Kwenu Viongozi wa Umoja Party

Kwenu Viongozi wa Umoja Party

Pokeeni pongezi zangu za dhati kwanza kwa kuwaza na kuamua kutengeneza chama chenye mlengo na falsafa anuia za Hayati na Kipenzi chetu Dr. Magufuli. Hakika mmefanya jambo kubwa nala kutukuka sana.

Pamoja na pongezi zangu nyingi napenda kuwatahadharisha na kuwaasa kuwa makini sana kwa kila hatua mnayoiendea kwa maana dhamana na imani ya watanzania inakwenda kuwekwa juu yenu. Ni ombi langu kwenu kuwa na dhamiri ile ile ya upendo kwa Tanzania na watu wake huku mkijibidiisha kwa kila namna kuhakikisha Tanzania inapata viongozi wenye kiu na dhamira ya kweli kufikia maono makubwa ya kipenzi chetu Magufuli.

Ni vizuri kufahamu ya kuwa Tanzania ya sasa haina upungufu wa vyama vya siasa au sera nzuri za uendeshaji wa nchi. Hivyo ni budi kwenu kuyasoma na kuyapatia ufumbuzi yote ambayo ni maidhafu ya vyama vya siasa vilivyopo sasa ambavyo vimeshindwa kuonesha dira ya kweli ya Taifa letu kwa miaka 50 hadi 100 ijayo. Magufuli aliipenda Tanzania na kuchukizwa kabisa kwa maneno na vitendo na hali mbaya ya umaskini, ufisadi na dharau ya watawala/mabwenyenye waliojimilikisha nchi dhidi ya tabaka kubwa la watanzania wanyonge.

Ni ombi langu kwenu kutanguliza uzalendo na elimu ya kisiasa kwa watanzania wote wapate kufahamu dira, muelekeo na falsafa za chama. Katika hatua hizi za mwanzo ni muhimu sana kuhakikisha mnatengeneza misingi imara ya kitaasisi kwanza kwa kuhubiri na tena kuonesha kwa vitendo ili watanzania wayaamini hayo mnayapeleka kwao. Pasiwepo na hila midomoni mwenu tena Amani, Upendo,Haki na Mshikamano visipungue katika majukwaa yenu. Njoo na majibu ya namna ambavyo Tanzania itaweza kuendelea kiuchumi, kijamii na kisiasa. Ni muhimu sana kuzisema changamoto zote na kuueleza uma watanzania ni kwa njia gani tutafikia maendeleo ya kweli. Watafuteni wazee wazalendo wawapatie hekima zao, wapongezeni wanaostahili pongezi, wakemeeni wanastahili makaripio.

Karibuni kwenye ulingo wa siasa za Tanzania, karibuni kwenye figisu za CCM, karibuni kwenye hila za CHADEMA, karibuni kwenye kichaka cha wahuni na watakatishaji wa udhalimu.

Umoja ni nguvu, Umoja ni Ushindi, Umoja ni Maendeleo.
Ata ACT Wazalendo cha akina Zitto wakat huo akina nape wanasubiria hatima Yao
 
Umoja party, walipo tupo!!

Huku ndio kuzikwa pembeni mwa JPM, zitto aipate hii
Nyinyi wanazi wa dikteta mwendazake mnafurahia uhuru wa kutoa maonj na kufanya siasa ambao mama yetu kipenzi ametupatia. Raisi anayejiamini na anayejitambua umetupatia watanzania.

Kumbukeni dikteta wenu alizuia wengine kufanya siasa na kutoa maoni...akabaki yeye tu.
 
Wapi nimeonyesha hofu kwenye maandishi yangu?
Maandishi yako yamejaa hofu na uoga mkubwa kwa kitu usichokifahamu hilo liko wazi sana. Mpaka sasa UP haijaweka manifesto yake wazi wala safu yake ya uongozi lakini unakuwa mstari wa mbele kuitabiria vibaya.
Tukubaliane jambo moja CCM wameshindwa kuliongoza taifa na tena kuna ombwe kubwa sana la kiuongozi Tanzania. Bahati mbaya zaidi kuna Kuta nene sana kupenyeza mawazo huru kwenye vyama vya siasa vyenye muelekeo wa kushika Dola. Hivyo ni lazima kwa manufaa ya Tanzania ya leo na kesho kuwa na msingi mpya wenye muelekeo wa maendeleo ya kisasa na fikra za kujitegemea kama ilivyo shauku ya watanzania wote.
Wamemaliza kazi ya kulisimamisha taifa (CCM) Sasa ni muda wa UP kuleta maendeleo ya kweli kwa watanzania wote.
Pamoja kwenye Umoja Bwana Tindo
Amani iwe nawe
 
