Kwanini wanashauri usivute gari lenye Automatic Gearbox ukipata break down, badala yake upakie kwenye Flatbed Truck

Kwanini wanashauri usivute gari lenye Automatic Gearbox ukipata break down, badala yake upakie kwenye Flatbed Truck

Huu uzi nilitamani ningepata Automatic Gearbox mbovu nikaufanyia video. Kwa maana ninaamini kwa njia hiyo wote mngenielewa vizuri. Hata hivyo nitajitahidi kuelezea kwa kadri nitakavyoweza.

Hebu iangalie hii picha vizuri. Hii ni cross section ya Gearbox ya automatic. 99% gearbox za automatic zipo hivi. Iangalie vizuri Oil pump ipo tu baada ya Torque Converter.
View attachment 2722983

Kwenye gearbox ukizima gari, Gearbox Oil inabakia maeneo mawili tu.

1. Kwenye torque converter.

2. Kwenye Sump ya Gearbox.

Sasa ipo hivi, unapovuta gari lenye automatic gearbox, engine inakuwa imezima, torque converter na Oil pump pia vinakuwa havizunguki. Hivi vitu huwa vinazunguka tu kama engine inazunguka.

Then Oil pump hazunguki, sehemu ya gearbox iliyobakia inazunguka bila Oil. Hivyo ni rahisi kuharibu gearbox.

Kuna baadhi ya gari mfano baadhi ya matoleo ya mercedes Benz gearbox inakuwa na secondary Oil pump na inakuwa na Tow mode(hii naomba isichanganywe na ile tow mode ya kuvuta trailer n.k.).

Hiyo secondary pump inakuwa activated utakapotaka kulivuta gari lako kwa ajili ya kusupply oil kwenye gearbox.

Ndio maana ukipata breakdown ushauri wa kwanza ita flatbed truck pakia au tow truck kama gari yako si AWD na mtanyanyua upande ambao ndio unadrive.

Na kama utaamua kuivuta gari yako basi fuata sheria hii.

1. Vuta kwa speed ndogo kwa kadri itakavyowezekana.
Hii ina maana haitakiwi kulisukuma gari (automatic gearbox) hata kama umeharibikiwa katikati ya barabara ?
 
Huu uzi nilitamani ningepata Automatic Gearbox mbovu nikaufanyia video. Kwa maana ninaamini kwa njia hiyo wote mngenielewa vizuri. Hata hivyo nitajitahidi kuelezea kwa kadri nitakavyoweza.

Hebu iangalie hii picha vizuri. Hii ni cross section ya Gearbox ya automatic. 99% gearbox za automatic zipo hivi. Iangalie vizuri Oil pump ipo tu baada ya Torque Converter.
View attachment 2722983

Kwenye gearbox ukizima gari, Gearbox Oil inabakia maeneo mawili tu.

1. Kwenye torque converter.

2. Kwenye Sump ya Gearbox.

Sasa ipo hivi, unapovuta gari lenye automatic gearbox, engine inakuwa imezima, torque converter na Oil pump pia vinakuwa havizunguki. Hivi vitu huwa vinazunguka tu kama engine inazunguka.

Then Oil pump hazunguki, sehemu ya gearbox iliyobakia inazunguka bila Oil. Hivyo ni rahisi kuharibu gearbox.

Kuna baadhi ya gari mfano baadhi ya matoleo ya mercedes Benz gearbox inakuwa na secondary Oil pump na inakuwa na Tow mode(hii naomba isichanganywe na ile tow mode ya kuvuta trailer n.k.).

Hiyo secondary pump inakuwa activated utakapotaka kulivuta gari lako kwa ajili ya kusupply oil kwenye gearbox.

Ndio maana ukipata breakdown ushauri wa kwanza ita flatbed truck pakia au tow truck kama gari yako si AWD na mtanyanyua upande ambao ndio unadrive.

Na kama utaamua kuivuta gari yako basi fuata sheria hii.

1. Vuta kwa speed ndogo kwa kadri itakavyowezekana.
Mimi nikadhani clutch inatenganisha Engine na Gear BOX ,kwamba engine inaweza kuwa inazunguka usipo engage clutch Drive shaft (iliyoungwa kwenye mfumo wa gear) kwenda kwenye differential (tairi za nyuma) inakuwa free kuzunguka tu,naomba unisahihishe mkuu.

Asante.
 
Mimi nikadhani clutch inatenganisha Engine na Gear BOX ,kwamba engine inaweza kuwa inazunguka usipo engage clutch Drive shaft (iliyoungwa kwenye mfumo wa gear) kwenda kwenye differential (tairi za nyuma) inakuwa free kuzunguka tu,naomba unisahihishe mkuu.

Asante.
Gearbox automatic haipo kama gearbox ya manual, anzia kubadili mtazamo wako hapa.

Automatic gearbox inakuwa na clutch pack kadhaa, na kila pack inakuwa na viclutch vyembamba sana, na eneo ambalo hivyo viclutch vinazunguka ni eneo dogo sana.

