Kwanini zabuni ya kuonesha Ligi Kuu Tanzania Bara haikutangazwa, kapewa Azam moja kwa moja?

Kwanini zabuni ya kuonesha Ligi Kuu Tanzania Bara haikutangazwa, kapewa Azam moja kwa moja?

Tender ilitangazwa na kampuni zili bid, wakati wa kufungua technical proposals zao ulifanyika kwa uwazi tena kwenye Tv last month na kipindi kilikuwa live. Ni vyema ungeuliza kuliko kuhitimisha kwa vitu ambavyo huna ufahamu navyo.

Pili, Je tenda hii ya Azam ina faida kwa mpira wetu wa Tz, jibu ni ndio, sponsor mkuu Vodacom anatoa 3bn kwa mwaka saivi wakati Azam yeye ni broadcasting right tu amekubali kutoa 22bn kwa mwaka, kabla Azam alikuwa anatoa 23bn kwa miaka mitano ( 4.5bn kwa mwaka) hivyo kupanda hadi 22bn kwa mwaka ni ongezeko kubwa hata clubs zenyewe hazikutegemea, tujifunze kushukuru.

Je, kwa nini TFF na Bodi ya ligi wamekubali mkataba wa miaka 10 badala ya mkataba mfupi, mazingira ya Tz ni tofauti na nchi zilizoendelea, huku viwanja vyetu camera sio plug and play, kuna uwezekazaji mkubwa inabidi ufanyike ili viwanja vyetu vyote uweze kuona camera kwa angles zote, mtu hawezi kuwekeza pesa nyingi halafu mkataba unaisha kabla hata hajamaliza kurudisha pesa yote.
Hawa ndio watanzania wamejaa uchawi na umaskini,hapo utakuta anamtolea maneno Mo ukimwambia lipa salary hata mchezaji mmja Domo linalegea
 
Mleta siredi unahitajika huku boss.


Umeandika makala ndefu bila kufanya utafiti upate ukweli.

Umeambulia za USO.
 
Ujuaji mwingi kumbe huna unachojua!
Tenda ilitangazwa na kati ya walioomba ni Azam Tv, Star Times na TBC. Kati ya wote hao ni Azam pekee aliyetoa dau lililonona, wengine wote ni aidha waliichukulia poa ligi yetu au hawakuwa na mtaji wa kutosha.
Kwa dau hilo la Azam ni wazi kuwa tunaenda kuwa na ligi bora sana na yenye ushindani cause zile kero ndogondogo zilizokuwa zinazikabili team zetu zitatatuliwa na ushindani utabaki kiwanjani na si nje ya hapo.

Yaan jamaa chenga sana nakumbuka msimu wa 2017-2017 ile mechi ya hisani Kati ya yanga na Azam ilirushwa na ATN sikumbuki ilikuaje wakapewa ile mechi lkn ilirushwa hovyo sana sikuwahi kuona looh......

Et leo hii azam yupo na mitambo ya kisasa kabisa anarusha pas na malalamiko yoyote watu tuongea tu ujinga kwann kapata kwa iyo mnataka turud enz za rtd sio [emoji23][emoji23][emoji23]
 
TFF na AZAM TV zimeingia mkataba wa kudhamini ligi ya soka Tanzania Bara bila ya kutangaza Tenda na Pia hakuna mikataba mirefu kama huubwa miaka kumi.Huu ni ukiukwaji wa utaratibu wa kuonyesha mechi za mpira wa miguu nchini.

Duniani kote Tenda zinatangazwa na kila kampuni inatoa ofa lakini haipewi kuonyesha mechi zote.Mfano ligi kuu ya Uingereza ofa ni kubwa mno kila timu kubwa na ndogo zinafaidika.

Wapo skysports, Bsports na Amazon. Ligi hii ya premier ya England ina thamani ya paundi za Uingereza Bilioni 6 na mkataba na Barclays bank mnono. Sasa hapa kwetu TFF itaingiaje mkataba wa miaka 10 na kampuni moja? Ama kweli fumbo mfumbie Mjinga,mwerevu hungamua.

