Kwanini unapaswa kununua bond au Hati fungani ya NMB?

Aisee hii ngumu kumeza....kwahyo kila mwez faida elfu 10!![emoji15] [emoji15]
ujinga huu,.alafu eti wanasema inanuifaisha watz
huu siulaghai,.nilikuwa na hamu sana ya kununua hati fungati,nlijua mwaka ukiisha nakimbizana na dangote au manji,...
kumbe ujingaujinga2
 
Eti 1M kwa miaka mitatu faida laki 3!!!?? Hyo faida muuza supu na chapati anaingiza kwa muda mfupi sio huo wa kwenu

Anyway.....mfumo wa uchumi ulivyo ni kwamba taasisi za kifedha kama benki huwa hazina urafiki na maskini (mwenye kipato kidogo) badala yake ni kumkamua alicho nacho kwa kutumia "lugha tamu inayovutia"
 
Imekaa poa sana, somo limeeleweka sanaa...
Ila tukija kwenye "time value of money" iyo Milion niliyoweka leo siku napewa itakua na dhamani sawa na Milion niliyo invest? maana hapo tayari nishakula "viinterest" vyangu.

pls Mkuu some help hapo
 

Mawazo kama hayo hapo juu ndio yanafanya maskini kuwa maskini na tajiri kuwa tajiri. Ni fikra. Kutotambua fursa ndio shida, inayofanya wengine wawe maskini na wengine matajiri.

Mtu anapewa fursa, lakini anachoweza kufanya ni kujiondoa na kufikiri hela inaongezeka kwa kuwa na hela nyingi. Wakati kila fursa ni nafasi ya kupata hela.

Yaani hata ukijenga nyumba, hutapata mrejesho wa faida kama kwenye hati fungani.

Watanzania wenye macho , hii ni fursa.
 
wamenikiosa.....niliikomalia sana hii deal nilijua inalipa
 
Kwa ndugu zangu wa mikoa mingine isio kuwa kipenzi wa banki hii na Nbc misishiriki kabisa kununua. Hata kuweka pesa hii benki ni wabaguzi kweli kwenye ajira tena ubaguzi ulokithiri. Hapa zaidi ni ni mkoa mmoja tu wa kaskazini. Wengini wa kuhesabu au wapo kwa address ya wakubwa.
Bank hizi ni nadra kuajiri waislam ...sana utawakuta wawili watatu watoto wa wakubwa au kitengo cha bank ya kiislam.
Hizi bank zilikua mali ya umma..hivyo kutoa ajira kwa misingi ya dini na kabila fulani haikubaliki....na tatasema ili waislam na wamakonde nao wapate kazi ...wacheni ubaguzi...
 
Naona Sera ya magufuli kuondoka hela za serikali kwenye mabenki imeanza saidia, sasa mabenki hayana hela za kukopesha lazima yakope kwa watu ili wakopeshe wengine!
Safi sana JPM,
 
Mmh bopwe sijakupata vrma
 
Naona Sera ya magufuli kuondoka hela za serikali kwenye mabenki imeanza saidia, sasa mabenki hayana hela za kukopesha lazima yakope kwa watu ili wakopeshe wengine!
Safi sana JPM,
Mmh sidhani kama hili liko kwa mtazamo huo
 
Naona Sera ya magufuli kuondoka hela za serikali kwenye mabenki imeanza saidia, sasa mabenki hayana hela za kukopesha lazima yakope kwa watu ili wakopeshe wengine!
Safi sana JPM,
Imesaidia nini sasa? Kama ni kweli hawana hela ya kukopesha si ndo wananchi watazidi kuumia au?
 
Hii inafaa wanaoweka pesa bank hawana cha kuzifanyia lakini si sisi waganga mjaaa...faida ni ndogo sana nikilinganisha nifanya biashara ya uchuuzi nitapata kubwa kuliko hiyo..

Hati fungani ya NMB ni kwa kila mmoja.
Hati fungani ya NMB inamlenga kila mmoja ambaye anataka kuwekeza na NMB ili kupata malipo ya kuridhisha. Hati fungani ya mauzo inawafaa wale ambao wanapenda malipo ya mara kwa mara au kipato endelevu au walio na upeo wa uwekezaji wa kati na wa muda mrefu. Ofa ya hati fungani ipo kwa ajili ya wale walio na wasio wateja wa NMB.
 
Tarehe 8 mwei huu wa June itakuwa siku ya mwisho kununua Bonds za NMB..
NMB ndio kampuni ya kwanza kuuza Bonds Tanzania kwa public...
Bonds tofauti na hisa huwa hazishuki thamani..ziko fixed
Nchi za wenzetu ni kawaida sana hapa ketu ndo baado tunaanza...

Ushauri wangu wale ambao mnaweza kununua bonds hizi mjitokeze kabla ya deadline
ili angalau zoezi hili liwe la mafanikio kampuni zingine zivutike kuuza bonds pia..

Kwa wale ambao hawajui tu ni kuwa NMB sasa ndo benki kuubwa kuliko zote Tanzania
kwa kila kitu.....(i stand to be corrected)

Kwa idadi ya wateja
ukubwa wa mtaji
thamani ya kampuni na kadhalika....

na sekta ya benki Tanzania bado changa sana...kwani watanzania wanaotumia banks
hawafiki mlioni 3 huku wenye uwezo wa kutumia bank wapo zaidi ya milioni 20

hii ina maana bank zitazidi tu kukua....na thamani ya hizi bank itazidi kuongezeka

mfano mzuri ni hisa tu za NMB....walionunua wakati zinaanza (IPO) leo thamani ya hisa zao
wengi ni mabilioni ya shilingi...na sasa watu kutoka Europe hadi USA wanakuja kununua hisa za NMB

Na hizi Bonds za NMB mwaka huu ndo mwanzo tu .....miaka michache ijayo usishangae zikavuta watu kutoka mbaali sana huku sisi wenyewe tukiwa hapa hapa...

Ningependa hii thread tueleweshane faida za bonds hizi.....na tuhamasishane......
 
Mi nitaweka 500,000 kwanza
Afu baada ya hapo tutaona itakuwaje
Tatizo la sisi Watanzania tunakujaga shitukia vitu muda ummeenda sana
Mfano kwenye hili la Bond mimi na 500,000 yangu siwezi faidi sana
Anaefaidi ni atae weka 1bil na kuendelea
 
Mi nitaweka 500,000 kwanza
Afu baada ya hapo tutaona itakuwaje


Mkuu bond ina tofauti na hisa
usiweke tu kutazama itakuaje
weka na uliza kabisa bond ikiiva utalipwa ngapi
na utalipwa tu....hakuna kupanda wala kushuka kwa thamani
weka hata milioni 500 kama una uwezo
kabla ya kuweka wanakupigia hesabu utalipwa ngapi ikiiva....unajua kabisa
 

Asante kwa ushauri
Kwa awamu hii mi nawashauri wanaojenga magorofa kariakoo bora wakanunue hizo bond wana uhakika wa kupata hela nyingi kwa mwaka kuliko kodi wanyoingiza kwa mwaka
 
Hivi walisema ukiweka unapata faida ya asilimia ngapi vile?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…