Na ama engine iwe on au gari ikiwa inavutwa engine iko off lazima kuna clutch pack moja au zaidi iwe inazunguka.

Ndio maana tunashauri usivute sababu engine ikiwa off oil pump nayo haizunguko hivyo oil haipandi, clutch zitazunguka bila oil kitu ambacho kinaweza kuziharibu, hapo sijagusia bearings nk.
 
Gearbox automatic haipo kama gearbox ya manual, anzia kubadili mtazamo wako hapa.

Automatic gearbox inakuwa na clutch pack kadhaa, na kila pack inakuwa na viclutch vyembamba sana, na eneo ambalo hivyo viclutch vinazunguka ni eneo dogo sana.

Na ama engine iwe on au gari ikiwa inavutwa engine iko off lazima kuna clutch pack moja au zaidi iwe inazunguka.

Ndio maana tunashauri usivute sababu engine ikiwa off oil pump nayo haizunguko hivyo oil haipandi, clutch zitazunguka bila oil kitu ambacho kinaweza kuziharibu, hapo sijagusia bearings nk.
Shukran
 
Ni ngumu kuelewa joto linazalishwaje kwa elimu ya mtaani.

Converter tu ndio inatunza oil hizo sehemu zingine zilizobaki hazina mahali pa kutunza oil. Ndio maana gari ikipaki masaa mengi oil nyingi inashuka chini.
Yani hata shepu yagiabox ulio idanlod na kutuwekea hapa huioni?
unapo jaza oil sampo Ina jaaa oil Hadi kipita valvu ches Sasa hebu gugo Tena uone umbali wa valvu ches na clutch ni kias Gani kama sio púa na mdomo.
 
Gearbox automatic haipo kama gearbox ya manual, anzia kubadili mtazamo wako hapa.

Automatic gearbox inakuwa na clutch pack kadhaa, na kila pack inakuwa na viclutch vyembamba sana, na eneo ambalo hivyo viclutch vinazunguka ni eneo dogo sana.

Na ama engine iwe on au gari ikiwa inavutwa engine iko off lazima kuna clutch pack moja au zaidi iwe inazunguka.

Ndio maana tunashauri usivute sababu engine ikiwa off oil pump nayo haizunguko hivyo oil haipandi, clutch zitazunguka bila oil kitu ambacho kinaweza kuziharibu, hapo sijagusia bearings nk.
wee jamaa muongo sana.hivi ushawahi kufanya sevis ukaona jinsi oil inavyo Toka?au ushawahi kufungua sampo ukaona oil inavyo Toka?au ushawahi kufungua valvu ches ukaona oil inavyo Toka?
kama ushawahi kufanya vyote nilivyo kuuliza hapa basi Acha kuropoka lakini kama hujawahi basi nihaki Yako kuropoka
 
wee
Haya maelezo ni kwa gearbox ambazo hazina dipstick, tushazoea kwenye gari za mjerumani. Ila gari yenye dipstick weka oil kiasi kinachotakiwa washa gari katembee ikipata moto njoo upime tena.
wee nishajua nibwege kumbe.yani uweke oil ukatembee ndio uludi kupima Tena kama ipo levo au haipo levo?

automatic ukiweka oil yagia box unaiwasha hapo ikae sailensa ukipima ndio unapata kipimo sahihi.sio Hadi uende kutembea ndio urudi kupima.
kajifunze Tena ufundi mkuu bado hujaiva.
 
Heheheh, we huoni kila mtu anakuattack, Hushituki kwamba kitu hakiko sawa?

Yaani uliposema engine ikiwa haipo on hamna joto linazalishwa kwenye gearbox umeongea kitu ambacho huna uelewa nacho wowote. Hakuna kitu kinachozunguka juu ya kingine halafu kisizalishe joto. Hakipo

View attachment 2724806

Hii ni gearbox ya Rav4 U140, ukianza kufungua gearbox, set ya kwanza ya clutch utakayokutana nayo ndio hiyo unayoiona hapo kwenye picha.

Kwa set kunakuwa na clutch(lined plates 4) na back plates 5. Na ukiwa umezikusanya pamoja zinatakiwa kuacha nafasi(clearance ya 0.6mm mpaka 1mm). Ni nafasi ndogo sana.

Na gearbox ikiwa inazunguka, hizo back plates hazizunguki, hivyo clutch zinakuwa zinazunguka katikati ya back plates. Pia hizo clutch upana wake hauzidi 4mm. Kwa anayezielewa hizi hesabu na jinsi hizo clutch zilivyokuwa ndogo halafu zizunguke bila oil, haziwezi kuwa na maisha marefu.
dah naona nitatumia muda mwingi kumpigia mbuzi gitaa.✋
 
Yani hata shepu yagiabox ulio idanlod na kutuwekea hapa huioni?
unapo jaza oil sampo Ina jaaa oil Hadi kipita valvu ches Sasa hebu gugo Tena uone umbali wa valvu ches na clutch ni kias Gani kama sio púa na mdomo.
Ukijaza oil haipiti valve body, na kudhihirisha hilo gari zisizokuwa na dipstick unajaza oil mpaka tundu la sample lianze kudondosha matone ndio inakuwa imejaa,

Utafunga koki utaenda kupiga misele ikishapata joto utarudi utafungua tena koki itamwagika tena kidogo, baada ya hapo itakuwa ipo kwenye level yake.

