Kwanini Zelensky analaumiwa kwa kuzuia uvamizi wa Putin

Kwanini Zelensky analaumiwa kwa kuzuia uvamizi wa Putin

Iyo Vita nimatokeo ya siasa baina ya mataifa mawili yenye nguvu za kivita duniani Kati ya urusi na USA. Tukumbuke tokea anguko la umoja wa kisovienti sisa za dunia zilikua na mlengo mmoja . Yaani USA na washirika wake EU kwa kimvuli Cha Uhuru na haki yaki demokrasia ili kulinda maslai yao hasa hasa ya kiuchumi na kisiasa duniani Kama ilivyo kua enzi za Vita baridi( ubepari na ukomonisti) tulishuudia dola nyingi kuangushwa na Vita vingi kupiganwa dunia nzima ( Cuba conflict, Korean war, Vietnam war... etc) ambapo ubepali ulishinda nakua kitovu Cha dunia kupitia USA.
Mashirika Kama UN , word bank , IMF ambao Yana makao yake makuu ni USA na yanatumia USA dollar kufanya malipo na mikopa yameendelea kumiliki siasa na uchumi wa dunia, hivyo mataifa yalio jaribu hivi kalibuni kukiuka mlengo huo wa siasa za dunia Kama libia , Iraq yalipata kichapo kwa kisingizio Cha ukiukaji wa haki za binadamu na demokrasia.
Urusi, china , Cuba , north Korea na baadhi ya inchi nyingi zilitumia diplomasia ya juu kuishi siasa za kikomonist na ubepali ama siasa zisizo fungamana na upande wowote kukwepa mkono wa chuma wa malekani ata sisi Tanzania ambao tuna siasa za ujamaa.
Itoshe kusema urusi kupitia Putin amekwepa mkono wa chuma wa USA ( maraisi wa tano) kujijenga kiuchumi na kujidhatiti kijeshi uku akijua wazi kabisa itafika mahala wata mshitukia na hatima yake ingelikua Kama Iraq au kwa gadafi asinge jizatiti hasa katika nguvu za kijeshi.
Maoni yangu. Ningekua zelesky ningeamua kuto ambatana na upande wowote baina ya wahasimu hao wawili wa tokea enzi za Vita baridi . Ili kuepuka kadhia za Vita zisizo isha kwenye aridhi ya wa Ukraine. Matokeo yake kuegemea upande mmoja kwa kimvuli Cha demokrasia aridhi ya waukraine imekua test ground ya fourth generation weapons Mara hypersonic , Mara air defense Mara armored vehicles na takataka nyingi na kuacha inchi magofu

Unataka kutuambia kuwa kwenye familia yako jilani yako ndo anakuchagulia cha kufanya au nini usifanye? Jilani anakupangia ni rafiki yupi uwe naye na nani asiwe rafiki yako? Una practice hicho nyumbani kwako au kwenu?
 
Mmmh hapa nahis hapana nahis kati ya Rep na Dema wanaopenda ngumi zaidi ni Rep mkuu manake nikimkumbuka Bush sina hamu mkuu
Sasa mkuu kwani Bush ndio Rais pekee wa Marekani. Na hapo nimeshasisitiza Republicans wakienda vitani huwa wanapigana kwelikweli hawana vita ndogo, kwenye Hip hop ni kama Kendrick Lamar, hatoi album kiholela ila akitoa anatoa kweli.
 
Rais Zelensky wa Ukraine amekuwa akilalamikiwa sana na Rais Putin wa Russia kwamba anatumiwa na West (USA, German, UK & allies). Malalamiko hayo yamezidi kukolezwa na Pro Russia na wanayoichukia USA na nchi za EU kwa sababu wanazozijua wao.

Inawezekana kabisa wanayoichukia USA & allies wakawa na sababu wanazoona za msingi kwa mitizamo yao, lakini kwa nini Rais Zelenskyy naye achukiwe na kulalamikiwa kwa kutetea nchi yake kisa tu eti wanaomuunga mkono na kumsaidia na USA na washirika wake.

Rais Putin kaenda mbali zaidi na kusema kuwa wanaomsaidia Ukraine wanarefusha vita (Prolong the war). Kwa nini Putin alalamike kuwa vita imekuwa ndefu. Yeye alipoivamia Ukraine alipanga vita iwe kwa muda gani.

