Laiti Rais samia angeijua historia ya soko la Kariakoo katika kupigania uhuru wa Tanganyika

Laiti Rais samia angeijua historia ya soko la Kariakoo katika kupigania uhuru wa Tanganyika

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Mama Samia leo asubuhi aliamkia Soko la Karikaoo kuangalia biashara inavyokwenda na kuzumgumza na viongozi wa soko.

Allah ana rehma zake na hutukumbusha mengi kwa njia ambazo mtu huwezi kutegemea.

Hapo aliposimama kwenye gari Rais Mama yetu Samia Soko la Kariakoo alikoelekeza sura yake ni Mtaa wa Swahili na kona ya Tandamti na ameupa mgongo Mtaa wa Swahhili na Mkunguni.

Hapo mbele yake ndipo ilipokuwa Ofisi ya Market Master Abdulwahid Sykes miaka ya 1950 Tanganyika inaanza harakati za kupigania uhuru wake kutoka kwa Waingereza.

Soko la Kariakoo na ofisi hiyo palikuwa moja ya ngome za harakati dhidi ya ukoloni.
Bahati mbaya historia hii haifahamiki ila kwa wachache sana.

Sehemu nyingine ambako vijana wanaharakati walikuwa wakipita kwa hili au lile katika siasa za ukombozi ilikuwa Ilala Welfare Centre ofisi ya Hamza Mwapachu.

Vilevile wanaharati walikuwa wakikutana nyumbani kwa Dossa Aziz Mtaa wa Congo na Mbaruku na nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu na nyakati za jioni wakikutana Tanga Club Mtaa wa New Street na Mkunguni.

Ilikuwa hapo sokoni Kariakoo ndipo Julius Nyerere akija kumuona Abdul Sykes ofisini kwake kuanzia mwaka wa 1952 na ndipo alipojuana na wazee mashuhuri wa mji maarufu kupita wote ni Mshume Kiyate.

Mzee Mshume akaunga uhusiano na Nyerere uliopitiliza siasa za TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika akamfanya Nyerere mfano wa mwanae.

Kueleza mchango wa Mzee Mshume katika TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika kutarefusha hii makala.

Hapo sokoni ndipo Mwalimu Nyerere alipofahamiana na Shariff Abdallah Attas kwa karibu sana kiasi safari ya kwanza ya Nyerere UNO mwaka wa 1955 mkewe Shariff Attas, Bi. Chiku bint Said Kisusa alikuwa mmoja wa akina mama waliomsindikiza uwanja wa ndege pamoja na Bi. Titi Mohamed na Bi. Tatu bint Mzee.

Hawa ndiyo walikuwa wanawake pamoja na Bi. Hawa Maftah na Bi. Halima bint Salum kwa kuwataja wachache waliojenga msingi wa akina mama kuipa TANU nguvu za kutisha katika mikutano yake Viwanja Vya Mnazi Mmoja na katika sanduku la kura.

Hii ndiyo iliyokuwa Kariakoo ambayo ile ofisi ya Abdul Sykes pale Kariakoo ilimpa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Baba wa Taifa Tanganyika.

Itapendeza sana kama CCM itaweka ukumbusho pale sokoni kama kumbukumbu ya wazalendo hawa wake kwa waume.

Vinginevyo tutabaki kuwa taifa lisilo na historia inayoeleweka ya ukombozi wake.

Picha ya Soko la Kariakoo kama lilivyokuwa katika miaka ya 1950 Ofisi ya Market Master ni hilo jengo dogo mkono wa kulia.

Picha ya chini kabisa Mshume Kiyate na Julius Nyerere, 1964.

1622550412784.png


1622550543504.png


1622550814675.png
 
Mzee Mohamed kichwa cha uzi huu kinaashiria kuwa mama Samia hajui historia ya kupigania uhuru wa tanganyika na uhusika wa soko la Kariakoo na unafikiri angejua kuna kitu angefanya, kwa nikujuavyo kiasi kidooogo sana wewe ukiamua unaweza mfikishia Mama historia hiyo "indirectly" kupitia "connection" zako, basi fanya hivyo tuonane "reaction" ya mama baada ya kujua historia hiyo!
 
