Kwanini Watanzania na Tanzania ni masikini pamoja na rasilimali (resources) tulizonazo?
Tuna mlima wa pili kwa urefu Duniani baada ya Mount Everest tuna ziwa lenye kina kirefu zaidi Duniani, tuna Ziwa kubwa zaidi Duniani lenye maji baridi yaani fresh water, ni nchi ya tatu Duniani japo baadhi ya data zilizofichwa zinaonyesha kuwa Tanzania ni nchi ya kwanza Duniani kwa kuwa na madini mengi na ndio maana Tanzanite inapatikana Tanzania peke yake sisi ni nchi tajiri tubadilishe fikra we are a donor country
Mbona wananchi masikini wa kutupwa tatizo lipo wapi au Chadema na Act?
 
Tuna mlima wa pili kwa urefu Duniani baada ya Mount Everest tuna ziwa lenye kina kirefu zaidi Duniani, tuna Ziwa kubwa zaidi Duniani lenye maji baridi yaani fresh water, ni nchi ya tatu Duniani japo baadhi ya data zilizofichwa zinaonyesha kuwa Tanzania ni nchi ya kwanza Duniani kwa kuwa na madini mengi na ndio maana Tanzanite inapatikana Tanzania peke yake sisi ni nchi tajiri tubadilishe fikra we are a donor country
Utajiri anaoweza kujivunia mwanadamu ni ule unaotokana na matumizi ya akili, weledi na nguvu zake katika kuyatumia mazingira aliyopo kujitengenezea utajiri, siyo kwa vile unavyovikalia.

Sisi ni maskini kwa sababu vyote ulivyovitaja siyo mazao ya akili, juhudi au weledi wetu.

Halafu huko kwenye madini umedanganywa sana. Hatuwezi kuingia hata kwenye top 20 ya nchi zenye madini mengi na aina nyingi. Tanzania siyo madini ya ajabu. Tanzania ni sapphire yenye vanadium. Sapphire zisizo na vanadium zinapatikana mataifa mengi.

Nchi zenye viwango vikubwa vya madini na madini aina nyingi katika Dunia ni:

1. CHINA
2. CANADA
3. USA
4. RUSSIA
5. AUSTRALIA
6. DRC
7. BRAZIL
8. SAUD ARABIA
9. INDIA
10. NIGER
11. VENEZUELA
12. DRC
13. NAMIBIA

Katika Africa, Tanzania haipo hata katika top 5. Katika Afrika nchi 5 zenye madini mengi kwa kiasi na aina ni
1) Niger
2) Namibia
3) DRC
4) Zambia
5) South Africa


Utajiri mkubwa upo kichwani na siyo ardhini. Itazame Japan, Switzerland, Holand, Belgium.

Tunatakiwa kujiuliza kwenye ulimwengu ambao utajiri hutegemea akili, weledi, juhudi na teknolojia, what is our uniquiness?

Mapato ya Belgium kwa mwaka ni sawa na mapato ya nchi zote za Africa ukiyaweka pamoja.
 
Bams,
Kuishia kutaja vitu tulivyonavyo ardhini hakutusaidii, tunatakiwa kuwekeza kwenye human resource ambao tutawawekea mikakati ya kubadilisha hivyo vitu vilivyo ardhini kuwa pesa. Wajapan, wamarekani, wachina etc wametupiga bao hapo. Waafrika tuansoma kwenye vitabu elimu tunaiacha humo tunaenda kupika vitumbua. Chemistry unafundishwa hujui hata matumizi ya calcium carbonate!
 
Dogo usijisumbue na ma theory ya ajabu ajabu....jibu analo D. Trump anatujua vizuri kwamba sisi ni shithole
Ili tuendelee tunahitaji mambo sita Watu , Ardhi,Siasa Safi,Uongozi bora,Mzungu na kumfufua Mganga aliyetuloga
 
thats a very easy question: jibu lake ni rahisi sana🙂 EDUCATION )

sio elimu hii ya ubishani but serious education: watu waongee mada kama wana elimu ya kutaka kusogea kwenda apa mpaka pale, pitia majukwaa mengi duniani nchi zilizoendelea, stakeoverflow: quora, stake exchange wanajadili matatizo na masuluhisho sisi tunajadili ulishawahi kula tunda kimasihara? kweli tutasogea: uchaguzi ulishaisha watu bado wanapiga kampeni, where in the world do people do this?
 
