Kwanini watoto wa Mzee Mchonga hawana nyadhifa kubwa Nchini?

Kwanini watoto wa Mzee Mchonga hawana nyadhifa kubwa Nchini?

Niliwahi kuwa kwenye mahusiano na binti wa kizanaki, akadai kuwa Makongoro amewahi kumtaka kimapenzi nikahisi ni uongo, ila nimeanza kumuamini baada kuona comment yako. Watoto wa wakubwa huwa wanakuwa na tabia ambazo sio nzuri.
Kwahiyo uliona wewe ndo mwenye haki ya kuwa na huyo binti na siyo makongoro?
 
Watoto wa Karume na Mwinyi walibebwa na system wakati watoto wa Nyerere hawajawahi kubebwa popote. Huyu Mwinyi alitoka shule tu na kupewa unaibu waziri baada ya baba yake kuondoka madarakani, na tangu hapo hajawahi kufanya kazi nyingine yoyote zaidi ya kuwa anateuliwa uwaziri miaka yote hadi sasa anakuwa rais. Alisomea udaktari lakini hajawahi kuandika prescription yoyte hata ya kutibu mafua.
Angalia anachofanya Mwinyi Zanzibar halafu useme alibebwa.jamaa anaonyesha njia
 
Angalia anachofanya mwinyi zanzibar alaf useme alibebwa.jamaa anaonyesha njia
Anachofanya sasa hivi na alifikaje hapo hayo ni mambo mawili tofauti. Katika watu takriban milioni 60 watanzania kuna watu ambao hawajulikani leo lakini wakipewa uongozi watafanya mambo mazuri sana; wanawezaje kuupata huo uongozi ndilo swali kuu hapa.
 
Watoto wa Karume na Mwinyi walibebwa na system wakati watoto wa Nyerere hawajawahi kubebwa popote. Huyu Mwinyi alitoka shule tu na kupewa unaibu waziri baada ya baba yake kuondoka madarakani, na tangu hapo hajawahi kufanya kazi nyingine yoyote zaidi ya kuwa anateuliwa uwaziri miaka yote hadi sasa anakuwa rais. Alisomea udaktari lakini hajawahi kuandika prescription yoyte hata ya kutibu mafua.
Rosemary Nyerere alikuwa Mbunge wa kuteuliwa mwaka 2000-2005 wakati wa Mkapa. Je baada ya kuwa Mbunge yeye mwenyewe binafsi alijiongeza kiasi gani? ukibebwa bebeka!!

Makongoro Nyerere alishinda ubunge wa Arusha mjini kwa NCCR mwaka 1995-2000. Je akiwa Mbunge ali behave namna gani kwa wapiga kura wake?

Emily Magige amewahi kama mara 2 kuwa Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mara?? je ali-perform vipi?

Andrew na John (RIP) wamewahi kuwa na matatizo ya afya ya akili. Madaraka anasimamia miliki ya Nyerere huko Butiama.

Je, ulitaka wabebwe kwa kiwango gani?
 
KATIKA MAMBO AMBAYO CCM NAWAONA WANAFIKI KATIKA HILO JAMBO WANASHINDWA KUWAPA HATA NAFASI MUHIMU SERIKALI NA NDIO MAANA TAIFA LINAENDELEA KUWA DUNI KIUCHUMI BABA WA TAIFA KANUNA HUKO
 
Rosemary Nyerere alikuwa Mbunge wa kuteuliwa mwaka 2000-2005 wakati wa Mkapa. Je baada ya kuwa Mbunge yeye mwenyewe binafsi alijiongeza kiasi gani? ukibebwa bebeka!! Makongoro Nyerere alishinda ubunge wa Arusha mjini kwa NCCR mwaka 1995-2000. Je akiwa Mbunge ali behave namna gani kwa wapiga kura wake? Emily Magige amewahi kama mara 2 kuwa Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mara?? je ali-perform vipi? Andrew na John (RIP) wamewahi kuwa na matatizo ya afya ya akili. Madaraka anasimamia miliki ya Nyerere huko Butiama. Je ulitaka wabebwe kwa kiwango gani?
Umetaja mambo ambayo ama siyo ya kubebwa (kama kugombea ubunge wa Afrika ya mashriki) au ni peripherals tu (kama mbunge wa kuteuliwa) kwani hayana nguvu kisiasa kama ya naibu waziri au waziri kamili ambaye anakuwa na madaraka nchi nzima.
 
Wanabodi, Salaam!
Kwa wabobezi wa saikolojia na sosholojia naombeni mniambie kwa nini tangu tupate Uhuru kisha kuungana Zanzibar na Tanganyika familia za Mwinyi na Karume tushapata marais mara mbili (Ally Hassan Mwinyi, Hussein Ally Hassan Mwinyi na Abeid Karume na mwanaye Aman Abeid Karume

Kwa familia ya Mwl Nyerere tangu ang'atuke nadhani mwaka 1985 hadi leo hakuna mtoto hata mmoja aliyeweza hata kufurukuta na kuingia kwenye tatu bora ya wagombea urais nchini - hata Madaraka Nyerere juzi tu kura za maoni kwa nafasi ya ubunge zilimtupa mbali kisha kamati kuu ya CCM haikurudisha jina lake.

