Kwanini vyombo vya habari bado vinaripoti kwa 'machale' taarifa za vyama vya siasa vya upinzani?

Kwanini vyombo vya habari bado vinaripoti kwa 'machale' taarifa za vyama vya siasa vya upinzani?

Kwani Jerad Hando amesharudi
Swali zuri.

Huyo mwandishi alitumia taaluma yake kuhoji mambo ya msingi ya kitaifa, lakini Kwa kuwa mmiliki wa chombo chake, ni "chawa" wa mama, amejikuta kitu kizito kinatua kichwani mwake😎

So sad
 
tatizo Tz hatuna vyombo vikomavu vya habari
Wamiliki uchwara, wahariri uchwara!
Mie nimeacha kabisa kununua magazeti labda kdg Mwananchi.
 
Kuripoti kwa weledi kutoka kwa hawa wanahabari wetu, usahau.


Mara nne kampuni yetu imewahi kutembelewa na viongozi wa Serikali. Wanapokuja wanatanguzana na waandishi wa habari waliowalipa. Baada ya kikao, mara zote, nikaja kuambiwa na maofisa wangu kuwa waandishi wa habari wamesema wanaomba milioni 1 wakati mwingine milioni mbili, eti ili waka-report huo mkutano wa viongpzi wa Serikali walipotembelea kampuni.

Mara zote mimi nilikataa, lakini wenzangu waliniambia kuwa ndiyo utaratibu ulipzoeleka. Ndiyo maana utakuta Waziri au mkuu wa mmoa, hata akifanya tukio dogo saa 8 usiku, lazima mwanahabari atakuwepo, na hasa kama tukio hilo litampandisha kuobekana ni mchapa kazi. Wanadai kuwa hata marehemu akuwa Waziri wa Ujenzi alitumia sana technique hiyo. Anaenda kwenye mradi wa ujenzi wa daraja saa 7 usiku, lakini mwanahabari yupo. Anatoa karipio kali huo usiku, na ilimpandisha sana mbele ya wananchi. Na aluzidisha zaidi baada ya kuwa Rais.

Hivyo kama vyama vya upinzani vinataka habari zake zitangazwe sawa na zile za CCM, labda wafanye yale ambayo CCM huwa wanafanya. Hata ndani ya Serikali au CCM, wale ambao hawatoi chochote kwa wanahabari, hata kama wanachapa kazi kiasi gani, habari zao hazitangazwi sana.

Huko Kanda ya Ziwa mpaka kuna kampuni ya habari za Waziri iliyojificha kwa jina la mtu mwingine lakini lengo la kampuni hiyo binafsi ya habari, ni kum-promote na kumpamba huyo Waziri ili aonekane ni mchapa kazi kwelikweli.
 
Hivi wewe voicer ni CHADEMA kumbee!!???
Maana nasoma mara kwa mara kuwa hapa jukwaani wana CHADEMA ndio wanaomtaja sana na mara kwa mara JPM,sasa wewe kila comment yako lazima umtaje huyo mwendazake!
Mimi sio mwana Chadema hata chembe!

Mimi ni mpenda haki na siasa za ukweli,bila makandokando yanayoendelea kwa pande zote!
 
Tena katika kipindi hiki, ambapo miswada wa marekebisho ya Sheria ya huduma za Habari, ndiyo hawakupaswa kabisa kuingia woga, wakati wana-ripoti habari zao
 
Back
Top Bottom