Kwanini Watanzania wengi hufukuza ama kupiga wanyama bila sababu?

Kwanini Watanzania wengi hufukuza ama kupiga wanyama bila sababu?

Hakuna siku nimeona huzuni kama siku nimeenda machinjioni (Mbalizi-Mbeya), sasa pale kweny karo la kuchinjia, ng'ombe anapelekwa mzobemzobe anavutwa mkia kutokana na zile damu kweye karo anateleza akianguka tu jamaa mmoja mbavu anakuja anamvuta mdomo yule ng'ombe shingo inajikaza, anakuja yule mchinjaji (Dingi mmoja wa kiislam) anapitisha kisu kikali mara moja tu damu zinaanza kumwagika huku ng'ombe anarusharusha miguu, Sasa kunakuwa na ng'ombe wengine ambao hawajachinjwa wako pembeni ukiwaona wanakuwa na hofu hadi wanajiharishia....na wanyama wanajua kifo na wanakiogopa sana.

Aisee inatisha sana wangekuwa wanawaficha wale wengine sio poa kabisa na siwezu shuhudia aiseee
 
Eheeee hapo hapo nguruwe nae anauliwa kikatili sana, hatua ya kwanza lazima apigwe mipini ya kutosha kichwani na shoka la chuma, akipoteza neti ndo anapigwa beto, unaambiwa nae akikiona kisu anaweza pita na mtu na lile domo lake kama msumeno anakuua, so kumuua lazima "wamsapraizi" na shoka then ndo achinjwe

Aiseee yaan hapo kwa ng’ombe wanaonea sana mpaka nimelia ,unajua ngombe huwa ana macho fulan hivi yanatia huruma kabisa sijui huwa ana huzuni muda wote na sielewi kwanini iliwekwa tuwale wanyama hawa ambao nao wana roho
 
Dunia ya kupenda wanyama
Nikaumbwa nikimuhusudu mnyama Nyoka ,Nawapenda sana Nyoka maisha tuloumbiwa na huyu mnyama ni kama Vita[emoji28][emoji28][emoji28]

[emoji23][emoji23] nyoka anatisha jamani
 
Hulka iliyorithiwa:
Bundi kasimama juu ya nyumba usiku, ooh! uchuro. Kumbe anajiimbia zake bongo fleva🙁huuu huuuu!! huu huuuu!!)
 
Kuna Hii tabia ya kuwapiga bundi kila Mara,
Uyu ndege kila anapoonekana lazima auwawe TU, amekua Kama nyoka Sasa.

Huu ukatili sijui lini utafika mwisho
 
Kuna wale paka wanaofugwa na kurandaranda kwenye pub au migahawa ya uswahilini. Kila wakiona mteja kapewa huduma ya chakula nao usogea miguni wakivizia wadondoshewe chakula. Uwa najiuliza kama hao paka ni wa wamiliki wa hizo pub au migahawa ambao wapo pale kwa lengo la kukubiliana na panya kwa nini wasiwe wanawaandalia hata makombo ya chakula kilichobakizwa na wateja kwa kuwawekea sehemu yao maalumu ili wasiwe wanawabugudhi wateja kwa kuwazongazonga miguuni? Maana mteja kula chakula huku kamkaushia paka anaemzongazonga huku akilia nako kunamletea aibu mbele ya wateja wengine na akisema ampe sehemu ya chakula alichohudumiwa kama ni kidogo basi yeye anaweza asishibe.

Hao paka hawana mtu bali huzaliana kwenye sehemu za mlo
Na riziki wanapata hapo hapo
Niliuliza wakasema sio wetu ni kama panya tu
 
Usisaidie Masikini kwani tabia zao ni zakishetani!
Na wengi ndio wenye tabia hiyo.

Afu atakuambia Paka ati anatumwa na wachawi [emoji3][emoji3] huoni hapo kunatatizo la msingi.
Kumhusisha Paka na matatizo yako ni Dalili ya kutojitambua
Point [emoji4][emoji106]
 
embu waza unakula samaki wa kuokwa/ nyama chomaa/ etc halafu paka anakuja anakukodolea macho na yalivyo makaliii hahaaaa lazima nimbamize kwa tonge la ugali

na umtizamapo machoni huruma inakujia unawaza anahisi njaa

Paka nawachukia kwa sababu hawaridhiki hata umpe nini bado atakuzungukia tu
Tofauti kabisa na Mbwa
Mbwa ni wazuri sana maana akishiba atalala zake hakusumbui na wewe utakula kwa amani
 
Hapana,huwezi kumruhusu mbwa amararue mtoto kwa kigezo cha kumfunza adabu,hicho ni kitendo cha kinyama,alikuwa na option nyingi sana za adhabu lakini sio hio.

Hata kama mtoto hakufa ila kitendo cha kumruhusu mnyama kumpa adhabu mtoto ni kudhalilisha utu.

Hana tofauti na wale wanaochoma moto watoto sehemu za mwili kisa kaiba hela ndani au kala mboga kwa kigezo cha adhabu.

Ametunga hii story sidhani kama ana roho chafu kiasi hicho ingawa binadamu anafanya mengi

Watoto hawajui kitu wanatakiwa kufundishwa maadili
Yaani umtupie mtoto mbwa je kama angemuua?
Halafu eti Polisi wakaiacha kesi iishe tu

Hakuna ukweli hapo
 
Kuna Hii tabia ya kuwapiga bundi kila Mara,
Uyu ndege kila anapoonekana lazima auwawe TU, amekua Kama nyoka Sasa.

