Kwanini tukienda hospitali zile fomu za NHIF hawafungi hesabu pale chini?

Kwanini tukienda hospitali zile fomu za NHIF hawafungi hesabu pale chini?

Bora hata hao wasiofunga hesabu lakini wameandika kiasi. Kuna hospitali ya meno nilienda Magomeni wao hawajaandika chochote zaidi ya kutaka nisaini tu.

Nilipokataa akaja daktari mkuu (mwenye hospitali) akajifanya kumuwakia aliyekuwa reception lakini wazi inaonekana ndio mchezo wao.

Kuna TMJ polyclinic iliyopo chang'ombe, wao wana kawaida ya kutuma msg baada ya siku 2 ya kwenda hospitali kuonyesha matibabu yako yaligharimu kiasi gani. Nilikwenda nikacheki malaria tu na kuonekana sina na sikupewa hata paracetamol, baada ya siku 2 msg imekuja matibabu yaligharimu 170,000.

NHIF ni wapigaji lakini wamiliki wa hospital wapigaji zaidi.
Mkuu kwanini usingewasiliana na mamlaka husika na kuuliza?
 
Kibima chenyewe watu huwa waakipokea kwa Basi tu.

Yaani mtu na kibima chako Cha NHIF unaona Kama unaibiwa kinoma [emoji1787][emoji1787]

Aisee

Mngekuwa mnajua hata huko hospital kwenyewe hao NHIF hawataki mwende ili wasilipe chochote.

Ningekuwa Mimi Daktari ukileta ubush lawyers nakuandikia Paracetamol tu, Dawa nyingine zote UTALIPIA hakuna Cha NHIF na hakuna kitu utafanya
Tatizo hujakua
 
Hospitali ya Moyo Muhimbili kila kitu kwa kompyuta daktari akiandika dawa au vipimo gharama zinajazwa kidigitali unaziona uki siqn kuchukua dawa .
Nadhani mfumo huu ungehusisha vituo vyote vya huduma
Waweke iwe sheria kwamba NHIF watakubali karatasi ambayo mgonjwa kasaigin na kuthibitisha matibabu
 
Waweke iwe sheria kwamba NHIF watakubali karatasi ambayo mgonjwa kasaigin na kuthibitisha matibabu
Form yoyote ikienda NHIF bila signature ya mgonjwa inakatwa yote hailipwi, hata kama Ina madai ya mamilioni
 
Nchi yetu ni Corrupt by far, kila sehemu kuna wizi wa aina yake. So as long as bima sio vocha kwamba ukitumia kiasi flani hupati tena huduma mie sina mpango nayo wao wapige tu. Hilo haliniuhusu alimradi matibabu nishapewa
 
Bora hata huko mnapewa hizo form huku niliko nahudumiwa mwisho nikitaka card naambiwa ni sign kwenye ki mashine hata huwezi jua gharama zilizotumika maana hatuzioni kabisa form zaidi tunapewa vi paper vya number
Ukisaini kwenye mashine siku wakituma madai NHIF unapata sms
 
Yanayofanyikaga kwenye hizo form vituo vyenyewe vinafaham, NHIF wao wenyewe wanafahamu cause wanakutana na case nyingi sana, hata wizara nayo inafahamu....

Nahisi wanasubiri video Moja ivuje, Wananchi walalamike sana mitandaoni. Then ndo waje kusema tunaunda kamati ya uchunguzi, kisha wachukue hatua na kutangaza utaratibu Mpya!

Nipo pale nimekaa.....
Nasubiri hili lije kutokea
 
hili la bima ya afya hasa hii NHIF niliwahi kufanya chunguzi zangu za kiakili nikaona ni win win situation kati ya mahospitali na wahusika, ila mzigo kamili unakuja kwa serikali.
ukienda hospitali za serikali haina shida sana kwenye huu upotevu labda wawe wanaiba ngazi za juu huko. ila hizi za private hadi madoctor wanaelewa wajibu wao wa kuingizia pesa hospital yao kupitia huu mfuko.

kwa mfano umeenda kutibiwa meno, ukiulizwa tu kama unavidonda vya tumbo haijalishi jibu gani umetoa kule kwenye form ishaandikwa kipimo tayari.

unaweza ukawa unafanyiwa minor surgery leo wakakuexamine tu na maandalizi madogo then utaambiwa uje wik ijayo kuziba. wakati huo wameshakuandikia gharama za kumuona doctor na wanakuandikia gharama ya surgery hata kama hujafanyiwa, na ukija wik ijayo unaandikiwa tena.

unaweza ukapewa madawa hata kama hujaenda kwaajili ya ugonjwa huo. utaulizwa kama una gas tumboni, ukijibu umeenda na maji. kama una tatizo la mifupa ukijibu umeenda.
 
Kweli Kabisa Inapendeza zaidi wakikupa hesabu zako palepalee unajua gharama ulizotumia
 
Ni kweli kabisa. Hili tatizo lipo. Kabla ya kusaini inabidi mstari wa kufunga uwekwe halafu nisaini. Kama NHIF mnashirikiana katika Hili, naomba Serikali iingilie kati si kubaki mnalalamika tu kwamba matumizi yamekuwa mkubwa wakati mnaacha mianya ya wizi ikiendelea.

