Kwanini wimbo wa Killy na Harmonize 'ni wewe' hautambi?

Kwanini wimbo wa Killy na Harmonize 'ni wewe' hautambi?

Huwa hizo L na R anazichanganya zaidi akijilazimisha kile Kiingereza chake cha kuungaunga, lakini mdogomdogo labda mbele ya safari atajifunza jinsi ya kuzitumia kiusahihi.
Yani nikisikiliza mara mbili tu anavyochanganya hizo Herufi Huwa Mzuka unakata! Bahati mbaya hili ni Janga la wasanii wetu karibia wote! Jux ndio Balaa!
 
Yani nikisikiliza mara mbili tu anavyochanganya hizo Herufi Huwa Mzuka unakata! Bahati mbaya hili ni Janga la wasanii wetu karibia wote! Jux ndio Balaa!
Mimi huwa sisumbuliwi na hizo 'l/r' wala 'th/s' wala 'dh/z' wala 'm/n' ili mradi tu km ujumbe umeeleweka!
 
Vannyboy yule pale ana Collabo na Maluma,yeye mwenyewe ktk Level tu ya EA.

Nigeria wanabebana na wanaijeria ni wabinafsi, Nigeria kuanzia mtangazaji Promota, mameneja, watangazaji na wasanii vision yao moja tuu kukuza Industry yao kwanza. Shaka Wale alizungumza hili wanaijeria walimshambuli wakiongozwa na BurnaBoy.

Nigeria zamani kidogo Trace na MTV zinaanza kuingia Afrika zilikuwa na watangazaji wengi wa SA na hata Playlist wa South walitawala ila sasa hivi vice versa Wanaija wamejaa MTV na Trace na ukitizama Playlist basi zaidi ya 40% ni wao tuu, kujua Wanaija wanajua kuhusu ubinafsi na fitina wanazijua.

Yaani kwa kifupi kila mdau anajua wajibu wake wa kupromote mziki wa Nigeria na si kwetu huku.

Nakumbuka Vanessa aliulizwa anaionaje safari ya mziki wa bongo kimataifa, akasema bado sana kwani inatakiwa katika media kubwa za burudani za Afrika na duniani tunatakiwa kuwa na watu wetu, kwa ajili tu kusaidia kupush mziki wetu na ukiangalia kwa sasa hatuna, zamani tulikuwa na Seven na Vanessa Mdee mwenyewe kwa sasa hatuna kote Nigeria wameshika wao.
Uchambuzi mzuri!
 
Nikiri kabisa nilikua siujui ila one nikasikia dogo mmoja anausikiliza alafu kaweka repeat 1 ikabidi niutafute mpaka leo most played song kwenye Playlist yangu
Ni mzuri sana kwakweli
 
Muziki wa Tanzania una makundi ya kimaslahi.

Media zinamiliki Wasanii na Matamasha. Huku zikipewa nguvu na Mashabiki uchwara waliojaa Chuki.

Hakuna independent promoters.

Yaani, Clouds wana tamasha la la Fiesta, na hivyo wasanii wataokubali kutumbuiza kwenye Tamasha lao cheaply ndio watakaokuwa wanapata strong promotion kwenye Media yao.

Hivyo hivyo kwa Wasafi ( Wasafi TV ), E! TV ( Muziki Mnene) na EATV.

Kwahiyo Kama wewe haupo kwenye MTANDAO huo maana yake, hutapata SHOWS Wala ngoma zako hazitapata rotation kubwa kwenye main stream media.

Na hii ndio sababu sasa hivi Msanii 'kutoka" na kuvuma nje ya mfumo huu ni ngumu sana. Hali hi, imewapoyeza pia wasanii wa zamani.

Vile vile, Kama Msanii huna uwezo wa kuandaa shows zako mwenyewe na Matamasha ndio basi tena.

Na kibaya akili za wabongo zilivyo na Ushabiki uchwara, mpaka playlist anatengenezewa, maana mpaka aambiwe na media fulani kiwa hiyo ngoma ni Kali.
Umenena!!!
 
nawasalimu kwa jina la JMT!
Nauzungumzia huu wimbo wa Killy aliyomshirikisha Harmonize uitwao 'ni wewe'. Jamani, huu wimbo unachosababisha usitambe ni nini haswaa kama sio uchawi tu?!!!

Melody nzuri,
Mashairi mazuri,
Beat poa kabisa ya kizamani na kisasa iliyotulia,
Shooting ni njema kabisa.

Vyote vinastahili kusikilizwa harusini, clubs na hata mitaani. Ajabu ni kuwa napita humo mwote na ni nadra kuusikia.

Nazisikia nyimbo zingine zinazopigwa mara kwa mara,.....nabaki nashangaa tu!

