Kwenu Viongozi wa Umoja Party

Kwenu Viongozi wa Umoja Party

Pokeeni pongezi zangu za dhati kwanza kwa kuwaza na kuamua kutengeneza chama chenye mlengo na falsafa anuia za Hayati na Kipenzi chetu Dr. Magufuli. Hakika mmefanya jambo kubwa nala kutukuka sana.

Pamoja na pongezi zangu nyingi napenda kuwatahadharisha na kuwaasa kuwa makini sana kwa kila hatua mnayoiendea kwa maana dhamana na imani ya watanzania inakwenda kuwekwa juu yenu. Ni ombi langu kwenu kuwa na dhamiri ile ile ya upendo kwa Tanzania na watu wake huku mkijibidiisha kwa kila namna kuhakikisha Tanzania inapata viongozi wenye kiu na dhamira ya kweli kufikia maono makubwa ya kipenzi chetu Magufuli.

Ni vizuri kufahamu ya kuwa Tanzania ya sasa haina upungufu wa vyama vya siasa au sera nzuri za uendeshaji wa nchi. Hivyo ni budi kwenu kuyasoma na kuyapatia ufumbuzi yote ambayo ni maidhafu ya vyama vya siasa vilivyopo sasa ambavyo vimeshindwa kuonesha dira ya kweli ya Taifa letu kwa miaka 50 hadi 100 ijayo. Magufuli aliipenda Tanzania na kuchukizwa kabisa kwa maneno na vitendo na hali mbaya ya umaskini, ufisadi na dharau ya watawala/mabwenyenye waliojimilikisha nchi dhidi ya tabaka kubwa la watanzania wanyonge.

Ni ombi langu kwenu kutanguliza uzalendo na elimu ya kisiasa kwa watanzania wote wapate kufahamu dira, muelekeo na falsafa za chama. Katika hatua hizi za mwanzo ni muhimu sana kuhakikisha mnatengeneza misingi imara ya kitaasisi kwanza kwa kuhubiri na tena kuonesha kwa vitendo ili watanzania wayaamini hayo mnayapeleka kwao. Pasiwepo na hila midomoni mwenu tena Amani, Upendo,Haki na Mshikamano visipungue katika majukwaa yenu. Njoo na majibu ya namna ambavyo Tanzania itaweza kuendelea kiuchumi, kijamii na kisiasa. Ni muhimu sana kuzisema changamoto zote na kuueleza uma watanzania ni kwa njia gani tutafikia maendeleo ya kweli. Watafuteni wazee wazalendo wawapatie hekima zao, wapongezeni wanaostahili pongezi, wakemeeni wanastahili makaripio.

Karibuni kwenye ulingo wa siasa za Tanzania, karibuni kwenye figisu za CCM, karibuni kwenye hila za CHADEMA, karibuni kwenye kichaka cha wahuni na watakatishaji wa udhalimu.

Umoja ni nguvu, Umoja ni Ushindi, Umoja ni Maendeleo.
Mbona huwasisitizii kuendeleza uharamia wa marehemu wa kuteka, kutesa, kuwapoteza na kuwabambikia kesi wale wote watakaowakosoa.

Kwa watu wengi wenye kuthamini utu wa mwanadamu, neno Magufuli ni dhihaka dhidi ya ubinadamu. Waende na jina hilo hilo kila mahali, watayapata majibu.
 
Kiuhalisia hayati Magufuli alikua ni kiongozi jasiri na shupavu kweli, lakini hakua na sifa za kuwa Rais.Nafasi ya juu kimamlaka kwa mtu kama yule ilikua ni uwaziri mkuu tu.Yaani juu yake inapaswa kuwa na mtu aliepevuka kwa hekima na maono ya kuvumilia kupishana maono na watu na kukubali kushaurika.

Lakini kiongozi aina ya Magufuli ni mtu mwenye kutumia maguvu mengi hata mahala pasipohitaji maguvu, mwisho wa siku mnaibomoa nchi badala ya kuijenga.Mungu amlaze pema huko alipo maana ametuachia somo kama taifa!!!
 
Bahati mbaya sana Mimi mwenyewe natamani kupata kadi hata leo na sijui ninaipatia wapi.
Kile kingine, utafiti wa TWAWEZA ulionesha kinaungwa mkono zaidi na watu wajinga, hiki huenda itakuja kufahamika baadaye kuwa kinaungwa mkono zaidi na maharamia wanaopenda kuua, kuteka, kupoteza watu. Hiki kitakuwa ni chama cha kishetani kwaajili ya kusimamia na kuendeleza matendo ya ibilisi.
 
