#COVID19 Kwanini Watanzania wengi wanakataa chanjo ya Corona?

#COVID19 Kwanini Watanzania wengi wanakataa chanjo ya Corona?

Chanjo itakuja na watu watachanjwa hasa wanao hudhuria hospital mara kwa mara na kwenye mikusanyiko itakuwa lazima hasa wabunge na sokoni na stendi wasiotaka kuchanjwa Kama Ngwajima itabidi wakae nyumbani na ubunge na uchungaji aache maana anakusanya watu na mikusanyiko inaleta kuambukizana.
Wewe SUBIRI mama SAmia hawaelewi watanzania kumgeuka ni dakika sifuri na kibarakoa chake
 
Ndio shida ya mama, anataka kurodhisha watu fulani, hana msimamo kabisa , mbona watu tulishasahau na tunaishi poa tu
Ila Tanganyika mwambieni kakwaa kisiki kwenye korona na kibarakoa chake kakwaa kisiki

Watanganyika ni wajeuri atalijua jiji
 
msimamo wa watanzania juu ya corona ni

1,corona ni ugonjwa wa mafua kama yalivyo mengine,na yuko tayari kuishi nao.
hata mheshimiwa anajua hilo,labda kuna namna anatafuta kuridhisha watu fulani.
Hao watu fulani hata afanyeje hawezi kuwaridhisha!! Wale ni kama kuzimu!! Kuzimu haiwezi kuridhika! Japo inataka moyo kwenda kinyume na matakwa ya hao watu fulani almaarufu kama mabeberu!!! Lengo la beberu ni kupiga pesa!! Wameona biashara kubwa kwenye corona!! Hebu fikiri kidogo, itatugharimu sh ngapi kuchanja watanzania milioni 60? Hiyo pesa mabeberu wanaitolea macho!! Wakikuona unashtuka wananuna!!
 
H
Kuna program inaitwa COVAX, chanjo za bei rahisi na kwa nchi nyingine wamepewa bure. Na wanaweza kuleta, zikauzwa;

Swala la muhimu, kina Gwajima wasizuie wenzao kupata chanjo kwa masuala ya imani. Ni kama nguruwe na pombe; kuna imani zinakataza, lakini zipo. Ukitaka kanunue.
Hiyo program ya covax siyo rahisi kivile kama unavyodhani!! Si rahisi kwa Taifa!! Nchi lazima ichangie pesa ndefu tu hata kama wewe utachanjwa bure
 
Chanjeni wenyewe halafu sisi tuwatazame mnavyoendelea kwa miaka 5!!
Naamini mabeberu wanachanjana maji (placebo), ili kutuingiza chaka na sisi tukubali chanjo huku wakitufanyia majaribio!! Nilichofurahi kuliko vitu vyote ni kuwa hakuna atakayelazimishwa kuchanjwa
 
nina wiki sasa tangu nipige chanjo na nipo mzima kabisa
 
Kuhusu utaratibu wa upatikanaji wa hii chanjo na dhima ya uendeshaji wa hii chanjo ndo hofu ya wengi inapo anzia , cha ajabu wasomi wengi hawataki kufikilisha bongo zao kujua haya mambo kiundani huko tu marekani watu kibao wanasikilizia output yake itakuwaje na wanagoma kuchanjwa, makapuni yanayoitengeneza yamejikita zaidi profit oriented na mtiti hii chanjo ipo kwenye trial inaitwa TRIAL VACCINE. ....sasa tukubaliane tumeridhia kuwa panya wa laboratory? [emoji38][emoji38]
2021-05-19%2014.31.25.jpg
2021-05-18%2000.07.43.jpg
Screenshot_2021-05-18_001600.jpg
 
4)Serikali iendele kusimamia njia za kujikinga na ugonjwa ichukue hatu kali bila kujali watanzania wanasemaje kwa ajili ya faida ya afya wengi
5) Serikali ichukue hatua kali kwa wanaotaka kuchanjwa ili kila mmoja wao apimwe kwa kipimo kipya cha kichina!
 
H

Hiyo program ya covax siyo rahisi kivile kama unavyodhani!! Si rahisi kwa Taifa!! Nchi lazima ichangie pesa ndefu tu hata kama wewe utachanjwa bure
Kama ni gharama, serikali iruhusu hata private companies walete, wenye uwezo wanunue. Kenya hapo kuna kampuni zilileta Sputnik vaccine, na watu wakanunua.

La muhimu serikali itengeneze mazingira watu waweze kupata chanjo, wasiweke vigingi.
 
