Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Huyu mwambaa hakika anastahili, sijui kama atalala siku 3 hizi, lbda akishika barua ya ajira [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] watu tunafurah sana humu kwenye uzii coz umegusaaa maishaa ya wengi humu na wwngine usio wajua kwa mara nyingine tenaaaa hongeraaaa sanaaa kaka.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Hongera sana broo! Bimafsi

Hongera sana broo! Binafsi nafurahi kuona shuhuda hizi....
Ahsante sana mkuu, Mungu ni mwema sana
how do you feel now?
Hii furaha haina kipimo kabisa, ni ndoto ya kila mmoja wetu kufurahi humu, hakika haielezeki.

Wenzangu hawakulala kwa furaha naona na mimi naelekea kufuata nyayo zao[emoji3][emoji3]
 
Ahsante sana mkuu, Mungu ni mwema sana
Hii furaha haina kipimo kabisa, ni ndoto ya kila mmoja wetu kufurahi humu, hakika haielezeki.

Wenzangu hawakulala kwa furaha naona na mimi naelekea kufuata nyayo zao[emoji3][emoji3]
Unakila sababu ya kufurahi wakati wa mungu ndiyo wakati sahihi
 
Dah kaka acha tu nifunguke ki ukweli sikuji wala hunijui zaidi ya sisi sote kukutana kwa comment za Jf tu

Lakini ukweli ni kwamba sijawahi acha kukuombea kwa Mungu upate mafanikio katika vita hii tangu nilipo anza kuziona comment zako humu

Zimetupa nguvu wengi sana hasa mimi

Amini hapa nilipo ninafuraha sana kuona kua nawe upo kwenye kundi la walio chaguliwa kujiunga na utumishi

Nakuomba sana kaka usitukimbie humu Jf wala hili jukwaa uwepo wako ni muhimu kuliko unavyo fikiria. Ni mtu unaetoa hoja kwa evidence kiasi kwamba ilikuwa rahisi kueleweka katika majibu yako

Mara nyingi mimi humu ni msoma comment tu ila kila siku huwa lazima niingie nipate darasa huru lenye manufaa na faida.

Naomba kawe mtumishi mwema kama ulivyo onesha wema wako humu.

Mwisho. Nawatakia kheri nyote mlio fanikiwa hili na kazi njema huko muendako.
Ahsante sana mkuu kwa Dua.
Mungu ni mwema wakati wote.
Mapambano yaendelee, hamna kukata tamaa.

Mimi humu siondoki hata nikija kubanwa na shughuli za mrija, sitakosa muda wa kuja kuchungulia humu hata dk 10
 
Finally I made it!

Kutana na Mwifwa- From three times defeat to Champion

Hii ndio ilikuwa safari yangu ya kusaka mrija wa Asali.

Mwaka 2021, safari hii ilishika kasi kwa kuapply mara 8( Sekta binafsi, Wizarani na Tamisemi). Kote niliangukia pua, Sekta binafsi sikubahatika hata kuitwa kwa usahili.

Mwaka 2022, kasi ikaendelea kushika kasi nilipoapply Wizarani na Tamisemi kabla ya kutimkia PSRS, mara hii niliangukia pua pia Wizarani na Tamisemi.

PSRS nilifanya application 5, 4 nikawa shortlisted, moja sikuwa shortlist kwa sababu isiyokuwa ya msingi maana hiyo sababu wangeizingatia nisingekuwa shortlist zile zingine 4.

Kwenye shortlist 4, tatu nikakandwa mfululizo hadi nikakata tamaa, ila wadau wa humu wakanipa moyo na nikapata nguvu ya kwenda kupambana.

Baada ya kwenda kwenye battle nikaingia oral kimasihara. The rest is history, what a joyful in my life history, my eyes are filled with joyful tears.

Join me in celebrating this remarkable history!!
KATIKA SIKU AMBAZO NIMEKUWA NA FURAHA KUBWA NI KUONA KAKA YANGU Mwifwa UMETIMIZI KAZI ULIYOIANZA SALAMA NA KUFANIKIWA KUPATA NAFASI.

Nimejifunza mengi kupitia wewe na Nimeamini vingi kupitia wewe, ujitoaji wako, uthubutu, wema wako na ukarimu hakika haujakutupa.

Mungu aendelee kutusaidia na sisi tuingie kwenye mrija ili tuungane wote kwenye tabasamu murua la utumishi wa umma.

Ukitenda wema na kujitoa kwa watu, hakika Mungu anakutoa like bora zaidi. [emoji3590]🫂[emoji120].
 
Nasubiri ushuhuda wa status ya mwifwa kwenye web[emoji3]
Hahahaaa, nilikuwa nasubiri hiki kitu nimniulize.

Nilikuwa muumini wa kutoangalia status tangu nifanye oral na hadi sasa ninapoandika hapa, sijaangalia wala kufungua web ya PSRS maana PDF nimetuniwa na wa karibu yangu kupitia WhatsApp na vigelegele kuanza moja kwa moja.

Nahisi hata nikiangalia kwa sasa na kuwapa mrejesho, mrejesho utakuwa ni kile nitakachokiona kwa sasa na yale mabadiliko siyajui maana sikuangalianga tangu nifanye oral.
 
Kaka, ninafuraha kwa ajili yako. Hongera sana na tunakutakia kila la kheri kwenye Utumishi.
Mkuu sina cha kuwalipeni isipokuwa ni Muumba pekee atawalipa kwa wema mliokuwa nao tangu mwanzo.

Wewe na wizy ni miongoni mwa watu mlionikalisha chini na kunikanda kwa nasaha kuhusu huu mrija wa NAOT maana nilikuwa nimeukatia tamaa. Hakika mlifanya kazi kubwa pamoja na wengine.

Tuendelee kuombeana, kutiana moyo, matumaini hadi kila mmoja wetu aweze kutimiza ndoto zake za mrija wa Asali
 
NAOT sijapata, ni vile tu nlishaga kuwa standby kuwa siwezi kupata so I feel kawaida. Sio kwa maswahibu nlokutana nayo hope niliezea humu. I believe in God, ni mipango ake tu[emoji3][emoji3][emoji3][emoji23]. Sema am so happy for u sana[emoji1431]
Usijali sana Dada, nafasi yako ipo ina njia ya kuipata ndio huenda bado hujaimaliza, ukiimaliza utaipata.

Tuendelee kuombena na kupambana zaidi
 
Niilikuwa nimeshaanza pitiwa na usingizi nimeshtuka naingia nakuta shangwe za Mwafwa Daah usingizi umesha nimefurahi mno yani hongera sana ni kati ya wadau ambao hamtasahaulika katika uzi huu nakuombea mno kijana mungu akutangulie nasisi tupo njiani tunakuja kuchukuwa barua suti zinamalizikia kukauka,,,,nashindwa hata niandike nini ila nimefurahi mno
Ahsante sana mkuu, Mungu ni mwema sana.

Mapambano yaendelee
 
Back
Top Bottom