Zingatia ilichosema
Ngulumto lakini cha kuongezea jitahidi kuwa smart pia kimavazi na ukiingia chumba cha usahili usikimbilie kukaa kwenye kiti subiri wakukaribishe hivyo ni vitu vidogo lakini vinakuongezea ufaulu
1. Facial expression - Usitie huruma ili uonekana unataka kazi au uonekane upo desperate na ujobless
2.Body language - Jifunze kuweka vizuri mwili wako kimkao na usikae kama roboti bali uwe unapoelezea kitu unachezesha na mikono kama vile unawafundisha.
3. Tone of voice - Toa sauti kwa kujiamini maana sauti yako inaweza ikawapa majibu kuwa hujiamini au unajiami.
3. Volume - Hakikisha unapojibu maswali sauti yako inasikika na wote, wasikuulize ulize uongeze saiti
4. Eye contact - Jitahidi unapojibu maswali unamwangalia usoni yule aliyekuuliza.
5. Usijipulizie pafyumu kali na usiende ukinuka kikwapa.
6. Interview ikiisha nenda nyumbani moja kwa moja usipige stori na mtu yoyote
7. Vaa vizuri pendeza
8. Soma vizuri job duties uzielewe na pia fahamu changamoto zinazotokana na hiyo kada yako ukiwa kazini na namna ya kuzitafutia ufumbuzi.
9. Kama hawaja specify ujibu point ngapi kila swali utakaloulizwa jibu point tano tano.
10. Andaa maswali ya kuwauliza angalau ma3, kama wakikuuliza DO YOU HAVE ANY QUESTIONS ?
Muhimu: Nenda kanisani na umuombe sana MUNGU ikiwezekana hata funga kwa ajili ya hiyo siku.