Dogo usijisumbue na ma theory ya ajabu ajabu....jibu analo D. Trump anatujua vizuri kwamba sisi ni shithole
Ili tuendelee tunahitaji mambo sita Watu , Ardhi,Siasa Safi,Uongozi bora,Mzungu na kumfufua Mganga aliyetuloga

uongozi gan unataka? watu wanapiga kazi hawafuatilii chama wala mgombea, bitcoin haina serikali we bado unaongelea uongozi
 
Kikubwa kwa swala la kuondokana na umaskini ni watu wote nchini kutambua wajibu wao lakini pia ni vyema vijana wakapewa nafasi au serikali ikafikilia na kuwa na mpango na kuwekeza nguvu kwa vijna kwani hao ndio nguvu kazi kwa taifa.
Na kuhusu swala lamalighafi zilizopo nchini hizo ni fursa nzuri hasa kwa kwa wasomi wanao maliza na walio maliza lakini pia hata kwa vijna wengine waliopo mtaani. Kwani sikazi zote zinaitaji wasomi hata ambao wapo mtaani zinawafaa kikubwa ni imani kuwepo kwa wataalamu wa ndani kwani hao ndio waliochaguliwa na kuonekana wanasifa...kama wakiaminiwa wana nafasi kubwa ya kuleta mabadiliko
 
Tuna rasilimali lakini hatuna wajasiriamali. Ah yes I know; unaweza ukalaumu mfumo na ukalaumu sheria na ukalaumu mazingira, ukalaumu siasa, ukalaumu mvua, ukamlaumu mkeo/mmeo blah blah blah... The blame game... so easy to play... actually everyone can play it. But solving real world problems? Oh boy... it is for the few; leaders (Definitely not bosses), ambitious, positive minded, persistent, proactive - entrepreneurs. They don't fight a system, they fight in the system.. they don't complain about unfriendly environment/ gvt/ whatever, they innovate, they adapt, they improvise and they deliver under those unfriendly 'factors'. Tunahitaji wajasiriamali wa kweli wa kutosha, na nchi itabadilika ndani ya muda mfupi sana (kiuchumi).Eee si ndio? Asa kumbe nini.

Nchi zilizoendelea zinapalilia sana utamaduni wa Ujasiriamali - kwasababu siku zote mjasiriamali analitazama tatizo kama fursa, anatafuta solution, anapiga pesa... win win situation; yeye na timu yake wanafaidika, nchi inafaidika. Haijalishi ni tatizo gani... nini, rushwa? kwake ni fursa, kwasababu akileta suluhisho la kibunifu la kuondoa rushwa manaake anakuwa milionea! Which makes me believe that saivi tunavyoongea kuna mjasiriamali yuko mahali fulani anabuni solution ya rushwa... and soon tutaisikia na tutabaki tunajiuliza tulishindwa nini kufikiria hicho kitu kabla yake. Wajasirimali ni problem solvers, they never blame anyone. Ni watendaji, wanafanya vitu, tunaona matokeo - mabadiliko yanatokea.

Unawachukulia poa wajasirimali eh? Well, labda hujajua ..FYI hizi ni baadhi tu ya kampuni zilizoanzishwa na wajasiriamali walioamua kutatua changamoto walizoziona kwa wakati huo na wanaendelea kufanya hivyo. What is more interesting ni kwamba hivi sasa wanatatua hadi changamoto za wakati ujao he he he😜😉 Na haya ni mapato yao kwa mwaka uliopita;

FACEBOOK REVENUE (2019) = $17.65 billion
GOOGLE REVENUE (2019) = $ 40.3 billion
AMAZON REVENUE (2019) = $70.0 billion
*Source: Statista

Kumbuka; hizi kampuni nilizoziorodhesha hapa hazina migodi, wala mbuga, wala mashamba, wala makinikia, wala Mlima Kilimanjaro, wala gesi, wala mafuta, wala hazina jeshi lake, wala mahakama zake, wala bunge lake, wala... you name it. Nchi ya Marekani inapata kodi kubwa sana toka kwa haya makampuni. Ajira zinazozalishwa na haya makampuni ndo usiseme... mpaka huku kwetu. Can you see it's ripple effect? Sasa BUDGET YA NCHI ya Tanzania (2019/2020) ni USD 14.3 billion, ina maana kampuni ya FACEBOOK peke yake ina mapato zaidi ya mapato tarajiwa ya nchi ya Tanzania. Naomba nikuulize wewe mwenzangu, Facebook wanauza nini? Google wanauza nini? Labda Amazon, lakini je, wanachokifanya ni rocket science? ....Ivi sijui kuna mtu ananielewa?

