Laana: Usije ingilia ugomvi wa wazazi hata siku moja

Laana: Usije ingilia ugomvi wa wazazi hata siku moja

Unaingilia ugomvi kusuluhisha. hapo hauna laana. Kwa mfano mzee akikuambia uende ukaibe, ukigoma akakuambia atakulaani, utaenda kuiba? Baba anampiga mama nisingiilie kuwaamua kisa nitalaaniwa. Haiwezekani.
Je, ni sahihi wewe kumpiga mkeo au kumtukana hata kama amekukosea? Je, maandiko ya vitabu vya dini vinasemaje?
Tumekuwa na hofu na dhana potofu kuwa ni sahihi kutoingilia ugomvi wa wazazi kwasababu tutalaaniwa ndiyo maana familia za kiafrika zimejaa umasikini, chuki na kiburi.
Baba anatelekeza familia, anaenda kusokojulikana tena akifika huko anaoa. Anawasahau, inapita miaka mingi. Hajui mnakula nini wala mnavaa nini.
Baadae baada ya kukua na kufanikiwa anakuja kwasabb mila za kiafrika hurusiwi kumhoji wala kumkataa mzazi. Anaanza kukupangia kumhudumia. Hapana aisee kupata laana ni pale unapokiuka matendo ya haki (matendo mema) ya mzazi.
Watu wengi wanafikiri kupata laana ni kutoka kwa wazazi ila laana unaweza kuipata kwa mtu yoyote na kutenda matendo machafu. Wewe unamwingilia mwanamke kinyume cha maumbile, ushoga, unampiga mkeo na kunyanyasa watoto wako hizo zote ni laana.
sahihi sana ulichokisema ndugu umezungumza ukweli mtupu kabisa,

ila kumbuka hili kazi ya moyo haiwezi kufanywa na miguu hata siku moja,

baba kukutuma kuiba na kukataa hilo sio ugomzi wa wazazi,
baba anampiga mama mbele yako suluhisho la kwanza kaite majirani ndio waje kuamulia suluhisho la pili amulia ugomvi lakini usije ukaingia sehemu yoyote ya kujua huyu ana haki au hana haki, usije ukamchukia mzazi akikushushia pamoja nawe hicho kipigo.

kuna siri kubwa ya wazazi katika ulimwengu wa kiroho na kimamla na kiutawala ambayo watu huwa hatuijui kabisa na usipoijua unaweza ona ni haki kabisa,
rudi katika kauli yangu usiingilie ugomvi wa wazazi hata kama unaona kabisa nani anamakosa ugomvi wa wazazi watoto hauwahusu hata siku moja,

baba kutelekeza familia hilo linahitaji busara yako na hekima yako kwa kufuata umelelewa vipi mazingira yamekukuzaje na jamii yako imekufunda namna gani na shida ya kufanya familia ikatelekezwa.

point yangu nikukumbusha tu kutokuingia ugomvi wa wazazi hakuna sababu yoyote ya mtoto inayokubalika kwa namna yoyote ile kumfanya akaingilia ugomvi wa wazazi,

nadhani sheria huwa unazijua mkuu
 
Kama mbariki Laana ni Mwenyezi Mungu basi naamini hata ukimpigia Magoti Yeye ambaye pia ndiyo Kawaumba hao Wazazi atakusamehe tu kwakuwa Yeye ndiyo kila Kitu.

Hii Kasumba ya kuamini kuwa ukiona hufanikiwi duniani au Mambo yako hayaendi basi huenda kuna Mzazi wako Mmoja au


Tunawashukuru Wazazi wetu kwa kutuleta hapa duniani, tunawapenda hata kama wapo wanaotuchukia na ndiyo maana wengine huwa kutwa tukiwa katika Dua au Sala zetu tunawaombea ila tusisahau kuwa mwenye Dhamana yako ya Kimaisha na ambaye akilipanga hata Watu wengine walipangue vipi, ipo Siku litaenda tu ni Mwenyezi Mungu ambaye ni Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo.
kukwama kimaisha haina maana kuna mzazi mmoja kakukosea, kila unapokwama haina maana kuna mzazi ulimkosea hivyo maisha yanakufanya ukwame sababu ya hiyo laana.

