Kwanini wakristo tunaamini Israel ni taifa la Mungu wetu huku Waisrael hawamuamini Yesu wala dini ya ukristo?

Israeli ya kwenye 'baibo' ni OG ila hii ya Netanyahu siyo.
 
Mbona nilishakujibu Hilo au hukuridhika?
Tofautisha kati ya kujibu na kuhubiri.

Maelezo unayotoa ni mahususi kwa mtu ambaye tayari anaamini ila kuna concept ndogo ambayo inamtatanisha hivyo anahitaji mahubiri kiasi ili kum shape.

Sasa mimi siamini na sitaki kuamini.

Sitaki kuamini kwasababu nataka kujua.

Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?
 
Hahahaha hutaki kuamini kwasababu unataka kujua pole sana sababu huwezi kujua pasipo kuamini.
 
Hahahaha hutaki kuamini kwasababu unataka kujua pole sana sababu huwezi kujua pasipo kuamini.
Wewe ndio unasema unajua kiswahili?

Kwa mujibu wa ufahamu wako unaona misingi ya ujuzi inapatikana kwenye imani au kwenye fact ambazo zimekuwa observed?
 

Wewe ndio unasema unajua kiswahili?

Kwa mujibu wa ufahamu wako unaona misingi ya ujuzi inapatikana kwenye imani au kwenye fact ambazo zimekuwa observed?
Yes, misingi ya ujuzi inapatikana kwenye imani lakini pia fact.
 
Wewe ndio unasema unajua kiswahili?

Kwa mujibu wa ufahamu wako unaona misingi ya ujuzi inapatikana kwenye imani au kwenye fact ambazo zimekuwa observed?
Vp umesepa!
 
Ni kutokusoma vizuri kitabu au aliyoyasema Yesu na kujua kusudi ni lipi?

Maana Yesu mwenyewe walipomkataa aliwaambia ufalme utahama kwenda taifa lingine litakalo mzalia muumba matunda.

Mathayo 21:43
Kwa sababu hiyo nawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake.

Ukianzia mstari wa 33 Yesu anawatolea mfano kuwaonyesha kila nabii aliyetumwa kwao walikuwa wanamkataa.
 
Hawa jamaa hawakubali ukinakili kwenye Bible coz hawaiamini, wao wanataka Mungu aonekane laivu awaambie wamwabudu. Wanadai biblia imeandikwa na watu. Wao wanataka Mungu aonekane kwanjia wanayoitaka wao na sio anayoitaka Mungu mwenyewe. Wanasahau kwamba hakuna mahali unaweza kumpata zaidi ya kwenye imani. Anaishi humo, ilimpendeza kuishi humo. Labda watueleze wao walitaka ajidhihirishe kwa mwanadamu kupitia njia ipi?
 
Wewe ni muislamu pyure kabisa kinachokusumbua ni kukosa kujiamini.Ungeandika tu andiko lako straight pasipo kufeki
 
Waisraeli walikuwepo tangu wakati wa Yesu, na wapo waliomwamini na kumfuata. Aidha, uwepo wa taifa la Israeli haukuanzia 1948!
Sasa mbona hakuna kanisa lililoanzishwa Israel?
-anglican
-roman catholic
Nk
 
Mimi sio mjuzi sana wa mambo ya dini lakini kwa uelewa wangu mdogo tu ntachangia mada.

★ Kwanza kabsa historia ya kwenye vitabu inasema yesu alikuja kwaajili ya kuukomboa ulimwengu, na kipindi hicho alizaliwa Israel ambapo ndo taifa teule kwa wakati huo. Lakini tukumbuke mpaka yesu anakuja watu wengi walikuwa wameyaacha mafundisho na sheria zake mungu ndio akamtuma kuja kufundisha watu neno la mungu.
Ikimbukwe pamoja na kufanya miujiza mingi na mafundisho mengi lakini asilimia kubwa ya watu wa Israel hawakuwa wakikubaliana nae maana yake walikuwa bado wapo kwenye njia za uovu. Nabii hasifiki kwao wakamuua waisrael wenyewe.