Sasa, hii hali ya watoto wa mwasisi wa taifa hili kutopenya kwenye vinyanganyiro vya nafasi za uongozi zinatokana na nini?
Wao na baba yao hawakuwa na hawana nia ya kujinufaisha kwa lolote.Hiyo familia itazidi kuheahimika kwa moyo wao huo.
 
Anachofanya sasa hivi na alifikaje hapo hayo ni mambo mawili tofauti. Katika watu takriban milioni 60 watanzania kuna watu ambao hawajulikani leo lakini wakipewa uongozi watafanya mambo mazuri sana; wanawezaje kuupata huo uongozi ndilo swali kuu hapa.
Kuna jambo halipo sawa kuhusu watoto wa Mwalimu manake hata wale waliowahi kupata kuwatumikia wananchi hawakuonesha consistence yoyote. Na kuhusu Hussein Mwinyi, CV yake inasema tofauti na unachosema wewe. Kwa bahati mbaya sifahamu taaluma ya afya inavyoendeshwa endeshwa lakini CV ya Hussein inaonesha badala ya kumaliza MD, amefanya kazi Muhimbili kama Registral na MD, Kaiuruki kama Specialist na Lecturer. CV yake inaonesha amepata nafasi ya kwanza ya uteuzi miaka 7 baada ya kuwa ameshachukua MD (awamu ya Mkapa).

Nisichofahamu ni kuona muda huo ambao ni takribani miaka 9 pia alikuwa anasoma Masters na PhD UK. Sasa kama udaktari na wenyewe unaweza kusoma bila coursework, hapo ndo sina uhakika. Sasa kama unaweza kusoma bila kuingia darasani (hususani masters) sioni kubebwa kwa Hussein kunaingiaje ingiaje hapo hasa ukizingatia wakati anachukua uteuzi kwa mara kwanza, alishakuwa mbunge. CV inaonesha amemaliza MD 1991, wakati ubunge na uteuzi ni mwaka 2000.
 
Wao na baba yao hawakuwa na hawana nia ya kujinufaisha kwa lolote.Hiyo familia itazidi kuheahimika kwa moyo wao huo.
OK, kweli?
Nafikiria tu Kibaki alivyomwibua Uhuru Kenyatta na kumpandisha - Kenyan wengi waliimba George Saitoti nk

Basi kwa vyovyote vile kuna jambo!
 
Wao na baba yao hawakuwa na hawana nia ya kujinufaisha kwa lolote.Hiyo familia itazidi kuheahimika kwa moyo wao huo.
Tusidanganyane. Makongoro ameshawahi kufanya siasa lakini zikamshinda. Kuna binti mwingine wa Mwalimu alishawahi kuteuliwa ubunge lakini haku-shine.
 
And always karma is a bitch
Ukiwa na nafasi chochote uwatendeacho watu familia yako uliyoiacha duniani ndo itaathirika.Kizazi cha mobotu,bokasa,idiamini na madikteta wote hakina heshima tena duniani hakisafishiki kizazi na kizazi zinaitwa dead family uzao mfu. Familia ya bob marley, mandela, uitwa living family familia zinazoishi milele.
Ukiwatendea watu mabaya umeharibu uzao wako utakuwa ni wenye laana maisha yote duniani
 
Wanabodi, Salaam!
Kwa wabobezi wa saikolojia na sosholojia naombeni mniambie kwa nini tangu tupate Uhuru kisha kuungana Zanzibar na Tanganyika familia za Mwinyi na Karume tushapata marais mara mbili (Ally Hassan Mwinyi, Hussein Ally Hassan Mwinyi na Abeid Karume na mwanaye Aman Abeid Karume

Kwa familia ya Mwl Nyerere tangu ang'atuke nadhani mwaka 1985 hadi leo hakuna mtoto hata mmoja aliyeweza hata kufurukuta na kuingia kwenye tatu bora ya wagombea urais nchini - hata Madaraka Nyerere juzi tu kura za maoni kwa nafasi ya ubunge zilimtupa mbali kisha kamati kuu ya CCM haikurudisha jina lake.

Sasa, hii hali ya watoto wa mwasisi wa taifa hili kutopenya kwenye vinyanganyiro vya nafasi za uongozi zinatokana na nini?
Nyerere alikuwa mjanja ila hakupenda watoto wake wawe kama yeye.

Najua sijaeleweka ila nitarudi...
 
Kiongozi umesahau hao marais mababa na watoto wao ni huko visiwani bara hatuna huo utamaduni wa monarchy! hata huyu alieko visiwani angetaka urais bongo labda angetoswa! soma stages of human development and evolution of man utaelewa!!bahati mbaya wenzetu bado wako nyuma kidogo upstairs!
 
Kuna siri hapo kwenye chanzo cha kifo chake, pengine mjukuu au kitukuu cha nyerere akaja kuwa raisi
 
Back
Top Bottom