Kwenu Viongozi wa Umoja Party

Kwenu Viongozi wa Umoja Party

Na hii nayo watamlaumu JPM au mama anaupiga mwingi sasa?
Uovu ukipandikizwa katika nchi, huchukua muda kupotea kabisa. Tabia hizi za kinyama, marehemu alizipa nguvu sana, hata zikaota mizizi. Haziwezi kuondoka kwa siku moja.
 
Ni mjinga anayeweza kuamini kuwa mrengo wa mawazo ya Magufuli yangelifikisha Taifa hili mbali. Endeleeni kujifurahisha!
Taifa litafika mbali kwa kuendekeza KAZI NA BATA ???!!!
 
Pokeeni pongezi zangu za dhati kwanza kwa kuwaza na kuamua kutengeneza chama chenye mlengo na falsafa anuia za Hayati na Kipenzi chetu Dr. Magufuli. Hakika mmefanya jambo kubwa nala kutukuka sana.

Pamoja na pongezi zangu nyingi napenda kuwatahadharisha na kuwaasa kuwa makini sana kwa kila hatua mnayoiendea kwa maana dhamana na imani ya watanzania inakwenda kuwekwa juu yenu. Ni ombi langu kwenu kuwa na dhamiri ile ile ya upendo kwa Tanzania na watu wake huku mkijibidiisha kwa kila namna kuhakikisha Tanzania inapata viongozi wenye kiu na dhamira ya kweli kufikia maono makubwa ya kipenzi chetu Magufuli.

Ni vizuri kufahamu ya kuwa Tanzania ya sasa haina upungufu wa vyama vya siasa au sera nzuri za uendeshaji wa nchi. Hivyo ni budi kwenu kuyasoma na kuyapatia ufumbuzi yote ambayo ni maidhafu ya vyama vya siasa vilivyopo sasa ambavyo vimeshindwa kuonesha dira ya kweli ya Taifa letu kwa miaka 50 hadi 100 ijayo. Magufuli aliipenda Tanzania na kuchukizwa kabisa kwa maneno na vitendo na hali mbaya ya umaskini, ufisadi na dharau ya watawala/mabwenyenye waliojimilikisha nchi dhidi ya tabaka kubwa la watanzania wanyonge.

Ni ombi langu kwenu kutanguliza uzalendo na elimu ya kisiasa kwa watanzania wote wapate kufahamu dira, muelekeo na falsafa za chama. Katika hatua hizi za mwanzo ni muhimu sana kuhakikisha mnatengeneza misingi imara ya kitaasisi kwanza kwa kuhubiri na tena kuonesha kwa vitendo ili watanzania wayaamini hayo mnayapeleka kwao. Pasiwepo na hila midomoni mwenu tena Amani, Upendo,Haki na Mshikamano visipungue katika majukwaa yenu. Njoo na majibu ya namna ambavyo Tanzania itaweza kuendelea kiuchumi, kijamii na kisiasa. Ni muhimu sana kuzisema changamoto zote na kuueleza uma watanzania ni kwa njia gani tutafikia maendeleo ya kweli. Watafuteni wazee wazalendo wawapatie hekima zao, wapongezeni wanaostahili pongezi, wakemeeni wanastahili makaripio.

Karibuni kwenye ulingo wa siasa za Tanzania, karibuni kwenye figisu za CCM, karibuni kwenye hila za CHADEMA, karibuni kwenye kichaka cha wahuni na watakatishaji wa udhalimu.

Umoja ni nguvu, Umoja ni Ushindi, Umoja ni Maendeleo.
MAGUFULI ALICHUKIA "KATIBA MPYA" HIVYO HICHO CHAMA HAKITUFAI WANANCHI TUNATAKA CHAMA KINACHOPIGANIA UPATIKANAJI WA "KATIBA MPYA" ILI TUONDOKANE NA HII KATIBA YA CHAMA YA KIFALME

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Uharamia na ukatili siyo sehemu ya uzalendo.