Kile kingine, utafiti wa TWAWEZA ulionesha kinaungwa mkono zaidi na watu wajinga, hiki huenda itakuja kufahamika baadaye kuwa kinaungwa mkono zaidi na maharamia wanaopenda kuua, kuteka, kupoteza watu. Hiki kitakuwa ni chama cha kishetani kwaajili ya kusimamia na kuendeleza matendo ya ibilisi.
[emoji106]
 
Maandishi yako yamejaa hofu na uoga mkubwa kwa kitu usichokifahamu hilo liko wazi sana. Mpaka sasa UP haijaweka manifesto yake wazi wala safu yake ya uongozi lakini unakuwa mstari wa mbele kuitabiria vibaya.
Tukubaliane jambo moja CCM wameshindwa kuliongoza taifa na tena kuna ombwe kubwa sana la kiuongozi Tanzania. Bahati mbaya zaidi kuna Kuta nene sana kupenyeza mawazo huru kwenye vyama vya siasa vyenye muelekeo wa kushika Dola. Hivyo ni lazima kwa manufaa ya Tanzania ya leo na kesho kuwa na msingi mpya wenye muelekeo wa maendeleo ya kisasa na fikra za kujitegemea kama ilivyo shauku ya watanzania wote.
Wamemaliza kazi ya kulisimamisha taifa (CCM) Sasa ni muda wa UP kuleta maendeleo ya kweli kwa watanzania wote.
Pamoja kwenye Umoja Bwana Tindo
Amani iwe nawe

Nimecheka kwa nguvu, eti nina hofu, hofu niipate toka kwa hilo tawi la ccm. Bado mnaamini mnaweza kuvuta watu kwa mitazamo na mipango ya kiccm? Ngoja muingie uwanjani ndio mtajua kizazi kimeshabadilika.
 
Kiuhalisia hayati Magufuli alikua ni kiongozi jasiri na shupavu kweli, lakini hakua na sifa za kuwa Rais.Nafasi ya juu kimamlaka kwa mtu kama yule ilikua ni uwaziri mkuu tu.Yaani juu yake inapaswa kuwa na mtu aliepevuka kwa hekima na maono ya kuvumilia kupishana maono na watu na kukubali kushaurika.

Lakini kiongozi aina ya Magufuli ni mtu mwenye kutumia maguvu mengi hata mahala pasipohitaji maguvu, mwisho wa siku mnaibomoa nchi badala ya kuijenga.Mungu amlaze pema huko alipo maana ametuachia somo kama taifa!!!
Wew hujui kitu hata sifa za kiongozi huzijui unazungumzia siasa za uongo uongo yule alikuwa reformist
 
Mmeichoka ccm Wakati ndio imewaanzisha, au unadhani tutapotea maboya kirahisi hivyo? Hii mbinu ya kuanzisha chama na kuja na gia hizo ccm ilifanikiwa zamani, kwa sasa tunawachora tu.
Chadema haitakuja kuaminika tena kamwe
 
Ni mjinga anayeweza kuamini kuwa mrengo wa mawazo ya Magufuli yangelifikisha Taifa hili mbali. Endeleeni kujifurahisha!
Yanaweza kulipeleka taifa mbele kwa speed ya mara 10 zaidi ya ilivyo sasa just kukiwa na check and balances!

Mnakimbilia kudhoofisha alichofanya Magufuli kwa sababu alikuwa kiongozi wa chuma kwa ku sabotage mazuri yake yote kwa mabaya machache.

Ndio alikuwa bold ila tukumbuke maendeleo yoyote hayaji kirahisi hata maendeleo binafsi hata hao matajiri unaowaona walipitia session za ukatili sana kufikia hapo walipo leo. Ndio iko hivyo sababu maisha ni vita mkuu.

