Kwanini Watanzania na Tanzania ni masikini pamoja na rasilimali (resources) tulizonazo?
hivi kama baba mwenye nyumba kasema hajui! wewe mtoto utajuaje?
 
(1) watu wanajituma sana ila mshahara laki moja
(2) usipochanga kwa wenzio, nani atakuchangia ya kwako?
(3) watu wanatunza hela ila benki hakuna faida. unaweka milioni tano benki kwa mwaka unapata riba chini 4.5%, si haki
(4)malengo yapo sana, mtaji hakuna. mkopo mpaka uwe na mali isiyohamishika au hati.
(5) hahahahahaha...
(1)Fanya kazi kwa kujituma utauondoa umasikini kwenye maisha yako.
(2)chunga matumizi ya fedha unazopata.acha matumizi yasiyo ya lazima mfano
pombe kuhonga sherehe zisizo na ulazima n.k
(3)anza utamaduni wa kuweka akiba benki.
(4)Jiwekee malengo ya kuanzisha mradi.
(5)Acha nasema acha kulaumu upande mwingine kwamba umekusababishia umaskini bado mtanzania una nafasi kubwa ya kuhama toka kwenye umaskini zingatia hatua hizi tano nilizokupa.asante kwa kusoma paragraph hizi.
 
Uchu wa kujilimbikizia mali wa viongoz wetu na kukosa akili ya maendeleo ndo kitu kinacho turudisha nyuma,angalia jinsi mataifa mengine wanavyotamani nchi ka tanzania,lakin viongoz wa nchi hii wamejaa tamaa na dhiki la pesa kiasi cha kudirik kuziuza maliasiri za nchi.umaskin tunautaka wenyewe kwa kutojiamin na kupenda kufanya kazi mfano VIJANA wa siku hizi kufanya kazi ni tatizo kubwa lakin starehe wako mbele sana,kuanzia viongoz wa nchi hadi vijana tunapenda mtelemko.
 
hivi kama baba mwenye nyumba kasema hajui! wewe mtoto utajuaje?

Kama baba ameshakuwa zoba ndio inabidi watoto mchangamke sasa, la sivyo mnaoumia ni watoto. Hivyo tujadiliane hapa ili tukijua chanzo hasa ni rahisi kila mtu kucheza upande wake.
 
Uchu wa kujilimbikizia mali wa viongoz wetu na kukosa akili ya maendeleo ndo kitu kinacho turudisha nyuma,angalia jinsi mataifa mengine wanavyotamani nchi ka tanzania,lakin viongoz wa nchi hii wamejaa tamaa na dhiki la pesa kiasi cha kudirik kuziuza maliasiri za nchi.umaskin tunautaka wenyewe kwa kutojiamin na kupenda kufanya kazi mfano VIJANA wa siku hizi kufanya kazi ni tatizo kubwa lakin starehe wako mbele sana,kuanzia viongoz wa nchi hadi vijana tunapenda mtelemko.
Kujilimbikizia mali kwa viongozi ndio chanzo kikuu cha umasikini wa mamilioni ya watanzania?

Unafikiri ni nini kinasababisha watu wapende mteremko?
 
Watanzania ni maskini kutokana mambo makuu yafuatayo; Elimu, Siasa, Rushwa, Uongozi na idadi ya watu. Nitayajadili haya mambo makuu matano kila moja kwa nafasi yake.

Elimu ina mchango mkubwa sana wa kumtoa mtu kwenye umaskini. watanzania tutabaki kuwa maskini mpaka pale kwanza tutakapobadili mfumo wetu wa elimu na kuwa na elimu ya ushindani, elimu ya kujitambua, elimu itakayoweza badili mfumo wetu wa fikra. Elimu ya sasa ni elimu inayomwekea mazingira yule anayeipata ashindwe kujitambua yuko kwenye mazingira gani na afanye nini ili atoke pale alipo.

