Kwanini vyombo vya habari bado vinaripoti kwa 'machale' taarifa za vyama vya siasa vya upinzani?

Kwanini vyombo vya habari bado vinaripoti kwa 'machale' taarifa za vyama vya siasa vya upinzani?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Ni wazi kuwa Rais wa awamu ya 6, Dkt Samia Suluhu Hassan, ameondoa zuio haramu za kufanyika shughuli za kisiasa za vyama vya upinzani na hivyo kurejesha ukuaji wa kidemokrasia Kwa vyama vya upinzan hapa nchini, ambao ulikuwa umeminywa Kwa kiasi kikubwa Kwa zaidi ya miaka 6 ya utawala wa awamu ya 5 ya Mwendazake.

Lakini jambo la ajabu ninaloliona ni Kwa vyombo vya habari nchini, kuendelea kutoa taarifa za vyama vya kisiasa vya upinzani Kwa "machale" makubwa.

Inafahamika pia kuwa vyombo vya habari ni Mhimili wa 4 wa Dola, usio rasmi.

Tunajua pia kuwa vyombo vya habari kama vile luninga ya TBC na gazeti la Habari Leo, ni vyombo vya umma, vinavyoendeshwa kwa kodi zetu wananchi wa vyama vyote vya siasa, iwe ni CCM au CHADEMA, kwa hiyo vinapaswa vilipiti Kwa usawa habari za vyama vya siasa, bila kufanya upendeleo.

Vinapaswa vyombo vya habari hapa nchini visiwe "biased" wakati wa kuripoti taarifa zao,ziwe za CCM au Chadema, viripoti sawa.

Lakini sivyo vinavyofanya hivi Sasa, kwani mfano TBC inaendeleza mapambio yake ya "kumsifu na kumwabudu" Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan.

Vinapaswa vyombo vya habari hapa nchini, viige mfano wa nchi jirani ya Kenya, namna vinavyoripoti taarifa ya vyama vya kisiasa nchini mwao bila upendeleo.

Tulijionea wakati wa uchaguzi Mkuu uliopita wa Kenya namna vyombo vya habari vya nchi hiyo vilivyokuwa huru, wakiripoti mubashara, shughuli za kisiasa, ziwe za chama tawala au vyama vya upinzani.

Utashangas hapa nchini kwetu, Kwa tukio dogo kabisa linalofanywa na Mwenyekiti wa CCM, Samia Suluhu Hassan inarushwa mubashara na luninga ya Taifa, wakati hotuba ya viongozi wa kitaifa wakihitubia, hawaonyeshi mubashara!

Kama kweli Taifa letu linataka kukuza Demokrasia nchini, basi vyombo vya habari nchini, vinapaswa vibadilike katika utendaji wake.

Kwani LAZIMA vifahamu kuwa enzi zile za kutishiwa kufungiwa, kama vilivyokuwa vikifanyiwa na utawala wa awamu ya 5, hadi kutishwa kuwa "you don't have that freedom to that extent" umeshapitwa na wakati.

Mungu ibariki Tanzania
 
Acha ujinga kijana, utatumiwa na wanasiasa uchwara hadi lini? Mbona mnaendekeza malalamiko yasiokuwa na msingi? Hata kama uchawa lkn muda mungine mpunguze kidogo mahaba yasiokuwa na tija kwa vyama vyenu na waajiri wenu wanaowatuma kuandika upuuzi mitandaoni.

Kama vyama vinakosa wahudhuriaji wa mikutano kama tulivyoona Mwanza na Musoma hilo sio tatizo la wanahabari bali ni tatizo la walamba asali kupoteza sifa kwa wananchi na wale wanaowaongoza katika vyama vyao.

Unafikiri ni mwananchi gani mwenye akili zake ataacha shughuli zake aje awasikilize wanasiasa uchwara? Watu wengi wamejifunza kupitia siasa za majitaka za enzi za kuwachafua kina Lowasa bila ushahidi na hadi ule mchakato wa 2015 katika uchaguzi mkuu. So sio rahisi kudanganyika tena.

Watanzania sio wasahaulifu kihivo.
 
Sasa uchawa wangu uko wapi hapo?

Hivi kuusema ukweli kuwa vyombo vya habari hapa nchini viko "biased" katika kuripoti habari za vyama vya kisiasa hapa nchini, ambapo ndiyo "reality" ndiyo huo unaouita uchawa?😎

Nyinyi wahafidhina wa CCM, acheni "kuchachawa" kwani mliigeuza hii nchi kuwa ni ya kwenu peke yenu, Kwa kutumia vyombo vya dola na kuwageuza viongozi wa vyama vya upinzani nchini kuwa "wahaini" ndani ya nchi yao!
 