Wanayoiunga Ukraine na kuisaidia ni wengi zikiwemo nchi zote za EU. Nafika mahala najiuliza maswali mengi sana. Machache nitayauliza na mengine mtaongezea;

1. Kwa nini Rais Zelenskyy analaumiwa kwa kuzuia uvamizi wa Putin dhidi ya nchi yake.

2. Je, Putin na Pro Russia wanaamini kuwa Ukraine haina haki ya kujilinda na kupigania nchi yake?

3. Je, Rais Zelenskyy kafanya kosa kuamuru majeshi yake yapigane na Russia kutetea uhuru wake na kulinda mipaka yake?

4. Putin alipoivamia Ukraine alipanga vita iwe kwa muda gani mpaka afike mahala alalamike kuwa vita inarefushwa?

5. Kwa nini lawama zote anapewa USA huku akijumuishwa na NATO ili hali wanayoiunga mkono Ukraine na kuisaidia wako wengi?

6. Kwa nini hatusikii lawama nyingi zikielekezwa kwa German, Ufaransa, UK, Turkey, Italy na wengine wakati wote hawa wanatoa silaha kuisaidia Ukraine?

7. Kwa nini Rais Putin na Pro Russia wanamlaumu sana Rais Zelensky kwa kusaidiwa na USA.

8. Je, Putin na Pro Russia walitaka Ukraine asisaidiwe na marafiki zake kutetea na kupigania nchi yake?

9. Je, Rais Putin wakati anatangaza kuivamia Ukraine hakujua kuwa Ukraine ni nchi na ina nchi marafiki akiwemo USA ambao wanaweza kumsaidia kama ilivyo desturi ya mwanadamu kuwa rafiki yako au ndugu yako akipatwa na matatizo lazima umsaidie?

10. Kwa nini Putin kila hotuba yake anailaumu sana NATO huku akijua kuwa NATO ni mbwa tu wa USA na EU? Kwanini asihangaike na mwenye mbwa kuliko mbwa mwenyewe.

Tunahitaji kutafakari na kupata majibu ya haya maswali ili tujifunze zaidi. Mwenye majibu ya haya maswali tafadhari atusaidie. Tunahitaji tu majibu siyo porojo na propaganda na matusi.
Putin alitaka aingie Ukraine ajipigie tu kwa siku 3 au wiki kakutana na upinzani mkali uliopelekea majeshi yake kusambaratika na vifaru vyake kulipuliwa
 
Mkuu sijui kama kuna mwenye majibu,hata putin mwenyewe majibu hana.
Putin alijidanganya kwa kuzdhani Zele ni muigizaji tuu na hakuna mtu wa kumsaidia.

Alisahau kwamba wapinzani wake wa tangu vita baridi hawawezi kumtazama tuu akiendelea kujitanua wakamchekea.Kitendo cha kumchekea putin ataendelea kuvivamia vinchi vyote vidogo karibu yake na kuunda upya urusi iliyosambaratika,na akifanikiwa marekani na washirika wake watakuwa hatarini.
Hoja yako imeeleweka kwamba;
1. Putin/Russia angeachwa angeendeleza tabia ya kuvamia nchi huru kama alivyofanya labla kwa kujimegea Crimea, mikoa miwili ya Georgia nk.

2. PUTIN hakujua kuwa wanaume wanamsubiri kwenye uchochoro siku nyingi. Kwa hiyo kuivamia Ukraine ni kama alinasa kwenye mtego bila kujua ndo maana analalamika Ukraine kupewa silaha na marafiki zake
 
Trump hawezi kumaliza vita hizo ni Polimilai tu

Ana ahadi ngapi ambazo kazishindwa?

Tena zile ambazo zilionekana rahisi kutekelezeka lakini alishindwa

What makes you think he would make it happen on this?
Nimeweka possibilities mbili sasa sijui hujaona
1) Kumaliza vita mapema sana (kasema mwenyewe na hakupendekeza option nyingine)
2) Vita kuendelea kwa kasi kubwa (Republicans kama ni vita wanaenda jumla jumla)
 
Nimeweka possibilities mbili sasa sijui hujaona
1) Kumaliza vita mapema sana (kasema mwenyewe na hakupendekeza option nyingine)
2) Vita kuendelea kwa kasi kubwa (Republicans kama ni vita wanaenda jumla jumla)
Option ya kwanza haiwezi kutokea.
 