Kumbe ndio maana kuna Rais alikuwa anapenda kuongea na wazee - maana mmetoka mbali.
 
Uzalendo...
Naamini angekuwa anajua kuwa pale alipokuwapo miaka 70 iliyopita ndipo Baba wa Taifa alipokutana kwa karibu sana na wananchi wa mwanzo waliomuunga mkono asingepita hivi hivi.

Kwake ingekuwa nafasi ya kuwaadhimisha wazalendo wale kwa angalau kuwataja na kuwakumbusha wafanya biashara wa Kariakoo kuwa wamepokea kijiti kutoka kwa wenzao waliowatangulia miongo saba iliyopita.
 
Kipaji, Elimu & hekima za Mwalimu Nyerere zilisaidia nchi yetu kupata uhuru kwa amani na kwa wakati

Sifa hizo zilisaidia pia kujenga taifa lenye nguvu, umoja na mshikamano mkubwa

Nina hakika Hayati Julius Nyerere alikuwa ni mpango wa Yehova
Uzalendo...
Umoja ulidumu kwa kipindi kile cha kudai uhuru.

Baada ya uhuru misuguano ndani ya TANU ikaanza.

Mwaka wa 1963 ndani Kamati Kuu ya TANU ulizuka mzozo baina ya Rajab Diwani, Selemani Kitundu, Julius Nyerere na Bi. Titi Mohamed.

Bi. Titi na Nyerere kauli zikapishana.

Mwaka huo huo Bukoba katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wagombea wa TANU Waislam walipingwa kwa sababu kuwa hawana elimu na Kanisa likaweka wagombea wake wenye elimu.

Mjini Tabora Regional Commissioner Richard Wambura akapambana na Bilal Rehani Waikela kwenye mkutano wa hadhara.

Mwaka huo huo 1963 Baraza la Wazee wa TANU likavunjwa kwa kuchanganya dini na siasa.

Kufikia mwaka wa 1964 hali ilikuwa si shwari.

Uhuru ukawa umekuja na changamoto kubwa.

Bi. Titi Mohamed na Tewa Said Tewa wakawekewa mkakati wasishinde ubunge uchaguzi wa mwaka 1965 na kweli wakashindwa.

Yako mengi.

Kilele mwaka wa 1993 kwa mara ya kwanza Waislam wakapambana na askari waliokuja kutawanya maandamano ya kukamatwa masheikh kuhusu mabucha y nguruwe.

Yaliyofuatia baada ya hapo sote tunayajua.
 
Historia hii haijafutwa kimakosa, haisemwi na haijaandikwa kwa sababu ya mapinduzi yaliyofanywa kipindi hiko, wapigania uhuru wengi walikuwa waislam ila baada ya uhuru waliofaidika wengi walikuwa upande wa pili.

Historia ya nchi hii, itabaki na mambo ya stone age tu hata machifu wengi historia yao ikoo juu juu kimkakati
 
Mama Samia leo asubuhi aliamkia Soko la Karikaoo kuangalia biashara inavyokwenda na kuzumgumza na viongozi wa soko.

Allah ana rehma zake na hutukumbusha mengi kwa njia ambazo mtu huwezi kutegemea.

Hapo aliposimama kwenye gari Rais Mama yetu Samia Soko la Kariakoo alikoelekeza sura yake ni Mtaa wa Swahili na kona ya Tandamti na ameupa mgongo Mtaa wa Swahhili na Mkunguni.

Hapo mbele yake ndipo ilipokuwa Ofisi ya Market Master Abdulwahid Sykes miaka ya 1950 Tanganyika inaanza harakati za kupigania uhuru wake kutoka kwa Waingereza.

Soko la Kariakoo na ofisi hiyo palikuwa moja ya ngome za harakati dhidi ya ukoloni.
Bahati mbaya historia hii haifahamiki ila kwa wachache sana.

Sehemu nyingine ambako vijana wanaharakati walikuwa wakipita kwa hili au lile katika siasa za ukombozi ilikuwa Ilala Welfare Centre ofisi ya Hamza Mwapachu.

Vilevile wanaharati walikuwa wakikutana nyumbani kwa Dossa Aziz Mtaa wa Congo na Mbaruku na nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu na nyakati za jioni wakikutana Tanga Club Mtaa wa New Street na Mkunguni.