Alichokuwa anakifanya Magufuli, hakina tofauti na kile alichokifanya fashisti Stallin, aliyekuwa Rais wa Urusi, ambaye alikuwa kiongozi muuaji aliyekuwa akiimba kila siku kuwa anayepingana naye, amekosa uzalendo.

Madikteta wengi, hujificha kwenye neno uzalendo. Anaua watu kwa kisingizio kuwa eti wale wanaomkosoa wamekosa uzalendo. Anafungia vyombo vya habari kwa kudai vyombo hivyo vimekosa uzalendo.

Magufuli, bila ya kumtaja kama mtu aliyekuwa katili, dikteta, mwongo aliyehubiri tofauti na kilichopo moyoni mwake na anayetenda, na sisi tutakuwa ni wanafiki. Magufuli hata apambwe vipi, kuna siku ambayo uovu wake wote utawekwa wazi, na watu watabakia midomo wazi, na jina hilo litakuwa likitajwa kwa ubaya zaidi kuliko kwa mema.
Ndio maana Urusi IPO hapo ilipo Leo ! Hali kadhalika kwa Mao tze Tung wa China ! Watu walikuwa wanatayarishwa wawe wazalendo wa kweli na askari hodari wa kuijenga na kulinda taifa lao !! Taifa imara haliwezi kujengwa kwa KAZI NA BATA !! Ndio maana bara la Africa lipo nyuma kimaendeleo kuliko mabara yote Ulimwenguni pamoja na rasilmali zote zilizopo !! Akili zetu tumezielekeza kwenye KAZI NA BATA !! unayajua ma Vieite wewe ???!!! Tutasubiri sana !!!
 
Maneno unayoongea mtu anaweza fikiri labda kulikuwa na vita mfano Hii ya Urusi na Ukraine, yaan unaweza kudhani kulikuwa na kitu kikuuuubwa kibaya wakati wa uongozi wa huyo
u kipenzi cha Watanzania JPM Kumbe ni katika kushughulikia wahuni, wazembe , kuondoa takataka zilizofoji vyeti kazini, kusimamia miradi ikamilike kwa ubora na gharama nafuu, kubana matumizi na kuzuia safari za kisengesenge.

Pole sana kama ulikuwa mhanga, nachojua ni kwamba hata nyumbani kwako ukiwa na mtoto mtukutu unapojaribu kumnyoosha anaweza kukimbilia mtaani akawaacha wenzake waadilifu, Hatuwezi kushangilia utepetevu kama huu unaoendelea unaowafurahisha ninyi na ndo maan UP ni suluhisho
 
Tunataka tuende njia kama ya USA na George Washington.
Ndio maana Urusi IPO hapo ilipo Leo ! Hali kadhalika kwa Mao tze Tung wa China ! Watu walikuwa wanatayarishwa wawe wazalendo wa kweli na askari hodari wa kuijenga na kulinda taifa lao !! Taifa imara haliwezi kujengwa kwa KAZI NA BATA !! Ndio maana bara la Africa lipo nyuma kimaendeleo kuliko mabara yote Ulimwenguni pamoja na rasilmali zote zilizopo !! Akili zetu tumezielekeza kwenye KAZI NA BATA !! unayajua ma Vieite wewe ???!!! Tutasubiri sana !!!
 
Yaani mnakinasibu kuwa kitakuwa ni chama bora kwa sababu kitakuwa na mlengo wa fikra za mtu? Hiyo ni sawa na kuweka rehani akili zenu. Kwa mtazamo wa mbali pia inaonekana kitakuwa na sura ya ukanda flani kitu ambacho si afya katika kujenga jamii yenye umojaanye.
 
Hivi ni kitu gani cha ziada kinakuwepo katika kuua au kupoteza watu, au kuwashambulia wanaokukosoa. Au hata kuwagunga watu kwa kuwaonea?

