Kwanini wanafunzi wasianze kidato cha kwanza na michepuo ya sayansi (Physics, Chemistry) au arts kwa kuzingatia matokeo ya Darasa la Saba?

Hongera sana mkuu...
 
Kama mfumo wa sasa uendelee basi uende hivyo hivyo mpaka kidato cha nne kwa wanafunzi wote na sio kuwachuja ikifika form II kwamba huyo atasoma Physics na Chemistry lakini yule hasomi.

Kama tunataka michujo basi ianzie form I kwa kuzingatia matokeo ya darasa la saba...
 
Huu utafiti wako wa wanafunzi wa kike na kiume nina mashaka nao sana mkuu...
 
sekondari akili ya kijana wa kiume ndo inaanza kutulia....mimi wazo nalopendekeza miaka ya shule ya msingi ipunguzwe hadi miaka 6 au iongezwe hadi miaka 8 ya sekondari o level iwe 3 .
Asante kwa ushauri wako mkuu
 
Changamoto ni nyingi. Ufaulu unapimwa na storage capacity na sio thinking capacity.. Ukute mtoto wako ni 2GB na memory iko full tayari. iyo form 4 izo 4GB storage anazitolea wapi ?
 
Mkuu, sasa kwa hali hii wale wadogo zetu wenye thinking capacity nzuri si wanaonewa na mfumo wetu huu wa elimu...
Ni kweli kuna mambo ambayo viongozi wanahitajika wayape kipaumbele cha kwanza maana akili ikiwa vizur kutokana na msingi mzur wa elimu tunauhakika wa kuwa na maendeleo kwani tuna uhakika wa kuwa na wasomi wenye uwezo mkubwa wakufikiri...
 
Ni kweli kuna mambo ambayo viongozi wanahitajika wayape kipaumbele cha kwanza maana akili ikiwa vizur kutokana na msingi mzur wa elimu tunauhakika wa kuwa na maendeleo kwani tuna uhakika wa kuwa na wasomi wenye uwezo mkubwa wakufikiri...
Ninakubaliana sana na hii kauli yako mkuu
 
Changamoto ni nyingi. Ufaulu unapimwa na storage capacity na sio thinking capacity.. Ukute mtoto wako ni 2GB na memory iko full tayari. iyo form 4 izo 4GB storage anazitolea wapi ?
Unapanua harddisk katika ubongo wake mkuu. Hahahaaaaa I am just kiding bro.
 
Labda kwa sasa hivi. Miaka hiyo wale waliosoma sekondari za ufundi masomo kama History, Geography na Biology walikuwa hawasomi/haafanyii mtihani form four.
Wewe utakuwa ni mhenga sana mkuu...
 
Reactions: SMU
Naipinga hoja hii kwa sababu zifuatazo;

1. Huku mwanzoni unapata msingi tu wa masomo yote. Hivyo kupata msingi mzuri ndiyo kunafanya mtu awe na uelewa mzuri kwenye michepuo yake

2. Masomo hutegemeana, unaposoma somo hili, kuna pahala patakusaidia kwenye somo jingine, hasa huku mwanzoni. Hivyo basi kuwafanya wanafunzi waanze michepuo mapema, ni kuwaondolea misaada ya masomo mengine kwenye michepuo yao.

3. Ili kujua mwanafunzi aende mchepuo gani, kwanza inatakiwa apite kote ndipo atakapojua uwezo wake upo upande gani. Unaweza ukamuweka mwanafunzi kwenye PCM mapema lakini ujuwe huko pengine atakuwa anafuata mkumbo tu, usikute anaweza art zaidi kuliko PCM. Hajijui uwezo wake kamili upo wapi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…