Kwanini watu wanahoji Rais Magufuli kupeleka maendeleo Chato na Geita kwa ujumla?

Kwanini watu wanahoji Rais Magufuli kupeleka maendeleo Chato na Geita kwa ujumla?

The Assassin

JF-Expert Member
Joined
Oct 30, 2018
Posts
4,942
Reaction score
20,077
Watu wanahoji kwa nini Rais Magufuli anapeleka maendeleo kwao, Chato na Geita kwa ujumla, kama vile watu wa Chato au Geita hawastahili kupata maendeleo, sasa asipeleke Chato apeleke wapi?

Unapokuja kwenye rasilimali za nchi hii haziko kwenye mgawanyo sawa, kuna mahala pengine utafikiri sio Tanzania hii na mahala pengine utafikiri ni gerezani.

Mfano, Serengeti ndio mbuga maarufu kuliko zote Tanzania, kwa takwimu za Tanapa, zaidi ya 80% ya watalii na mapato ya utalii nchini yanatokana na mbuga ya Serengeti ila nenda Serengeti kwenyewe uone watu wake wakoje, wanaoneemeka ni wengine kabisa. Hata chuo tu cha utalii au chuo cha wanyamapori hakikujengwa Serengeti, vyuo vikajengwa mahala ambapo hata panya hayupo. Hata Hotel moja ya kueleweka haipo Mugumu, na hili sio bahati mbaya, lilifanyika makusudi kabisa.

Ukienda Kanda ya Ziwa kwa ujumla hakuna chuo kikuu chochote cha serikali ukiachana na Chuo Kikuu Huria, sehemu nyingine vyuo vya serikali vimejaa eneo moja kama siafu. Hili pia halikuwa linafanyika kwa bahati mbaya, ni makusudi kabisa. Mwaka huu NBS walitoa takwimu za mikoa masikini zaidi, miwili ilitoka Kanda ya Ziwa, Geita na Kagera, unajiuliza kanda tajiri kwa rasilimali kiasi kile inakuaje masikini, jibu ni moja tu, mgawanyo usio sawa wa rasilimali za nchi.

Sasa pale Rais anapojaribu kuwakumbuka watu waliokuwa wamesahaulika kwenye keki ya taifa hili, maneno yanakuwa maneno, kwamba awaache wale ambao hawakuwa na kitu awakumbuke wale walionavyo vimejaa, haiwezekani.

Watu mnapata wapi ujasiri kuhoji watu wa Chato na Geita kukumbukwa kwenye keki ya taifa?
 
Hapana.

Serengeti hai contribute 80% na siyo chanzo kikuu cha mapato ya utalii.

Pamoja na hayo wananchi wa maeneo yanayopakana na Serengeti wanastahili kufaidika na mapato yanayopatikana hapo.

Suala hili liliwahi kuzungumziwa na Mh. Mbatia bungeni alipokuwa akilaumu kwamba wananchi wanaopakana na vyanzo vya utalii kama Mlima Kilimanjaro, Serengeti, Ngorongoro, Katavi, etc hawapewi GAWIO kutoka katika mapato ya vyanzo hivyo vya utalii.
 
Hakimu Mfawidhi, Watu wa Kibondo kwa nini nao wasihoji kutokana na ubovu wa barabara zao hasa nyakati za mvua? Huku wakisikia na kuona ktk vyombo vya habari ya kuwa wenzao wanakula mema ya nchi.
tapatalk_1575814995710.jpeg
 
Mtu yeyote mwenye akili timamu atawekeza kwenye mikoa hiyo ya Kanda ya Ziwa na mikoa kama Tabora n.k
Kwani wapiga kura Wasukuma na Wanyamwezi ni zaidi ya theluthi mmoja ya wananchi wote wa Tanzania wanaostahili kupiga kura. Wengi wape.
 
Watu wanahoji kwa nini rais Magufuli anapeleka maendeleo kwao, Chato na Geita kwa ujumla, kama vile watu wa Chato au Geita hawastahili kupata maendeleo, sasa asipeleke Chato apeleke wapi?

Watu mnapata wapi ujasiri kuhoji watu wa chato na geita kukumbukwa kwenye keki ya taifa?
Hao wanaohoji ni wivu tuu unawasumbua!, charty begins at home.
P
 
..hapana.