Muuaji, hata afanye nini, siamini kama huyo anaweza kuwa mtu mzuri kwa kipimo chochote kile.

Hicho chama, kama kweli kitaenda kwa wananchi kuwa kipo akwaajili ya kuenzi yale maovu ya marehemu, hakika kuna maeneo kitatemewa hata mate.
Wewe ni anti-jpm lakini usije ukaona jamii ya twitter na jf ukafikiri ndiyo Tanzania.....hakuna MTU mwenye akili timamu anayeweza kumlinganisha samia na jpm....magufuli ni wa watanzania na samia ni wa wanufaika.....so if wewe ni mmoja wao endelea kulambiswa asali.
 
Ndugu,
Ukiamua kuwa huru na mawazo yako utamuona Magufuli katika picha nyingi sana. Kimoja ambacho wote tunakubaliana ni kuwa Magufuli alikua mzalendo na mwenye upendo wa dhati kwa Tanzania. Alihubiri Tanzania yenye maendeleo na aliamini katika watanzania hivyo alipandikiza mbegu ya ujasiri na uzalendo kwetu wote. Sisi tuliobaki tumejifunza mengi na tunaanzia hapo kuhakikisha kweli tunaisimamisha Tanzania ya mfano na mkombozi wa bara la Africa
Pumbaf uzalendo gani wakati nchi ilikuwa inaliwa kama mchwa?

Kwa ripoti ya CAG inaonyesha kuwa hakujawahi kufanyika ufisadi kama wa awamu ya 5.

Alafu unatuletea ngonjera eti alikuwa na uzalendo na upendo.
 
Hakuna jipya hapo kama kweli mna nia ya kuanzisha chama anzisheni,lakini hiyo kauli mbiu yenu ya kusema mnaienzi au kudumisha legacy aliyoiacha hayati JPM,haitowafikisha popote,sababu ni kwamba mtanzania wa kawaida anaelewa fika kwamba Magufuli alikuwa ni kiongozi wa CCM,na nyie kama mtazinadi sera zake itapelekea kukikuza zaidi CCM,hii itakuwa ni faida kubwa sana kwa wana CCM,mtakuwa mmewapigia kampeni isiyo na malipo.
 
Yaani mnakinasibu kuwa kitakuwa ni chama bora kwa sababu kitakuwa na mlengo wa fikra za mtu? Hiyo ni sawa na kuweka rehani akili zenu. Kwa mtazamo wa mbali pia inaonekana kitakuwa na sura ya ukanda flani kitu ambacho si afya katika kujenga jamii yenye umojaanye.
Unajua maana ya fikra wewe?
Dunia inaendeshwa na fikra za wafu kama ulikua ufahamu demokrasia ni zao la fikra za mfu, mpaka kesho uislamu umesimama kwa fikra za Muhammad, ukristo ni zao na muendelezo wa fikra za Yesu, uchina ni zao la fikra za mfu.
Upeo wako ni mdogo inaonekana huwezi kung'amua vitu ndio maana unaushirika na wahuni.
Sasa kaa ukifahamu kwa fikra na falsafa za Magufuli UP Itasimama hakuna wa kuizuia. Tunakwenda kulisimamisha dola ya Tanzania kwa uongozi imara na madhubutu. Tanzania ni nyota na ukombozi wa Africa.
 
