Kwanini Watanzania wengi hufukuza ama kupiga wanyama bila sababu?

Kwanini Watanzania wengi hufukuza ama kupiga wanyama bila sababu?

Hhah napenda paka alikuwa akiona hujatandika kitanda haji kulala ukitandika tu anakuja lala weeeeee akiamka anaenda sehemu yake ya kukojoa anakojoa hajawah kukojoa kitandani au kujisaidia popote ndani kisha huyo anakufata umfatie nyama,kuna siku nikamkuta chooni anakojoa [emoji23][emoji23][emoji23] nilicheka mno
Ikifika usiku wakati wa kulala nae anaenda kupanda kitandani kulala kile kile kitanda habadilishi,anajiingiza kwenye blanket basi hicho kitanda ni aunt yangu,muda mwingine aunt kapitiwa usingizi paka anaenda penyeza kwenye blanket analala akamtengenezea sehemu yake ya kulala akawa anamuekea alale lakin sasa mkiaka asubuhi anapanda kitandani analala ndani ya blanket nikija kutoa blanket anakuwa mkali tunaanza kuvutiana blanket nilikuwa nacheka jamani,mkifunga mlango kama hajaingia ndani wee atapiga piga huo mlango na kulia mpaka mtamfungulia aje alale ndani eti kulala nje hawezi
Safi sana aiseee
 
Mimi nilifundishwa kutokupiga wanyama hata viumbe vingine visivyo na madhara kwenye mazingira yetu siui mijusi hata wadudu wengine warukao ambao hawana madhara nawafukuzia nje huko pamoja na ndugu zake Chura mpaka watoto nao hasa wa kiume tunaenda sawa maana sio waoga..
 
Hapo ulivuka mstari mkuu,watoto wengi hufanya mambo kwa mazoea ya kuiga matendo ya jamii,

Ilibidi wewe kama mtu mzima ukae nao uwaelimishe kwamba huyo mbwa wasimsumbue na kisha uwape onyo kwamba wakirudia kuna hatua za kinidhamu utawachukulia.

Baada ya hapo wangerudia ni bora ungechapa hata viboko, viboko dawa nzuri sana kwa watoto wa aina hii, ndiyo adhabu ambayo hata imeruhsiwa katika vitabu vitakatifu.

Huyo mbwa aliewararua kucha zake zingewatoboa macho hao watoto si wangekuwa vipofu maisha yote?

Ni vema kutoa adhabu inayostahilika kuliko kutoa adhavu unayoitaka wewe.
Mkuu; Wewe sio mgeni na suala la kumchapa viboko mtoto wa mtu. Ukijaribu tu kufanya hilo mzee, timbwili lake ni balaa hususan akija mama mzazi. Hakuna rangi utaacha kuona. Atakufedhehesha na kukudhalilisha mno hadharani kuliko maelezo.😭😭
Kwa maelezo yangu labda sikuwa detailed ni kwamba nimekuwa nikiongea nao kirafiki na kuwaelimisha madhara ya mbwa na Ubaya wa kumpiga mbwa kwani mbwa hajawachokoza. Hilo liliwahusu hata wazazi wao na shuleni.
By the way, unafahamu kwamba mbwa hutunza kisasi? Wewe kama ulimpiga mbwa kwa makusudi tuseme 2021 jua kwa uhakika siku akipata nafasi leo 2022 lazima akutie jeraha hata kama umejichanganya kwenye kundi la watu au pamepita muda mrefu. Atalipiza kisasi tu na watu wengi wanalijua hilo.
Zoezi la adhabu hufanyika kwa uangalifu.
Hata hivyo mkuu; haitatokea hata siku moja mbwa akang'ata usoni. au machoni kama ulivyotahadharisha. Mbwa mara zote hung'ata makalio, mapaja au mkono. Ni mara chache sana mgongoni na ni pale mtu anapokimbia na bahati mbaya akaanguka chini. Mtu huangukia tumbo(kifudifudi) na mbwa hung'ata mgongo.
Pamoja na hayo, labda nikuwekee tu wazi kwamba mm ni Mtaalam wa mifugo na ninafahamu ninacho kisema.
 