kuna kitu kimoja cha muhimu nikukumbushe kabla haujafika mbali, Africa tumekuwa ni watu wa mila,jadi pamoja na desturi zetu hizi mambo zimekuwepo toka enzi na enzi,
kuna misingi mingi sana iliyomo katika hizi vitu hatuijui sababu yakukulia katika mazingira yasiokuwa rafiki katika kujifunza na kuelewa nini tunapaswa kufanya.
Haya mambo yalitufanya wa africa tuweze kuishi maisha ya kiroho ambayo ndio moja kwa moja yameumana na mifumo ya asili kabisa yanayohusu ulimwengu huu.
Nakudokeza na siri hii sasa jambo la kwanza linalotufelisha katika mafanikio yetu binafsi ni kushindwa kujua namna gani tunaweza kutumia wazazi wetu katika kufanikiwa,
jambo la pili nakudokeza mzazi akikukunjia hakuna mungu wala shetani anayeweza kukusikiliza katika ulimwengu huu na sayari zote kwa ujumla.
huyo mungu mtoa laana uliyemsema angeweza kukulaani moja kwa moja maana yake hata pesa angekupa direct utoboe maisha.

sasa akili yako inajua kuwa kila mwenye maisha magumu anakosana na wazazi kitu ambacho tayari upo kinyume kabisa na wala sijasema hivyo mimi nimeongelea matokea ya hii laana ilivyo.
sio kila ugumu wa maisha unatokana na laana za wazazi hata siku moja ila kuna baadhi ya watu hiki kitu kinakuwa kinawatafuna.
 
Labda Kuna level ya ugomvi, lkn Kuna ugomvi unaoathiri afya yenu! Biblia inasema enyi wazazi msiwachokoze watoto.
Shida kubwa nyingine ndio hiyo biblia haijwahi kukufunddisha mambo ya kiroho hata siku moja yenyewe imekaa kimafumbo sana na kwa uandishi wa alama, ni ndumu sana kuiweka biblia kuwa msingi wa kutatua matatizo kwasababu hata isipokuwepo watu tunaweza kukaa na tukajadili kupata ufumbuzi wa shida zinazotukabili, ndio maana wengine hawana biblia wala hawaitumii lakini wanaishi vyema na kutatua matatizo yao.

Wazazi kuchokoza hilo sijalizungumzia bali nimelizungumzia suala la kuingilia ugomvi wa wazazi na ukauhukumu na kuona nani anamakosa na kumfanya mmoja kweli kumuona mkosaji, hii kesi ya wazazi mtoto hauna nafasi hata kidogo, ndio maana hata wazee wakikaa kujadili midogogoro ya ndoa mtoto haujawahi kuitwa kuenda kutoa mawazo yako binafsi,
fumba macho ugomvi wa wazazi haukuhusu kabisa we endelea kuwapa heshima zao pamoja wala usijaribu kuwapatanisha au kudodosa acha kabisa limekaa hivyo.
nyongeza hili suala limekaa kiroho zaidi kuliko kimwili namna unavyoweza kufikiria

1. Baba anampiga mama makonde usiku wa manane watoto mmelala, mnasikia mama analia kwa kuugulia na baba anashusha makonde! Utaangalia tu kwa kusema huhusiki na ugomvi? Au utaamka kwenda kuwatanganza wazazi kwa majilani ili waje
Option nzuri ya kwanza ni bibi na babu wazazi wa wahusika unaweza kuwaambia lolote, ikishindikana msaada wapili majirani wanaweza kuhusika kuamulia,
suala la kutoa siri za ndani hilo ni la kwako ila kama mtoto unaishi katika jamii unaweza tambua hili sio sana na huwezi jua jirani yupi naweza anaza naye atoe msaada basi akili yako haijakomaa kabisa inabidi uwe mpole,
solusheni ya watoto imekaa kiuwezo sana wa watoto kuweza kung'amua hili ni nini na hili ni nini,
na andiko langu linawahusu hasa watoto waliopevuka kiakili na kimwili kiasi kwamba wanauwezo wa kuanza kugusa ugomvi wa wazazi kwa namna moja ama nyingine

waamue ugomvi?