WIZARA YA HABARI NA MICHEZO IINGILIE KATI MKATABA HUU KWA SABABU KUU TATU; 1)Tenda itangazwe na makampuni mengi ya utangazaji yatatoa ofa ambazo zitasaidia hata timu ndogo(2) TV moja isepewe asilimia 100 kama ilivyo sasa,zigawanywe kutokana na pesa wanazo ofa(3)Mkataba uwe wa miaka 3 mitatu tu na siyo 10.Kwa wengi na kwa sasa mabillioni wanayaona mengi lakini kwa miaka 10 ni pesa ndogo sana.

Hapa pana mambo ambayo inabidi yaangaliwe.TFF wasitufanye Watanzania wajinga na mbumbumbu. HAKUNA MIKATABA YA KUONYESHA MIPIRA KWA TELEVISION MOJA KWA MIAKA KUMI TENA KWA KIASI KIDOGO CHA PESA. TFF VUNJENI MKATABA NA AZAM TANGAZENI TENDA, TV NYINGI ZITAKUJA NA OFA , TIMU ZOTE ZITAFAIDIKA ZENYE UWEZO NA AMBAZO HAZINA. WIZARA YA HABARI, MICHEZO, BMT AMKENI.
Nimesoma imebidi nicheke tu kwanza naomba acha kufananisha wanachofanya EPL kutaka kukileta fananisha chungwa na chungwa. Hiyo Billion 6 uliyotaja ni ya ndani tu UK kuna international bidding na sponsers wengine ni kama 80% ya bugdet ya Tanzania. Tuache hilo turudi hapa unasema ziko TV nyingi nchini wanataka hebu usitaje nyingi taja moja tu maana nikisema nyingi hutaweza taja moja tu. League hii ilikuwepo kabla hata ya Azam Tv kuanza sasa walikuwa wapi hao? tuseme wapo na unataka wafanye bid je unajuwa bid ina base katika commercial na technical tuache commercial unaweza kusema wako matajiri na nani anavifaa nchi hii wa kuweza kurusha mpira live coverage nchi nzima? ITV, TBC, Wasafi..... tunabaki kuongelea juu juu tu wakati ukweli tunaujuwa AZAM hana mpinzani nchi sio mpinzani wa karibu ni hakuna kabisa. Wewe unadhani ni kuonesha tu huku nyuma kuna gharama za production kuna team kubwa inafanya kazi wewe unawasha TV unapata bidhaa huko EPL production inafanywa na EPL broadcasters wanapewa bidhaa tu iko ready ya kiwango. Nakuhakikishia siku Azam wakija kufunga biashara na ndio siku tutauzika mpira wetu. Miaka 8 nyuma hakuna hata aliyekuwa na habari na league yetu kaja Azam kakuvisha vizuri umependeza kidogo sasa unataka kujifanya mimi level nyingine unaanza kudharau bwana aliyekupendezesha. Mimi nataka utaje kampuni moja tu Tanzania ya kushindana na Azam, kwa taarifa yako hata EPL mwakani wameongeza contract tu kwa Sky na BT bila bidding pia kuna kitu kinaitwa single source justification unaweza kununua sehemu moja ukithibitisha hakuna mtu mwingine anauza bidhaa hii sio kila kitu bidding.
 
Tenda ilitangazwa, tatizo wengi hamfuatiliii. Mkisikia kitu kimetangazwa, mnakurupuka na kuongea mashudu. Uwe unauliza kwanza! Hii ishu ilitangazwa mno kwenye vipindi vya michezo na magazeti. Acha kukurupuka, unajiaibisha.
Sisi wabongo kama kawaida yetu alishinda yule Vunja bei ndio watu wanaamka tenda ilitangazwa lini hatukubali utasema tuna billion2. Kama sheria zinatungwa bungeni kimya wakipigwa na rungu la sheria utasikia hii sheria gani mbaya hatuijui. Sasa tender Azam ashindane na kina Agape na TBC 🤣 kwenye technical tu wanakatwa kabla hata ya kufungua commercial.
 