Huu ukatili sijui lini utafika mwisho

Jamaa alijenga nyumba sehemu ilikuwa bado pori na bundi walikuwa wengi sasa ndugu wakija hawalali kwa kelele
Siku moja mshkaji kashindwa kulala katoka na Pistol kauwa mmoja
Mwenyewe katoka akidhani mwizi
Bundi wawili walikufa siku hiyo wengine wakakimbia

Tatizo ndio likaanza
Nyoka waliongezeka sana kwa sababu walipata amani kwa Bundi

Kila kiumbe kina sababu ya uwepo wake
 
Aisee me nisingekuwa na mudA wa Kuna kukuuliza Wala kuendesha kesi ilikuwa ni kuwatia vilema wote wewe na mbwa wako,huwezi linganisha thamani ya mtoto na ya mbwa,never hata kiuumbaji Mungu alimpendelea zaidi binadamu
Lakini usisahau. Unaweza ukaenda na hasira zako kwa nia ya kutia vilema wote yeye na mbwa wake halafu kibao kikageuka na ukajikuta wewe ndo unatiwa kilema. Hilo pia linawezekana au vp. Hasira Hasara.
 
Jamaa alijenga nyumba sehemu ilikuwa bado pori na bundi walikuwa wengi sasa ndugu wakija hawalali kwa kelele
Siku moja mshkaji kashindwa kulala katoka na Pistol kauwa mmoja
Mwenyewe katoka akidhani mwizi
Bundi wawili walikufa siku hiyo wengine wakakimbia

Tatizo ndio likaanza
Nyoka waliongezeka sana kwa sababu walipata amani kwa Bundi

Kila kiumbe kina sababu ya uwepo wake
Nakazia.
 
umenikumbusha utotoni nilkua na hyo tabia ya kuwinda mijusi na kuifanyia operation kwa kiwembe, akifa naenda kuzika..nilitenga kabisa makaburi na mochwari ya mijusi.

Nilkua katili kwa wadudu yani walikua wakiniona wanaanza mbio...ila cha kushangaza kwenye ndege na wanyama hawa nilkua na huruma nao sana.Nilkua siwezi kuchinja kuku kabisa, walikua wakichinja kama kuku namjua nilkua nalia hatari 😂 , bora nifuge kuku mpaka afe mwenye kuliko kuchinja.

Siku hizi niko peace na viumbe hai sipendi kuvidhuru, nikiona watu wana piga wanyama najisikia vibaya niko radhi nikule hela uache kumpiga huyo mnyama.

Kuna siku nilkua natoka kwenye mishe zangu maeneo flani hivi nikakutana na mzee fulani alikua watoto wameshika mbwa wawili mmoja mkubwa kengine kadogo, cjui hata hao mbwa waliwakosea nini.

Walikua wanataka kuwaua kwa kuwa nyonga ( just imagine ) kwanza hao mbwa walikua wamesha chapika hatar...pona yao ilikua ni mimi kutokea.

Niliwaomba wasiwadhuru hao mbwa lakin wapi mpaka nikatoa buku ten nikampa huyo, uzur alkua ni choka mbaya alikubali akanipa hao mbwa.

Niliwahudumia hao mbwa asee jinsi nilivyo wakuta na walivyo kuwa ni vitu viwili tofauti.Na huyo mbwa mkubwa kumbe alkua na mimba siku alivyozaa cjui alifuata nini barabarani akapigwa tairi na gari la wagonjwa akafa.Aliacha vitoto 6 vidogo hatar hata havioni kasheshe ikawa ni kuvilea, sema nilipambana navyo mpaka vikakua vikubwa.
Hongera zako ila jiongeze na kwa upande wa Wadudu uwapende pia usiwatendee jeuri. Utabarikiwa sana mkuu.
 
Kuna Hii tabia ya kuwapiga bundi kila Mara,
Uyu ndege kila anapoonekana lazima auwawe TU, amekua Kama nyoka Sasa.

Huu ukatili sijui lini utafika mwisho
Imani za Kishirikina ndo kisababishi kikuu. Imani hiyo ikiisha basi na Ukatili dhidi ya wanyama hao utakua kwishney.
 
Yani kunguru apite mbele yangu akae site nzuri jiwe linamuhusu
Kwa sababu gani?? Umekosa cha kufanya? Mbona wakipita mbele yako vibaka, wezi, wahuni na watu wa namna hiyo na pengine unawafahamu wana tabia hiyo jiwe haliwahusu?
 
Napenda sana mbwa, hawa viumbe wana mapenzi ya dhati kiukweli, ni wavumilivu sana, wapo tayari kufa ili waukokoe.
Yap! Hongera sana mkuu. Watu wanajisahau sana kiulinzi. Eti mtu ananunua bunduki ili ajilinde lakini anasahau kwamba hapo ni yeye ndiye anageuka kuwa mlinzi wa hiyo bunduki kwani akijisahau kidogo tu "wenyewe" wanakuja kuichukua na wala hiyo bunduki haitapiga kelele kumuamsha kwamba kuna kitu sio cha kawaida huko nje na Polisi watamsumbua atoe maelezo ilikuwaje-kuwaje bunduki kupotea?
Tofauti na Mbwa atakuamsha ili ujiweke tayari kuna kitu huku nje ujiandae na bado haishii hapo tu bali atakuwa bega kwa bega na wewe kwenye mapambano ili akuokoe wewe na mali zako.
NB: Sijasema au kushauri watu msinunue bunduki. La hasha. Nunueni kwa Amani zenu.
 
Back
Top Bottom