Mwishowe nimeona nihitimishe tu kuwa kumbe hapa Bongo kwenye muziki inabidi uroge pia, yaani ni WACHAWI KUMBE!
Uchawi upo. Hebu fikiria Steve nyenyere eti msanii nae
 
Yani nikisikiliza mara mbili tu anavyochanganya hizo Herufi Huwa Mzuka unakata! Bahati mbaya hili ni Janga la wasanii wetu karibia wote! Jux ndio Balaa!
Nashindwa kujua hasa kinachosababisha uzuzu huu ni kitu gani, tena hili janga ni kubwa zaidi kwa artists wa kiume.
 
Kama kuna uchawi mbona hawapati grammy na kwenye mpira mbona hawana kombe lolote la maana???
 
Aisee, hivi ugonjwz huu jf utaisha lini?!!!!
Ukianzisha mada inayohusu wabunge unaitwa mbunge,
Ukuanzisha inayohysu walimu unahisiwa kuwa ni mwalimu,
Polisi unahisiwa ni polisi,
Ulinzi, utahisiwa mlinzi,
N.k

Yaani tabu tupu!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nashindwa kujua hasa kinachosababisha uzuzu huu ni kitu gani, tena hili janga ni kubwa zaidi kwa artists wa kiume.
Kabisa! Wasanii wakike kwakweli wanajitahidi Sana! Hawa wasanii hasa Wakubwa walitakiwa wawe na Team ya watu wa Sarufi warekebishe Makosa kama Haya! Makosa kama Haya yanaondoa ladha kabisa Ya Muziki.
 
  • Thanks
Reactions: Qwy
Mimi huwa sisumbuliwi na hizo 'l/r' wala 'th/s' wala 'dh/z' wala 'm/n' ili mradi tu km ujumbe umeeleweka!
Kwakweli Mimi Huwa napatwa na Ghadhabu ya Kufa Mtu! Huwa nataman niwachane sema ndio Sina Pa kuwapata! Maana page zao sifuatilii kiivyo!
 
Kabisa! Wasanii wakike kwakweli wanajitahidi Sana! Hawa wasanii hasa Wakubwa walitakiwa wawe na Team ya watu wa Sarufi warekebishe Makosa kama Haya! Makosa kama Haya yanaondoa ladha kabisa Ya Muziki.
Wakishaanza kuokotaokota vijisenti wanawaona wasomi si lolote si chochote hivyo umuhimu wa perfection kwenye sarufi wanaudharau plus the majority of their fans nao ni walewale tu sifuri kichwani, nadhani kwa factors hizo pamoja na nyingine kadhaa ndivyo vinapelekea yote haya.
 
Wakishaanza kuokotaokota vijisenti wanawaona wasomi si lolote si chochote hivyo umuhimu wa perfection kwenye sarufi wanaudharau plus the majority of their fans nao ni walewale tu sifuri kichwani, nadhani kwa factors hizo pamoja na nyingine kadhaa ndivyo vinapelekea yote haya.
Masuala ya herufi hatakwa ninyi mnaojiita Wasomi ni trash.

Mara nyingi Hawa wapiga kelele mitandaoni wa sarufi ni wapuuzi fulani ambao hawana Cha maana wanachofanya zaidi ya porojo na majungu...

Unazungumzia sarufi na herufi as if kwenye Muziki watu wanaiba Kiswahili sanifu.

Muziki una lugha yake Kama ilivyo kwenye mpira. Sioni sababu kubwa ya kulazimisha mashairi ya Muziki yafanane na mashairi ya kimapokeo.
 
Masuala ya herufi hatakwa ninyi mnaojiita Wasomi ni trash.

Mara nyingi Hawa wapiga kelele mitandaoni wa sarufi ni wapuuzi fulani ambao hawana Cha maana wanachofanya zaidi ya porojo na majungu...

Unazungumzia sarufi na herufi as if kwenye Muziki watu wanaiba Kiswahili sanifu.

Muziki una lugha yake Kama ilivyo kwenye mpira. Sioni sababu kubwa ya kulazimisha mashairi ya Muziki yafanane na mashairi ya kimapokeo.
You must be very stupid, inaelekea umedandia tu bila kuelewa tunachokijadili ni nini.
Kuingia kwenye discussion na judgemental mentality huku ukiitumia post ya mwisho kama ndiyo reference umefeli sana, literally topic inahusu kuzichanganya L na R kunavyoharibu ladha na primarily ndiyo main issue kwa aliyeianzisha kujadili hiki ulichokuta tunajadiliana.
Na vilevile for your information hakuna mtu anayemlazimisha mtu mwingine kitu chochote kama ulivyotanabaisha kwenye bandiko lako, kuelimishana si porojo wala majungu kwani wote tunajifunza mambo mapya kila uchwao.
Humu haujui maisha ya mtu, wala umri, wala kazi anayoifanya na hata nchi anayoishi hivyo point yako kuwa watu wanao-discuss issues hawana cha maana wanachofanya is an absurdly sickening statement kwani kama wewe uko humu kwa kuwa haujui unachofanya maishani usidhani wote humu wako kwenye category hiyo kama wewe.
 
Back
Top Bottom