Habari zipi ambazo haziko reported?

Punguza bias
 
Wana njaa balsa. Wameweka taalum kando wanatumia matumbo kuandika taarifa

Halafu hayo hayo maandishi ya habari yakikutana na dhahma yanataka viongozi wa upinzani wawapiganie na kuwasemea!

Hakuna kundi kubwa lililojaa wanafiki kama waandishi wa habari, ni wachache sana wenye misimamo yao ya dhati wengi ni machawa waendekeza bahasha na mbeleko.
 
Asante Mystery kwa mada nzuri.. Hii trauma ya katazo bado ganzi yake haijavitoka vyombo vyetu vya habari ama la vimetishiwa kisirisiri! Tofauti na hapo kuna uchawa ndani yake na viashiria vyote vya kujikomba kwa shukrani ya teuzi mbalimbali

Bado tuna vyombo vya habari visivyo huru na tuna waandishi wa habari wasiojiamini.
 
Mkuu mtoa mada, umeelezea kitu muhimu mno na kinachotakiwa kwa consumers ambao wanaona haki yao inaburuzwa, ni kutumia ile power ya mlaji, hit them kwenye pockets zao, usiangalie TBC TV, na magazeti uchwara haya usinunue.

Binafsi gazeti la Mwananchi siligusi since walivyoingia uoga na wakanyamaza kabisa kumpigania mwandishi wao aliyepotea kwenye mazingira ya utatanishi Mr.Azory, Aljeezeera bado hadi leo wanampigania waandishi wao waliofungwa Egypt 🇪🇬 na yule aliyegigwa risasi pale Palestine, Editors ni waoga wa kizuzu na wachumia tumbo.
 
Halafu hayo hayo maandishi ya habari yakikutana na dhahma yanataka viongozi wa upinzani wawapiganie na kuwasemea!
Hakuna kundi kubwa lililojaa wanafiki kama waandishi wa habari, ni wachache sana wenye misimamo yao ya dhati wengi ni machawa waendekeza bahasha na mbeleko.

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
Absolutely true by 💯 percent ✔️
 
Vyombo Hakuna Wakati Wa Jiwe Ndiyo Walifyata Mkia Saa Hizi Watafanyaje
 
Lakini jambo la ajabu ninaloliona ni Kwa vyombo vya habari nchini, kuendelea kutoa taarifa za vyama vya kisiasa vya upinzani Kwa "machale" makubwa.
Ni kweli
Inafahamika pia kuwa vyombo vya habari ni Mhimili wa 4 wa Dola, usio rasmi.
True
Tunajua pia kuwa vyombo vya habari kama vile luninga ya TBC na gazeti la Habari Leo, ni vyombo vya umma, vinavyoendeshwa Kwa Kodi zetu wananchi wa vyama vyote vya siasa, iwe ni CCM au Chadema, Kwa hiyo vinapaswa viripoti Kwa usawa habari za vyama vya siasa, bila kufanya upendeleo.
Naunga mkono hoja
Vinapaswa vyombo vya habari hapa nchini visiwe "biased" wakati wa kuripoti taarifa zao,ziwe za CCM au Chadema, viripoti sawa.
Ni kweli
Lakini sivyo vinavyofanya hivi Sasa, kwani mfano TBC inaendeleza mapambio yake ya "kumsifu na kumwabudu" Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan.
Is there a problem kumsifu rais Samia kama anafanya mambo mazuri?. Hebu tuambiane ukweli kuna kiongozi gani mwingine anayestahili sifa na hakusifiwa?.
Vinapaswa vyombo vya habari hapa nchini, viige mfano wa nchi jirani ya Kenya, namna vinavyoripoti taarifa ya vyama vya kisiasa nchini mwao bila upendeleo.
Naunga mkono hoja
Utashangas hapa nchini kwetu, Kwa tukio dogo kabisa linalofanywa na Mwenyekiti wa CCM, Samia Suluhu Hassan inarushwa mubashara na luninga ya Taifa, wakati hotuba ya viongozi wa kitaifa wakihitubia, hawaonyeshi mubashara!
It's true, mkutano wa Chadema ulipaswa kurushwa live mubashara na TBC, lakini hapa naomba TBC isilaumiwe, jee Chadema walitoa mwaliko? na kuomba live coverage TBC wakakataa?. Kwenye live za taasisi huwa zinalipiwa na TBC ndio the cheapest, jee Chadema wana that capacity kulipia live ya 3 hours kutokea Mwanza?.
Kama kweli Taifa letu linataka kukuza Demokrasia nchini, basi vyombo vya habari nchini, vinapaswa vibadilike katika utendaji wake.
True naunga mkono hoja 100% kwa 100%
P
 
Shetani ameacha kovu. Linafutika taratibu taratibu.
Kwanini Sasa vyombo vya habari, visiufute haraka haraka?

