Laana: Usije ingilia ugomvi wa wazazi hata siku moja

Laana: Usije ingilia ugomvi wa wazazi hata siku moja

Si kweli hata kidogo mkuu.
Yaweza iwe kweli sio kweli hata kidogo, pia labda ungeongeza sababu zako kidogo kwanini unasema sio sahihi.

ila pia hata kabla sijasikiliza sababu zako nikusisitize kuwa hili suala la ugomvi wa wazazi nisheria ya ulimwengu nikanuni iliyopo kuanzia kiroho hadi kimwili, mtoto hana sababu yoyote inayokubalika na kumfanya aingilie ugomvi wa wazazi.

Hili suala ni ulikubali au ulikatae linabakia kuwa hivyo jua chomoza mashariki na kuzama magaribi, kwa ufupi mzazi hakosei wala hana kosa kwa mtoto juu ya ugomvi wa wazazi.

wengi sana walioziona hizo haki wametafunwa vyema kabisa na hawajui nini kinawatafuna
 
Mzazi hakosei kwa mtoto hilo weka akilini haijarishi unayaona makosa kwa kiwango cha namna gani,
ukiona imeshindikana kabisa kuvumilia peleka mashitaka kwa wazazi wao, wao binafsi ndio watayajenga na watajua ni ni namna gani ya kuliweka sawa.

ila katika yote unaloweza kulifanya nikuwa mfariji tu kwa mzazi anayeonewa wala sio kuwa mshauri namna yakumaliza mgogoro wewe nikuwa mfariji tu baaaasi,

Ulimwengu umeweka sheria zake na kanuni zake mzazi hawezi kosea hata siku moja, mtoto ukiona mzazi anakosea kaa nalo moyoni usiingilie ugomvi hata kidogo,
labda nikusisitize kwa kauli hii NI MWIKO MTOTO KUINGILIA UGOMVI WA WAZAZI, NI KOSA KUBWA SANA TENA SANA MTOTO KUINGILIA KOSA LA WAZAZI, ACHA KABISA HILO NI BOMU LA NYUKLIA KABISA MKUU.
Hatuwezi kuhukumu maana ni wazazi tayr ila Kuna vitu vinakera usione wengine walikimbia kwao matatizo ndo hayo unajua chanzo cha mgogoro kabisa ukiachana na hilo Kuna baadhi ya watu baba zao ni walevi wa kutupa ndo matatizo mara wachelewe kurudi mara ivi kutokuhudumia familia kazi kulewa tu
 
Hatuwezi kuhukumu maana ni wazazi tayr ila Kuna vitu vinakera usione wengine walikimbia kwao matatizo ndo hayo unajua chanzo cha mgogoro kabisa ukiachana na hilo Kuna baadhi ya watu baba zao ni walevi wa kutupa ndo matatizo mara wachelewe kurudi mara ivi kutokuhudumia familia kazi kulewa tu
Nikweli kabisa mkuu kuna changamoto nyingi sana watoto tunakuwa tunazipitia sana sana kutokana na hii migogoro,
ila ndio zinatujenga muda mwingine inafanya nasisi pia tuje kukaa katika familia zilizojengeka vyema na kutusaidia tusije fanya vitu ambavyo watoto wetu watapitia hali tulizopitia.
 
NIkukumbushe tu kuhusu hili ugomvi wa wazazi hauna huyu mwenye haki huyu mwenye makosa,
nakusisitiza tena hakuna mwenye haki ugomvi wa wazazi mtoto unayeweza kumuona,

ndio maana hata siku moja hata kama unaweza kusuluhisha ugomvi wa wazazi ni mwiko hata siku moja kumkalisha chini mzazi mmoja au wote kusuruhisha ni mwiko na haiwezekani hata kidogo.

narudia tena ndugu ugomvi wa wazazi mtoto haumuhusu hata kidogo, unaloweza kulifanya nikuwa mfariji tu ila usijaribu hata kidogo kujaribu kusema huyu ana haki au hana haki,

sheria za ulimwengu hazilitambui hilo la mzazi mwenye haki ama asiyekuwa na haki sheria za ulimwengu zinatambua mtoto hupaswi kujihusisha na ugomvi wa wazazi.

pia kwa ziada ugomvi wa wazazi haujakaa kimwili hukumu zake kama unavyofikiria utamuona nani ana haki nani hana haki,

mbaya sana mzazi akajifanya mjinga na akakubaliana na kauli zako akakusikiliza, lakini ndani ya moyo akasema huyu mtoto leo anajifanya mkubwa wakunikanya mimi,
yaani unacheka na mzazi afu kumbe moyon kakukunjia ogopa sana tena sana ndugu yangu ni hatari mno.

nisikuchoshe na maelezo mengi ila tambua tu hauna uhakimu wowote katika kesi ya wazazi wala hauna hata asilimia ya 000000000.00001 kuingilia mgogoro huo, usije kujaribu kamwe ndugu yangu
Mkuu hutambui unachozungumza.
 
