Kwanini Watanzania wengi hufukuza ama kupiga wanyama bila sababu?

Kwanini Watanzania wengi hufukuza ama kupiga wanyama bila sababu?

Hapana,huwezi kumruhusu mbwa amararue mtoto kwa kigezo cha kumfunza adabu,hicho ni kitendo cha kinyama,alikuwa na option nyingi sana za adhabu lakini sio hio.

Hata kama mtoto hakufa ila kitendo cha kumruhusu mnyama kumpa adhabu mtoto ni kudhalilisha utu.

Hana tofauti na wale wanaochoma moto watoto sehemu za mwili kisa kaiba hela ndani au kala mboga kwa kigezo cha adhabu.
Wewe endelea kuwalea watoto wako ki-junior junior Ila akija kukutana na wahuni watamuingiza kwny Banda la mbwa na Cha kufanya hamna.
 
Kaka hichi ulichokiandika nikosa kubwa sana. Hawa wanyama wafungwao ni wanyama kama tulivyo sisi, kwanini yale mabaki tunayokula sisi tunawapa wao. Wale wanyama wanahitaji chakula kisafi na mahali pasafi kama sawa na mazingira tunayokula chakula chetu sisi tunaojiita wanadamu


Sisi pia ni wanyama kama walivyo wao kwanini tuwaweke store na wakati unaweza hata muombea kwa jirani mwenye banda na asubuhi ukamchukua kwa shughuli yako?
Paka shenzi kabisa unasaga Dona yako fresh unahifadhi kwenye kilindo ye anafukua unga anakata gogo afu anafukia
 
Ni ujinga tu....hapa mtaani kwetu kuna watoto walikuwa wanatoka shule siku moja nikawaluta wanasalandia mbwa wangu aliyekuwa kwenye kibanda chake tena ndani ya geti wameshika mawe wamtungue. Nikawavizia na nikabahatiak kumkamata mmoja. Nikamuingiza ndani na kumfungulia mbwa amrarue na alimng'ata vizuri tu. Akaenda kwao kisha akarudi na wazazi wake kuja kulalamika na kunishitaki. Nikawaambia ukweli kilichotokea, baba wa mtoto kwa ujinga alionao alkasema eti huu ni mtaa wa Kiislam unafuga mbwa wa nini? Nikamjibu tu vibaka wengi wa hapa mtaani ni waislam Mze baba akanishangaa, wakaenda nishitaki Polisi Mabatini ila kesi haikufika mbali, ilifutwa. Yule dogo ni mwaka sasa hajathubutu kuja kurusha mawe tena, yuko tu makovu yake ya kujitakia.
Aisee me nisingekuwa na mudA wa Kuna kukuuliza Wala kuendesha kesi ilikuwa ni kuwatia vilema wote wewe na mbwa wako,huwezi linganisha thamani ya mtoto na ya mbwa,never hata kiuumbaji Mungu alimpendelea zaidi binadamu
 
Dunia ya kupenda wanyama
Nikaumbwa nikimuhusudu mnyama Nyoka ,Nawapenda sana Nyoka maisha tuloumbiwa na huyu mnyama ni kama Vita😅😅😅
 
Sisi tupo kitofauti sana na mambo ya wanyama.

Hebu chukulia mfano yanayoendelea Ukraine, mtu unamkuta anaenda kutafuta hifadhi pamoja na mnyama wake
 
Tabia na mazoea.....

Haya maambo Yana fanywa Sana na wenzetu huko kufuga wa nyama na kuwa treat well kama anavyo lelewa binadam au mtoto,
Na huko kwa wenzetu Hilo haijatokea kwa bahati mbaya ni kuringana na mazingira yaliyopo huko.....
Zipo sababu nyingi tuu zinazo fanya mambo yawe hivyo mfano mdogo wao kulea wa nyama na kuwatret hivyo ya weza kuwa ni upweke Sasa huku kwetu haipo iyo kitu ndio maana

Nina kubaliana kabisa na mtoa Mada kuwa hiyo ni tabia ya hovyo but ndio maisha yetu haya hatuwezi badilika kirahis hivyo
 
Utotoni kulikuwa na michezo ya watoto kwenda kuwinda mijusi then kuwachezea na kuwaua.

Mzee alinifundisha si vizuri kuua kiumbe bila sababu. Walikuwa wananiita mlokole. sababu nilikuwa nikiwakataza nikisema sio vizuri.😂
umenikumbusha utotoni nilkua na hyo tabia ya kuwinda mijusi na kuifanyia operation kwa kiwembe, akifa naenda kuzika..nilitenga kabisa makaburi na mochwari ya mijusi.

Nilkua katili kwa wadudu yani walikua wakiniona wanaanza mbio...ila cha kushangaza kwenye ndege na wanyama hawa nilkua na huruma nao sana.Nilkua siwezi kuchinja kuku kabisa, walikua wakichinja kama kuku namjua nilkua nalia hatari 😂 , bora nifuge kuku mpaka afe mwenye kuliko kuchinja.

Siku hizi niko peace na viumbe hai sipendi kuvidhuru, nikiona watu wana piga wanyama najisikia vibaya niko radhi nikule hela uache kumpiga huyo mnyama.

