Kwanini watoto wa Mzee Mchonga hawana nyadhifa kubwa Nchini?

Kwanini watoto wa Mzee Mchonga hawana nyadhifa kubwa Nchini?

Baada ya kushuhudia madhila yatokanayo na siasa na unafiki wake ndo maana walishindwa.Makongoro alipata kuwa mbunge wa Arusha mjini kupitia Nccr Mageuzi.Wakati huo baba yake bado yupo, ukipata jibu kwanini bb nccr na siyo ccm utakubaliana na mimi
Sasa kwanini basi hakuendelea ku-excel kupitia upinzani?! Ni wanasiasa wangapi leo hii wapo juu lakini uwezo wao muda wote umekuwa ni kupitia huko huko upinzani?!
 
Wanabodi, Salaam!
Kwa wabobezi wa saikolojia na sosholojia naombeni mniambie kwa nini tangu tupate Uhuru kisha kuungana Zanzibar na Tanganyika familia za Mwinyi na Karume tushapata marais mara mbili (Ally Hassan Mwinyi, Hussein Ally Hassan Mwinyi na Abeid Karume na mwanaye Aman Abeid Karume

Kwa familia ya Mwl Nyerere tangu ang'atuke nadhani mwaka 1985 hadi leo hakuna mtoto hata mmoja aliyeweza hata kufurukuta na kuingia kwenye tatu bora ya wagombea urais nchini - hata Madaraka Nyerere juzi tu kura za maoni kwa nafasi ya ubunge zilimtupa mbali kisha kamati kuu ya CCM haikurudisha jina lake.

Sasa, hii hali ya watoto wa mwasisi wa taifa hili kutopenya kwenye vinyanganyiro vya nafasi za uongozi zinatokana na nini?
Mtoto wa Nyerere!!!
Makongoro!!!
 
Tukisema Mwl hakuwaandaa sio kweli maana watoto wake wote wana elimu nzuri tu, na hayo ndo maandalizi tosha, Kinachotakiwa ni viongozi Kuwashika mkono, hilo ndo linakosekana, kwani hata hao watoto wa Mwinyi na Karume wana pata support kwa kushikwa mkono, sasa katambi ana elimu gani na uzoefu upi kumshinda Makongoro nyerere? , hata Uhuru Kenyatta alikuwa introduced by the system na Moi baadae Mwai kibaki akamteua kwenye serikali yake kuwa waziri wa fedha na safari yake ikaanza hivyo, kumbuka Mwai na Uhuru ni mtu na mtoto wake.

Usanii wa CCM ndo mtakapo ujua, kwenye shida utawasikia Mwl nyerere alisema hivi , ni wanafiki kuliko watu wote duniani.
Hivi mtu kama Hussein Mwinyi mtasemaje kwamba anashikwa mkono wakati aliteuliwa kuwa naibu waziri baada ya kushinda uchaguzi wa ubunge jimboni?! Ikiwa hata Magufuli ambae hakufahamika na yeyote aliteuliwa unaibu waziri baada ya kushinda ubunge huko kwao; kwanini tuone mtu kama Mwinyi anashikwa mkono wakati na yeye amepitia njia ile ile wanayopitia wanasiasa wengine?
 
Hussein Ali Mwinyi na Amani Abed Karume wamepata walichopata kwakuwa wana sifa za kutosha.
Makongoro na Madaraka wamekosa walichotaka kwenye siasa sababu hawana sifa.
Kwenye siasa unashinda kwa sifa zako binafsi hata kama mzazi wako alikuwa kiongozi mkubwa.
Hakuna kitu kigumu kwenye.siasa kama za Tanzania kuchanua wakati mzazi wako alikuwa kiongozi mkubwa.
Mara nyingi wapinzani wako watakusema vibaya kuwa unabebwa nk.
Lakini ukiwa na sifa njema wapinzani wako wanakwama.
Ushindi wako unatokana na mambo mengi yanayokuhusu wewe mwenyewe.
 