Mifano iko wazi sana, utaona mtu yuko tayari kutaja kiwango chetu cha elimu kwa majigambo bila kuweza kusema kiwango chake cha elimu kimemsaidiaje au amefanya nini kuikwamua Tanzania kutoka kwenye umasikini. Hii ni hatari sana kwa msomi kutokutambua elimu inamsaidiaje. Kuna wanaoitwa wasomi nchi akiliongelea au kulichambua jambo unaashindwa kupata tofauti ya mtazamo wake na yule kijana mchunga ng'ombe wa kule kijijini kwetu ......... . Kuna mwanaharakati mmoja wa India alishawahi sema kwamba kama elimu kama haijaijngia kwenye ufahamu wako, moyoni mwako na kubadili vile unavyofikiri na mtazamo wa dunia basi elimu hiyo haina tofauti na joho ulilolivaa asubuhi siku yako ya maafali na kulivua jioni yake.

Kiongozi wa Indonesia alishwahi kusema Afrika tunasoma tusivyovihitaji na tunavihitaji vitu tusivyovisomea. Indosea ilipata uhuru wake miaka karibu sawa na Tanzania lakini tazama leo wako wapi.

Siasa imetoa mchango mkubwa sana kwenye kufanikisha nchii inakuwa masikini mpaka leo. Ni wanasiasa wanaoshiriki kutunga kanuni na sheria za nchi. Wanatunga sheria ambazo zinazomkandamiza mtanzania asipate elimu itakayoweza kumfumbua macho au kupata ufahamu wa kujitambua ni mazingira gani anayoishi au yanayomzunguka. Kwa wasomi waliowengi wanaona njia pekee ya kujikomboa ni siasa inafanya mpaka wanasahau kuwa taaluma yao inaweza leta tofauti kimaisha. Wanasiasa mejitengenezea mazingira kwamba maendeleo ya nchi au sehemu hayawezi kuja bila kupitia wao na mbaya zaidi hii imekaa kwenye ufahamu wa watanzania walio wengi na kuwaona wanasiasa ni mungu watu.

Unaposikia mwanasiasa anaizungumzia Tanzania wenye fikra tunajua hali ni mbaya. Wanayozungumza kama Tanzania haina wenyewe, Tanzania ni kama mkate wa bofro basi wanastahili kugawana na yeyote Yule anayekuja kumuomba. Na mbaya zaidi ni wanasiasa ni wale wale, majina ni yale yale mawazo ni yale yale vina "mutate" tangu nchi hii inapata uhuru, hivyo unazani lini tutatoka kwenye umasikini.

Rushwa imechangia kwa kiasi kikubwa nchi kuwa maskini kwa kiasi hiki. Rushwa imekuwa ni tamaduni kwetu na kufanya swala uaminifu lisiwepo kabisa au lisipate nafasi kwenye mitazamo yetu ya ukombozi wa kimaisha. Hakuna sehemu yenye haki kila kona lazima utoe fedha ili mambo yaende hii ni kansa na inarudisha sana nyuma maendeleo ya nchi hii.

Uongozi bado tatizo kubwa kwenye nchi nyingi maskini za kiafrika. Watu wanaacha majukumu yao ya kuhudumia wananchi badala yake wanajinufaisha wao na familia zao. Tanzania tunaenda kupata katiba mpya lakini swala la kujiuliza ni muongozo gani mpya utakaotolewa na katiba utakao weza badili mfumo wa uongozi wa nchi hii kujikwamua kutoka kwenye janga la umasikini.

Katiba ni kama msingi tu wakufanya yaliyosahihi na kila kiongozi anakuja na ilani yake je ni mangapi yaliyotengenezeka kwenye hizo ilani zao iwe wawepo madarakani au wasiwepo madarakani.

Idadi ya watanzania walio wengi ni vijana je vijana wanatambuaje umuhimu wao kwa taifa hili. Kuna vijana wengi wamesomi ila siasa za nchi hii zimewafanya kusahau umuhimu wao kwenye nchi yao. Dini imekuwa kama ndiyo mkate na siagi wakati hivi vitu tumeletewa tu havikuanzia Tanzania. Unakuta vijana wanalumbana wewe muislamu! wewe mkristo! lakini wanashindwa kutambua wao ni watanzania sasa busara iko wapi hapo?

Tunaambiwa vijana ni taifa la kesho lakini matendo tunayoyapa mkazo kwenye maisha yetu ya kila siku yanawafanya wanasiasa waamini kuwa hatuko tayari hata kwa hiyo kesho. Tazama wastani wa umri wa viongozi wa Afrika linganisha na wastani wa nchi zilizoendelea utaona tofauti unajieleza wazi kuwa hatuthaminiwi na kutokana na kutojithamini sisi wenyewe.

