Kwanini Tanzania haikupata waandishi vitabu maarufu yaani "African Writers"?

Kwanini Tanzania haikupata waandishi vitabu maarufu yaani "African Writers"?

Nigeria bila kumtaja Chinua Achebe umewapunja sana hata kama umemtaja Soyinka
 
Kama ungefanya ka research kidogo ungekutana na vitabu kama Kisima cha Giningi, Kuli, Adili na Nduguze, waandishi na watunzi nguli, Kiu, Kwaheri Ukoloni, kwaheri uhuru, nk ama ungekutana manguli kama SHAABAN Robert, E. Kezirahabi, PENINA Mlama, Mohammed Shafi, Julius Nyerere, Mzee Said Abdullah, nk..

Vitabu vya kiswahili havina tija.
 
'Julius nyerere and all Tanzanians'...so where do you peg yourself! and what have you done to make the indifference??? You are so mouthful blindly pitting yourself against your inner self

Nimekugusa kwenye ukweli umeanza matusi. Vitabu vyako vya kiswahili peleka vikasomwe uswahilini.
 
Watanzania ni wajinga akiwemo mm ndo maana hakuna African Writer kutoka Tanzania.....

Wote wanakariri,
Tatizo watz hatueleweki utamaduni wetu. Ukiangalia kwa kuandikia lugha yetu inaonyesha ni kama tumekataa utumwa wa lugha, lakini kwa upande mwingine unaweza kusema lugha ya wenzetu hatuijui vizuri au pengine tunaandika mambo yanayoikumba jamii yetu tu, japo matatizo ya waafrika yanafanana.
 
Msingi wa lugha ya kiingeleza hatukuwa nao.

Ukiziangalia hizo nchi zote ulizozitaja utaona kuwa zilitawaliwa na Mwingeleza.

Siye kijerumani kabla yakuota mizizi akaja mwingereza.
Naye toka 1920s akatupa Uhuru 1961.

Wakati huko Kenya na Uingeleza mkoloni alikaa tangu 1880s mpaka 1960s.

Msingi wetu ulikuwa hafifu.

Naye Nyerere akaupiga pigo la mwisho kwa kukifanya Kiswahili lugha rasmi ya taifa huku akikipa kiingereza nafasi ya pili.
Well said.
 
Tuko wajinga kutokana na ujinga uliotengenezwa na CCM.

Ujinga wetu sio wa asili ni wa kutengenezwa mkuu, ila akitokea mwerevu mmoja kututoa ujinga anapigwa risasi.
Yes. [emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]Na hilo ccm hawalitaki.
 
1: Nigeria kulikuwa na Wole Soyinka, Chinua Achebe.
2: Kenya kulikuwa na mtu kama Ngugi wa Thiongo.
3: Uganda kulikuwa na Okot P'Bitek.

Wote hawa waliitwa African writers na vitabu vyao vilisomwa kwenye "english literature" katika nchi nyingi.

Ukiangalia list yote ya "African writers" huoni na kujivunia mtanzania hata mmoja. Tujiulize kwa sababu za ukweli, kwa nini Tanzania hatukupata wala mmoja kwenye hao "African writers"?
Henry ole Kulet wa Is it possible na Kitabu cha The wrath of God nadhani ni wabongo
 
Naona umemsahau Severin R.Ndunguru mwandishi wa vitabu vya fasihi kwa lugha ya kiingereza.
Ameandika vitabu hivi 1.A WREATH OF FR MAYER OF MASASI (kinatumika O level Literature)2.DIVINE PROVIDENCE 3.SPARED
Nadhani can be the best in Tanzania huyo jamaa kajitahidi sana japo inaonekana amekolea kwenye useminari!!! Personally I salute him!!!

Kama unamjua naomba historia yake fupi huyu ndugu Severin Ndunguru
 
Henry ole Kulet wa Is it possible na Kitabu cha The wrath of God nadhani ni wabongo

Inaelekea hii topic imewakuna. Watanzania sasa mmeenda kufukua vitabu mlivyovificha uvunguni kwa sababu havina mvuto.

Hivi watanzania mnavyopenda kusifiwa kwa tu-mambo tudogo-tudogo, hivyo vitabu vyenu kama vingekuwa popular si mngepiga kelele hadi dunia ikapofuka?


Havina mvuto viliishia kuwa kama hadithi za bibi.
 
Hivyo votabu vya AWS vingi vilikosoa mamlaka zilizokuwepo. Hapa kwetu huo ni uhaini.

Kwa hiyo Tanzania ilitaka tusome serikali za wenzake zilivyoadabishwa na waandishi na sisi baba zetu wasiandike au wakiandika walambe miguu serikali.
 
Naona wachangiaji wengi wanatumia lugha kama kigezo cha kututoa ktk AWS. Lakini nakumbuka kuna vitab vingi vimetafsiriwa. Hivyo vingeweza kutafsiriwa na kuingia ktk AWS
 
Kwa hiyo Tanzania ilitaka tusome serikali za wenzake zilivyoadabishwa na waandishi na sisi baba zetu wasiandike au wakiandika walambe miguu serikali.


Hahahaa

Kuna jamaa anitwa Mwijage alijaribu. Yaliyompata hatosahau kama bado yuko hai.

download (2).jpeg
 
Nimesoma vitabuvyake tu ila ukitaka kupata wasifu wake nadhani waweza kwenda Mkuki na Nyota Publishing House hawa jamaa ndio wachapishaji wakuu wa vitabu vyake
Nadhani can be the best in Tanzania huyo jamaa kajitahidi sana japo inaonekana amekolea kwenye useminari!!! Personally I salute him!!!

Kama unamjua naomba historia yake fupi huyu ndugu Severin Ndunguru
 
Hakuna mwenye shida navyo ndiyo maana hata kwenye "Africa writers" havimo, yaani hata waafrika hawana habari navyo na hawavihitaji.


Ebrahim Hussein kupitia tamthiliya yake ya KINJEKITILE(imeandikwa kwa Kiingereza) yumo kwenye orodha ya AFRICAN WRITES SERIES
 
Nimesoma vitabuvyake tu ila ukitaka kupata wasifu wake nadhani waweza kwenda Mkuki na Nyota Publishing House hawa jamaa ndio wachapishaji wakuu wa vitabu vyake
OK pia nimepata habari kuwa 2014 alishatangulia mbele ya haki!!!
 
Naona wachangiaji wengi wanatumia lugha kama kigezo cha kututoa ktk AWS. Lakini nakumbuka kuna vitab vingi vimetafsiriwa. Hivyo vingeweza kutafsiriwa na kuingia ktk AWS

Too late. Tuliishia kuimba "Zidumu fikra za mtu".
 
Ebrahim Hussein kupitia tamthiliya yake ya KINJEKITILE(imeandikwa kwa Kiingereza) yumo kwenye orodha ya AFRICAN WRITES SERIES
Mnavyopenda kusifiwa si ndiyo tungeongoza kuisoma O-level!!!

Kubalini ukweli watanzania kuwa si kwamba watu hawakujua kutunga bali tulikalia kuimba fikra za kiumbe mwenzetu.

Mimi ningeletewa vya watazania wakati ule ningevisoma.
 
Back
Top Bottom