Haya maneno unayatoa wapi mkuu!?
binadamu tunatofautiana mwingine anajua moja mwingine anajua mbili,
nikufufata tu sheria na kanuni za ulimwengu, baadhi wanabahati zakujua na kutambua mapema,
ni ngumu kujifunza kila mtu asipokuwa na sababu ya kujifunza hivyo ni vyema kutoa maonyo ya madhara yanayoweza kutokea.

Usianike mahindi usiku sababu hakuna jua, hakuhitaji maelezo ya kwanini jua haliangazi usiku.

Kamwe Usiingilie ugomvi wa wazazi haijarishi unaona mmoja mkosefu kiasi gani, laana yake hakuna anayeweza kukukomboa nayo zaidi ya mzazi mwenyewe
 
binadamu tunatofautiana mwingine anajua moja mwingine anajua mbili,
nikufufata tu sheria na kanuni za ulimwengu, baadhi wanabahati zakujua na kutambua mapema,
ni ngumu kujifunza kila mtu asipokuwa na sababu ya kujifunza hivyo ni vyema kutoa maonyo ya madhara yanayoweza kutokea.

Usianike mahindi usiku sababu hakuna jua, hakuhitaji maelezo ya kwanini jua haliangazi usiku.

Kamwe Usiingilie ugomvi wa wazazi haijarishi unaona mmoja mkosefu kiasi gani, laana yake hakuna anayeweza kukukomboa nayo zaidi ya mzazi mwenyewe
Hizo sheria umezitoa wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Labda Kuna level ya ugomvi, lkn Kuna ugomvi unaoathiri afya yenu! Biblia inasema enyi wazazi msiwachokoze watoto. Kuna scenario mbili nilikutana nazo nikupe mfano:

1. Baba anampiga mama makonde usiku wa manane watoto mmelala, mnasikia mama analia kwa kuugulia na baba anashusha makonde! Utaangalia tu kwa kusema huhusiki na ugomvi? Au utaamka kwenda kuwatanganza wazazi kwa majilani ili waje waamue ugomvi?

2. Niliwahi kuona baba mlevi kupindukia na anachofanya yeye anabeba kitu chochote na kwenda kunywea pombe! Wewe Kama mtoto ukiingia kwenye maamuzi ya kumzuia ni kuingia naye ugomvi, je utaacha nyumbani kwenu pawe peupe maana atanywea Hadi vyakula na nguo hata Kama ni soksi zako na madaftari atabeba. Au utaajiri mtu wa kukusaidia kumlinda mzee maana najua watapigana tu!

Sema mkuu tusiingilie ugomvi wa mahusiano ya wazazi, lkn wazazi wasiwachokoze watoto, kama wewe n mzazi na kwa namna moja umesababisha mtoto kuact different nakuambia hio laana haiwez kumpata kamwe hata ufanye Nini! Maana ukishakua mtoto hasa wa kiume unageuka mlinzi wa rasilimali za nyumbani na mlinzi wa wadogo zako na wazazi!

Kama n mzazi jiheshim usilete ugomvi mbele ya watoto au watoto wanasikia mnawaweka majaribuni na Mungu atawahesabia haki kwa sababu hio.
 
Habari ya siku nyingi ndugu zangu, ngoja niende kwenye hoja moja kwa moja

Masuala ya ugomvi na migogoro ya ndoa kwa wazazi wetu ni mambo ambayo huwa tunakumbana nayo mara kwa mara na kwa asilimia kubwa sana japo sio kila familia au kila mtoto huweza kuyapitia haya mambo.

Ila niwape angalizo ndugu zangu katika masuala ya matatizo ya kifamilia ya wazazi usije hata siku moja ukaegemea upande wa mtu mmoja hata kidogo, kubwa unaloweza kulifanya ni kumfariji tu yule aliyeathirika zaidi kuwa na moyo mmoja wakusimama naye na kuhakikisha msongo na kukata tamaa isiwe sehemu yake.