Utathaminiwa kama na wewe unajithamini lakini kutwa nzima unakaa kupiga soga tu la siasa na dini nani atakukabithi majukumu hata ya uongozi wa wilaya ukiachilia mbali ya nchi. Tunapenda mambo ambayo hayana thamani kwetu wala kwa nchi yetu. Kama kila kijana angeamuwa kufanya kidogo kwa nchi hii Tanzania ingekuwa mbali sana. Mother Teresa "you do not have to do great things, do small things in a great way". Lakini tunategemea serikali tu ndiyo mkombozi wetu, hata kwenye vitu vidogo tu unasikia "tunaomba serikali itufanyie ......" ni up. umba .vu wa kutojitambua.
Tubadili mitazamo yetu tuanze kuiondoa ile sumu na kasumba tunayopandikiziwa na wanasiasa. Tuanzishe mijadala ya ufumbuzi wa matatizo ya nchi yetu, tunafanyaje ili tutoke hapa tulipo. Mfano mdogo huu uzi haujafika hata page kumi sababu hauna siasa au dini hivyo wao hauwahusu. Ni hatari sana, ni hatari sana

Hizi ndizo sababu kuu zinazotufanya tuwe maskini kwa mtazamo wangu. Lakini Mwl. Nyerere aliwahi kusema " It can be done play your part".
 
Ni maskini kwa sababu:-
1: viongozi hawajitambui kwanini wao ni viongozi.
2: mfumo wetu wa elimu unatuburuza na sio challenging. Unatuandaa ndivyo sivyo (kuajiriwa).
3: mgawanyo wa rasilimali sio sawa kwani hauna vipaumbele na vinavyopangwa ni changa la macho.
3: sheria zinazotungwa ni kwa kuwalinda watawala hata kama ni wevi kama walivyo sasa.
4: umbumbu wa watawala waliopo juu ya sekta wanazoziongoza.
5: wizi wa pesa zetu na usimamizi mbovu wa rasilimali zilizopo kwa kuwapa wageni wakwepa kodi.
6: serikali kutokukusanya kodi kikamilifu na hasa kwenye majumba ya kupangisha kama ilivyo kwa nchi nyinginezo.
7:siasa chafu zilizojaa rushwa kwa kuwa wagombea ni wale walioshindwa kwenye madarasa yao na mifano ipo (mulugo).
Sababu ni nyingi but raia wapewe elimu ya uraia ili wajikomboe toka kwa manyang'au haya.
 
mwenzako anapeleka sokoni iphone5 we unapeleka kahawa, hamuwezi mkawa sawa, f*ck kilimo kwanza, mwendo technology kwanza
 
Tushazoea vya bure hatupendi jituma,hatupendi jaribu na hata tukijaribu 99.9% watakukatisha tamaa,hata serikal yetu haiko tayar kuwasaidia vijana...wanajal matumbo yao,ni heri uongoz wapewe wanaojua sias na uchumi pia wawe matajiri
 
...mkuu sisi tutajuaje wakati mkuu wa kaya mwenyewe hajui...
 
Watanzania ni maskini kutokana mambo makuu yafuatayo; Elimu, Siasa, Rushwa, Uongozi na idadi ya watu. Nitayajadili haya mambo makuu matano kila moja kwa nafasi yake.

Elimu ina mchango mkubwa sana wa kumtoa mtu kwenye umaskini. watanzania tutabaki kuwa maskini mpaka pale kwanza tutakapobadili mfumo wetu wa elimu na kuwa na elimu ya ushindani, elimu ya kujitambua, elimu itakayoweza badili mfumo wetu wa fikra. Elimu ya sasa ni elimu inayomwekea mazingira yule anayeipata ashindwe kujitambua yuko kwenye mazingira gani na afanye nini ili atoke pale alipo.