Hakuna jipya hapo kama kweli mna nia ya kuanzisha chama anzisheni,lakini hiyo kauli mbiu yenu ya kusema mnaienzi au kudumisha legacy aliyoiacha hayati JPM,haitowafikisha popote,sababu ni kwamba mtanzania wa kawaida anaelewa fika kwamba Magufuli alikuwa ni kiongozi wa CCM,na nyie kama mtazinadi sera zake itapelekea kukikuza zaidi CCM,hii itakuwa ni faida kubwa sana kwa wana CCM,mtakuwa mmewapigia kampeni isiyo na malipo.
Watanzania wote wanajua Magufuli alikua CCM lakini hakujinasibisha na CCM. Mlengo wake siku zote ulikua Tanzania kwanza amefanya juhudi nyingi kupitia CCM lakini hakufanikiwa kwa sababu CCM has been broken beyond repair.
Binafsi ninaona CCM kupitia kwa muasisi wake Baba wa taifa Mwl. Nyerere imefanya kazi kubwa naya kutukuka ya kusimika mizizi ya taifa na kutengeneza misingi imara ya umoja na Mshikamano.
Kwa sasa mahitaji ya taifa ni tofauti kabisa na yale ya kipindi cha ukombozi hivyo yanahitaji fikra tofauti kuvuka kwenye mkwamo uliopo Sasa.
Magufuli alitengeneza blue print na sisi kama wana UP tunakwenda kiiteleza. Jambo hili litapingwa sana na wote wanaofurahia/kunufaika na hali mbaya umaskini uliopo nchi, wala rushwa, wahujumu uchumi, wapiga madili na wenye vyeti feki, wabadhirifu na wahuni wote.
Lakini yeyote mwenye nia njema hakika hawezi acha kuunga mkono harakati za UP.

Umoja ni Nguvu, Umoja ni Upendo, Umoja ni Maendeleo.
 
Ndio maana Urusi IPO hapo ilipo Leo ! Hali kadhalika kwa Mao tze Tung wa China ! Watu walikuwa wanatayarishwa wawe wazalendo wa kweli na askari hodari wa kuijenga na kulinda taifa lao !! Taifa imara haliwezi kujengwa kwa KAZI NA BATA !! Ndio maana bara la Africa lipo nyuma kimaendeleo kuliko mabara yote Ulimwenguni pamoja na rasilmali zote zilizopo !! Akili zetu tumezielekeza kwenye KAZI NA BATA !! unayajua ma Vieite wewe ???!!! Tutasubiri sana !!!
Unazungumzia kitu ambacho huna uelewa wa ndani. Uchumi wa China umeshikiliwa na mataifa ya Magharibi. Tafuta kwenye orodha ya makampuni makubwa kabisa 10 ya nchini China, niambie ni mangapi yanamilikiwa na wachina/China. Unaelewa kilichofanyika nchini China miaka 2000 kilichosababisha China yenye uchumi hohe hahe mpaka kufikia ukuaji wa 12% kwa mwaka?

Hivi unajua kuwa katika real development (human development), China ni nchi ya 89, ikizidiwa na nchi kama Botswana? Usione wachina wanazurura Duniani kote, ukadhani wanapenda. Hali zao za kimaisha na duni sana, japo Serikali ina pesa nyingi.

Huko Urusi kuna makampuni zaidi ya 1000 ya nchi za Magharibi. Unafuu wa uchumi wa Urusi, ulikuja baada ya kuachana na Leninism, na kuruhusu uwekezaji wa nje na uchumi huria lakini bado kuna pengo kubwa sana la maendeleo ukilinganisha na nchi kama US, UK, Belgium, Germany, Japan, Italy, Norway, n.k.

Hakuna nchi hata moja ya kidikteta ambayo wananchi wana maendeleo halisi. Urusi ni nchi ya 52 kwenye human development.
 
Upo sahihi sana. Ndiyo maana naamini kuwa waanzilishi wa hiki chama, ama watakuwa ni wanafiki sana, au wana upeo mdogo sana.

Huwezi kufanya kitu ambacho unasema unamuenzi mtu ambaye yeye hakukitaka kabisa.
Wenzako hawawalengi wananchi wenye uelewa,la hasha wanawalenga walalahoi,wanyonge na hohehahe

Wanawalenga watu ambao hawajui kuhoji yanayoendea Tanzania

Wanawalenga watu ambao wana chuki na watumishi wa umma,matajiri na wenye nacho

Hivyo nina uhakika watapata wajinga wengi

Watawapata wanyonge wengi wa Magufuli
 
Back
Top Bottom