Hivi vyombo vya habari vinaingiaje woga wa kuripoti habari bila upendeleo, wakati Rais mwenyewe, Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa kuzuiwa Kwa mikutano ya kisiasa, ilikuwa ni zuio haramu, kulikofanywa na utawala wa awamu ya 5?
 
Ni wazi kuwa Rais wa awamu ya 6 Dkt Samia Suluhu Hassan, ameondoa zuio haramu za kufanyika shughuli za kisiasa za vyama vya upinzani na hivyo kurejesha ukuaji wa kidemokrasia Kwa vyama vya upinzan hapa nchini, ambao ulikuwa umeminywa Kwa kiasi kikubwa Kwa zaidi ya miaka 6 ya utawala wa awamu ya 5 ya Mwendazake.

Lakini jambo la ajabu ninaloliona ni Kwa vyombo vya habari nchini, kuendelea kutoa taarifa za vyama vya kisiasa vya upinzani Kwa "machale" makubwa.

Inafahamika pia kuwa vyombo vya habari ni Mhimili wa 4 wa Dola, usio rasmi.

Tunajua pia kuwa vyombo vya habari kama vile luninga ya TBC na gazeti la Habari Leo, ni vyombo vya umma, vinavyoendeshwa Kwa Kodi zetu wananchi wa vyama vyote vya siasa, iwe ni CCM au Chadema, Kwa hiyo vinapaswa vilipiti Kwa usawa habari za vyama vya siasa, bila kufanya upendeleo.

Vinapaswa vyombo vya habari hapa nchini visiwe "biased" wakati wa kuripoti taarifa zao,ziwe za CCM au Chadema, viripoti sawa.

Lakini sivyo vinavyofanya hivi Sasa, kwani mfano TBC inaendeleza mapambio yake ya "kumsifu na kumwabudu" Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan.

Vinapaswa vyombo vya habari hapa nchini, viige mfano wa nchi jirani ya Kenya, namna vinavyoripoti taarifa ya vyama vya kisiasa nchini mwao bila upendeleo.

Tulijionea wakati wa uchaguzi Mkuu uliopita wa Kenya namna vyombo vya habari vya nchi hiyo vilivyokuwa huru, wakiripoti mubashara, shughuli za kisiasa, ziwe za chama tawala au vyama vya upinzani.

Utashangas hapa nchini kwetu, Kwa tukio dogo kabisa linalofanywa na Mwenyekiti wa CCM, Samia Suluhu Hassan inarushwa mubashara na luninga ya Taifa, wakati hotuba ya viongozi wa kitaifa wakihitubia, hawaonyeshi mubashara!

Kama kweli Taifa letu linataka kukuza Demokrasia nchini, basi vyombo vya habari nchini, vinapaswa vibadilike katika utendaji wake.

Kwani LAZIMA vifahamu kuwa enzi zile za kutishiwa kufungiwa, kama vilivyokuwa vikifanyiwa na utawala wa awamu ya 5, hadi kutishwa kuwa "you don't have that freedom to that extent" umeshapitwa na wakati.

Mungu ibariki Tanzania
Mkuu Mystery, umeongelea jambo la msingi sana. Wanahabari wengi wanaonekana bado wanapima uelekeo wa upepo. Bado wanasita kujiachia, pengine bado wanabanwa na mamlaka zao za kiutendaji.

Hata kama katazo haramu la mikutano vya vyama vya siasa limeondolewa kupitia tamko la Rais, lakini inaonekana bado kuna kumbukumbu mbaya inataeala ya mazingira ambayo vyombo vya habari vimeptia katika kipindi cha miaka 6 ya utawala wa JPM. Jambo ambalo bado limeviacha vyombo vingi vikiwa bado vimegubikwa na "fear of unknown".

Suala lingine ambalo linaweza kutokuonekana kwa urahisi kwa macho ya kawaida, lakini pengine lipo, ni kukosekana kwa utayari wa uhuru wa kupashana habari za kisiasa kwa wahafidhina waliopo katika chama tawala hali inayopelekea tishio kwa uongozi wa vyombo vya habari.

Pengine hii inatokana mikwala iliyowahi kupigwa chini ya zulia. Na pengine bado wanasikilizia pia kuondolewa kwa tishio hilo la kimya kimya ambalo linawaumizwa vichwa na kusubiri nalo litolewe pia kauli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
😇😇😌
Biased? Hata kutaja Hayati J.P.M imekushinda.