Kama jirani yako yupo kwenye mikakati akishirikiana na adui yako kutaka kukumaliza, baada ya kufabamu hilo utachukua atua gani?
 
Wewe unavyoona Zelensky anajitetea au anaiteketeza nchi?
Hata akiiteketeza nchi yake lakini ni bora na wewe unakuwa umemtoa na wewe mangeu mvamizi ili akiparamia taifa jingine ajui ataumia tena mfano china kaogopa kuivamia Taiwan maana kaona Urusi anavyopata hasara na vikwazo juu
 
Hata akiiteketeza nchi yake lakini ni bora na wewe unakuwa umemtoa na wewe mangeu mvamizi ili akiparamia taifa jingine ajui ataumia tena mfano china kaogopa kuivamia Taiwan maana kaona Urusi anavyopata hasara na vikwazo juu
Ndivyo unavyojidanganya china ameohopa kuichukua Taiwan? Hilo ni suala la muda tu tuombe uhai. Ngoja kwanza Russia amelize kuwafunza adabu manyangau alafu china ajichukulie Teiwani yake kiulaini. Hasara gani aliyopata urusi dhidi ya vikwazo vilivyowekwa?
 
Anachokifanya RUSSIA [emoji635] pale Ukraine [emoji1255] ni sahihi kabisa na kila mpenda amani haki na maendeleo anatakiwa akisapoti
 
Suala la zelensky kuiingiza Ukraine kwnyw machafuko lilikua suala la muda TU tangu zelensky kipind hicho hajawa hata raisi.

Kwa taarifa yako, zelensky alishakua agent wa CIA tangu kipind anasoma mpk Anafanya uchekeshaji Kisha kuingia Kwny siasa.

Zelensky ndo Alikua kiongozi wa mapinduzi ya 2014 kule Ukraine kwa kivuli Cha USA, kuingoa serikali pro Russia ya raisi aliyekua madarakani.

Lengo la zelensky kua raisi, Ni maksudi alisukwa ili aje kutumika kuiangusha russia.

Ndo maana baada ya zelensky kua raisi zikaanza reforms MBALIMBALI pale Ukraine na kulijengea uwezo mkubwa jeshi la Ukraine na kwa Kasi Sana ili lije kupambana na jeshi la Russia endapo wataingia vitani.

Kabla ya uvamizi, ulaya nzima hakuna jeshi lililkua na uwezo mkubwa was kijeshi kuzidi au hata kulingana na Ukraine.


Ujue hata Waukraine wenyewe walishapiga Sana kelele zelensky asiwe raisi wa nchi ila wakapuuzwa, ubabe ubabe wa USA na demokrasia ya mchongo akajikuta keshakua raisi[emoji4]

Soma Hii tweet hapa Chini wizara ya ulinzi inalalamika Miaka hiyo[emoji116]View attachment 2633558
Tukiacha kukuuliza maswali magumu huenda ukazoea kupiga porojo na propaganda.

1. Hebu tutajie ni mwaka gani Zelenskyy alijiunga na CIA? hebu tupe na source kabisa.

2. Kama Zelenskyy aliongoza mapinduzi ya 2014. Kwa nini basi hakuwa Rais wa mpito badala yake akawa Oleksandr?

3. Kwa nini Zelenskyy hakugombea Urais baada ya serikali ya mpito ya Oleksandr kwenye uchaguzi wa 2014 na badala yake akagombea Petro kama Zelenskyy ndo aliyeongoza mapinduzi?

4. Umesema kuwa Zelenskyy alikuwa comedian, aliwezaje kuwa kiongozi wa mapinduzi wakati hakuwa na cheo chochote jeshini?

5. Umesema baada ya mapinduzi ilifanyika reform kwenye jeshi la Ukraine na kuwa jeshi lenye nguvu sana ulaya nzima. Je, una màana bara ka Ulaya au Ulaya mtaa uliopo Buza? Kwa hiyo German, UK, France wote walikuwa hawaoni ndani kwa jeahi la Ukraine? This is ridiculous.

NASUBIRI MAJIBU


 
Back
Top Bottom