katiba hizungumzi mambo ya awamu inazungumzia kipindi kilichobaki na kuonesha kua anayechukua mikoba ni Rais anayejitegemea ndio maana Samia ataruhusiwa kugombea kipindi kimoja tu kama atataka kufanya hivyo.Uko sahihi.
Na katiba iko wazi kwamba makamu wa Rais ataapishwa kuwa rais ili kumalizia kipindi kilichobakia kwa awamu ile.
Ukweli tupo awamu ya tano,sio ya sita,hatujafanya uchaguzi,ila yeye ni rais wa sita ktk awamu ya tano,
ni bora uombe kuelekezwa awamu hazitokani na chama kilichopo au serikali bali tunatumia awamu kuangali Rais aliyeko madarakani ni wangapi.Tungeangalia vipindi basi pengine tungelikuwa awamu hata ya kumi maana mwinyi mkapa na kikwete wametumia miaka 30 jumlisha ya JPM ni 35 ukigawanya na 27 ya baba wa taifa.Ni bora uombe kuelemishwa kuliko kuleta hoja dhaifu.Samia ni Rais Kamili kwa mujibu wa sheria na katiba.
Awamu moja maana yake ni rais mmoja.Awamu nane za marais Zanzibar
Jina Muda wa Utawala Chama Sheikh Abeid Amani Karume 12 Januari 1964 7 Aprili 1972 ASP Skeikh Mwinyi Aboud Jumbe 11 Aprili 1972 30 Januari 1984 ASP, 1977 CCM Ali Hassan Mwinyi 30 Januari 1984 24 Oktoba 1985 CCM Idris Abdul Wakil 24 Oktoba 1985 25 Oktoba 1990 CCM Salmin Amour 25 Oktoba 1990 8 Novemba 2000 CCM Amani Abeid Karume 8 Novemba 2000 2010 CCM Ali Mohamed Shein 3 Novemba 2010 2020 CCM Hussein Ali Mwinyi 3 Novemba 2020
Kama ulikuwa na majibu yako hukupaswa kuuliza humu, maana kila anae kujibu unamkejeli
Kila Rais ni awamu moja. Tuna marais sita waliokwisha ongoza nchi ndani ya mihula mitano.Hatulazimishwi ila kwenye kile kiti tangu tupate uhuru ni mtu wa 6 kukikalia kama amiri jeshi mkuu
1-Nyerere
2-Mwinyi
3-Bro Ben
4-Jeikei
5-Jeipiemu
6-Sa100
Nina F ya Hesabu ila Hesabu hii naimudu bila shida
Awamu moja maana yake ni rais mmoja.
Wakiwa kumi Hizo ni Awamu kumi.
Hii ni Awamu ya sita ya muhula wa tano wa urais.
So awamu ina miaka mingapi?So akitokea akafariki..ghafla..Mpango atakuwa Rais wa Saba katika awamu ya Saba sio!?
Ujinga mtupu ..Yani majitu nmnakomaa kwa kitu ambacho kipo wazi ..awamu Gani inakuwa na miaka minne..ama Tisa!?
ajamu ina msaada gani ktk maendeleo ya jamii?hicho ni kipindi tu sawa na jina tunachoitaji ni Haki,na maendeleo si awamu
kwa hiyo lengo lako lilikua kumkosoa RAIS au kujua kwa nini anasema tupo awamu ya sita?
nadhani mawazo yako ni too "GENERAL"Another Zany.
Wewe tunajua tatizo lako lilipo endelea kupambana na hali.Angalia ulivyo Juha ( Fool ) hivi siyo Wewe ambaye katika posts zako za Awali katika Uzi huu huu ulikuwa Unabisha na Ukweli tuliokupa?
Sasa inakuwaje sasa hivi unaanza Kulainika na Kubadilika Kinafiki hivi? Tafadhali endelea Kuuamini tu ule Upumbavu wako sawa?
Nasisitiza Kwako tena kuwa Mama Samia Suluhu Hassan ni Rais wa Sita katika Awamu ya Tano iliyo katika Muhula wake wa mwisho ( wa pili )
Nimemaliza.
Kwa hiyo katiba ingekuwa inataka rais akifa ufanyike uchaguzi mwingine je samia angekuwa ni rais wa awamu ya ngapi?Swali ambalo anatakiwa kujiuliza ni kuwa iwapo jpm angekuwa amesafiri au yuko kwenye matibabu ya muda mrefu automatically anayeongoza nchi ni yeye, je angesimama kwenye jukwaa na kusema hii ni serikali ya awamu ya sita? Then jpm akirudi anasema ni serikali ya awamu ya 5. Awamu za serikali zinatokana na UCHAGUZI sasa hapa hakuna uchaguzi mwingine uliofanyika.
Wewe tunajua tatizo lako lilipo endelea kupambana na hali.
TUPO AWAMU YA SITA NA MAMA ATAPITISHWA NA CHAMA KUGOMBEA TENA 2025 KIPINDI CHA PILI CHA AWAMU YA SITA. MSIMAMO WA CHAMA UPO PALE PALE🤣, NGOJA APEWE UENYEKITI.
Kwa hiyo upo uwezekano wa samia kuwa rais kwa jumla ya miaka 14?Nikieleweka na Watu ( Members ) ambao ni Werevu ( Intelligent ) kama Wewe na Wenzako baadhi hapa huwa ninafurahi sana tu.
Nasikitika kuna baadhi ya Watu hapa wanajiita Wasomi lakini Jambo dogo tu hili wameshindwa Kulielewa na hata Kulichambua.
Kama Rais Samia ataendelea Kusema ( Kusisitiza ) Yeye ni Rais wa Awamu ya Sita nitaamini kuwa ana IQ Ndogo na nitamdharau pia.
Rais Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan ni Rais wa Sita katika Awamu ya Tano iliyo katika Muhula wake ( wa mwisho ) wa Pili.
Nimemaliza.
Kwa hiyo kuna uwezekano wa samia kuwa rais kwa Muda wa miaka 14 kama Mungu atamjalia pumzi?Unauliza maswali yako unajijibu mwenyewe, nimezungumzia ilani ya 2020 ambayo ndio Samia anaimalizia toka kwa mwenzake sio ya 2015, na zaidi Katiba inasema Rais atakapofariki makamu wake atamalizia kipindi kilichobaki, sasa kama huyu anamalizia kipindi kilichobaki hiyo awamu mpya inatoka wapi? huyu anamalizia kipindi kilichobaki kwenye awamu ya mwenzie.