Haya jamani. Tutafika. Lakini sijawahi kuona nchi yeyote inayohangaika kuweka wapinzani wao mbele. Ukidai waanzishe T.V yao wenyewe halafu wakataliwe kuonyesha mubashara, ntakuelewa. Zaidi ya hapo utasubiri sana.

Chadema wana vitengo vyao vya habari. Angalia Chadema Digital wapo Yuuutubu. bureee

Usizushe
 
Ni wazi kuwa Rais wa awamu ya 6 Dkt Samia Suluhu Hassan, ameondoa zuio haramu za kufanyika shughuli za kisiasa za vyama vya upinzani na hivyo kurejesha ukuaji wa kidemokrasia Kwa vyama vya upinzan hapa nchini, ambao ulikuwa umeminywa Kwa kiasi kikubwa Kwa zaidi ya miaka 6 ya utawala wa awamu ya 5 ya Mwendazake.

Lakini jambo la ajabu ninaloliona ni Kwa vyombo vya habari nchini, kuendelea kutoa taarifa za vyama vya kisiasa vya upinzani Kwa "machale" makubwa.

Inafahamika pia kuwa vyombo vya habari ni Mhimili wa 4 wa Dola, usio rasmi.

Tunajua pia kuwa vyombo vya habari kama vile luninga ya TBC na gazeti la Habari Leo, ni vyombo vya umma, vinavyoendeshwa Kwa Kodi zetu wananchi wa vyama vyote vya siasa, iwe ni CCM au Chadema, Kwa hiyo vinapaswa vilipiti Kwa usawa habari za vyama vya siasa, bila kufanya upendeleo.

Vinapaswa vyombo vya habari hapa nchini visiwe "biased" wakati wa kuripoti taarifa zao,ziwe za CCM au Chadema, viripoti sawa.

Lakini sivyo vinavyofanya hivi Sasa, kwani mfano TBC inaendeleza mapambio yake ya "kumsifu na kumwabudu" Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan.

Vinapaswa vyombo vya habari hapa nchini, viige mfano wa nchi jirani ya Kenya, namna vinavyoripoti taarifa ya vyama vya kisiasa nchini mwao bila upendeleo.

Tulijionea wakati wa uchaguzi Mkuu uliopita wa Kenya namna vyombo vya habari vya nchi hiyo vilivyokuwa huru, wakiripoti mubashara, shughuli za kisiasa, ziwe za chama tawala au vyama vya upinzani.

Utashangas hapa nchini kwetu, Kwa tukio dogo kabisa linalofanywa na Mwenyekiti wa CCM, Samia Suluhu Hassan inarushwa mubashara na luninga ya Taifa, wakati hotuba ya viongozi wa kitaifa wakihitubia, hawaonyeshi mubashara!

Kama kweli Taifa letu linataka kukuza Demokrasia nchini, basi vyombo vya habari nchini, vinapaswa vibadilike katika utendaji wake.

Kwani LAZIMA vifahamu kuwa enzi zile za kutishiwa kufungiwa, kama vilivyokuwa vikifanyiwa na utawala wa awamu ya 5, hadi kutishwa kuwa "you don't have that freedom to that extent" umeshapitwa na wakati.

Mungu ibariki Tanzania
Maneno aliyo wahi kuyasoma Bashiru hayapaswi kupuuzwa kuwa Chama kilichopo madarakani kisipotumia vizuri dola kubaki madarakani likitoka hakirudi tena kwa hiyo vyombo vya habari vyetu bado vinauo uoga bado.
 
Acha ujinga kijana, utatumiwa na wanasiasa uchwara hadi lini? Mbona mnaendekeza malalamiko yasiokuwa na msingi? Hata kama uchawa lkn muda mungine mpunguze kidogo mahaba yasiokuwa na tija kwa vyama vyenu na waajiri wenu wanaowatuma kuandika upuuzi mitandaoni.

Kama vyama vinakosa wahudhuriaji wa mikutano kama tulivyoona Mwanza na Musoma hilo sio tatizo la wanahabari bali ni tatizo la walamba asali kupoteza sifa kwa wananchi na wale wanaowaongoza katika vyama vyao.

Unafikiri ni mwananchi gani mwenye akili zake ataacha shughuli zake aje awasikilize wanasiasa uchwara? Watu wengi wamejifunza kupitia siasa za majitaka za enzi za kuwachafua kina Lowasa bila ushahidi na hadi ule mchakato wa 2015 katika uchaguzi mkuu. So sio rahisi kudanganyika tena.

Watanzania sio wasahaulifu kihivo.
Hata kama we ni chawa, sio kwa kiasi hili. Huoni hata aibu kwa familia yako?
 
Back
Top Bottom