Watoto wa Mwalimu Nyerere hawakuandaliwa vyema kwa "kazi kubwa" ! Mwalimu alikuwa busy sana na mambo ya Uhuru na Ukombozi wa Afrika!

Katika kufeli kwa Watoto wa Mwalimu Nyerere ,Mama Maria anaomchango mkubwa sana!
Watoto wengi uaribika kimalezi kama mama ni legelege na si mentor mzuri.

Pia waliomzunguka Mwalimu Nyerere akina Joseph Butiku walikuwa watu wabinafsi sana na wasiomwambia Mwalimu ukweli kuhusu malezi ya familia yake.

Walibaki kumwabudu na kumsifia tu Mwalimu bila kuangalia succession plan yake.
Familia ya Mwalimu Nyerere imedhihirisha kabisa kuwa " Leaders are made and not born"!

Kwa akili (IQ) aliyokuwa nayo Mwalimu Nyerere hata kama angeoa mwanamke " dull" kiasi gani lazima angezaa " nyoka" walau mmoja au wawili!
Case closed.
 
KATIKA MAMBO AMBAYO CCM NAWAONA WANAFIKI KATIKA HILO JAMBO WANASHINDWA KUWAPA HATA NAFASI MUHIMU SERIKALI NA NDIO MAANA TAIFA LINAENDELEA KUWA DUNI KIUCHUMI BABA WA TAIFA KANUNA HUKO
Ndiyo hapa uko sahihi, mzee wa Taifa kakunja roho, yaan aliowaachia madaraka wanagawana vyeo kwa watoto wao, halafu yeye jasho lake halina maslahi kwa wanae.
 
Wanabodi, Salaam!
Kwa wabobezi wa saikolojia na sosholojia naombeni mniambie kwa nini tangu tupate Uhuru kisha kuungana Zanzibar na Tanganyika familia za Mwinyi na Karume tushapata marais mara mbili (Ally Hassan Mwinyi, Hussein Ally Hassan Mwinyi na Abeid Karume na mwanaye Aman Abeid Karume

Kwa familia ya Mwl Nyerere tangu ang'atuke nadhani mwaka 1985 hadi leo hakuna mtoto hata mmoja aliyeweza hata kufurukuta na kuingia kwenye tatu bora ya wagombea urais nchini - hata Madaraka Nyerere juzi tu kura za maoni kwa nafasi ya ubunge zilimtupa mbali kisha kamati kuu ya CCM haikurudisha jina lake.

Sasa, hii hali ya watoto wa mwasisi wa taifa hili kutopenya kwenye vinyanganyiro vya nafasi za uongozi zinatokana na nini?
Kikwete tunajiandaa na tumejiandaa kweli kweli, uongo ndugu zanguuu?
 
Wanabodi, Salaam!
Kwa wabobezi wa saikolojia na sosholojia naombeni mniambie kwa nini tangu tupate Uhuru kisha kuungana Zanzibar na Tanganyika familia za Mwinyi na Karume tushapata marais mara mbili (Ally Hassan Mwinyi, Hussein Ally Hassan Mwinyi na Abeid Karume na mwanaye Aman Abeid Karume

Kwa familia ya Mwl Nyerere tangu ang'atuke nadhani mwaka 1985 hadi leo hakuna mtoto hata mmoja aliyeweza hata kufurukuta na kuingia kwenye tatu bora ya wagombea urais nchini - hata Madaraka Nyerere juzi tu kura za maoni kwa nafasi ya ubunge zilimtupa mbali kisha kamati kuu ya CCM haikurudisha jina lake.

Sasa, hii hali ya watoto wa mwasisi wa taifa hili kutopenya kwenye vinyanganyiro vya nafasi za uongozi zinatokana na nini?
Ndio muelewe tukisema nyerere alikuwa mzalendo wa kweli. Anamapungufu yake kama binadamu ila alikiwa ni mzalendo sana kwa taifa lake.

Ndio maana hata watoto wake hakutaka wajihusishe na siasa kwasababu sio biashara ya familia kama hawa wa sasa ambao baba mama mtoto wote wanataka madaraka.
 
Back
Top Bottom