Mkuu; Wewe sio mgeni na suala la kumchapa viboko mtoto wa mtu. Ukijaribu tu kufanya hilo mzee, timbwili lake ni balaa hususan akija mama mzazi. Hakuna rangi utaacha kuona. Atakufedhehesha na kukudhalilisha mno hadharani kuliko maelezo.[emoji24][emoji24]
Kwa maelezo yangu labda sikuwa detailed ni kwamba nimekuwa nikiongea nao kirafiki na kuwaelimisha madhara ya mbwa na Ubaya wa kumpiga mbwa kwani mbwa hajawachokoza. Hilo liliwahusu hata wazazi wao na shuleni.
By the way, unafahamu kwamba mbwa hutunza kisasi? Wewe kama ulimpiga mbwa kwa makusudi tuseme 2021 jua kwa uhakika siku akipata nafasi leo 2022 lazima akutie jeraha hata kama umejichanganya kwenye kundi la watu au pamepita muda mrefu. Atalipiza kisasi tu na watu wengi wanalijua hilo.
Zoezi la adhabu hufanyika kwa uangalifu.
Hata hivyo mkuu; haitatokea hata siku moja mbwa akang'ata usoni. au machoni kama ulivyotahadharisha. Mbwa mara zote hung'ata makalio, mapaja au mkono. Ni mara chache sana mgongoni na ni pale mtu anapokimbia na bahati mbaya akaanguka chini. Mtu huangukia tumbo(kifudifudi) na mbwa hung'ata mgongo.
Pamoja na hayo, labda nikuwekee tu wazi kwamba mm ni Mtaalam wa mifugo na ninafahamu ninacho kisema.
Kwa hiyo una ID mbili,
Moja umeleta kisa, ingine unajitetea nayo,

Wewe ni Katili hata uandike magazeti vipi na una bahati mimi sio member wa hiyo familia ya mtoto, ilikua unapewa kesi moja takatifu (kukusudia kuua mtoto) ungekaa jela hadi ujue tofauti ya Mnyama na Mtoto,

eti namuhudumia Mbwa sijui nini, aiseee! kuna watu sijui mnaishi sayari gani.
 
Kweli mmerogwa leo mnavyowatetea mbwa sasa! Ila mnavyoshabikiaga kupiga mke aloooo hadi shetani anaogopa.
 
Kwa hiyo una ID mbili,
Moja umeleta kisa, ingine unajitetea nayo,

Wewe ni Katili hata uandike magazeti vipi na una bahati mimi sio member wa hiyo familia ya mtoto, ilikua unapewa kesi moja takatifu (kukusudia kuua mtoto) ungekaa jela hadi ujue tofauti ya Mnyama na Mtoto,

eti namuhudumia Mbwa sijui nini, aiseee! kuna watu sijui mnaishi sayari gani.
Mkuu; kwa uhakika sina ID mbili labda unishawishi ili niwe nazo. Ni sahihi ungenipa kesi lakini ujue na Kesi huamuliwa na Mahakama sio Mlalamikaji. Kama nia yako ni ili nikae jela (kwa kunikomoa) kwanza zingatia kwamba Mtuhumiwa hawekwi jela bali huwekwa Mahabusu. Pili kumbuka kwamba mahabusu au kama wewe unavyoita ni jela huko wanakaa watu sio mbuzi. Kwa hiyo kama hoja yako eti ni kesi takatifu (kukusudia kuua mtoto), itaonekana ina mashiko basi nitakaa huko kama wanavyokaa huko watu wengine. Wewe unaogopa jela? By the way, ww ni Ke au Me? Kama ni Ke , basi hiyo comment yako inayapa uzito maneno yangu kwamba akija mama .....timbwili lake...
 
Asili ya mwafrika huwa hapendi wanyama na hili huusishwa na Imani za kishirikina mf. Paka,panya,bundi,nyoka,njiwa,mijusi, fisi na vingine vingi. Wazee wetu ndio chanzo.
Mifugo haitakiwi kudhurula mitaani, baadhi ya nchi za ulaya, kunakikosi maalumu huwa kina dili na mifugo inayo dhurula mtaani.

Mbwa wako wakimkuta mchana, hata kama yupo karibu na kwako, wanamkamata kwa kutumia sitiki maalumu, zenye kamba yenye mtego. Kisha kumchukua kwa gari maalumu na kuondoka nae.
 
Mifugo haitakiwi kudhurula mitaani, baadhi ya nchi za ulaya, kunakikosi maalumu huwa kina dili na mifugo inayo dhurula mtaani.

Mbwa wako wakimkuta mchana, hata kama yupo karibu na kwako, wanamkamata kwa kutumia sitiki maalumu, zenye kamba yenye mtego. Kisha kumchukua kwa gari maalumu na kuondoka nae.
Huku Tz. wanapokuwa ni wengi wanazurura mitaani, hospitali, machinjioni, kwenye majalala(Vizimba) au sokoni na ikaonekana ni kero au tishio kwa usalama wa watu, hupunguzwa kwa kupigwa risasi lakini ni kwa kuzingatia Utaratibu sio kiholela.
 