Clutch na sump haviko pua na mdomo pia kigodoro cha oil filter kinazuia oil kuja free sehemu ya juu ya gearbox.
 
wee jamaa muongo sana.hivi ushawahi kufanya sevis ukaona jinsi oil inavyo Toka?au ushawahi kufungua sampo ukaona oil inavyo Toka?au ushawahi kufungua valvu ches ukaona oil inavyo Toka?
kama ushawahi kufanya vyote nilivyo kuuliza hapa basi Acha kuropoka lakini kama hujawahi basi nihaki Yako kuropoka
Siyo kufungua tu hivyo ulivyotaja hapo, naweza kufanya vitu vingi kwenye hizo gearbox mpaka kufanya rebuild,

Screenshot nimepost asubuhi ni manual ambazo wanazo Automatic Transmission Service Group hawa jamaa wamebobea kwenye hizo gearbox tu. Na ndio wanaotoa hizo manual.

We ukifungua gearbox unaangalia clutch kama zimeisha kwa macho ila wenzako wana gauges, clearance ya 0.5mm huwezi kuona kwa macho.
 
Siyo kufungua tu hivyo ulivyotaja hapo, naweza kufanya vitu vingi kwenye hizo gearbox mpaka kufanya rebuild,

Screenshot nimepost asubuhi ni manual ambazo wanazo Automatic Transmission Service Group hawa jamaa wamebobea kwenye hizo gearbox tu. Na ndio wanaotoa hizo manual.

We ukifungua gearbox unaangalia clutch kama zimeisha kwa macho ila wenzako wana gauges, clearance ya 0.5mm huwezi kuona kwa macho.
toka hapa.automatic giabox zikiunguza clatch zinatengenezeka au hazitengenezeki?
 
Ukijaza oil haipiti valve body, na kudhihirisha hilo gari zisizokuwa na dipstick unajaza oil mpaka tundu la sample lianze kudondosha matone ndio inakuwa imejaa,

Utafunga koki utaenda kupiga misele ikishapata joto utarudi utafungua tena koki itamwagika tena kidogo, baada ya hapo itakuwa ipo kwenye level yake.

Clutch na sump haviko pua na mdomo pia kigodoro cha oil filter kinazuia oil kuja free sehemu ya juu ya gearbox.
daa wee jamaa kwamaelezo haya nimegundua kuwa kumbe uko mweupe kabisa kwenye fani ya ufundi magari.

nyie ndio vijana makinda mnao ya giabox zawatu.

narudia mara yamwisho kukuelekeza kijana nihivii👉

ukitaka kuweka oil ya giabox kwenye auto cars unaweka oil kama inaingia Litasita unaweka nne then unaiwasha gari ikae sailensa unamaliza oil iliyo bakia
hapo ukipima oil dipstick itakuonesha kuwa oil ipo levo wee bwana mdogo sAwa?

Hamna haja yakwenda kupiga misele ndio urudi kupima🤣🤣🤣

unanichekesha kifala yani.

halafu unasema kitako Cha oil filter kinaziba valvu ches body yote kiasi chakuzuia oil isipenye juu kwenye valvu ches?uko Silias mjomba?
 
wee nishajua nibwege kumbe.yani uweke oil ukatembee ndio uludi kupima Tena kama ipo levo au haipo levo?
Kwa hiyo mtu akiwa anafahamu kitu ambacho wewe hufahamu anageuka kuwa bwege?
automatic ukiweka oil yagia box unaiwasha hapo ikae sailensa ukipima ndio unapata kipimo sahihi.sio Hadi uende kutembea ndio urudi kupima.
kajifunze Tena ufundi mkuu bado hujaiva.
Nisije nikawa nabishana na mtu anarekebisha gari za miaka ya 80, siku, sheria ya kuweka oil ya auto gearbox siku zote ni weka oil kiasi kinachotakiwa washa gari nenda kazurule likishapata moto, rudi angalia kwenye dipstick kama Oil iko level, kama imezidi punguza kama iko chini ongeza,

Kwa gari ambazo hazina dipstick, na ndio na ndio gari za sasa, unaweka oil kiasi kinachotakiwa unawasha gari unaenda kuzurula, likipata moto unafungua drain valve, oil itakayomwagika ndio iliyozidi.

Na kuna gearbox hazina drain valve, lazima uwe na pump kudrain au kuweka Oil, na level ya Oil utacheck ndani kwenye gari au kwa mashine.

Kitu cha mwisho oil level ya gearbox inapimwa baada ya gari kuwa imetembea na ni ya moto, na siyo baada ya kuwasha. Kuna sababu juu ya hili.
 
Back
Top Bottom