Hata ingetangazwa.
Ungeweka bei gani KUSHINDANA NA bakhresa.
Vitu vingine inabidi muviache Tu vipite
 
TFF na AZAM TV zimeingia mkataba wa kudhamini ligi ya soka Tanzania Bara bila ya kutangaza Tenda na Pia hakuna mikataba mirefu kama huubwa miaka kumi.Huu ni ukiukwaji wa utaratibu wa kuonyesha mechi za mpira wa miguu nchini.

Duniani kote Tenda zinatangazwa na kila kampuni inatoa ofa lakini haipewi kuonyesha mechi zote.Mfano ligi kuu ya Uingereza ofa ni kubwa mno kila timu kubwa na ndogo zinafaidika.

Wapo skysports, Bsports na Amazon. Ligi hii ya premier ya England ina thamani ya paundi za Uingereza Bilioni 6 na mkataba na Barclays bank mnono. Sasa hapa kwetu TFF itaingiaje mkataba wa miaka 10 na kampuni moja? Ama kweli fumbo mfumbie Mjinga,mwerevu hungamua.

WIZARA YA HABARI NA MICHEZO IINGILIE KATI MKATABA HUU KWA SABABU KUU TATU; 1)Tenda itangazwe na makampuni mengi ya utangazaji yatatoa ofa ambazo zitasaidia hata timu ndogo(2) TV moja isepewe asilimia 100 kama ilivyo sasa,zigawanywe kutokana na pesa wanazo ofa(3)Mkataba uwe wa miaka 3 mitatu tu na siyo 10.Kwa wengi na kwa sasa mabillioni wanayaona mengi lakini kwa miaka 10 ni pesa ndogo sana.

Hapa pana mambo ambayo inabidi yaangaliwe.TFF wasitufanye Watanzania wajinga na mbumbumbu. HAKUNA MIKATABA YA KUONYESHA MIPIRA KWA TELEVISION MOJA KWA MIAKA KUMI TENA KWA KIASI KIDOGO CHA PESA. TFF VUNJENI MKATABA NA AZAM TANGAZENI TENDA, TV NYINGI ZITAKUJA NA OFA , TIMU ZOTE ZITAFAIDIKA ZENYE UWEZO NA AMBAZO HAZINA. WIZARA YA HABARI, MICHEZO, BMT AMKENI.
Yani huwezi ata kutumia nguvu nyingi kuuliza mtoa mada ni shabiki wa team gani hapa Tanzania, waga mnakurupuka sana ndugu zetu na kufanya baadhi ya washabiki wenzenu ambao ni smart kuonekana nao ni wale wale

Tenda ilitangazwa kupitia vyombo vya habari na kimoja wapo ni TBC, walioomba wakaomba na aliopata ndio huyo sasa, katafute tena data kuwa ligi ya uingereza ina wamiliki wa haki za matangazo wangapi, mwenye haki ni mmoja Tu na anawauzia hao wengine wote kina bein sports,Super sports nk

Lakini pia kuhusu miaka mingi bado huna hoja mkuu, kagugo mkataba wa laliga niwa miaka mingapi, lakini pia Kwa akili ya haraka haraka unazani ni nani ambae angeweza kutoa hela hiyo aliyotoa Azam? Na kuhusu thamani ya pesa kuwa ni ndogo miaka ya badae we hujaona hiyo hela inaongezeka kila msimu? Unajua mkataba wa Kwanza ulikuwa Una thamani ipi? Na huu umeongezeka mara ngapi ya ule wa Kwanza?
 
Namba 2 unakosea.
Ni BT na Sky
Mkuu nakubaliana na ww kabsa na kwamba bt sports yupo lakini hua anaonyesha meschi zisizozidi 58 kwa msimu tu kati ya 380 na, pia mkataba mpya kuna amazon sports wao wanaonyesha mechi zisizozidi 20 tu.

Kwa mechi zingine zote wananunua rights toka sky sports.

Kiufupi hii issue ya tv rights za epl ni ndefu na inahitaji muda kuelezea.

Nakubali mkuu, tuendelee kulijenga taifa na tuepuke wapotoshaji.......
 
Kiuzalendo zaidi Hii tenda walitakiwa wapewe TBC
 
Back
Top Bottom