Kama ni gharama, serikali iruhusu hata private companies walete, wenye uwezo wanunue. Kenya hapo kuna kampuni zilileta Sputnik vaccine, na watu wakanunua.

La muhimu serikali itengeneze mazingira watu waweze kupata chanjo, wasiweke vigingi.
Nyie watu wa mitandaoni ni shida sana si ajabu hizo chanjo zikaja na msitokee kuchanjwa mkawa mnasikilizia kwanza wakati kumbe nyie ndio mlioziomba humu.
 
Mafua haijawahi kuwa tatizo kwetu.kwahyo kununua chanjo ni kupoteza hela. Hiyo tuna matumiz nayo mengi

Sent from my CPH1937 using JamiiForums mobile app
Kamati ya corona ingetuambia tumeathirika kiasi gani kwa kipindi chote hiki kisha ndio wangetokea hayo mapendekezo ya nini tufanye ila wao wamekuja moja kwa moja na mapendekezo yao ya chanjo.
 
Kwa anaefahamu what is placebo effect phenomena basi anajua fika what is going on na hzo chanjo,,,, kwa uharaka wa utengenezaj wa hizi chanjo what i expected ni kuwa
1) tutapata a new study au new knowledge about virus ( from dna to membrane)
2) new ways ya kufanya DNA/ RNA manipulation,,

Siku wakitoa a new study ya covid-19 ntaichoma
 
Baada ya kamati ya corona iliyoundwa na Rais wetu Mh Samia suluhu kupendekeza Wantanzania kupata chanjo, Watanzania walio wengi wamepinga sana kupata chanjo ya Covid 19.

Kwa hali Hii serikali inatakiwa iangalie kwa namna nyingine kwa Maana nchi na uongonzi wake ni watu ambao ni watanzania wala siyo kulazimisha ,naamini kupitia Rais wetu itaangalia zaid maoni ya Watanzania.

Mapendekezo yangu

1)Serikali iwe na Msemaji Mkuu wa Covid 19 ambaye ni Dr hasa kama katibu Mkuu prof Abel Makubi , awe siyo Mwanasiasa
2)Swala la chanjo huwezi lipinga kwa maana ndio Suluhisho la Kudhibiti ugonjwa tunakoelekea
3) Kwa Hali ya uelewa chanjo kwa sasa serikali isilazimishe ielewee wananchi wengi wako kwanin hawaitaki chanjo
4)Serikali iendele kusimamia njia za kujikinga na ugonjwa ichukue hatu kali bila kujali watanzania wanasemaje kwa ajili ya faida ya afya wengi
Wewe nae,,eti ichukue hatua kali,,mtaani kwako wamekufa wangapi ???mambo ya India unatuletea huku???mnataka tuvae barakoa zenye Wadudu wa COVID 19...Mnataka kutuuua....
Mmemuua JPM,mnataka na Watanzania muwaue,,,??
 
kwann tulazimishane chanjo! hatutaki chanjo sababu ugonjwa haupo! corona ni ugonjwa wa saikolojiko wazungu wanapiga pesa. haya makapuni ya chanjo huenda ndio yameleta huu ugonjwa ili kujitajirisha kupitia chanjo.
 
Hivi wabongo mkuu unawajua ama unawasikia??
Subiri chanjo iletwe hapa halafu uone msongamano kwenye kuchanjwa. Hawa watu waone hivi hivi tu ni vigeu geu hatari ni watu wa kwenda na upepo unakoenda.

Mi nna imani watanzania wengi watachanjwa, hii chanjo haitakua lazima ila itakua lazima kwa namna moja ama nyingine. Inawezekana kuna huduma utazikosa bila kua na chanjo na hivyo kukulazimu uchanjwe, sidhani kama serikali itaileta tu afu iwe hiyari kirahisi namna hiyo.

Ni kama waliposema kujisajili kwa ajili ya vitambulisho vya taifa watu walikua wajajivutavuta, wakagusa panauma kwenye laini za simu, mpaka leo nida kuna watu wanazisakama hizo namba tu mambo yao yaende.
Hahahahahahah...... Kwaiyo watanzania ni watu was kudemka na upepo
 
Nyie watu wa mitandaoni ni shida sana si ajabu hizo chanjo zikaja na msitokee kuchanjwa mkawa mnasikilizia kwanza wakati kumbe nyie ndio mlioziomba humu.
Sio kila kitu lazima kiwe kwa ajili yangu au yako ndio ukitetee.
 
Back
Top Bottom