Ukimchukia baba na akajua sababu ya mama au ukimchukia mama akajua sababu ya baba nakuhakikishia ndugu yangu nenda hata kwa mwamposa na shehe unayemjua wewe hii laana itakutafuna sana tena sana utakuwa ni mtu wa hatua mbili mbele tatu nyuma pasipo hata kuwa na suluhisho.

Narudia tena Mzazi awe na kosa au asiwe na kosa ila ukaingilia ugomvi wao ukamchukua mmoja wapo na akakufuta katika akili yake na moyo wake umekwisha kabisa.

HIli suala halina tiba yoyote zaidi ya kwenda kujiungamanisha na mzazi wako tena kabla hajaondoka hapa duniani na kama haujajifungamanisha naye akaondoka katika maisha haya hata ungekuwa mlokole wakuhamisha milima kwa maombi utahusika tu kwenda kutambika kumuomba msamaha mzazi wako.

Ndugu zangu hili suala limekaa kiroho sana namna ambayo huwezi tambua kiwepesi wepesi, laana ya kuingilia ugomvi wa wazazi na mzazi akaju umeegemea upande mmoja na akakukatia tamaa hii laana hakuna kiumbe wakuitoa chini ya jua na ulimwengu mzima zaidi ya mzazi wako,

Lasivyo itaendelea kuwasumbua hadi watoto wako pamoja na wajuu zako,

Na mara nyingi hizi laana zao zikisha kukalia wewe katika maisha hautaona la maana lolote wala hautakuwa na ahueni mahusiano yatakusumbua kama sio mahusiano basi maendeleo itakuwa shida kama sio maendeleo kipato kugumu kama sio kipato kigumu basi ipo sehemu ya muhimu kwako utakwama na hautaweza kujinasua hata kidogo,

Ukienda kuombewa na kuroga kwa waganga utapata ahueni ya mwezi mmoja tu na wala hautapata jibu la moja kwa moja hata siku moja.

Laana Hii ikikuvaa inatoka kwa njia moja tu wewe kwenda kwa mzazi wako ili arudishe moyo wako tena kwa ajili yako.

Sababu kubwa ya laana ya mzazi kuwa na nguvu nikwasababu kiroho kwa hapa duniani wazazi ndio miungu yako , wawe hai wasiwe hai wazazi wako ndio alfa na omega wako hapa duniani,

Siku nyingine nitakuja kueleza aina za laana ambazo wazazi wanaweza kukuachia,
Ukiwa na swali lolote unaweza ukauliza jisikie huru kabisa.


NASISITIZA HAKUNA MTUMISHI WALA SHEHE WALA MUNGU WALA SHETANI ANAYEWEZA KUITOA HII LAANA.

Muwe na jioni njema...!
Kama mbariki Laana ni Mwenyezi Mungu basi naamini hata ukimpigia Magoti Yeye ambaye pia ndiyo Kawaumba hao Wazazi atakusamehe tu kwakuwa Yeye ndiyo kila Kitu.

Hii Kasumba ya kuamini kuwa ukiona hufanikiwi duniani au Mambo yako hayaendi basi huenda kuna Mzazi wako Mmoja au Wote wawili umewakosea ni ya Kipumbavu kwani tukiiamini sana ndiyo inaenda kuharibu hadi Saikolojia zetu na kujikuta hatufanyi la maana.

Tupunguze huku Kutishana juu ya Wazazi Wetu na kuwaona kuwa Wao ni kila Kitu na kwamba hawakosei au hata Wao pia Wakitukosea hawapaswi Kujirudi Kwetu Watoto Kuomba Radhi hata kama siyo kwa Moja kwa Moja bali hata Kidiplomasia tu.

Migogoro mingi ya Wazazi na Watoto huwa inaibuliwa na Vyanzo vingi na kuna Watoto wengine Wanagombana na Wazazi wao kwa Kuchonganishwa na Ndugu, Jamaa na Marafiki au wemgine hata kwa Kurogwa au wengine hata Kufitinishwa na Ndugu zao wa Damu kabisa.

Sikatai kuwa kweli ukimkosea Mzazi wako huwezi pata Laana ila hata hiyo laana yenyewe huwa inaangaliwa na Mwenyezi Mungu kwa aina ya Kosa na tuache Kudanganyana hapa kuwa yaani Mzazi wako akiamua tu Kukulaani vile anavyojisikia basi hapo hapo inakupata.