2. Niliwahi kuona baba mlevi kupindukia na anachofanya yeye anabeba kitu chochote na kwenda kunywea pombe! Wewe Kama mtoto ukiingia kwenye maamuzi ya kumzuia ni kuingia naye ugomvi, je utaacha nyumbani kwenu pawe peupe maana atanywea Hadi vyakula na nguo hata Kama ni soksi zako na madaftari atabeba. Au utaajiri mtu wa kukusaidia kumlinda mzee maana najua watapigana tu!
vyombo vya baba yako na mama yako kama vinakuuma kajenge kwako nunua vya kwako full stop

Sema mkuu tusiingilie ugomvi wa mahusiano ya wazazi, lkn wazazi wasiwachokoze watoto, kama wewe n mzazi na kwa namna moja umesababisha mtoto kuact different nakuambia hio laana haiwez kumpata kamwe hata ufanye Nini! Maana ukishakua mtoto hasa wa kiume unageuka mlinzi wa rasilimali za nyumbani na mlinzi wa wadogo zako na wazazi!

Kama n mzazi jiheshim usilete ugomvi mbele ya watoto au watoto wanasikia mnawaweka majaribuni na Mungu atawahesabia haki kwa sababu hio.
mtoto kuact tofauti ni kawaida kabisa kwasababu kuna hali zinakugusa moja kwa moja ukiwa mazingira husika,
ndio maana nikakuambia hakikisha usifanye kitu kikaonyesha kwa mzazi mmoja umeambatana na mzazi mwingine,
hizo hali nikuachana nazo tu na kuvumilia mtoto halikuhusu

kubwa unaloweza kulifanya nikuwa mfariji tu kwa mzazi aliyeathirika zaidi ili kumsaidie asije akaingia katika hatua mbaya zaidi ila sio kuwa hakimu wa shida husika
 
Ukiwa mdogo unahisi mara zote baba anamuonea mama. Anza kuishi na mke ndo utapata jibu sahihi.
Umenikumbusha hii:
"By the time you realise that your father was right, you will have a son who thinks that you are wrong". Charles Wadsworth
😊
 
Sijaelewa. Yan ukiwa tu mzazi huwezi kukosea. Yan anatoka kwenye ubinadamu anaenda kwenye umalaika au? Hakosei tena. na endapo akikosea je?
 
Sijaelewa. Yan ukiwa tu mzazi huwezi kukosea. Yan anatoka kwenye ubinadamu anaenda kwenye umalaika au? Hakosei tena. na endapo akikosea je?
 
Sijaelewa. Yan ukiwa tu mzazi huwezi kukosea. Yan anatoka kwenye ubinadamu anaenda kwenye umalaika au? Hakosei tena. na endapo akikosea je?
sio ukiwa mzazi huwezi kosea soma tena andiko liko wazi kabisa mbona
 
Laana ni wazazi kupigana na mnajua mnawatoto. Mnapopishana mwanamke jishushe mwanaume usitumie jazba kuongea na mkeo.

Kwa kifupi msikilizane. Haiwezekani mtu uliyemchagua kwa mapenzi ya dhati leo awe adui yako hadi ushindwe kushusha hasira zako na kuleta Amani moyoni.
 
Mouu natambua unachomaanisha, lakini nikupe tu ukweli kwamba kwenye ugomvi wa wazee huwezi kua neutral hata siku moja

Nikupe tu mtano mwepesi, kuna gomvi zinazohusisha kupigana maknde kuchomana visu kuharibiana mali n.k,

Katika vurugu za dizaini hizi ni lazima utakua na upande na ni wazi kwamba utasimama upande wa HAKI bila kujali ni mzazi yupi unamtetea

Kwa kufanya hivyo tu utakua umeingia moja kwa moja kwenye mgogoro ea wazi ama wa siri baina yako na mzazi ambaye hukusimama naye

Itoshe tu kusema kama umeamua kusimama upande wa HAKI basi hakuna laana yoyote inayoweza kuiparamia haki na kufanikiwa NEVER