I wish vijana tungeacha staili ya wazee wetu ya kukimbilia kutafuta wa kumlaumu kwa kila kitu. Let us take the responsibility, the future is in our hands. Umaskini tumeukuta, sio kosa letu. Lakini kama umaskini utaendelea ni kwasababu tunaacha kuwa watendaji tunakazana kuwa 'walaumuji'(blamers) na tunatarajia kuwa kuna mtu kutoka tusikokujua atakuja kurekebisha mambo. Na nchi hii ina wasomi wengi tu tunaowajua simply kwasababu wanajinadi na PhD zao, masters sijui na mbwembwe kibao - ila matokeo ya hizo ndude zao ndo hatuyaoni - ivi ndugu wasomi mnakwama wapi?🤔🤔🤔 Ah hapana, siwalaumu.. najaribu kuwaza kwa sauti teh teh teh teh tiiiiih!

Kabla hujamlaumu mtu jiulize; (Wewe) Umetimiza wajibu wako katika nafasi yako? Je, unafanya nini kuondoa changamoto zinazosababisha umasikini uendelee kuwepo kwako binafsi kwa kuanzia, kisha kwa familia, halafu jamii inayokuzunguka na hatimaye taifa.

Enough talk, let's get to work - find solutions.

Naomba kuwasilisha.
 
Tatizo tuna umaskini wa vitabuni wa kuandikiwa na watu wasiotujua, hatuandiki yetu wenyewe , tuna copy na ku-pasty ngonjela nyiingi, tena tunapewa na yule anayetufanya tuwe maskini. sipendi hizi fikra! njoo na chako kama kijana msomi Mwafrica km ifuatavyo;

Si kweli watanzania hatujakumbwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe, mpaka leo tunayo hiyo vita, Burundi, Rwanda, Zaire, Somalia, S/ Sudan, Zimbabwe, Msumbiji, Ethiopia ni vita yako wewe Mtanzania uliyeleta huu uzi Hapa funguka, inakuhusu mazimaa!

Mfano rahisi kwa wagumu wa kuelewa Una amani gani dada yako wanapigana na mumewe hawana chakula hawazalishi chochote zaidi ya kuzozana? watoto wake wanakuja kwako ili mgawane kilichopo? utatajirika kweli?

Kinyume na hayo yoote hapo juu sisi ni matajiri ni ile mbaya, tumejitahidi sana, tatizo la watu wenye fikra Mgando wanataka wawe kama N/york, wako vile kwa sababu ya physical and Body Morphology yao inawaruhusu wawe vile! na sisi tuwe hivi!
wao wakituiga wanakufa kama kuku, sisi tukiwaiga hatufi! ivo kupelekea kuwatamani!

Hayo yoote uliyoorodhesha Madini,Chuma sijui utalii! utamuuzia nani Africa hii, zaidi ya kumuuzia adui yako,Anapandisha bei uyeye na kushusha bei yeye, anaye fanya ndugu zako majirani wapigane? si atachukua bure tu!

Unataja Madini ya thamani meengi ki-kasuku, thamani ipi? utaifanyia nini chenye tija hapa Africa,wasomi kabisa mnawaza kuuza tuu, mtumie, sijui mle baasi. Innovation = 0.

Hivi unajua unapotembea/gari kutoka mbagalla mpaka city centre, unazalisha Mega watts kibao! hapo mpaka mzungu aje akwambie! Hayo yote ulotaja wamewaambia wao, siyo wazo lenu hata wakiondoka leo wakiacha mashine zao na kila kitu, mtaenda kutega bakulri tu.

Ningekuona wa maana kama ungesema tufanyeje ili hizi Mali zetu tuuziane Africans, wenyewe kwa wenyewe! na kwa faida .

Ajabu sasa wasomi wengi ukiwauliza kazi ya Gold ni nini? hawajui zaidi ya Mikufu na Pete!