Halafu nijuavyo Mzazi anayejitambua akiona yuko katika Mzozo au Mgogoro na Mwanae atafuta njia za Busara na Hekima hata kupitia kwa Ndugu au Marafiki zako ili mkae chini myamalize.

Kwa mfano unaweza kukuta labda Kibinadamu tu umemkosea Mzazi wako au hata hujamkosea popote ila kwa kuona kuwa Mzazi wako hana raha au futaha nawe ukataka kukaa nae chini myamalize lakini unakuta Mzazi huyo huyo hataki au anakukwepa huku akiendelea Kukuchukia. Je, hapa unadhani anayepata sasa Laana ya kweli ni Wewe Mtoto au Yeye Mzazi wako?

Na nijuavyo ni kwamba Laana mbaya duniani ni ya Mama Mzazi kwani Yeye ndiyo kwa 85% anakuhusu na pia Yeye ndiyo anajua Baba yako halisi ni nani. Laana za Baba huwa hazina Nguvu kwakuwa hata Kibaiolojia tu yeye ni mpandaji wa Mbegu kisha anasepa zake ila anayehangaika na hiyo Mbegu mpaka kuja duniani ni Mama na ndiyo maana unaambiwa ukimkosea tu Mama yako Mzazi wahi upesi mno ukampigie Magoti umuombe Radhi na mpeane Mikono na yataisha.

Mwanadamu kufanikiwa duniani Kimaisha hakutokani tu na Baraka za Wazazi wake bali pia ni Mipango yake, Malengo yake, Mikakati yake, Kujituma Kwake, Kujitambua Kwake na kubwa zaidi ni Kumuamini na Kumtumainia zaidi Mwenyezi Mungu kwani ana Falsafa yake Kuu ya kuwa huwa hawahi wala hachelewi katika Kumbariki Mtu au Mwanadamu.

Ni kweli tuwapende Wazazi wetu na hasa hasa tuwaombee sana kwa Mwenyezi Mungu na hata Wao pia wanatakiwa Kutupenda, Kutuombea na Kutusamehe Watoto wao pale ambapo kweli wanaona tumewakosea ila tuache Kutishana kuwa kama hufanikiwi Kimaisha hapa duniani basi huenda kuna mahala umemkosea Mzazi au Umewakosea Wazazi huu ni Uswahili na Upuuzi mkubwa mno.

Kwahiyo Watu wote duniani ambao wana Maisha magumu ni kutokana na Kukosana na Wazazi wao au Kuingilia Maugomvi yao? Je, hakuna Watoto ambao wana Mahusiano mazuri na Wazazi wao lakini bado tu Maisha yanawapiga? Je, hakuna Watoto ambao tunajua fika kuwa hawako vyema Kimahusiano na Wazazi wao lakini bado wana Maisha mazuri na tena Kutwa yanazidi tu kuwa mazuri?

Tunawashukuru Wazazi wetu kwa kutuleta hapa duniani, tunawapenda hata kama wapo wanaotuchukia na ndiyo maana wengine huwa kutwa tukiwa katika Dua au Sala zetu tunawaombea ila tusisahau kuwa mwenye Dhamana yako ya Kimaisha na ambaye akilipanga hata Watu wengine walipangue vipi, ipo Siku litaenda tu ni Mwenyezi Mungu ambaye ni Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo.
 
Unaingilia ugomvi kusuluhisha. hapo hauna laana. Kwa mfano mzee akikuambia uende ukaibe, ukigoma akakuambia atakulaani, utaenda kuiba? Baba anampiga mama nisingiilie kuwaamua kisa nitalaaniwa. Haiwezekani.
Je, ni sahihi wewe kumpiga mkeo au kumtukana hata kama amekukosea? Je, maandiko ya vitabu vya dini vinasemaje?
Tumekuwa na hofu na dhana potofu kuwa ni sahihi kutoingilia ugomvi wa wazazi kwasababu tutalaaniwa ndiyo maana familia za kiafrika zimejaa umasikini, chuki na kiburi.
Baba anatelekeza familia, anaenda kusokojulikana tena akifika huko anaoa. Anawasahau, inapita miaka mingi. Hajui mnakula nini wala mnavaa nini.
Baadae baada ya kukua na kufanikiwa anakuja kwasabb mila za kiafrika hurusiwi kumhoji wala kumkataa mzazi. Anaanza kukupangia kumhudumia. Hapana aisee kupata laana ni pale unapokiuka matendo ya haki (matendo mema) ya mzazi.
Watu wengi wanafikiri kupata laana ni kutoka kwa wazazi ila laana unaweza kuipata kwa mtu yoyote na kutenda matendo machafu. Wewe unamwingilia mwanamke kinyume cha maumbile, ushoga, unampiga mkeo na kunyanyasa watoto wako hizo zote ni laana.
NIkukumbushe tu kuhusu hili ugomvi wa wazazi hauna huyu mwenye haki huyu mwenye makosa,
nakusisitiza tena hakuna mwenye haki ugomvi wa wazazi mtoto unayeweza kumuona,