..Serengeti hai contribute 80% na siyo chanzo kikuu cha mapato ya utalii.

..pamoja na hayo wananchi wa maeneo yanayopakana na Serengeti wanastahili kufaidika na mapato yanayopatikana hapo.

..suala hili liliwahi kuzungumziwa na Mh.Mbatia bungeni alipokuwa akilaumu kwamba wananchi wanaopakana na vyanzo vya utalii kama mlima Kilimanjaro, Serengeti, Ngorongoro, Katavi, etc hawapewi GAWIO kutoka ktl mapato ya vyanzo hivyo vya utalii.
Hizi ni takwimu za tanapa na wizara ya utalii, sasa ningetegemea ukaja na takwimu kupinga hili, sijaziona.
 
Mikoa ya Tabora, Kigoma, Katavi na Rukwa ni mikoa pekee ambayo kwa kiwango kikubwa sana imetelekezwa na awamu zote.

Ukifika mikoa hiyo unafiikiri wanaoishi huko siyo watanzania, viongozi hufika wakati wa kampeni tu.
Watu wa Kibondo kwa nini nao wasihoji kutokana na ubovu wa barabara zao hasa nyakati za mvua? Huku wakisikia na kuona ktk vyombo vya habari ya kuwa wenzao wanakula mema ya nchi.View attachment 1285596
 
..hapana.

..Serengeti hai contribute 80% na siyo chanzo kikuu cha mapato ya utalii.

..pamoja na hayo wananchi wa maeneo yanayopakana na Serengeti wanastahili kufaidika na mapato yanayopatikana hapo.

..suala hili liliwahi kuzungumziwa na Mh.Mbatia bungeni alipokuwa akilaumu kwamba wananchi wanaopakana na vyanzo vya utalii kama mlima Kilimanjaro, Serengeti, Ngorongoro, Katavi, etc hawapewi GAWIO kutoka ktl mapato ya vyanzo hivyo vya utalii.
Hasa hasa Kilimanjaro
 
Hakimu Mfawidhi, Kwa uelewa wako, unaamini kuwa airport kubwa ikijengwa Chato, ndiyo itaondoa umaskini?

Umaskini hauondolewi na serikali bali unaondolewa na mtu mmoja mmoja. Serikali kazi yake ni kujenga mazingira wezeshi.

Najiuliza, hivi shughuli kuu za kiuchumi za wananchi wa Chato na Geita kwa ujumla ni nini? Nahisi ni kilimo, ufugaji na uvuvi. Kama nipo sahihi - cha kujiuliza, airport ya Chato itamsaidia namna gani na kwa kiasi gani mvuvi, mfugaji na mkulima wa Chato? Namna nyingine, uwanja ule ni prestige tu kuliko kuwabadilisha wananchi wa Chato na Geita.

Kwa kadiri ya report ya kitengo cha takwimu, Mikoa mitatu inayoongoza kwa utajiri Tanzania ni
1) Dar
2) Kilimanjaro
3) Njombe

Sasa niambie, mkoa kama Njombe umepewa upendeleo gani na serikali hata ukaweza kuizidi mikoa kama Arusha au Mwanza?

Wanaofikiria kuwa upendeleo wa serikali katika kutoa huduma ndio utaleta maendeleo wanajidanganya.

Ndege zitatua Chato lakini wasafiri hawatakuwa wa Chato. Daraja litajengwa Busisi lakini watakaopita na magari ya kifahari juu yake hawatakuwa wananchi wa Misungwi au Sengerema. Faida kubwa kwao itakuwa kuwa kwanza kila siku kuyaona magari yakipita kwenye daraja refu.

Kama kuna kanda au mkoa ambao ni maskini na wanaamini kuwa ni kwa sababu serikali haikuwapendelea, waende wakawaulize watu wa Njombe ni kwa vipi wanaweza kuwa na vipato vizuri huku Serikali kwa muda mrefu ikiwa imewasahau? Nadhani makanisa yameshirikiana na wanachi vizuri zaidi katika kuyatafuta maendeleo kuliko hata serikali.

Kupendelewa kunadumaza akili, huondoa fikra za jitihada na hujenga utegemezi.
 
Back
Top Bottom