Hata wewe ili kufika ulipo kuna watu ilikuwa lazma uwashinde ama kwa juhudi au kwa hila ili uonekane bora na upate nafasi zaidi. You can not escape from that reality. Sasa ni nini kinakufanya umuone Magufuli ni monster wakati unaishi katika uhalisia huo huo
 
Ni mtazamo wako lakini ukikaa ukawa huru utagundua kulikuwa na kitu cha ziada kwa JPM
Hivi ni kitu gani cha ziada kinakuwepo katika kuua au kupoteza watu, au kuwashambulia wanaokukosoa. Au hata kuwagunga watu kwa kuwaonea?

Muuaji, hata afanye nini, siamini kama huyo anaweza kuwa mtu mzuri kwa kipimo chochote kile.

Hicho chama, kama kweli kitaenda kwa wananchi kuwa kipo akwaajili ya kuenzi yale maovu ya marehemu, hakika kuna maeneo kitatemewa hata mate.
 
Ni mjinga anayeweza kuamini kuwa mrengo wa mawazo ya Magufuli yangelifikisha Taifa hili mbali. Endeleeni kujifurahisha!
Ni wato wenye upeo mdogo ndio wanaoamini kiwa sera za marehemu zingetufikisha popote. Kama anageishi zaidi, watu wanaochelewa kuelewa ndiyo wangetambua uhovyo wa sera zake ambazo zingezidi kulididimiza Taifa katika kila nyanja ya maendeleo.
 
Hiki Chama na wafuasi wake ni contradictions tupu

Magufuli aliziba kabisa space ya kisiasa iliyokuwepo Tanzania, na kusema CCM itatawala milele

Licha ya kuzuia mikutano ya vyama, Magufuli alianzisha uhuni mwingi ambao haukuwahi kuwepo kwenye siasa za Tanzania, kuteua makada wa CCM Kama wakurugenzi, kuengua watu kwa vigezo kuwa hawajui kusoma, kutekwa watu wakati wa kurudisha fomu

Sasa kwa Chama chochote Cha upinzani hakiwezi kusema kinamuenzi Magufuli sababu uwepo wake tu tayari una contradict aliyoamini na kuyafanya Magufuli
Upo sahihi sana. Ndiyo maana naamini kuwa waanzilishi wa hiki chama, ama watakuwa ni wanafiki sana, au wana upeo mdogo sana.

Huwezi kufanya kitu ambacho unasema unamuenzi mtu ambaye yeye hakukitaka kabisa.
 
Ndugu,
Ukiamua kuwa huru na mawazo yako utamuona Magufuli katika picha nyingi sana. Kimoja ambacho wote tunakubaliana ni kuwa Magufuli alikua mzalendo na mwenye upendo wa dhati kwa Tanzania. Alihubiri Tanzania yenye maendeleo na aliamini katika watanzania hivyo alipandikiza mbegu ya ujasiri na uzalendo kwetu wote. Sisi tuliobaki tumejifunza mengi na tunaanzia hapo kuhakikisha kweli tunaisimamisha Tanzania ya mfano na mkombozi wa bara la Africa
Uharamia na ukatili siyo sehemu ya uzalendo.

Alichokuwa anakifanya Magufuli, hakina tofauti na kile alichokifanya fashisti Stallin, aliyekuwa Rais wa Urusi, ambaye alikuwa kiongozi muuaji aliyekuwa akiimba kila siku kuwa anayepingana naye, amekosa uzalendo.

Madikteta wengi, hujificha kwenye neno uzalendo. Anaua watu kwa kisingizio kuwa eti wale wanaomkosoa wamekosa uzalendo. Anafungia vyombo vya habari kwa kudai vyombo hivyo vimekosa uzalendo.

Magufuli, bila ya kumtaja kama mtu aliyekuwa katili, dikteta, mwongo aliyehubiri tofauti na kilichopo moyoni mwake na anayetenda, na sisi tutakuwa ni wanafiki. Magufuli hata apambwe vipi, kuna siku ambayo uovu wake wote utawekwa wazi, na watu watabakia midomo wazi, na jina hilo litakuwa likitajwa kwa ubaya zaidi kuliko kwa mema.
 
Back
Top Bottom