Pamoja na kufuga kuku ila hua si chinji kutokana na vile ninavyowalea nao pia Huwa wananipenda,Huwa sijiskii poa kabisa kuwachinja
 
Umenikumbusha miaka ya utotoni jirani yetu karudi shamba saa tisa mchana huku kabeba samaki wake wa kukaanga ili wapike ugali wa mchana baada ya kazi ngumu ya shamba. Baada ya kuingia nyumbani kwake na vijana wake na kuweka samaki mezani jikoni ili mapishi yaanze huko nje ikatokea tafrani (ugomvi) majirani zake wanapigana baada ya kuitana wachawi, jamaa na vijana wake wakakimbilia ugomvi huko nje. Baada ya ugomvi kwisha na yeye kurudi ndani akakuta paka ndiyo anamalizia kutafuna samaki wa mwisho. Kwa hamaki jamaa na vijana wake wakafunga milango na kufanikiwa kumkamata yule paka. Adhabu waliompa ni kumwagiwa mafuta ya taa na kumuwasha moto!! Basi paka akachomoka huku anawaka moto mbio akapanda ukutani nyumba ya jirani ya nyasi, na mara nyumba yote ikaanza kuungua moto na mwishowe kuteketea yote na mahindi yaliyokuwepo darini.. [emoji23] [emoji23]

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787]dah, nimecheka sana
 
Hakuna siku nimeona huzuni kama siku nimeenda machinjioni (Mbalizi-Mbeya), sasa pale kweny karo la kuchinjia, ng'ombe anapelekwa mzobemzobe anavutwa mkia kutokana na zile damu kweye karo anateleza akianguka tu jamaa mmoja mbavu anakuja anamvuta mdomo yule ng'ombe shingo inajikaza, anakuja yule mchinjaji (Dingi mmoja wa kiislam) anapitisha kisu kikali mara moja tu damu zinaanza kumwagika huku ng'ombe anarusharusha miguu, Sasa kunakuwa na ng'ombe wengine ambao hawajachinjwa wako pembeni ukiwaona wanakuwa na hofu hadi wanajiharishia....na wanyama wanajua kifo na wanakiogopa sana.
 
Hakuna siku nimeona huzuni kama siku nimeenda machinjioni (Mbalizi-Mbeya), sasa pale kweny karo la kuchinjia, ng'ombe anapelekwa mzobemzobe anavutwa mkia kutokana na zile damu kweye karo anateleza akianguka tu jamaa mmoja mbavu anakuja anamvuta mdomo yule ng'ombe shingo inajikaza, anakuja yule mchinjaji (Dingi mmoja wa kiislam) anapitisha kisu kikali mara moja tu damu zinaanza kumwagika huku ng'ombe anarusharusha miguu, Sasa kunakuwa na ng'ombe wengine ambao hawajachinjwa wako pembeni ukiwaona wanakuwa na hofu hadi wanajiharishia....na wanyama wanajua kifo na wanakiogopa sana.

Dah! angalau hao wengine wasione, ila huo ni ukatili kwan hamna jinsi nyingine nzuri ya kuchinja

Ila kitimoto si ndio naskia anapigwagwa shoka la kichwa kabla ya kuchinjwa mpaka anakata network, waafrika mungu atusamehe tu
 
Hakuna siku nimeona huzuni kama siku nimeenda machinjioni (Mbalizi-Mbeya), sasa pale kweny karo la kuchinjia, ng'ombe anapelekwa mzobemzobe anavutwa mkia kutokana na zile damu kweye karo anateleza akianguka tu jamaa mmoja mbavu anakuja anamvuta mdomo yule ng'ombe shingo inajikaza, anakuja yule mchinjaji (Dingi mmoja wa kiislam) anapitisha kisu kikali mara moja tu damu zinaanza kumwagika huku ng'ombe anarusharusha miguu, Sasa kunakuwa na ng'ombe wengine ambao hawajachinjwa wako pembeni ukiwaona wanakuwa na hofu hadi wanajiharishia....na wanyama wanajua kifo na wanakiogopa sana.
Ni kweli na inasikitisha sana (Inhumane killing). Kiutaratibu inatakiwa mnyama wa kuchinjwa aingie eneo la kuchinjwa peke yake wengine wasione japokuwa watakuwa wameshtuka kwa harufu ya damu. Na kabla hajachinjwa anapotezwa fahamu ndipo Mchinjaji amchinje na sio hivyo kavu-kavu anajiona Live. Hupotezwa fahamu kwa kuwa stunned kwa kutumia umeme au kumgonga kwa nguvu na kitu kizito manually kichwani.
 