Ilikuwa hapo sokoni Kariakoo ndipo Julius Nyerere akija kumuona Abdul Sykes ofisini kwake kuanzia mwaka wa 1952 na ndipo alipojuana na wazee mashuhuri wa mji maarufu kupita wote ni Mshume Kiyate.

Mzee Mshume akaunga uhusiano na Nyerere uliopitiliza siasa za TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika akamfanya Nyerere mfano wa mwanae.

Kueleza mchango wa Mzee Mshume katika TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika kutarefusha hii makala.

Hapo sokoni ndipo Mwalimu Nyerere alipofahamiana na Shariff Abdallah Attas kwa karibu sana kiasi safari ya kwanza ya Nyerere UNO mwaka wa 1955 mkewe Shariff Attas, Bi. Chiku bint Said Kisusa alikuwa mmoja wa akina mama waliomsindikiza uwanja wa ndege pamoja na Bi. Titi Mohamed na Bi. Tatu bint Mzee.

Hawa ndiyo walikuwa wanawake pamoja na Bi. Hawa Maftah na Bi. Halima bint Salum kwa kuwataja wachache waliojenga msingi wa akina mama kuipa TANU nguvu za kutisha katika mikutano yake Viwanja Vya Mnazi Mmoja na katika sanduku la kura.

Hii ndiyo iliyokuwa Kariakoo ambayo ile ofisi ya Abdul Sykes pale Kariakoo ilimpa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Baba wa Taifa.

Itapendeza sana kama CCM itaweka ukumbusho pale sokoni kama kumbukumbu ya wazalendo hawa wake kwa waume.

Vinginevyo tutabaki kuwa taifa lisilo na historia inayoeleweka ya ukombozi wake.

Picha ya Soko la Kariakoo kama lilivyokuwa katika miaka ya 1950 Ofisi ya Market Master ni hilo jengo dogo mkono wa kulia.

Picha ya chini kabisa Mshume Kiyate na Julius Nyerere, 1964.

View attachment 1804842

View attachment 1804844

View attachment 1804850
Bwana Mohamed kila mada unadandia kupenyeza sumu yako. Du! Sasa mambo ya kupigania uhuru na ziara ya rais wapi na wapi kaka yangu? Bado hujachoka kuwa stori ya hao wazee unaowahusudu waonekane ndio walifaa kuongoza nchi hujachoka kaka yangu? Hata wakitambulika wakiwa marehemu itawasaidia au kukusaidia nini? Pamoja na uzee huu bado unawaza kinyume mwanangu?
 
To be fair mama Samia anataka kuboreshwa kwa soko na liwe na mandhari nzuri na siyo ule ushalabaghala kama ule, utafikiri mazizi ya wanyama?!
#nakaziiendelee
 
History nzuri japo imeingia walakini kwa kuingiza udini. Ukiingiza udini sisi ambao hatufahamu tunahisi kuna mahala unapindisha ili uweze kutetea dini yako. Hivyo story inakosa kuaminika kutokana na malengo ya mtoa mada.
Niliichukua vizuri lakini nimeifuta kwa kiasi kikubwa kwani nahisi kuna uongo umedumbukizwa.
Nimechukua Jiografia basi,, imenitosha.
 
Mama Samia leo asubuhi aliamkia Soko la Karikaoo kuangalia biashara inavyokwenda na kuzumgumza na viongozi wa soko.

Allah ana rehma zake na hutukumbusha mengi kwa njia ambazo mtu huwezi kutegemea.

Hapo aliposimama kwenye gari Rais Mama yetu Samia Soko la Kariakoo alikoelekeza sura yake ni Mtaa wa Swahili na kona ya Tandamti na ameupa mgongo Mtaa wa Swahhili na Mkunguni.

Hapo mbele yake ndipo ilipokuwa Ofisi ya Market Master Abdulwahid Sykes miaka ya 1950 Tanganyika inaanza harakati za kupigania uhuru wake kutoka kwa Waingereza.

Soko la Kariakoo na ofisi hiyo palikuwa moja ya ngome za harakati dhidi ya ukoloni.
Bahati mbaya historia hii haifahamiki ila kwa wachache sana.