Hapa tulipo tumejitahidi sana, sisi siyo Maskini, tukiachwa na chokochoko za weupe tungekuwa mbali zaidi yao, na siyo lazima tuvumbue kama wao tungekuja na yetu mapya zaidi, mfano wao wangefanikiwa kwenda Mars sisi tungekwenda kwenye jua kabisaaa! sema tu Mungu amekuchapa kofi,

UFISADI;
Wanajamii ndo mafisadi wakubwa ikiwa ni pamoja na wewe! bila kuwaunga mkono hao wezi na kuwapa heshima wasingeiba, jamii yenu inaheshimu sana mwenye nacho, sasa je kwa nini nisiibe na mali inapita mikononi mwangu?

By the way Lazima aishi kifalme ili kututia moyo wananchi kuwa kumbe tuna Mali za kutosha na tuzalishe zaidi kwa kumpa hela inayo kidhi mahitaji yake ya msingi. kama huduma yake kwa umma inaridhisha.

Kama kiongozi anakuwa ombaomba inakatisha tamaa! hayo ni ya kiafrica zaidi, achana sijui na nanai wa nani alisema!
 
Tuna rasilimali lakini hatuna wajasiriamali. Ah yes I know; unaweza ukalaumu mfumo na ukalaumu sheria na ukalaumu mazingira, ukalaumu siasa, ukalaumu mvua, ukamlaumu mkeo/mmeo blah blah blah... The blame game... so easy to play... actually everyone can play it. But solving real world problems? Oh boy... it is for the few; leaders (Definitely not bosses), ambitious, positive minded, persistent, proactive - entrepreneurs. They don't fight a system, they fight in the system.. they don't complain about unfriendly environment/ gvt/ whatever, they innovate, they adapt, they improvise and they deliver under those unfriendly 'factors'. Tunahitaji wajasiriamali wa kweli wa kutosha, na nchi itabadilika ndani ya muda mfupi sana (kiuchumi).Eee si ndio? Asa kumbe nini.

Nchi zilizoendelea zinapalilia sana utamaduni wa Ujasiriamali - kwasababu siku zote mjasiriamali analitazama tatizo kama fursa, anatafuta solution, anapiga pesa... win win situation; yeye na timu yake wanafaidika, nchi inafaidika. Haijalishi ni tatizo gani... nini, rushwa? kwake ni fursa, kwasababu akileta suluhisho la kibunifu la kuondoa rushwa manaake anakuwa milionea! Which makes me believe that saivi tunavyoongea kuna mjasiriamali yuko mahali fulani anabuni solution ya rushwa... and soon tutaisikia na tutabaki tunajiuliza tulishindwa nini kufikiria hicho kitu kabla yake. Wajasirimali ni problem solvers, they never blame anyone. Ni watendaji, wanafanya vitu, tunaona matokeo - mabadiliko yanatokea.

Unawachukulia poa wajasirimali eh? Well, labda hujajua ..FYI hizi ni baadhi tu ya kampuni zilizoanzishwa na wajasiriamali walioamua kutatua changamoto walizoziona kwa wakati huo na wanaendelea kufanya hivyo. What is more interesting ni kwamba hivi sasa wanatatua hadi changamoto za wakati ujao he he he😜😉 Na haya ni mapato yao kwa mwaka uliopita;

FACEBOOK REVENUE (2019) = $17.65 billion
GOOGLE REVENUE (2019) = $ 40.3 billion
AMAZON REVENUE (2019) = $70.0 billion
*Source: Statista

Kumbuka; hizi kampuni nilizoziorodhesha hapa hazina migodi, wala mbuga, wala mashamba, wala makinikia, wala Mlima Kilimanjaro, wala gesi, wala mafuta, wala hazina jeshi lake, wala mahakama zake, wala bunge lake, wala... you name it. Nchi ya Marekani inapata kodi kubwa sana toka kwa haya makampuni. Ajira zinazozalishwa na haya makampuni ndo usiseme... mpaka huku kwetu. Can you see it's ripple effect? Sasa BUDGET YA NCHI ya Tanzania (2019/2020) ni USD 14.3 billion, ina maana kampuni ya FACEBOOK peke yake ina mapato zaidi ya mapato tarajiwa ya nchi ya Tanzania. Naomba nikuulize wewe mwenzangu, Facebook wanauza nini? Google wanauza nini? Labda Amazon, lakini je, wanachokifanya ni rocket science? ....Ivi sijui kuna mtu ananielewa?