Dah! angalau hao wengine wasione, ila huo ni ukatili kwan hamna jinsi nyingine nzuri ya kuchinja

Ila kitimoto si ndio naskia anapigwagwa shoka la kichwa kabla ya kuchinjwa mpaka anakata network, waafrika mungu atusamehe tu
Eheeee hapo hapo nguruwe nae anauliwa kikatili sana, hatua ya kwanza lazima apigwe mipini ya kutosha kichwani na shoka la chuma, akipoteza neti ndo anapigwa beto, unaambiwa nae akikiona kisu anaweza pita na mtu na lile domo lake kama msumeno anakuua, so kumuua lazima "wamsapraizi" na shoka then ndo achinjwe
 
Eheeee hapo hapo nguruwe nae anauliwa kikatili sana, hatua ya kwanza lazima apigwe mipini ya kutosha kichwani na shoka la chuma, akipoteza neti ndo anapigwa beto, unaambiwa nae akikiona kisu anaweza pita na mtu na lile domo lake kama msumeno anakuua, so kumuua lazima "wamsapraizi" na shoka then ndo achinjwe

Hapo mbeya uliposema wanawaonea ng’ombe ambao wapole angekuwa huyo jamaa na lile pua lake angepita na sheik mchinjaji, oh sorry kumbe hamnaga sheik anaochinja ile kitu
 
viumbe hivi tumepewa mamlaka ya kuvitawala kwa haki na sio kuvinyanyasa ama kuvitesa, viumbe hivi kuvifanyia ubaya ni sawa na kumtemea mate usoni Muumba wetu alietuumba sisi na hivyo viumbe. Hata Biblia imeweka wazi sehemu nyingi juu ya kuwajali wanyama, Kwa upande wa uislam Mtume (pbh) alikuwa na paka wake aliemjali sana alimwita "Muezza"

kuna hizi tabia mbaya sana zimezoeleka na watanzania wengi kwa wanyama 👇👇

-unakuta tu mtaani mbwa anajipitia zake, mtu anaanza kumrushia mawe.

-nyumbani kwako unafuga paka, ukimualika mgeni anaanza kumfukuza sshh tokaa!! aende wapi sasa wakati hapo ni kwao ?

-Mtu kashiba nyama, anaenda kuitupa badala ya kumpa paka mwenye njaa,

-kuku yupo bize anatafuta chakula, mara mtu anaanza kumkimbiza tu bila sababu.

-Mbuzi ameletwa kwajili ya sherehe, usiku umefika anaachwa ukutani badala ya kumweka hata stoo aweze kupumzika, kujikinga na baridi, mvua, n.k.

-usiombe kukutana na mtu anatumia ng'ombe kulima, yani hizo stiki huyo ng'ombe anazokula na matusi juu ni balaa.

-Dume limempanda jike, mtu anaanza kuwarusha mawe.

-mbuzi analia meee meee kwavile ndivyo alivyoumbwa, mtu anachukia anaenda kumpiga.

-Punda anabebeshwa mizigo mizito yani hata kutembea inakuwa shida lakini mtu wala hajali.

-Mbwa kila usiku anakulinda wewe, familia yako na mali ila kibanda chake hakijasafishwa mwaka mzima kimejaa viroboto, chakula chake ni makombo kila siku, yani mtu hajiongezi hata kumpa nyama mara moja kama shukrani ya ulinzi anaompa.


Hivi hawa wanyama wanakosa lipi?
Nakubaliana na wew asilimia mia moja,hawa ni viumbe ambao wameumbwa na Mungu afu sisi viumbe watu tunajiona ndo wazur zaidi kuliko wao,lakin wapo kwa ajili ya kusaidiana kwa ya kwetu,
 
-Mtu kashiba nyama, anaenda kuitupa badala ya kumpa paka mwenye njaa,
Kaka hichi ulichokiandika nikosa kubwa sana. Hawa wanyama wafungwao ni wanyama kama tulivyo sisi, kwanini yale mabaki tunayokula sisi tunawapa wao. Wale wanyama wanahitaji chakula kisafi na mahali pasafi kama sawa na mazingira tunayokula chakula chetu sisi tunaojiita wanadamu

-Mbuzi ameletwa kwajili ya sherehe, usiku umefika anaachwa ukutani badala ya kumweka hata stoo aweze kupumzika, kujikinga na baridi, mvua, n.k.
Sisi pia ni wanyama kama walivyo wao kwanini tuwaweke store na wakati unaweza hata muombea kwa jirani mwenye banda na asubuhi ukamchukua kwa shughuli yako?
 
Back
Top Bottom