Sehemu nyingine ambako vijana wanaharakati walikuwa wakipita kwa hili au lile katika siasa za ukombozi ilikuwa Ilala Welfare Centre ofisi ya Hamza Mwapachu.

Vilevile wanaharati walikuwa wakikutana nyumbani kwa Dossa Aziz Mtaa wa Congo na Mbaruku na nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu na nyakati za jioni wakikutana Tanga Club Mtaa wa New Street na Mkunguni.

Ilikuwa hapo sokoni Kariakoo ndipo Julius Nyerere akija kumuona Abdul Sykes ofisini kwake kuanzia mwaka wa 1952 na ndipo alipojuana na wazee mashuhuri wa mji maarufu kupita wote ni Mshume Kiyate.

Mzee Mshume akaunga uhusiano na Nyerere uliopitiliza siasa za TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika akamfanya Nyerere mfano wa mwanae.

Kueleza mchango wa Mzee Mshume katika TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika kutarefusha hii makala.

Hapo sokoni ndipo Mwalimu Nyerere alipofahamiana na Shariff Abdallah Attas kwa karibu sana kiasi safari ya kwanza ya Nyerere UNO mwaka wa 1955 mkewe Shariff Attas, Bi. Chiku bint Said Kisusa alikuwa mmoja wa akina mama waliomsindikiza uwanja wa ndege pamoja na Bi. Titi Mohamed na Bi. Tatu bint Mzee.

Hawa ndiyo walikuwa wanawake pamoja na Bi. Hawa Maftah na Bi. Halima bint Salum kwa kuwataja wachache waliojenga msingi wa akina mama kuipa TANU nguvu za kutisha katika mikutano yake Viwanja Vya Mnazi Mmoja na katika sanduku la kura.

Hii ndiyo iliyokuwa Kariakoo ambayo ile ofisi ya Abdul Sykes pale Kariakoo ilimpa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Baba wa Taifa.

Itapendeza sana kama CCM itaweka ukumbusho pale sokoni kama kumbukumbu ya wazalendo hawa wake kwa waume.

Vinginevyo tutabaki kuwa taifa lisilo na historia inayoeleweka ya ukombozi wake.

Picha ya Soko la Kariakoo kama lilivyokuwa katika miaka ya 1950 Ofisi ya Market Master ni hilo jengo dogo mkono wa kulia.

Picha ya chini kabisa Mshume Kiyate na Julius Nyerere, 1964.

View attachment 1804842

View attachment 1804844

View attachment 1804850
Ushauri wangu kwako, andika kitabu kipe jina mchango wa soko la kariakoo kupigania uhuru wetu. Itatusaidia tusiolijua hilo.
 
nk.Ushauri wangu kwako, andika kitabu kipe jina mchango wa soko la kariakoo kupigania uhuru wetu. Itatusaidia tusiolijua hilo.
Lihakanga,
Historia ya Kariakoo nimeieleza katika kitabu cha Abdul Sykes kuanzia mpangilio wa biashara ndani ya soko; wapi paliuzwa tumbuku, wapi matunda, wapi samaki nk.

Nimeeleza hata makabila na biashara walizokuwa wanafanya.
Wanyamwezi waliuza viazi vitamu, Waluguru machungwa, Wamashomvi samaki nk.

Nikaeleza wafanyakazi wake, Shariff Attas alikuwa ''collector,'' wa ushuru wa nafaka, Mshume Kiyate dalali wa samaki wabichi, ng'onda na papa nk, kutoka mbali hadi Mafia.

Abdul Sykes akiuza kadi za TANU Kariakoo hadi siku akavamiwa na Town Clerk Mzungu ofisini na ukazuka ugomvi mkubwa baina yao.

Kwa kuhofu Abdul Sykes atafukuzwa kazi wazee wa sokoni wakamsomea dua na wakachinja mnyama.

Dua ambayo Nyerere alisomewa nyumbani kwa Jumbe Tambaza na Rashid Ali Meli pia akasomewa na hawa wote kwa ajili ya kuwakinga na shari za Waingereza.

Nakushukuru hata hivyo kwa ushauri wako.
 
Back
Top Bottom