La mwisho hapa kwenye hili ni kwamba hata kama upande wa HAKI ulioamua kusimama utamgusa mzazi mmoja pekee,

Jaribu kumaintain heshima yako vilevile kwa wote, upendo vilevile n.k na hata ikitokea mmoja unampa salamu hapokei... Wewe endelea tu kumsalimia hivyo hivyo na kumjali hata ipite miaka 50
Ugumu ni kujua kama kweli wewe mtoto umesimama kwenye Haki???
Mara nyingi ugomvi wa wazazi hauanzi mbele ya watoto. Huanza na wao wawili kimya kimya chumbani kwao na baadae unatoka nje. Ndipo unapoona wameshikiana silaha au vitu vywnye ncha kali.
Lakini kuna tatizo moja hapo kwa wazazi wetu, na bahati nzuri humu JF kuna wazazi wengi na mimi pia ni mzazi, tunafahamu kwamba akina mama au wake zetu ndio hua wanakua wakwanza kwenda kujisafisha/kushtaki kwa watoto. Kwamba baba yenu amefanya moja mbili tatu. Watoto wanakaa nayo moyoni tu kwamba baba mkorofi.
Siku ugomvi huo ukawa mkubwa na kutoka nje, watoto kwa vyovyote wanaegemea kwa mama kwa sababu tayari wanataarifa mapema ya baba yao.
Ikumbukwe sisi wanaume/akina baba tunahifadhi vitu moyoni, hatukimbilii kwa watoto kama akina mama wanavyofanya, ndio maana kwenye migogoro hii ya ndoa, mkorofi mara nyingi inaonekana ni Mwanaume.
Ni vyema kama mleta maada alivyoshauri, kutoegemea upande wowote. Amulia ugomvi, baadae wakalishe
 
Ushawahi kuona mzazi ambae haelewek.. unagraduate anachukia.. unaenda kutafuta maisha anachukia.. narud na picha ya graduation nyumban wanaweka chini ya kabati.. wewe ni mtoto wake likija kwny swala la kuwakomoa ndugu zake tu.. ataanza ee mwnanangu amesoma.. mwanangu hv.. jana tu baada ya kunikazia nmehangaika mwnyw nimepata kibarua kwa muhindi.. anakuja ba idea eti ooh nenda jkt sasa.. kuna rafk zangu watakuunganisha ukimaliza course.. kweli kijana wa miaka 27 inaenda 28 unamwambie jkt leo.. alikua kwako toka akiwa na miaka 25 amemaliza degree hakuna alichosaidia zaidi ya kuniuliza najitolea kwny mashirika kwa faida gani.. Sasa huyo nae ni Baba au laana kamili.. mama yangu kafariki nna miaka miwili lakn tokea naanza kupata akili naskia negativity za mama kutoka kwa Baba.. nahajawah kwenda hata kuangalia kaburi.. watu wanapga wazazi wao kwa sababu.. na kuna wazazi wana nuksi sana.. tena sanaa
 
Ushawahi kuona mzazi ambae haelewek.. unagraduate anachukia.. unaenda kutafuta maisha anachukia.. narud na picha ya graduation nyumban wanaweka chini ya kabati.. wewe ni mtoto wake likija kwny swala la kuwakomoa ndugu zake tu.. ataanza ee mwnanangu amesoma.. mwanangu hv.. jana tu baada ya kunikazia nmehangaika mwnyw nimepata kibarua kwa muhindi.. anakuja ba idea eti ooh nenda jkt sasa.. kuna rafk zangu watakuunganisha ukimaliza course.. kweli kijana wa miaka 27 inaenda 28 unamwambie jkt leo.. alikua kwako toka akiwa na miaka 25 amemaliza degree hakuna alichosaidia zaidi ya kuniuliza najitolea kwny mashirika kwa faida gani.. Sasa huyo nae ni Baba au laana kamili.. mama yangu kafariki nna miaka miwili lakn tokea naanza kupata akili naskia negativity za mama kutoka kwa Baba.. nahajawah kwenda hata kuangalia kaburi.. watu wanapga wazazi wao kwa sababu.. na kuna wazazi wana nuksi sana.. tena sanaa
Pole snaa

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom