Kwenu watoto wa kiume, Mapenzi ya baba kwako utayatambua ukianza kujitegemea na kuhama kwenu, huenda utaona hata yale ya mama hayafikii

Kwenu watoto wa kiume, Mapenzi ya baba kwako utayatambua ukianza kujitegemea na kuhama kwenu, huenda utaona hata yale ya mama hayafikii

Kama kutoka nyumbani, kupata mke na mtoto na kujitegemea ndo chanzo cha kuutambua upendo wa baba. Basi hiyo kanuni kwangu sijui kwanini imefeli. Kina ninavyopambana na kustep ndo nazidi kupunguza upendo juu yake

Ngoja tu niishie kusema

I HATE MY DADY
Alikufanya nini?
 
Mama anaapeal kwenye emotions za wanae

Baba kwenye Reasoning zao

Mtoto anaendeshwa na hisia
Mtu mzima ALIYEJITAMBUA hujifunza kuweka hisia pembeni!


Emotions are bigger than Reasoning for the many!

So anaonekana na wengi wazee wa mafeeling mama ndo kila kitu!

Lakini ukikaa ukareason kidogoo tuu utamuona mama is nothing kabisa!

Think uone Baba alivyo hana mpinzani!

Mama atakunyima kitu kiujanja ujanja
Baba atakunyima kitu Kwa kukupa za uso

Utachagua Mwenyewe!

Ukiacha kuruhusu hisia zikuendeshe Utaelewa!

Baba ndo kila kitu!
Mama kawaida tuu!

Mama ni Waongo na Manipulators kwa watoto wao
Mara chache kumwambi mwanae Ukweli!

Baba atakuchana live, jicho kwa jicho, jino kwa jino ukiwa na akili utamuelewa baba

Mwana Mpumbavu = mama ake
Mwana mwenye akili = Baba yake
 
Kwa sababu nazidi kujitambua na kumlinganisha na mimi mwenyewe. Huwa naona kama alifeli vibaya. Hapo namlinganisha na mimi ninavyowajibika kwa wanangu. Ninavyojari matatizo yao na ninavyoteseka kama watakuwa wanapitia magumu
Kama ni hivi tu huna haja ya ku HATE… nilidhani amekufanyia madhila flan.. We pambana na hali yako na jitahidi kuwa baba “bora” kuliko alivyokuwa mzee..
 
Nakumbuka nilipopata kazi, baada ya kukaa mwezi mmoja mzee alinitumia laki nne na sikuwa nimeomba, akaniambia kwamba mwanzoni mwa kazi unakuwa na mahitaji mengi Sana, na Kweli muda huo nilikuwa na uhitaji mkubwa sana kwasababu nilikuwa nahitaji kununua vitu vingi.

Ila mama (pamoja na kumpa mzigo mkubwa kutoka kwenye pesa ya kujikimu) lakini alikuwa anadai pesa zaidi kwa sababu tu nimepata kazi inayonipa pesa.

Mimi ni mamas boy lakini Ile kitu ilinisaidia Sana kujua mzee ananijari Sana kuliko ninavyofikiria.
 
Mama ni moyo ana mapenzi ya dhati yaliyovuka mipaka kwa mwanae, leo hii hata mama yako ukimwambia unataka kuwa msanii atakupa sapoti, mapenzi ya dhati kuna muda huwa yanapofusha kushindwa kuona uhalisia, hapo unakuta mtu hana kipaji wala bidii, hana connections, n.k

Baba ni kichwa, mlinzi na mtafutaji, leo hji ukimwambia unataka kuwa msanii atatafakari na kuona mbali maana ukiwatoa kina Diamond, Kiba, Harmonize na wasanii wengine wachache waliofanikiwa, kuna lundo kubwa sana la wasanii miaka nenda rudi wamesota (kwa ambao tumekaa na wasanii tunajua msoto wake), atakupa makavu na hatakusapoti kwa sababu anahofia wewe kuwa wasanii wale miaka nenda rudi hata hawasikiki, atakwambia ni bora akufanyie connection kwa rafiki yake fundi seremala ujifunze hio stadi nawe uwe fundi ama hata akutaftie shamba ukalime uwe na uhakika hata wa kula na kuja kilisha familia yako.

Hapo ukitumia hisia utaona mama anakupenda ila ukitumia akili unaona baba anakujali.

ila kadri umri unavyoenda mtoto wa kiume akiacha kuwa tegemezi na kuanza kujitegemea, kuhama, kujitaftia ridhiki, kuwa na familia, n.k basi hapo ukaribu kwa baba unaongezeka maana wanaanza kufanana, mtoto na baba wote wanajitaftia ridhiki, mtoto na baba wote wameoa, mtoto na baba wote walihama kwao kujitegemea, n.k.

