Kwanini wakatoliki wanamuomba Mungu awajalie moyo wa ufukara na siyo ya utajiri kama vile Mungu alivyosema atatubariki?

Ufukara wa moyo ni katika imani, na ni tofauti na ufukara wa mwili.
Mkuu moyo uko wapi mpaka iwe tofauti..? ukiwa ndani ya moyo fukara na nje ya mwili wewe ni fukara pia maana moyo upo ndani ya mwili na ndivyo ilivyo imani.. huwezi ukawa fukara moyoni alafu ukafanya matendo ya kimwili katika utajiri.

Mfano. Moyo ukihuzunika hata nje ya mwili inajifunua kwamba una hudhuni na wakati mwingine kuugua na kulia kwa uchungu.. na hivyo hivyo ukiwa fukara moyoni hata kimwili utakua fukara na ndiyo itakua umejifunga kiimani
 
Napia ili uweze kuwa mtu mwema unatakiwa uwe kiroho na siyo kuwa na moyo wa kifukara..

rejea matendo ya rohoni.

Wagalatia 5:22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.

Sasa kwanini wao wakatoliki wautake ufukara na siyo kutaka matendo mema kama ilivyowazi kwenye maandiko kama kweli wanachomaanisha ni kizuri. Kwanini wasiende direct wanazunguka mbuyu..
 
Hapo msamiati 'Heri' ulitumika vibaya
Kiuhalisia badala ya Heri ilitakiwa iwe
'Wamebarikiwa'
Ikiwa Maana Wamebarikiwa maskini,webarikiwa wanyonge
Ukiwa maskini ukibarikiwa ina maana wewe ni tajiri,
Ukiwa mnyonge utapewa moyo wa ushujaa,

Na Sio Heri,Heri,Heri ambayo inasound ki lay man ukisoma. Hata Bible ya kingereza
Inasema Blessed all........
 
Nipo mkoa unaosifika Kwa kuwa na makanisa mengi uchwara ya kikristo.
Ninachokiona na kukishuhudia kwa hawa watu. Aisee! nitadumu mno kwny ukatoliki nikishindwa kabisa bora niwe mpagani.PERIOD.
 
Moyo wa ufukara...
1. Kuona mali si kitu mbeke ya uzima wa milele.

2. Kugawa ulichobarikiwa kwa maskini.

3. Majivuno kupitia mali si kitu, maana tulivikuta na tutaviacha.

4. Mali za dunia hazina msaada kwenye ukimbozi wa roho yako.
 
Sasa kuhusu hiyo michango iliyokithiri hayo ni mambo ya kibinadamu zaidi. Sadaka ni unatoa chochote kulingana na uwezo wako, so ni jukumu lako wewe kuamua kama uwaridhishe bonadamu au umridhishe Mungu. Akili kichwani mwako.
 
Yesu alizaliwa ukoo wa kifalme! Chumba alichozaliwa yesu walipachagua kwa kuwa palikuwa mahali pa utulivu. Kumbuka wakati huo kilikuwa kipindi cha mwisho wa mwaka wakati wa sensa ya watu na makazi kati ya mwezi 9-11 na kila mtu alikuwa anaenda kuhesabiwa hivyo nyumba hiyo ya mbari ya daudi ilijaa wageni mama mariam angepata wapi utulivu ili aweze kujifungua ?
 
Haimaanishi hivyo Muombe Mungu akupe akili ya kulitafakar na kulijua neno laMungu
( Moyo wa ufukara, moyo usio na tamaa, moyo wa kuwapenda wengine, moyo usio na ubinafsi, moyo wa kujitolea kwa ajili ya wengne)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…