Kwanini watoto wa Mzee Mchonga hawana nyadhifa kubwa Nchini?

Kwanini watoto wa Mzee Mchonga hawana nyadhifa kubwa Nchini?

Niliwahi kuwa kwenye mahusiano na binti wa kizanaki, akadai kuwa Makongoro amewahi kumtaka kimapenzi nikahisi ni uongo, ila nimeanza kumuamini baada kuona comment yako. Watoto wa wakubwa huwa wanakuwa na tabia ambazo sio nzuri.
kumtongoza msichana ni tabia isiyo nzur??
 
Ndio muelewe tukisema nyerere alikuwa mzalendo wa kweli. Anamapungufu yake kama binadamu ila alikiwa ni mzalendo sana kwa taifa lake.

Ndio maana hata watoto wake hakutaka wajihusishe na siasa kwasababu sio biashara ya familia kama hawa wa sasa ambao baba mama mtoto wote wanataka madaraka.
Ok, lkn wahenga walisema "mtoto wa nyoka ni nyoka"?
 
Wanabodi, Salaam!
Kwa wabobezi wa saikolojia na sosholojia naombeni mniambie kwa nini tangu tupate Uhuru kisha kuungana Zanzibar na Tanganyika familia za Mwinyi na Karume tushapata marais mara mbili (Ally Hassan Mwinyi, Hussein Ally Hassan Mwinyi na Abeid Karume na mwanaye Aman Abeid Karume

Kwa familia ya Mwl Nyerere tangu ang'atuke nadhani mwaka 1985 hadi leo hakuna mtoto hata mmoja aliyeweza hata kufurukuta na kuingia kwenye tatu bora ya wagombea urais nchini - hata Madaraka Nyerere juzi tu kura za maoni kwa nafasi ya ubunge zilimtupa mbali kisha kamati kuu ya CCM haikurudisha jina lake.

Sasa, hii hali ya watoto wa mwasisi wa taifa hili kutopenya kwenye vinyanganyiro vya nafasi za uongozi zinatokana na nini?
Siasa ni moja ya kazi miongoni mwa kazi nyingi ndani ya jamii za watu. Mtu anaweza akachagua kufanya siasa au kutofanya siasa. Wahenga waliwahi kusema kuwa "Ni rahisi kumsukuma Punda kufika mtoni, lakini si rahisi kumlazimisha ayanywe maji ya mtoni."

Mtu atafanya kazi ambayo nafsi yake imemtaka akaifanye na sio uungwana kwa mtu kufanya kazi ambayo nafsi yake haikutaka. Kwa kufanya hivyo, Ni rahisi kupelekwa kuzuka kwa mtokeo mabovu ya kazi hiyo. Hakuna kanuni ya maisha ambayo huwaongoza watu itokayo nje ya nafsi ya mtu mwenyewe. Mazingira huwezesha kanuni hiyo ya mtu ili matokeo ya kazi ya mtu yaweze kuwa na tija kwa jamii, lakini sio kutoa kanuni juu ya maisha ya mtu huyo!

Baba anaweza kuwa daktari na mama akawa nesi lakini mtoto akawa mwalimu wa historia, na hiyo si miujiza balo ndio kanuni ya maisha itokayo ndani ya nafsi ya mtu mwenyewe.

Katika jambo hili, ningependa hoja ikae katika misingi ya kidemokrasi na usawa. Kwamba suala la uongozi lisitegemee zaidi ukoo wa viongozi balo uwezo na utayari wa mtu anayetaka kuongoza. Dhambi ni kushangaa kwa nini watoto wa Rais fulani hawajawahi Marais, dhambi ni kumlazimisha kila mtoto wa Rais basi naye awe Rais n.k. Jambo la kheri ni kuona kwamba hata mtoto wa Rais fulani anaouwezo wa kuongoza na kwa dhati anataka kweli kuongoza hivyo atafaa kuwa Rais. Hapo tumetumia vigezo vya uwezo na sio ukoo, jambo hilo ni la kheri na ndio usawa ndani ya demokrasi.

Karibuni Dodoma.
 
Lakini Mwalimu alikuwa na watoto wengi mmoja wao alikuwa classmate Mkwawa High school, alikuwa Emily Magige, kama sikosei alisoma shahada ya Engineering USDM miaka ya sabini

Sio huyo tu kaka zake walikuwa wanajeshi maofisa wenye ujuzi.
Na wewe umezeeka sasa, story yoka imetusaidia nin wala haiendani na uzi
 
Wakuu naombeni mnijuze, licha ya kusoma sana na baba yao kuwa mpigania uhuru wa Taifa hili, kwanini watoto wa mzee mchonga wapo wapo tu, hawana nyadhifa kubwa, hawana mbele wala nyuma? Hali ni tofauti kwa watoto wa Mzee ruksa, Mzee Karume, JK na wengineo kwanini?
Hivi hili swali lilijibiwa kweli ?
 
Waungwana, Naomba anaefahamu awataje Watoto wa Baba wa Taifa Mwalimu JK Nyerere na Mama Maria Nyerere kwa mtiririko yaani wa kwanza mpaka wa mwisho.
 
Back
Top Bottom