Kwanini wapinzani wanapenda kutumia media za nje kuzungumzia mambo yetu ‘ya ndani’?

Kwanini wapinzani wanapenda kutumia media za nje kuzungumzia mambo yetu ‘ya ndani’?

Kwani kuna media yoyote ya ndani inayoweza kumpa mtu coverage kama mtu huyo hazungumzi maneno ya kumsifu Rais?

Media zote za ndani ama kwa woga au unagiki, hawataki kuripoti chochote cha vyama vya upinzani. Wanaalikwa kwenye mikutano, hata kwenda tu wanaogopa! Halafu utegemee waongee na wapinzani?

Hakuna awamu ambayo imeua haki za maoni ya watu kama hii. Nadhani itabakia kwenye kumbukumbu za Taifa kwa miaka mingi. Awamu hii imejaribu sana kutaka kuendesha nchi kidikteta. Cha kushukuru ni uwepo wa jamii ya kimataifa.


Sent using Jamii Forums mobile app
Hakika
 
Sasa imekuwa kama imehalalishwa vile kwa viongozi wa upinzani kuvikacha vyombo vya habari vya ndani na kukimbilia media za nje na za washindani wetu wa kiuchumi.

Alianza Zitto na zile fedha za kusaidia elimu ya watoto wa kike lakini kwa bahati nzuri WB wakamshushua na kumpuuza. Zitto aliitumia BBC badala ya media za ndani.

Sasa Tundu Lissu naye anayarudia makosa yaleyale, hivi kwanini mnakwepa media zetu?

Inakera sana.

Maendeleo hayana vyama!
Mkuu, vyombo vya ndani ndio vinawakimbia Wapinzani. Hata ilitokea wakafanya mahojiano maswali yao yanakuwa HAYAJASHIBA. Utakuta wanamhoji Mnyika kwa maswali yale yale wanayomhoji BABA LEVO, Au maswali wanayomuuliza SHILOLE watamuuliza Halima Mdee.
 
Katika ulimwengu huu tuliopo wa kiteknolojia, hakuna sababu ya msingi ya kumkosoa mtu kwa kutumia media za nje kuzungumzia mambo ya "ndani" ya nchi yake unless nchi hiyo haina uhuru unaopasa wa vyombo vya habari.

Kama Twitter tu ni media ya nje kwa nchi mbalimbali lakini viongozi mbalimbali ulimwenguni wamekuwa wakiitumia kuzungumzia mambo mengi tu ya nchi zao tena hata hayo ya "ndani" unayoyasema.
Labda TWITER ni ya ndani kwa kila nchi...

BTW, kwani media ipo limited kutangaza habari za nchi zilipo ofisi za medio husika..!? NINI MAANA YA BBC KTANGAZA KWA LUGHA YA KISWAHILI..!? Kwani media za Tanzania, hazina kipengere cha HABARI ZA NJE YA TANZANIA..!? Kwani watu wa huko nje ya Tanzania, huwa hawatumii media zilizopo Tanzania kusema ya kwao..!?

Binafsi, naona MTOA MADA HAJATUMIA AKILI YAKE KUFIKIRI NJE YA BOX..
 
Mkuu, vyombo vya ndani ndio vinawakimbia Wapinzani. Hata ilitokea wakafanya mahojiano maswali yao yanakuwa HAYAJASHIBA. Utakuta wanamhoji Mnyika kwa maswali yale yale wanayomhoji BABA LEVO, Au maswali wanayomuuliza SHILOLE watamuuliza Halima Mdee.
Na maswali yenyewe tanakaa kikada sana
 
Mexicana, siku hizi kila ndege ikitoka kwa Wazungu na kutua KIA, mh. Waziri wetu wa utalii anatupa taarifa ya idadi ya wazungu!! Wazungu ni wazuri kuliko ‘WAJUMBE’!
Jibu murua kabisa..!!! Watu hawafikirii kwa undani wanapotia hoja zao...
 
Sasa imekuwa kama imehalalishwa vile kwa viongozi wa upinzani kuvikacha vyombo vya habari vya ndani na kukimbilia media za nje na za washindani wetu wa kiuchumi.

Alianza Zitto na zile fedha za kusaidia elimu ya watoto wa kike lakini kwa bahati nzuri WB wakamshushua na kumpuuza. Zitto aliitumia BBC badala ya media za ndani.

Sasa Tundu Lissu naye anayarudia makosa yaleyale, hivi kwanini mnakwepa media zetu?

Inakera sana.

Maendeleo hayana vyama!
Wanadhani huko ndo kuna wapiga kura! Tutakachowafanya 28 October watakuja kusimulia!
 
Wananguvu sana govt ya ccm wakawafingie KTN
johnthebaptist,

Umeamua kupost hii ili kutusanifu au unamaanisha kweli?

Media gani Mkubwa ya ndani iliyo na guts za kumwendea Tundu Lissu na kufanya naye mahojiano kuelezea SERA na MIPANGO yake kama akiwa Rais?

Ni mwandishi gani wa "Tanzania ya Magufuli " wa TV ama Redio anaweza kuwa "hajipendi" amuulize Tundu Lissu maswali kama aliyoulizwa na KTN na Majibu take kisha chombo chake na yeye mwenyewe visiweze kula "ban" kwa "uchochezi?"
 
Bongo kuna media gani kama sio utopolo tu yani Very unprofessional kama ITV
 
Usi
Kama mnatumia fedha na silaha kuwalazimisha wanahabari wa Kibongo kurusha maneno ya jiwe huku mkiwakataza kurusha habari za kumwambia ukweli huyo jiwe unadhani tufanye nini kama si kutumia vuombo vya nje!
Usikwepeshe maneno waambie ukweli serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania haipendi kukosolewa na chombo chochote Cha Cha habari kitakachofanya hivyo kesi za kishamba au kubambikiziwa Kodi zitamhusu wao wanataka kusikia magufuli apokewa na mabilioni ya wananchi chato au CCM yavuna wanachadema milioni 700 katavi.
 
Media za ndani zinawaminya wapinzani...kila wakizungumza live matangazo yanakatwa ,
 
Sasa imekuwa kama imehalalishwa vile kwa viongozi wa upinzani kuvikacha vyombo vya habari vya ndani na kukimbilia media za nje na za washindani wetu wa kiuchumi.

Alianza Zitto na zile fedha za kusaidia elimu ya watoto wa kike lakini kwa bahati nzuri WB wakamshushua na kumpuuza. Zitto aliitumia BBC badala ya media za ndani.

Sasa Tundu Lissu naye anayarudia makosa yaleyale, hivi kwanini mnakwepa media zetu?

Inakera sana.

Maendeleo hayana vyama!
Hivi vya ndani haviwezi kutangaza vitapingwa fine na TCRA kwa kukiuka maadili ya uandishi.
 
Chombo chetu cha umma ni tbc, wanaopelekea kutumiwa kwa vyombo vya nje ni hawa ccm kukihodhi
Vyombo gani vimebana.....Lisu na Zitto jana walikuwa mubashara ITV au unazungumzia vyombo gani bwashee?
 
Back
Top Bottom