Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Chawene ashikilie hapo aweke pin kabisa pakilegea tu watoto wa mkulima tumeisha haiwezekani upate g.p.a ya kuhonga na kazi nayo ya kuhonga wapite PSRS wakapate fair competition.
Kwanza ilitakiwa wote warudi PSRS hata hao TRA warudishe usaili PSRS hakuna chochote cha maana kama ni spidi mbona nao bado, mpaka sasa ni miezi 3 toka tangazo la ajira hapo mpaka nao kwenda kuita watu kazini inaweza tena ikachukua miezi 3 , warudishwe tu PSRS wasitafute chaka la kupitisha ndugu na watoto wao na wa wakubwa wao.
 
Unajua nadhani humu wengi ni graduate na ndio maana mnamzuka sana na psrs.

Kwa mfano kada yangu mimi niliyosoma utumishi lazima waajiri kila mwaka watu zaidi ya mia.

Lakini mwaka 2021 nilijiunga na ajira portal mwanzoni mwa mwaka ila sikuona post hadi mwaka 2022 .

Na nilipokuwa na pitia mkeka ya zamani kuna muda pdf zilikuwa hata mwezi hazitoki sasa ninashangaa vijana mnavyopaniki nakutaka utumishi akuwekee mkeka kila siku kitu ambacho hakiwezekani.

Utumishi ukiingia kwenye oral kinachobaki ni subra na uvumilivu.
 
Utumishi haiwezi kupokonywa kufanya mchakato wa ajira kwa taasisi za umma ila taasisi za umma ndo zinazoongoza kumkwamisha psrs.

Ila rungu alishapewa kwa mujibu wa sheria na ukapitishwa na bunge so sheria inabidi iondolewe na bunge.

Suala lingine

Utumishi niseme nao hawataki kuendana na speed za taasisi.

Ilitakiwa kuanzia kutangaza ajira ,interview na placement zingechukua mwezi mmoja au miwili.

Kuliko miezi miwili hadi sita kama ilivyosasa.
 
Hivi replacement ndo nini??
 
Ni kweli kabisa, sijaona mabadiliko yoyote zaidi ya kuweka njia ya watu wao.
 
Dah hatari sana jamaa inaonekana wanawanyooshea sana hakuna ch3nga chenga alf taasisi zinapelekewa watumishi wasio wataka hii nchi ngumu snaa kuna watu wanaona kama yao vile
Hii ipo mzee, kuna taasisi tumelamba asali lakini unaona wazi kabisa hawakufurahishwa sio tuliokuwa nje ya mfumo wao kutoboa ilhali kuna raia wamejitolea kwa muda mrefu wamedunda, lakini ndio hivyo tena Mungu ni mwema alitupigania na tukapenya

Na hii ilinipa funzo moja, hizi taasisi au mamlaka zenyewe zingeendesha usaili hakuna hata mmoja ambae angetoboa

Na hii ni funzo kwetu, hii PSRS pamoja na vipengele vyake ila imekuwa msaada mkubwa kwa ambao hatukuwa na connection kabisa, tuiombee iendelee kuwepo

Hili suala likirudi kwenye taasisi husika, aisee watakaotoboa ni wachache sana, kuna ubinafsi mkubwa sana na kujuana

NB: Taasisi niliyotoboa (nilipost huko nyuma kwenye uzi huu shukrani zangu nisingependa kurudia) niliomba field miaka miwili nikakosa, baada ya kuhitimu nikaomba intern mara 2 niliambatanisha kila kitu mavyeti yote ila hata ujumbe wa kuitwa tu kwenye usaili sikuitwa😂😂💔

Hatimae, Utumishi wakatangaza nafasi nikajilipua. . .nilimtanguliza Mungu mbele sikuwa na uzoefu kivileee ila nikapiga moyo konde, nikapenya Written, baada ya Oral nikasubiri sana (miezi 7 kitaa, hapa katikati nilipiga interview nyingi tu ila sikupenya. . .) mpaka nikahisi ndio basi tena, ila baadae mkeka ukatoka na jina langu tena la kwanza!🙏🏿

So kuwa mvumilivu ipo siku utatoboa na usikate tamaa, apply tu ukiitwa Dodoma nenda, ukikosa nauli piga moyo konde, subiria inayofuata ila usisite kujaribu wala usione hatari kutumia hela yako kwenye usaili.
 
Kwenye Jopo la Oral interview psrs, anakuwepo member mmoja kutoka taasisi husika. Kwahiyo madai yao kuwa wanapelekewa watumishi wasio na vigezo ni uongo. Figisu tu
Vip wale wanaoenda fanya interview Kisha hajapangiwa alipoomba wakapata placement na wanapangiwa kutoka data base unataka sema kuna wawakilishi wa taasisi kwenye jopo la oral pia

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Vip wale wanaoenda fanya interview Kisha hajapangiwa alipoomba wakapata placement na wanapangiwa kutoka data base unataka sema kuna wawakilishi wa taasisi kwenye jopo la oral pia

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Database inaonesha alama zako zote ulizopata kuanzia oral mpaka written, pia kumbuka CV yako ipo pale na yale maswali uliyokuwa unajibu yalielezea vitu kuhusu wewe na ndio maana hata kwenye kupangiwa sio wote ambao wanatoboa kwenye database, ikiwa perfomance yako ilikuwa chini sana kwenye oral + written unaweza usitoboe kwenye mkeka wowote, na akapangiwa mwengine ambae alikuwa na ufaulu wa juu kuliko wewe katika nafasi kama yako hata kama alifanya kwenye usaili mwingine
 
Vip wale wanaoenda fanya interview Kisha hajapangiwa alipoomba wakapata placement na wanapangiwa kutoka data base unataka sema kuna wawakilishi wa taasisi kwenye jopo la oral pia

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
📌 sometimes unakuta wamepata placement tokea database mahali pazuuuuri kuliko walipoomba na kufanyia interview wakaachwa
 
Ukiona hujapangiwa hapo jua vigezo kuna wenzako walikuzidi. Lakini pia haya ni mapungufu madogo yanayoweza kurekebishwa na sio kuondoa kabisa mamlaka ya kuajiri
Vip wale wanaoenda fanya interview Kisha hajapangiwa alipoomba wakapata placement na wanapangiwa kutoka data base unataka sema kuna wawakilishi wa taasisi kwenye jopo la oral pia

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…