yote kwa yote wote wana umuhimu, ukipatwa na tatizo mama atakuwa karibu na wewe sana huku mzee akihangaika huko nje kukunasua kwenye tatizo kadri ya uwezo wake wote, hapo ndipo wengi wanakosea wanadhani mama ndie mwenye umuhimu zaidi lakini wanasahau baba yupo nje anapambana ili kuwanasua kwenye matatizo ya ujinga kwa kuwapa mahitaji ya elimu, kuwaondolea njaa kwa kuwalisha, kuwasitiri kwa kuwavisha, kuhakikisha hamlali nje kwa kulipia kodi ya nyumba au kujenga, kuwatoa uvivu kwa kuwapa kazi za kufanya nyumbani, kuwanusuru katika maamuzi mabaya yanayoweza kuwapeleka jela kwa kuwatia adabu tangu mkiwa wadogo, n.k. mchango wa baba ukitaka kuujua kama wewe ni mtoto wa kiume anza kujitegemea nakwambia utaujua tu, ongeza mke uwe na familia utapata oicha nzuri zaidi... ila kama bado unaishi kwenu bado hujawa mwanaume wa kuondoka kwenye kiota ukajitegemee hapo itakua kazi kuona mapenzi ya baba.
sacrifice ya baba haizungumziki. happy fathers day
 
Kama kutoka nyumbani, kupata mke na mtoto na kujitegemea ndo chanzo cha kuutambua upendo wa baba. Basi hiyo kanuni kwangu sijui kwanini imefeli. Kina ninavyopambana na kustep ndo nazidi kupunguza upendo juu yake

Ngoja tu niishie kusema

I HATE MY DADY
Pamoja na kupambana kwako Amini Amini Amini nakuambia siku watoto wako wakiwa wakubwa hawatajua thamani yako kiuhalisia mpaka watakapoanza kujitegemea.
Tena muda Mwingi mama yao atakua anawaambia kama sio Mimi baba yenu asingewasomesha mana Mimi ndio nilikua namshikia bango awasomeshe. Yeye alikua anawaza pombe TU na Wanawake. Baba yenu ni mbishi sana.
Watoto watalishwa sumu mpaka waone kuwa wewe si lolote SI chochote na maendeleo yako ni Kwa sababu ya mama yao.

Wanaume wanasiri nzito sana. Baba anaweza akajua kuwa mtoto Fulani sio wake lakini kamwe hawezi kumwambia au kuwatangazia watu au kuwaambia watoto wengine kuwa huyu sio mtoto wangu ana baba yake . Lakini Mama akisikia TU kuwa baba ana kamchepuko hata kama ni kusikia bila ushahidi atawasimulia watoto na kuwaaminisha kuwa baba hawajali anajali Wanawake TU.


Mtume Muhamad aliwahi kuonyeshwa Moto wa jehanam ,kule motoni aliona Wanawake wengi kuliko wanaume. Mtume akamuuliza Allah , ni Kwa Nini Wanawake ni wengi kuliko wanaume kule motoni?
Alijibiwa kuwa ni Kwa sababu hawaridhiki na Yale wanayofanyiwa na waume zao.

Miaka ya Karibuni nikasikia mhubiri mmoja wa Kongo aliyewahi kwenda kuzimu akaona pia kuwa Wanawake walikua wengi kuliko wanaume.

Wanaume wameumbwa Kwa mfano wa Mungu katika kulea familia.
Mungu alijua kuwa Wanawake ni katili sana Kwa mtoto au kiumbe asichokitoa tumboni mwake , Wanawake wanapenda Kwa sababu Fulani . Vizazi vijavyo Kwa hulka za Kiafrika Vijana wengi hawataoa mana kuishi na Mwanamke wa Kiafrika itakua ni ngumu sana hasa katika mazingira ya umaskini mana thamani ya BINADAM inaangaliwa kwa kile alicho nacho kuanzia kwenye familia.
Kwanza changamoto za Karne zijazo zitakua ni kubwa mno na mitandao itakua wazi sana. Hakutakua na uwezekano hata wa kuchepuka bila kujulikana. Hivyo Ndoa zitakua ni ngumu sana Kwa watu wengi na kuuana Kwa wivu wa mapenzi kutaongezeka sana. Mana kila kitu kitakua kinawekwa wazi. Itakua ni rahisi kujua alipo mtu yeyote Kwa wakati wowote unapotaka. New World Order inakuja Kujenga misingi ya uadilifu mkubwa na itakua kitanzi kwa wanadamu.

Hebu angalia Wanawake wakikasirika wanavyoweza Kupiga mtoto na kumtolea maneno mabaya kama Mbwa, ngombe wewe, muone bichwa lake , sura mbaya kama Nini? Hapo anamtukana mtoto aliyemweka tumboni miezi Tisa. Fikiri angekua angekua hampati Kwa uchungu mkubwa ingekuaje? Fikiri Mwanamke anaweka mtoto tumboni miezi 9 halafu anamtupa kisa hajapata matunzo Toka Kwa baba yake.!! Utagundua kuwa thamani ya mtoto kwa Mama yake ni Kwa sababu Kuna mwanaume au wanaume wanaomsaidia kimalezi na kuana mtoto anakua akiwa na Afya na hata kujitegemea!
 
Back
Top Bottom