Kile kingine, utafiti wa TWAWEZA ulionesha kinaungwa mkono zaidi na watu wajinga, hiki huenda itakuja kufahamika baadaye kuwa kinaungwa mkono zaidi na maharamia wanaopenda kuua, kuteka, kupoteza watu. Hiki kitakuwa ni chama cha kishetani kwaajili ya kusimamia na kuendeleza matendo ya ibilisi.
Mawazo hayapigwi rungu sikupingi ndugu. Lakini hatuwezi kukihukumu chama ilihali bado hakijaanza kufanya kazi. Fear of unknown ni changamoto kwa wengi hivyo ni kazi ya viongozi kuhakikisha falsafa, itikadi na sera za chama zinaeleweka vyema.
Nakumbuka Mzee Mangula akisema waliteuliwa vijana 75 kuhubiri falsafa ya azimio la Arusha. Vivyo hivyo ni muhimu kwa Umoja party kutumia mbinu hiyo.
 
Siyo jbo la ajabu hata kidogo. Kuna watu wanamkumbuka Dictator Id Amin mpaka leo. Kuna watu, Ujerumani wanamtukuza Hitler mpaka leo.

Shetani yupo, kwa sababu hajawahi kupungukiwa wa kumsujudia.
Ni mtazamo wako lakini ukikaa ukawa huru utagundua kulikuwa na kitu cha ziada kwa JPM
 
Mtaeneza vipi Chama chenu wakati hakuna mikutano?
Kiongozi shupavu anapimwa wakati wa dhiki na mashaka. Uwezo wa kusimamisha chama wakati huu mgumu ni mtihani wa kwanza mgumu na muhimu tuwe mashuhuda
 
Yani wewe uwe miongoni mwao alafu ujipongeze, hakuna Chama hapo na mmearibu kuja na jezi yenye picha ya uyo ndugu yenu, nawambieni hata hadhi ya TADEA hamtafika, huwezi anzisha chama shagala bagala namna hiyo, kwamba Iyo ccm A nayo ije na jezi ya mwl Nyerere ndo itakubalika?

Mmeshindwa kabla ya kuanza ,
Ahsante mkuu,
 
Hongera sana mkuu
Legacy is what you leave behind for others

Kuna wachache wasio na maarifa walidharau na kukebehi kwamba tunalinda legacy ya JPM.

Pasi na kufahamu legacy haitetewi bali inajitetea yenyewe, mbegu aliyoipanda JPM inakwenda kuzaa matunda soon and very soon yawezekana isiwe 2025 lakini kwa uwezo wa Mungu. Fikra za Tanzania kwanza zitashinda. Tanzania ni taifa lenye baraka ya ukombozi lazima tukaikomboe Africa kiuchumi ila kwanza ni lazima sisi wenyewe kuonesha mfano.

Vijana na wote wenye mapenzi mema tusimame kwa pamoja maana kama sio sisi ni nani?
Mwisho wa ccm umekaribia,mwisho wa dhuruma na uporaji umekaribia,
 
Aliyeua demokrasia, kuzuia mikutano ni Magufuli. Labda kabla ya kufariki kwake aliwaachia wosia kuwaambia kuwa amefungulia demokrasia.

Samia kama ataamua amuenzi marehemu, hamtafanya hata kikao cha sebuleni.
Hiki Chama na wafuasi wake ni contradictions tupu

Magufuli aliziba kabisa space ya kisiasa iliyokuwepo Tanzania, na kusema CCM itatawala milele

Licha ya kuzuia mikutano ya vyama, Magufuli alianzisha uhuni mwingi ambao haukuwahi kuwepo kwenye siasa za Tanzania, kuteua makada wa CCM Kama wakurugenzi, kuengua watu kwa vigezo kuwa hawajui kusoma, kutekwa watu wakati wa kurudisha fomu

Sasa kwa Chama chochote Cha upinzani hakiwezi kusema kinamuenzi Magufuli sababu uwepo wake tu tayari una contradict aliyoamini na kuyafanya Magufuli
 
Kiongozi shupavu anapimwa wakati wa dhiki na mashaka. Uwezo wa kusimamisha chama wakati huu mgumu ni mtihani wa kwanza mgumu na muhimu tuwe mashuhuda
Huu sio wakati mgumu, wakati mgumu ilikuwa 2016-2020 viongozi wa upinzani walivyokuwa wakitekwa na kuuawa
 
Pokeeni pongezi zangu za dhati kwanza kwa kuwaza na kuamua kutengeneza chama chenye mlengo na falsafa anuia za Hayati na Kipenzi chetu Dr. Magufuli. Hakika mmefanya jambo kubwa nala kutukuka sana.