Nssf zamani walikuwa wanafunga, baadaye wakaacha. Kama wanachama tunaomba Hili litazamwe upya.
Tokeni kwenye Kazi za makaratasi hamieni kwenye Technology.

Tengenezeni mifumo hospital na vituo vya afya vyote viwe vinatumia hiyo mifumo. Mteja alipewa huduma anaetumiwa stakabadhi kwenye simu kama meseji muone kama kutakuwa na janja janja tena.

nhhshdhd

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu kwanini usingewasiliana na mamlaka husika na kuuliza?
Ilishawahi tokea zamani kidogo rafiki yangu alireport kwa kupiga simu yao ya toll free. Kilichotokea walimwabia awape jina lake na namba ya kadi watafuatilie. Na iliishia hapo hapo.

Hili tatizo limekwenda deep kuliko tunavyodhani. Ukiona mtu yupo comfortable kuibia Serikali elewa ana mtu wa Serikali anaemshika mkono.

Kinachotugharimu watanzania ni kuwa wavivu wa kufichua maovu na pengine uvivu huo unaletwa na kujua kwamba hakuna kitakachofanywa hata yakifichuliwa.
 
Ilishawahi tokea zamani kidogo rafiki yangu alireport kwa kupiga simu yao ya toll free. Kilichotokea walimwabia awape jina lake na namba ya kadi watafuatilie. Na iliishia hapo hapo.

Hili tatizo limekwenda deep kuliko tunavyodhani. Ukiona mtu yupo comfortable kuibia serikali elewa ana mtu wa serikali anaemshika mkono.

Kinachotugharimu watanzania ni kuwa wavivu wa kufichua maovu na pengine uvivu huo unaletwa na kujua kwamba hakuna kitakachofanywa hata yakifichuliwa.
Mkuu wewe andaa email tuma wizara ya afya cc takukuru na ikulu
 
Form yoyote ikienda nhif bila signature ya mgonjwa inakatwa yote hailipwi , ata kama Ina madai ya mamilioni
Kwamba NHIF lazima wapitie kila kadi kuangalia Signature?
 
Labda kama wakujazie ugonjwa tofauti ICD code zinatambulisha umetibiwa Nini , na government ya Tanzania imeweka SOP kila ugonjwa na dawa zake ukikiuka form nzima hailipwi

Kila kilimo lazima iweke code ulitaka kuangalia nini na mwisho unaweka code umetibiwa nini na matibabu dawa unazotakiwa kutoa zinajulikana ukienda kinyume wanakata form nzima
Kwani kila hospital si wanakuwa na care zao za kumuhudumia mgonjwa, mfano Serikali wakaweka hiyo unayosema wewe Sop kila ugonjwa na dawa zake sasa mfano hospital za private zina huduma zao mfano mrahisi kuna hospital moja nilienda kitu walichoniandikia dukani wanauza elfu 5, ila wao wakaniandikia elfu 40 je hayo malipo yakienda NHIF inamaana hawatalipa kwa sasababu ya SOP yao ama
 
kwani kila hospital si wanakuwa na care zao za kumuhudumia mgonjwa,mfano serikali wakaweka iyo unayosema wewe Sop kila ugonjwa na dawa zake sasa mfano hospital za private zina huduma zao mfano mrahisi kuna hospital moja nilienda kitu walichoniandikia dukani wanauza elfu 5,ila wao wakaniandikia elfu 40 je hayo malipo yakienda nhif inamaana hawatalipa kwa sasababu ya SOP yao ama
Hujaelewa ,
Ni kwamba kuna SOP government ya Tanzania imeweka kwa matibabu ya kila ugonjwa na kila level ya hospital na kila uwezo WA Daktari

-Kuna Daktari akiandika dawa za aina flani form nzima inakatwa
-Kuna level ya hospital ikitoa huduma flani form nzima inakatwa
-umetibu ila hujafuata utaratibu wa wizara wa matibabu form nzima inakatwa

Na nhif Wana price kwa kila dawa na medical consumables price zao wao nhif na sio za kituo
 
Bora hata hao wasiofunga hesabu lakini wameandika kiasi. Kuna hospitali ya meno nilienda Magomeni wao hawajaandika chochote zaidi ya kutaka nisaini tu.

Nilipokataa akaja daktari mkuu (mwenye hospitali) akajifanya kumuwakia aliyekuwa reception lakini wazi inaonekana ndio mchezo wao.

Kuna TMJ polyclinic iliyopo chang'ombe, wao wana kawaida ya kutuma msg baada ya siku 2 ya kwenda hospitali kuonyesha matibabu yako yaligharimu kiasi gani. Nilikwenda nikacheki malaria tu na kuonekana sina na sikupewa hata paracetamol, baada ya siku 2 msg imekuja matibabu yaligharimu 170,000.

NHIF ni wapigaji lakini wamiliki wa hospital wapigaji zaidi.
Nimewahi kumpeleka Mtoto kumwona Dokta wa kawaida kabisa, ila ilikuwa ni ishu ya Ngozi, akaandikiwa vidawa viwili vya kupaka, DLDM vinauzwaga 3000.

Baada ya muda natumiwa sms kuwa yale matibabu yaligharimu Tsh. 90,000.
 
Back
Top Bottom