashukuru mimi sijakuzwa hivyo.
jawabu ni moja tu watanzania htusomi hata virabu vyetu wenyewe ,sasa mtu anakurupuka kusema hakuna waandishi wakati vitabu vipo kwa kuwa tu kwa sababu zisizojulikana alisomeshwa akina okomkwo na ikemefuna basfi ndio hatuna waandishi?
Mlaumu nyerere.
 
Pia yumo Ishmael MBISE. Huyu kwa sasa ni Profesa wa Literature, Chuo Kikuu Tumaini Makumira. Aliandika: Blood on Our Land. Waandishi wa Kazi za Fasihi wako WENGI tu. Pamoja na Shaaban Robert, wapo pia: Kezilahabi, Semzaba, Aldni Mutembei, Mulokozi, Angoro Anduru, Kaigarula, Penina Muhando-Mlama, Ebrahim Hussein, Richard Mabala, Profesa Mbogo, Julius Nyerere, Gabriel Ruhumbika, Amandina Lihamba, Balisidya, Ndulute, nk. Wengi wa hawa waliandika kazi zao za Fasihi kwa lugha ya Kiswahili.
Ieleweke pia kuwa Africa Writers' Series, ni kampuni la uchapishaji wa kazi za Fasihi za Kiafrika (zilizoandikwa na Waafrika) kuhusu Afrika. Lugha ya uchapishaji ni Kiingereza. Kwa maana hii, kukosa kuchapisha kazi ya Fasihi katika AWS, haimaanishi Watanzania Hawajabobea katika kazi za Fasihi. Kwa waliosoma Fasihi shule za sekondari na vyuo, wamesoma kazi nyingi tu za fasihi zilizotayarishwa na Watanzania.
ahsante mkuu maana nilijihisi mleta uzi anatutukana watanzania kuwa hatuvijaui vitabu vya watunzi wetu! bora unedhihirisha yeye na wapuuzi wenzake tu ndio hawana akili ya kusoma vitabu vyetu
 
Subiost: 23965581 said:
Mnavyopenda kusifiwa si ndiyo tungeongoza kuisoma O-level!!!

Kubalini ukweli watanzania kuwa si kwamba watu hawakujua kutunga bali tulikalia kuimba fikra za kiumbe mwenzetu.

Mimi ningeletewa vya watazania wakati ule ningevisoma.
Tatizo lako umeanzisha thread ukiwa na biases na conclusion zako tayari.Naona hueleweki unalaumu tu mara African Writers Series mara hakuna Mtanzania aliyeandika Literature in English...Penda kujifunza vitu vipya na kama hujui kitu ni vizuri kuuliza kwa wabobezi na wataalamu kama sisi.."learning is a continuous process and we keep on learning each day"
Kwa taarifa yako novel ya "A WREATH FOR FR MAYER OF MASASI" imeandikwa na Mtanzania mwenzetu Severin Ndunguru imeithinishwa na Wizara ya Elimu kutumika kufundishia Literature O level
Vilevile novel ya "THE CHOICE" Iliyoandikwa na Mtanzania Juma Mwamgwirani nayo iliithinishwa na EMAC (Education Materials Approval Committee ) kutumika O level.
 
1: Nigeria kulikuwa na Wole Soyinka, Chinua Achebe.
2: Kenya kulikuwa na mtu kama Ngugi wa Thiongo.
3: Uganda kulikuwa na Okot P'Bitek.

Wote hawa waliitwa African writers na vitabu vyao vilisomwa kwenye "english literature" katika nchi nyingi.

Ukiangalia list yote ya "African writers" huoni na kujivunia mtanzania hata mmoja. Tujiulize kwa sababu za ukweli, kwa nini Tanzania hatukupata wala mmoja kwenye hao "African writers"?

African English writers - sisi tuliamua kujenga lugha ya kiswahili.
 
Umetaja nchi 3 zenye waandishi mahili kati ya 52, hao wengine vp nao wana mazingira kama yetu?

Swali ala ajabu kweli. hivi unapotaja kwamba nchi yako haichukui kombe la dunia unaikimbiza akili yako kujilinganisha na vilaza wengi ambao hawajawahi kulichukua?

Nimeanzisha thread kujadili ili liwe somo kwa vizazi vijavyo visizubae na kujipendekeza kwa kuimba fikra za mtu anayekaa sehemu fulani wakati dunia inakimbia.

Kubali tatizo rekebisha tatizo. Ubishi utakufanya ugeuke jiwe japo wabishi wengi hubisha eti ili wasigeuke jiwe. Ujinga.

Na inawezekana huko kwingine kuna matatizo kama kwetu yaani kujipendekeza kwa wakubwa badala ya kuwa na fikra za ubunifu bila kujali zitawaudhi viongozi.
 