ndio maana hata siku moja hata kama unaweza kusuluhisha ugomvi wa wazazi ni mwiko hata siku moja kumkalisha chini mzazi mmoja au wote kusuruhisha ni mwiko na haiwezekani hata kidogo.

narudia tena ndugu ugomvi wa wazazi mtoto haumuhusu hata kidogo, unaloweza kulifanya nikuwa mfariji tu ila usijaribu hata kidogo kujaribu kusema huyu ana haki au hana haki,

sheria za ulimwengu hazilitambui hilo la mzazi mwenye haki ama asiyekuwa na haki sheria za ulimwengu zinatambua mtoto hupaswi kujihusisha na ugomvi wa wazazi.

pia kwa ziada ugomvi wa wazazi haujakaa kimwili hukumu zake kama unavyofikiria utamuona nani ana haki nani hana haki,

mbaya sana mzazi akajifanya mjinga na akakubaliana na kauli zako akakusikiliza, lakini ndani ya moyo akasema huyu mtoto leo anajifanya mkubwa wakunikanya mimi,
yaani unacheka na mzazi afu kumbe moyon kakukunjia ogopa sana tena sana ndugu yangu ni hatari mno.

nisikuchoshe na maelezo mengi ila tambua tu hauna uhakimu wowote katika kesi ya wazazi wala hauna hata asilimia ya 000000000.00001 kuingilia mgogoro huo, usije kujaribu kamwe ndugu yangu
 
Unaingilia ugomvi kusuluhisha. hapo hauna laana. Kwa mfano mzee akikuambia uende ukaibe, ukigoma akakuambia atakulaani, utaenda kuiba? Baba anampiga mama nisingiilie kuwaamua kisa nitalaaniwa. Haiwezekani.
Je, ni sahihi wewe kumpiga mkeo au kumtukana hata kama amekukosea? Je, maandiko ya vitabu vya dini vinasemaje?
Tumekuwa na hofu na dhana potofu kuwa ni sahihi kutoingilia ugomvi wa wazazi kwasababu tutalaaniwa ndiyo maana familia za kiafrika zimejaa umasikini, chuki na kiburi.
Baba anatelekeza familia, anaenda kusokojulikana tena akifika huko anaoa. Anawasahau, inapita miaka mingi. Hajui mnakula nini wala mnavaa nini.
Baadae baada ya kukua na kufanikiwa anakuja kwasabb mila za kiafrika hurusiwi kumhoji wala kumkataa mzazi. Anaanza kukupangia kumhudumia. Hapana aisee kupata laana ni pale unapokiuka matendo ya haki (matendo mema) ya mzazi.
Watu wengi wanafikiri kupata laana ni kutoka kwa wazazi ila laana unaweza kuipata kwa mtu yoyote na kutenda matendo machafu. Wewe unamwingilia mwanamke kinyume cha maumbile, ushoga, unampiga mkeo na kunyanyasa watoto wako hizo zote ni laana.
Hili la kumla nyuma mke NI penzi halina laana...haswa Kama mnakubaliana..NI penzi Tu....
 
Hizo sheria umezitoa wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
kuna wakati haja kubwa na msingi nikupokea tiba kutoka kwa tabibu, kujua dawa imetoka wapi ni vyema kujifunza kuwa tabibu,
si kila kilicho msaada lazima tukijue mwanzo wake, bali wale waliotayari kujua huweza kujua

sijajua shida ni ipi kujifunza kuzuia kuingia katika matatizo yanayoweza kukwepeka au kujifunza kwanini liwe tatizo
 
Back
Top Bottom