Kuna siku nilkua natoka kwenye mishe zangu maeneo flani hivi nikakutana na mzee fulani alikua watoto wameshika mbwa wawili mmoja mkubwa kengine kadogo, cjui hata hao mbwa waliwakosea nini.

Walikua wanataka kuwaua kwa kuwa nyonga ( just imagine ) kwanza hao mbwa walikua wamesha chapika hatar...pona yao ilikua ni mimi kutokea.

Niliwaomba wasiwadhuru hao mbwa lakin wapi mpaka nikatoa buku ten nikampa huyo, uzur alkua ni choka mbaya alikubali akanipa hao mbwa.

Niliwahudumia hao mbwa asee jinsi nilivyo wakuta na walivyo kuwa ni vitu viwili tofauti.Na huyo mbwa mkubwa kumbe alkua na mimba siku alivyozaa cjui alifuata nini barabarani akapigwa tairi na gari la wagonjwa akafa.Aliacha vitoto 6 vidogo hatar hata havioni kasheshe ikawa ni kuvilea, sema nilipambana navyo mpaka vikakua vikubwa.
 
Mimi sina shida na wanyama nipo peace nao. Lakin yale manyau yanakuja mlangoni usiku kuwanga na yanalia kama mtoto mdogo huwa sina simile nayo. Nikitoka ni jabali tu
 
Mimi napenda wanyama wengine wanaofugwa ila mbwa na paka siwapendi !! Nikimkuta sehemu sitampiga kwa ukatili nampita tu !! Ila kuwatunza nyumbani kwangu sipendi kabisa ! Wengine kama mbuzi , kuku , kondoo hao fresh
 
Ni ujinga tu....hapa mtaani kwetu kuna watoto walikuwa wanatoka shule siku moja nikawaluta wanasalandia mbwa wangu aliyekuwa kwenye kibanda chake tena ndani ya geti wameshika mawe wamtungue. Nikawavizia na nikabahatiak kumkamata mmoja. Nikamuingiza ndani na kumfungulia mbwa amrarue na alimng'ata vizuri tu. Akaenda kwao kisha akarudi na wazazi wake kuja kulalamika na kunishitaki. Nikawaambia ukweli kilichotokea, baba wa mtoto kwa ujinga alionao alkasema eti huu ni mtaa wa Kiislam unafuga mbwa wa nini? Nikamjibu tu vibaka wengi wa hapa mtaani ni waislam Mze baba akanishangaa, wakaenda nishitaki Polisi Mabatini ila kesi haikufika mbali, ilifutwa. Yule dogo ni mwaka sasa hajathubutu kuja kurusha mawe tena, yuko tu makovu yake ya kujitakia.
Shukuru umekutana na wazazi wastaarabu sio watu wa visasi yaaani mchukue Mwanangu ufanye ulichotenda kisha nikuache aiseee utajua hujui😬
 
Kwa hiyo una ID mbili,
Moja umeleta kisa, ingine unajitetea nayo,

Wewe ni Katili hata uandike magazeti vipi na una bahati mimi sio member wa hiyo familia ya mtoto, ilikua unapewa kesi moja takatifu (kukusudia kuua mtoto) ungekaa jela hadi ujue tofauti ya Mnyama na Mtoto,

eti namuhudumia Mbwa sijui nini, aiseee! kuna watu sijui mnaishi sayari gani.

Kuna watu wana cold heart
 
umenikumbusha utotoni nilkua na hyo tabia ya kuwinda mijusi na kuifanyia operation kwa kiwembe, akifa naenda kuzika..nilitenga kabisa makaburi na mochwari ya mijusi.

Nilkua katili kwa wadudu yani walikua wakiniona wanaanza mbio...ila cha kushangaza kwenye ndege na wanyama hawa nilkua na huruma nao sana.Nilkua siwezi kuchinja kuku kabisa, walikua wakichinja kama kuku namjua nilkua nalia hatari 😂 , bora nifuge kuku mpaka afe mwenye kuliko kuchinja.

Siku hizi niko peace na viumbe hai sipendi kuvidhuru, nikiona watu wana piga wanyama najisikia vibaya niko radhi nikule hela uache kumpiga huyo mnyama.

Kuna siku nilkua natoka kwenye mishe zangu maeneo flani hivi nikakutana na mzee fulani alikua watoto wameshika mbwa wawili mmoja mkubwa kengine kadogo, cjui hata hao mbwa waliwakosea nini.

Walikua wanataka kuwaua kwa kuwa nyonga ( just imagine ) kwanza hao mbwa walikua wamesha chapika hatar...pona yao ilikua ni mimi kutokea.

Niliwaomba wasiwadhuru hao mbwa lakin wapi mpaka nikatoa buku ten nikampa huyo, uzur alkua ni choka mbaya alikubali akanipa hao mbwa.

Niliwahudumia hao mbwa asee jinsi nilivyo wakuta na walivyo kuwa ni vitu viwili tofauti.Na huyo mbwa mkubwa kumbe alkua na mimba siku alivyozaa cjui alifuata nini barabarani akapigwa tairi na gari la wagonjwa akafa.Aliacha vitoto 6 vidogo hatar hata havioni kasheshe ikawa ni kuvilea, sema nilipambana navyo mpaka vikakua vikubwa.
Bado vipo... Uliviuza?
 
Back
Top Bottom