Kwanini Yesu hakuwa na wanafunzi wanawake?

Kwanini Yesu hakuwa na wanafunzi wanawake?

Mungu si mtu,,,mbona mnapingana,

Tushike lipi?View attachment 2580809
Usiwaongezee maumivu swali lile linatosha kabisa,,hili unalowaongezea watajaza server za jf mpk uchakae,habari ya Mungu nwana Mungu roho Mungu mtoto Ina mapichapicha sana.

Na ukiwaambia watofautishe kati ya Mungu na Yesu napo linazuka Bomu la himars😁
 
Demu wake; Maria Magdalena asingekubali kurisk mahusiano yake. Itakuwa aliweka kauzibe.
 
Bila kudharau wanawake - tunatakiwa kutumia akili kutambua asili ya uumbaji na mgawanyo wa majukumu kwa jinsia
Hatujadharau wanawake,vitabu vyote vya dini mwanamke amepewa hadhi ya kipekee na utukufu usioelezeka ,Cha kushangaza yanayohubiriwa kwenye madhabahu ni tofauti na aliyofundisha Yesu kuanzia Kwa madam Mchungaji Rwakatare ,Zumaridi mpk Kwa Don Davie ,,,mmeitoa wapi hiyo amri ya kutuletea wachungaji na mitume ya kike Hali ya kuwa Yesu hakuwa expose wanawake??
 

Yesu Kristo alikuwa na wanafunzi wanawake, ingawa idadi yao ilikuwa ndogo ikilinganishwa na idadi ya wanafunzi wa kiume. Katika Agano Jipya, tunaona majina ya wanawake waliokuwa wanafunzi wa Yesu, kama vile Maria Magdalena, Maria mama yake Yakobo na Yosefu, Yohana na wengine wengi. Wanawake hawa walikuwa mashuhuda wa kwanza wa ufufuo wa Yesu na walikuwa na jukumu muhimu katika kueneza habari njema ya wokovu.
Inawezekana kwamba katika jamii ya Kiyahudi ya wakati huo, ilikuwa nadra sana kwa wanawake kuwa wanafunzi wa kiongozi wa kidini, na hivyo inawezekana kwamba jamii iliwazuia wanawake kufanya hivyo. Hata hivyo, Yesu alionyesha huruma na upendo kwa wanawake na alikuwa na uhusiano wa karibu sana na wanawake, hivyo inawezekana kwamba alikuwa na wanafunzi wanawake ambao hawajatajwa katika Maandiko Matakatifu
 
Hatujadharau wanawake,vitabu vyote vya dini mwanamke amepewa hadhi ya kipekee na utukufu usioelezeka ,Cha kushangaza yanayohubiriwa kwenye madhabahu ni tofauti na aliyofundisha Yesu kuanzia Kwa madam Mchungaji Rwakatare ,Zumaridi mpk Kwa Don Davie ,,,mmeitoa wapi hiyo amri ya kutuletea wachungaji na mitume ya kike Hali ya kuwa Yesu hakuwa expose wanawake??

Kupitia mwanamke Hawa/Eva dhambi iliingia ulimwenguni na kupitia mwanamke Mariam mwanamke alirudishiwa heshma kwa kumbeba Kristo Yesu
Na adhabu ya hiyo dhambi ndio ilimfanya mwanamke ashindwe kufanya baadhi ya majukumu

ADHABU YA MWANAMKE
MWANZO 3:15-16
15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.
16 Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.

LUKA 1:28-35
28 Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe.
29 Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?
30 Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.
31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.
32 Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake.
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.
34 Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?
35 Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.
 
Yesu alikuwa na wanafunzi wengi tu wanawake. Wengi sana! Kwa wale 12 ndio hapakuwa na mwanamke. Wale waliitwa mitume.

mfano mojawapo wa hao wanafunzi, ni Mariamu (siye mama yake Yesu) ,Martha, na Mariamu Magdalena et al

JESUS IS SAVIOR
 
1. Period kila mwezi, muda wa kuhubiri injili tungetaka kwenda kubadili taulo na kuoga.

2. Tungewatia majaribuni mitume sanasana Yuda sababu ana tamaa sana.

3. Tungekua hata wanawake wawili kwenye hiilo kundi tungegombana kila siku.
 
1. Period kila mwezi, muda wa kuhubiri injili tungetaka kwenda kubadili taulo na kuoga.

2. Tungewatia majaribuni mitume sanasana Yuda sababu ana tamaa sana.

3. Tungekua hata wanawake wawili kwenye hiilo kundi tungegombana kila siku.
4. Aliyaona mateso makali ya mitume mara baada ya kuwaacha wakatangaze injili
 
Back
Top Bottom