★ Kusambaa kwa dini ya ukristo kulianzishwa na Moja ya wanafunzi wa yesu, ukiuliza kwann kanisa halikianzia pale jibu ni kwamba kwa wakati huo usalama ulikuwa ni mdogo simple logic tu kiongozi wako ametoka kuuwawa kwa kutangaza injili je utaendelea kuitangaza mahali hapo jibu ni no.
Kwahyo baada ya yesu kufariki tamaduni za kiyahudi ziliendelea kama kawaida na pia dini ya ukristo haikutangazwa sana ndo mana Israel inabaki na ule utamaduni wao.

★Ukristo na uislam ipi ni dini ya kweli?
Kulingana na mafundisho mengi ya kwenye bible na Quran yote yanafundisha kumjua mungu na kufuata njia sahihi za kuishi hapa duniani mpaka mwisho wetu.

★ Mwisho sisi wafuasi wa dini hizi mbili zenye nguvu na ushawishi mkubwa yatupasa tuelewe ya kuwa hakuna dini mbaya kama tu inafundisha yaliyo mema ila inatokea waoziongoza hizi dini (viongozi) ni binadam kama sisi hivyo tutafakari mafundisho Yao, tulinganishe na maandiko ya kwenye vitabu vyetu tupime usahihi wake.
 
 
Unasoma Biblia ndugu yangu Muislamu? Soma Biblia ina majibu yote. Zamani nami nlikiwa mjinga kama wewe. Nikaja elewa. Sasa sina tena ujinga.
 
Hivyo ndivyo Biblia ndivyo inavyosema sio Wakristo kama unavyodai. Wayahudi kutomuamini Yesu ni kutimiza walichoaminishwa na wakuu wa dini ya Kiyahudi. Mathayo 28
12 "Wakakusanyika pamoja na wazee, wakafanya shauri, wakawapa askari fedha nyingi,
13 wakisema, Semeni, ya kwamba wanafunzi wake walikuja usiku, wakamwiba, sisi tulipokuwa tumelala.
14 Na neno hili likisikilikana kwa liwali, sisi tutasema naye, nanyi tutawaondolea wasiwasi." Mat.28:12-14.

Vv
 
Waisrael tyr wanajiona wako na akili kubwa sana kwa hyo acha wakristo waendelee kujipendekeza
 
Rulr number one kuna mungu wa kweli dini ya kweli na biblia ya kweli sema mzungu aliingilia kat na kuficha ficha baadh ya vifungu na kue dit kwa lengo la kuutawala ulimwengu din imetumika kama kigezo cha utawala ndio maana mpala leo wameficha kua hawa ni mwanamke wa pil baada ya lilith yaan adam na hawa waliumbwa pamoja na vitu vingine ving sanaaa kama shetan na mungu baada ya uasi waliwai kukutana na kupiga story mpaka shetan akampa ushaur mungu wa ayubu apokemywe mali zake zote na mungu akakubal ushaur wa shetan hiyvo kuna vingi vimefichwa kwa maslai ya wachache
 
Kwa sababu hatutafsiri maandiko kwa namna sahihi, bali tunatafsiri literally. Sidhani kama kilichoandikwa kwenye Biblia kina uhusiano wowote na taifa la Israeli lililo chini ya Netanyau. Kufanana kwa majina hakuna maana ya kufanana kwa maana. Mfano, kwenye Biblia kuna neno limeandikwa "mana" (chakula Wana wa Israeli walichopata kutoka mbinguni wakiwa jangwani). Kwenye kabila letu kuna neno "mana" pia lenye maana ya sehemu za siri za mwanamke. Kwa hiyo, mtu wa kabila langu akisoma neno "mana" kwenye Biblia na kutafsiri kuwa ni "sehemu za siri za mwanamke" ni sawa na sisi tunaosoma "Israeli taifa takatifu la Mungu" na kuona taifa hilo ni taifa linaloongozwa na Waziri Mkuu Netanyau.
 
Brain washed education
To make people fools
This is reward for our love
(Bob marley)
 

Mkuu, unapenda kutafuniwa tu? Jipe Mwezi, anaza Agano la Kale hadi jipya.....Unaweza kupata majibu.....! Ni hizi enzi za simu janja, unaweza kupata elimu ya bure kabisa....!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…