Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

wakuu lazima tutoe mrejesho hapa
hatimaye nimeangukia halmashauri leo

Nawashukuru ndugu zangu
nawashukuru psrs
Hongera sana jamaa, nilipelekwa huko pia, sema daah, nilienda ripoti hiyo mitaa, nilifika hoi na ni kijijini huko ndanindani, mwenyeji ananiambia hapa ndiyo senta na maeneo rasmi utakayofanyia kazi ni km 40 toka hapa, nikalengwa na huzuni kali.

Nikajisemea moyoni hivi hii placement yangu wamekosea nini??? Hahahaha halmashauri aka LGA, nimechoka, nilisepa na kurudi mkoani kwangu, wewe head wa dept. Hauwezi niforce nireport kituoni na nianze kazi wakati hela ya kujikimu na mshahara bado, na majibu simpo eti utapata wadau huko, nikasema head wa depts. Wengine ni waduanz...

Anyway tunashukuru kwa yote.
 
Daaah pole mkuu haya mambo bwana yamekaa zigzag kweli mimi nilipigwa chini LGA nimejikuta City centre kutokea database but all is well kikubwa kuanza kazi ramani zitajiseti.
 
Inahitaji moyo
 
Inahitaji moyo
Lakini mkuu kwa maisha yetu na background ya familia zetu wengine... hata upelekwe ndani ndani huko... unamrudishia Mungu sifa na utukufu..kwa sababu wengine tumesoma mpaka ndugu na jamaa wakae kikao kujadili wanapataje hela walau ww uende shule.... kwa hivo mtu kama huyo Mungu akimpa hata kama ni kidogo atashukuru mno
 

Umenena Mkuu, yatupasa kumshukuru Mungu yeye ndio mpangaji wa riziki zetu. Cha msingi tusivunjike moyo.!
 
Kwel mkuu kikubwa upo kwenye Ajira, jitihada zako, ufanisi wako na utendaji kazi wako ndo utakutoa kimaisha, popote nenda Napo uko kuna watu pia
 
Ni kweli mkuu cha muhimu malengo tu. Ukifika angalia fursa kama ni wilaya ya kilimo basi kopa benki ingia shambani. Walau uingize chochote cha kuboost salary
 
Hongera sana sana ,kada gani mkuu uliomba?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…