Mifano iko wazi sana, utaona mtu yuko tayari kutaja kiwango chetu cha elimu kwa majigambo bila kuweza kusema kiwango chake cha elimu kimemsaidiaje au amefanya nini kuikwamua Tanzania kutoka kwenye umasikini. Hii ni hatari sana kwa msomi kutokutambua elimu inamsaidiaje. Kuna wanaoitwa wasomi nchi akiliongelea au kulichambua jambo unaashindwa kupata tofauti ya mtazamo wake na yule kijana mchunga ng'ombe wa kule kijijini kwetu ......... . Kuna mwanaharakati mmoja wa India alishawahi sema kwamba kama elimu kama haijaijngia kwenye ufahamu wako, moyoni mwako na kubadili vile unavyofikiri na mtazamo wa dunia basi elimu hiyo haina tofauti na joho ulilolivaa asubuhi siku yako ya maafali na kulivua jioni yake.

Kiongozi wa Indonesia alishwahi kusema Afrika tunasoma tusivyovihitaji na tunavihitaji vitu tusivyovisomea. Indosea ilipata uhuru wake miaka karibu sawa na Tanzania lakini tazama leo wako wapi.

Siasa imetoa mchango mkubwa sana kwenye kufanikisha nchii inakuwa masikini mpaka leo. Ni wanasiasa wanaoshiriki kutunga kanuni na sheria za nchi. Wanatunga sheria ambazo zinazomkandamiza mtanzania asipate elimu itakayoweza kumfumbua macho au kupata ufahamu wa kujitambua ni mazingira gani anayoishi au yanayomzunguka. Kwa wasomi waliowengi wanaona njia pekee ya kujikomboa ni siasa inafanya mpaka wanasahau kuwa taaluma yao inaweza leta tofauti kimaisha. Wanasiasa mejitengenezea mazingira kwamba maendeleo ya nchi au sehemu hayawezi kuja bila kupitia wao na mbaya zaidi hii imekaa kwenye ufahamu wa watanzania walio wengi na kuwaona wanasiasa ni mungu watu.

Unaposikia mwanasiasa anaizungumzia Tanzania wenye fikra tunajua hali ni mbaya. Wanayozungumza kama Tanzania haina wenyewe, Tanzania ni kama mkate wa bofro basi wanastahili kugawana na yeyote Yule anayekuja kumuomba. Na mbaya zaidi ni wanasiasa ni wale wale, majina ni yale yale mawazo ni yale yale vina "mutate" tangu nchi hii inapata uhuru, hivyo unazani lini tutatoka kwenye umasikini.

Rushwa imechangia kwa kiasi kikubwa nchi kuwa maskini kwa kiasi hiki. Rushwa imekuwa ni tamaduni kwetu na kufanya swala uaminifu lisiwepo kabisa au lisipate nafasi kwenye mitazamo yetu ya ukombozi wa kimaisha. Hakuna sehemu yenye haki kila kona lazima utoe fedha ili mambo yaende hii ni kansa na inarudisha sana nyuma maendeleo ya nchi hii.

Uongozi bado tatizo kubwa kwenye nchi nyingi maskini za kiafrika. Watu wanaacha majukumu yao ya kuhudumia wananchi badala yake wanajinufaisha wao na familia zao. Tanzania tunaenda kupata katiba mpya lakini swala la kujiuliza ni muongozo gani mpya utakaotolewa na katiba utakao weza badili mfumo wa uongozi wa nchi hii kujikwamua kutoka kwenye janga la umasikini.

Katiba ni kama msingi tu wakufanya yaliyosahihi na kila kiongozi anakuja na ilani yake je ni mangapi yaliyotengenezeka kwenye hizo ilani zao iwe wawepo madarakani au wasiwepo madarakani.

Idadi ya watanzania walio wengi ni vijana je vijana wanatambuaje umuhimu wao kwa taifa hili. Kuna vijana wengi wamesomi ila siasa za nchi hii zimewafanya kusahau umuhimu wao kwenye nchi yao. Dini imekuwa kama ndiyo mkate na siagi wakati hivi vitu tumeletewa tu havikuanzia Tanzania. Unakuta vijana wanalumbana wewe muislamu! wewe mkristo! lakini wanashindwa kutambua wao ni watanzania sasa busara iko wapi hapo?