Pamoja na pongezi zangu nyingi napenda kuwatahadharisha na kuwaasa kuwa makini sana kwa kila hatua mnayoiendea kwa maana dhamana na imani ya watanzania inakwenda kuwekwa juu yenu. Ni ombi langu kwenu kuwa na dhamiri ile ile ya upendo kwa Tanzania na watu wake huku mkijibidiisha kwa kila namna kuhakikisha Tanzania inapata viongozi wenye kiu na dhamira ya kweli kufikia maono makubwa ya kipenzi chetu Magufuli.

Ni vizuri kufahamu ya kuwa Tanzania ya sasa haina upungufu wa vyama vya siasa au sera nzuri za uendeshaji wa nchi. Hivyo ni budi kwenu kuyasoma na kuyapatia ufumbuzi yote ambayo ni maidhafu ya vyama vya siasa vilivyopo sasa ambavyo vimeshindwa kuonesha dira ya kweli ya Taifa letu kwa miaka 50 hadi 100 ijayo. Magufuli aliipenda Tanzania na kuchukizwa kabisa kwa maneno na vitendo na hali mbaya ya umaskini, ufisadi na dharau ya watawala/mabwenyenye waliojimilikisha nchi dhidi ya tabaka kubwa la watanzania wanyonge.

Ni ombi langu kwenu kutanguliza uzalendo na elimu ya kisiasa kwa watanzania wote wapate kufahamu dira, muelekeo na falsafa za chama. Katika hatua hizi za mwanzo ni muhimu sana kuhakikisha mnatengeneza misingi imara ya kitaasisi kwanza kwa kuhubiri na tena kuonesha kwa vitendo ili watanzania wayaamini hayo mnayapeleka kwao. Pasiwepo na hila midomoni mwenu tena Amani, Upendo,Haki na Mshikamano visipungue katika majukwaa yenu. Njoo na majibu ya namna ambavyo Tanzania itaweza kuendelea kiuchumi, kijamii na kisiasa. Ni muhimu sana kuzisema changamoto zote na kuueleza uma watanzania ni kwa njia gani tutafikia maendeleo ya kweli. Watafuteni wazee wazalendo wawapatie hekima zao, wapongezeni wanaostahili pongezi, wakemeeni wanastahili makaripio.

Karibuni kwenye ulingo wa siasa za Tanzania, karibuni kwenye figisu za CCM, karibuni kwenye hila za CHADEMA, karibuni kwenye kichaka cha wahuni na watakatishaji wa udhalimu.

Umoja ni nguvu, Umoja ni Ushindi, Umoja ni Maendeleo.
Sema kipenzi chako na familia yako.
 
Hiki Chama na wafuasi wake ni contradictions tupu

Magufuli aliziba kabisa space ya kisiasa iliyokuwepo Tanzania, na kusema CCM itatawala milele

Licha ya kuzuia mikutano ya vyama, Magufuli alianzisha uhuni mwingi ambao haukuwahi kuwepo kwenye siasa za Tanzania, kuteua makada wa CCM Kama wakurugenzi, kuengua watu kwa vigezo kuwa hawajui kusoma, kutekwa watu wakati wa kurudisha fomu

Sasa kwa Chama chochote Cha upinzani hakiwezi kusema kinamuenzi Magufuli sababu uwepo wake tu tayari una contradict aliyoamini na kuyafanya Magufuli
Ndugu,
Ukiamua kuwa huru na mawazo yako utamuona Magufuli katika picha nyingi sana. Kimoja ambacho wote tunakubaliana ni kuwa Magufuli alikua mzalendo na mwenye upendo wa dhati kwa Tanzania. Alihubiri Tanzania yenye maendeleo na aliamini katika watanzania hivyo alipandikiza mbegu ya ujasiri na uzalendo kwetu wote. Sisi tuliobaki tumejifunza mengi na tunaanzia hapo kuhakikisha kweli tunaisimamisha Tanzania ya mfano na mkombozi wa bara la Africa
 
Back
Top Bottom