I wish vijana tungeacha staili ya wazee wetu ya kukimbilia kutafuta wa kumlaumu kwa kila kitu. Let us take the responsibility, the future is in our hands. Umaskini tumeukuta, sio kosa letu. Lakini kama umaskini utaendelea ni kwasababu tunaacha kuwa watendaji tunakazana kuwa 'walaumuji'(blamers) na tunatarajia kuwa kuna mtu kutoka tusikokujua atakuja kurekebisha mambo. Na nchi hii ina wasomi wengi tu tunaowajua simply kwasababu wanajinadi na PhD zao, masters sijui na mbwembwe kibao - ila matokeo ya hizo ndude zao ndo hatuyaoni - ivi ndugu wasomi mnakwama wapi?🤔🤔🤔 Ah hapana, siwalaumu.. najaribu kuwaza kwa sauti teh teh teh teh tiiiiih!

Kabla hujamlaumu mtu jiulize; (Wewe) Umetimiza wajibu wako katika nafasi yako? Je, unafanya nini kuondoa changamoto zinazosababisha umasikini uendelee kuwepo kwako binafsi kwa kuanzia, kisha kwa familia, halafu jamii inayokuzunguka na hatimaye taifa.

Enough talk, let's get to work - find solutions.

Naomba kuwasilisha.
Yaani wewe,umenikuna kipele! sijui kama ni ''me'' au ''ke'' but kwa mujibu wa Avatar ni ''ke'' Nimekupenda bure usilipe chochote sema unachotaka, ntalipa mimi binafsi
 
Wambandwa,
Samahani sijasoma andiko kwa kuwa nipo Job ila mtambo wa kuwafukarisha watanzania na Tanzania ni Ccm,ni bahati mbaya kwamba watanzania either hawauelewi ukweli huu au wanauelewa ila wameamua kujitoa ufahamu at their own expense,

JK pia alijaribu kuwaonesha ukweli huu indirect kwamba ccmhaiwezi kumtoa mkwere kwenye lindi la ufukara unaowakabili but either kwa ujinga wao au kwa kujitoa ufahamu wakagoma kumuelewa na ndo maana magufuli anajaribu kuharibu kila kitu kinachoweza kuwaamusha usingizini ili hawa wanaoitwa wanyonge waendelee kubaki gizani au kwenye usingizi totoro kwa faida ya mtesi wao CCM
 
Nguvu kama ujui ni kwamba nchi imethibitiwa na failures wa form IV, ambao wamejiendeleza kiujanjajaja kila sekta sasa Ubuntu wautoa wapi
 
Mfumo Wa ujamaa ndio umetuletea mawazo ya kimasikini rejea awamu ya kwanza nyerere akupenda watu wamiliki mali na kuwaaminisha watu utajiri ni ubepari na unyonyaji
 
Rasilimali zote zinazostahili kuondoa taifa letu kwenye dimbwi la umaskini zipo za kutosha.
Mfano:
Ardhi yenye rutuba ipo
Watu wasomi na wasio wasomi wapo wa kutosha
Mbuga za wanyama zinazovutia ulimwengu mzima zipo
Bahari kwa samaki na usafirishaji ipo
Maziwa na mito yenye maji safi na samaki nyingi yapo
Rasilimali zingine ..... ongezeeni.............

Watanzania tunakwama wapi?

Kuna kitu muhimu sana watanzania tumejaliwa tunu ya amani, hapa ndipo waga nakubali juhudi za tawala zetu zote kuanzia Mwl. Nyerere (nampongeza sana maana yeye ndo mwanzilishi)
Tuna central command moja tu bila shaka yoyote (hapa nitaeleza ski nyingine)

Tunaelekea uchaguzi mkuu, naomba tufunguke ili ikiwezekana vyama na wagombe waweze kuchukua maoni yetu na kuyaweka kwenye ilani zao ili hatimaye tuanze safari ya kuutokomeza umaskini na kufanya Tanzania kuwa taifa lenye ukanda huu wa Sub- Saharani Africa.
Landson Tz
 
Tanzania iuzwe yote tugawane hela kila mtanzania (sijui bado atakuwepo) atakuwa tajiri!

Maana Noah zetu ziliyeyuka!
 
Back
Top Bottom