Tunaambiwa vijana ni taifa la kesho lakini matendo tunayoyapa mkazo kwenye maisha yetu ya kila siku yanawafanya wanasiasa waamini kuwa hatuko tayari hata kwa hiyo kesho. Tazama wastani wa umri wa viongozi wa Afrika linganisha na wastani wa nchi zilizoendelea utaona tofauti unajieleza wazi kuwa hatuthaminiwi na kutokana na kutojithamini sisi wenyewe.

Utathaminiwa kama na wewe unajithamini lakini kutwa nzima unakaa kupiga soga tu la siasa na dini nani atakukabithi majukumu hata ya uongozi wa wilaya ukiachilia mbali ya nchi. Tunapenda mambo ambayo hayana thamani kwetu wala kwa nchi yetu. Kama kila kijana angeamuwa kufanya kidogo kwa nchi hii Tanzania ingekuwa mbali sana. Mother Teresa "you do not have to do great things, do small things in a great way". Lakini tunategemea serikali tu ndiyo mkombozi wetu, hata kwenye vitu vidogo tu unasikia "tunaomba serikali itufanyie ......" ni up. umba .vu wa kutojitambua.
Tubadili mitazamo yetu tuanze kuiondoa ile sumu na kasumba tunayopandikiziwa na wanasiasa. Tuanzishe mijadala ya ufumbuzi wa matatizo ya nchi yetu, tunafanyaje ili tutoke hapa tulipo. Mfano mdogo huu uzi haujafika hata page kumi sababu hauna siasa au dini hivyo wao hauwahusu. Ni hatari sana, ni hatari sana

Hizi ndizo sababu kuu zinazotufanya tuwe maskini kwa mtazamo wangu. Lakini Mwl. Nyerere aliwahi kusema " It can be done play your part".

Asante sana mkuu kwa mchango wako ulioshiba. Ulisema utarudi na umerudi kweli. Kila uliloongea ni kweli tupu na ushahidi uko wazi kabisa.
Napenda vijana tuchukue hatua ya kuwa sehemu ya suluhisho la matatizo haya. Napendelea tuwe tunaweka nyuzi nyingi za aina hii ili tuendelee kufunguana.
Tusiishie tu kushabikia siasa na kurusha lawama, hebu kila mtu afanye lile lililopo chini ya uwezo wake.

AMKA MTANZANIA.
 
Ni maskini kwa sababu:-
1: viongozi hawajitambui kwanini wao ni viongozi.
2: mfumo wetu wa elimu unatuburuza na sio challenging. Unatuandaa ndivyo sivyo (kuajiriwa).
3: mgawanyo wa rasilimali sio sawa kwani hauna vipaumbele na vinavyopangwa ni changa la macho.
3: sheria zinazotungwa ni kwa kuwalinda watawala hata kama ni wevi kama walivyo sasa.
4: umbumbu wa watawala waliopo juu ya sekta wanazoziongoza.
5: wizi wa pesa zetu na usimamizi mbovu wa rasilimali zilizopo kwa kuwapa wageni wakwepa kodi.
6: serikali kutokukusanya kodi kikamilifu na hasa kwenye majumba ya kupangisha kama ilivyo kwa nchi nyinginezo.
7:siasa chafu zilizojaa rushwa kwa kuwa wagombea ni wale walioshindwa kwenye madarasa yao na mifano ipo (mulugo).
Sababu ni nyingi but raia wapewe elimu ya uraia ili wajikomboe toka kwa manyang'au haya.

Asante mkuu. Hapo kwenye red ndio penye tatizo kubwa.
 
Tushazoea vya bure hatupendi jituma,hatupendi jaribu na hata tukijaribu 99.9% watakukatisha tamaa,hata serikal yetu haiko tayar kuwasaidia vijana...wanajal matumbo yao,ni heri uongoz wapewe wanaojua sias na uchumi pia wawe matajiri

Unafikiri kwa nini watanzania wanapenda vya bure mkuu?
 
Kama kilimo tu kimetushinda teknolojia tutaingiaje?

Wachina wahindi waliingiaje? kucopy na kupaste tu. peleka watu nje wakasomee on condition (kimkataba) lazima warudi kuapply waliojifunza. Au hata copy n paste hatuwezi?
 
Watanzania ni maskini kwa sababu ya aina ya elimu wanayopewa darasani "copy and paste education"
 
Back
Top Bottom