Tatizo lako umeanzisha thread ukiwa na biases na conclusion zako tayari.Naona hueleweki unalaumu tu mara African Writers Series mara hakuna Mtanzania aliyeandika Literature in English...Penda kujifunza vitu vipya na kama hujui kitu ni vizuri kuuliza kwa wabobezi na wataalamu kama sisi.."learning is a continuous process and we keep on learning each day"
Kwa taarifa yako novel ya "A WREATH FOR FR MAYER OF MASASI" imeandikwa na Mtanzania mwenzetu Severin Ndunguru imeithinishwa na Wizara ya Elimu kutumika kufundishia Literature O level
Vilevile novel ya "THE CHOICE" Iliyoandikwa na Mtanzania Juma Mwamgwirani nayo iliithinishwa na EMAC (Education Materials Approval Committee ) kutumika O level.

Mkuu,

Sijaanzisha thread kwa bias. hata kwenye fani zingine kama muziki hali ilikuwa ni hivyohivyo. Nikianzisha thread kwamba akina Manu Dibango, Tabu Ley, Rwambo, Sam Mangwana walikuwa wanatamba Africa na Tanzania hatukuonekana utakuja na majibu ya kitoto kwamba wapo akina Diamond. Ridiculous!
 
jawabu ni moja tu watanzania htusomi hata virabu vyetu wenyewe ,sasa mtu anakurupuka kusema hakuna waandishi wakati vitabu vipo kwa kuwa tu kwa sababu zisizojulikana alisomeshwa akina okomkwo na ikemefuna basfi ndio hatuna waandishi?

Vitabu ni biashara ya dunia nzima. Katika mambo ambayo huwezi kumlazimisha binadamu ni kumlazimisha asome kitabu unachokitaka wewe. Hivyo kama Tanzania ilikuwa ina mkakati tusome vitabu vyake tu basi imenoa kwa hilo na haya ndiyo matokeo yake.

Vitabu ni biashara ya dunia na vinatoka kila nchi. Kama vya wezako vilifikia kuitwa
 
Hatuko makini kabisa wabongo, nimesoma juzi uzi mmoja kuhusu KESI YA AY NA MWANA FA kuwa majina yao yalikosewa mpaka mahakamani.....
 
Pia yumo Ishmael MBISE. Huyu kwa sasa ni Profesa wa Literature, Chuo Kikuu Tumaini Makumira. Aliandika: Blood on Our Land. Waandishi wa Kazi za Fasihi wako WENGI tu. Pamoja na Shaaban Robert, wapo pia: Kezilahabi, Semzaba, Aldni Mutembei, Mulokozi, Angoro Anduru, Kaigarula, Penina Muhando-Mlama, Ebrahim Hussein, Richard Mabala, Profesa Mbogo, Julius Nyerere, Gabriel Ruhumbika, Amandina Lihamba, Balisidya, Ndulute, nk. Wengi wa hawa waliandika kazi zao za Fasihi kwa lugha ya Kiswahili.
Ieleweke pia kuwa Africa Writers' Series, ni kampuni la uchapishaji wa kazi za Fasihi za Kiafrika (zilizoandikwa na Waafrika) kuhusu Afrika. Lugha ya uchapishaji ni Kiingereza. Kwa maana hii, kukosa kuchapisha kazi ya Fasihi katika AWS, haimaanishi Watanzania Hawajabobea katika kazi za Fasihi. Kwa waliosoma Fasihi shule za sekondari na vyuo, wamesoma kazi nyingi tu za fasihi zilizotayarishwa na Watanzania.
Emmanuel mbogo ni hatr sana kiufup wangon fasih wanaijui ata yule
wapo watanzania wengi mf. bernad mapalala,novel yake inatumika mashuleni

View attachment 610234
Emanuel mbog ni hatar san wangon wana vision kubwa ya fasih at ndungur
 
Msingi wa lugha ya kiingeleza hatukuwa nao.

Ukiziangalia hizo nchi zote ulizozitaja utaona kuwa zilitawaliwa na Mwingeleza.

Siye kijerumani kabla yakuota mizizi akaja mwingereza.
Naye toka 1920s akatupa Uhuru 1961.

Wakati huko Kenya na Uingeleza mkoloni alikaa tangu 1880s mpaka 1960s.

Msingi wetu ulikuwa hafifu.

Naye Nyerere akaupiga pigo la mwisho kwa kukifanya Kiswahili lugha rasmi ya taifa huku akikipa kiingereza nafasi ya pili.
Kwa hiyo unaona nyerere alikuwa mpumbavu kwa kufanya kiswahili kuwa lugha ya kwanza na kingereza ya pili🙄🙄?!
 
Back
Top Bottom