Laiti Rais samia angeijua historia ya soko la Kariakoo katika kupigania uhuru wa Tanganyika

Laiti Rais samia angeijua historia ya soko la Kariakoo katika kupigania uhuru wa Tanganyika

Pale kariakoo kuna wazee wajanja wajanja Sana.
Kuna siku nilikwenda mtaa wa kariakoo na Livingston.
Nikakutana na wazee wamekaa kwenye benchi.
Wakaniuliza vipi kijana unataka gari, gemstones au madini.
ndo nikajua kuwa Wale wazee NI madalali.
 
History nzuri japo imeingia walakini kwa kuingiza udini. Ukiingiza udini sisi ambao hatufahamu tunahisi kuna mahala unapindisha ili uweze kutetea dini yako. Hivyo story inakosa kuaminika kutokana na malengo ya mtoa mada.
Niliichukua vizuri lakini nimeifuta kwa kiasi kikubwa kwani nahisi kuna uongo umedumbukizwa.
Nimechukua Jiografia basi,, imenitosha.
Mafiningo,
Udini ikiwa unakusudia Uislam ni shida sana kuuepuka katika historia ya TANU uhuru wa Tanganyika.

Kwa nini?

Wazee wetu waliunda African Association (AA) 1929 ili kujitoa katika mikono ya Father Gibbons wa Minaki Mission ambaye yeye ndiye alikuwa mwakilishi wa Waafrika.

Ndipo wakaunda AA na majority wa hawa waasisi walikuwa Waislam akina Kleist Sykes, Mzee bin Sudi, Ibrahim Hamisi kwa kuwataja wachache.

Kisha hawa wazee wetu wakaunda Al Jamiatul Islamiyya Fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) mwaka wa 1933 pembeni ya AA ili wasipitishe mambo ya Uislam AA lakini viongozi wakiwa ni wale wale waliokuwa wanaongoza AA.

Hawa waasisi wa AA ndiyo waliokuja kuunda TANU na ndiyo wanachama wa mwanzo na viongozi wa mwanzo pia wakiwa watu waliokuwa karibu sana na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Hauko peke yako unaetaabishwa na historia hii.

Wengi wangependa kama historia hii ikabadilishwa na tuondoe mchango wa Waislam katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Haiwezekani kuifuta historia.

Huwezi kusomesha historia ya uhuru wa Kenya bila kuwataja Wakikuyu na Mau Mau ukisema kufanya hivyo ni ukabila.

Chuo Cha CCM Kivukoni walijaribu na wakachapa kitabu amacho haya yote unayosoma kutoka kwangu hayapo.

Balaa lake ndilo hili leo wewe unasoma historia ya kweli unateseka.

1622608376932.png


1622608471852.png


Vipi mimi leo nisijifaharishe na historia ya wazee wangu hawa anbao wengine niliwaona kwa jicho langu udogoni?
 
Bwana Mohamed kila mada unadandia kupenyeza sumu yako. Du! Sasa mambo ya kupigania uhuru na ziara ya rais wapi na wapi kaka yangu? Bado hujachoka kuwa stori ya hao wazee unaowahusudu waonekane ndio walifaa kuongoza nchi hujachoka kaka yangu? Hata wakitambulika wakiwa marehemu itawasaidia au kukusaidia nini? Pamoja na uzee huu bado unawaza kinyume mwanangu?
Father...
Sikudandia.

Pale aliposimama Mama Samia kwangu kunanikumbusha mengi katika historia ya Kariakoo.
Kwanza na hili sikueleza.

Hapo nyuma ya Ofisi ya Market Master, babu yangu Shariff Muhammad alikuwa na matundu ya njiwa hiyo ndiyo ilikuwa biashara yake.

Hivi ninavyoandika ni kama vile namuona kasimama mbele ya matundu yake na chini pametapakaa mtama aliokuwa akiwalisha njiwa wake.

Mimi sijapatapo kusema kuwa wazee wangu ndiyo walostahili kuongoza Tanganyika.

Labda nikueleza kidogo historia ya hawa wazee.

Mkutano wa kumwingiza Nyerere katika uongozi wa TAA ulifanyika Nansio, Ukerewe nyumbani kwa Hamza Mwapachu na Abdul Sykes alisafiri na Ali Mwinyi Tambwe, Secretary wa Al Jamiatul Islamiyya kwenda Nansio kupata kauli ya Mwapachu kuhusu Nyerere.

Ushauri wa Mwapachu ulikuwa Abdul ampishe Nyerere na amsaidie kushinda uchaguzi wa TAA 1953 na mwaka unaofuata, 1954 TANU iundwe.

Na Hamza Mwapachu alitoa sababu zake.

Kisa kirefu.

Mimi nayajua haya yote.

Sasa ikiwa huu ndiyo ukweli wa historia ya uhuru vipi mimi nitatamani kuwa historia iwe vinginevyo?

Mimi nimefaidika sana kwa kuandika historia ya kweli ya TANU na uhuru wa Tanganyika na kubwa ni kuondoa dukuduku lililosonga moyo wangu kwa kuona kuwa wazee wangu waliofutwa katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika nimeweza kuwaandikia kitabu kizima na kikapata umaarufu katika vyuo vikuu duniani vinavyosomesha African History.

Sijachoka na wanafunzi wangu hawajachoka kama wewe ulivyokuwa hujachoka unashindwa kustahamili unaniandikia na mimi kama nifanyavyo kwa wenzako sijachoka kuisomesha historia hii.

Kama nafsi yako inaumizwa na ukweli wa historia hii ni bahati mbaya sana kwako.

Sikudandia.

Mama Samia kanikumbusha mengi kwa kusimama pale aliposimama katika soko la Kariakoo.

Pale mbele yakeilikuwa Ofisi ya Market Master, Brian Hodges Mwingereza na alipoacha kazi ndiyo akaingia Abdulwahid Sykes na akabadili historia nzima ya soko lile kuwa moja ya ngome dhidi ya ukoloni.

Father...
Nahitimisha.

Sikujua kuwa kuwafuta Waislam katika historia ya uhuru wa Tanganyika ni kuondoa sumu.

Umenisaidia pakubwa.
 
Mafingo,
Udini ikiwa unakusudia Uislam ni shida sana kuuepuka katika historia ya TANU uhuru wa Tanganyika.

Kwa nini?

Wazee wetu waliunda African Association (AA) 1929 ili kujitoa katika mikono ya Father Gibbons wa Minaki Mission ambaye yeye ndiye alikuwa mwakilishi wa Waafrika.

Ndipo wakaunda AA na majority wa hawa waasisi walikuwa Waislam akina Kleist Sykes, Mzee bin Sudi, Ibrahim Hamisi kwa kuwataja wachache.

Kisha hawa wazee wetu wakaunda Al Jamiatul Islamiyya Fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) mwaka wa 1933 pembeni ya AA ili wasipitishe mambo ya Uislam AA lakini viongozi wakiwa ni wale wale waliokuwa wanaongoza AA.

Hawa waasisi wa AA ndiyo waliokuja kuunda TANU na ndiyo wanachama wa mwanzo na viongozi wa mwanzo pia wakiwa watu waliokuwa karibu sana na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Hauko peke yako unaetaabishwa na historia hii.

Wengi wangependa kama historia hii ikabadilishwa na tuondoe mchango wa Waislam katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Haiwezekani kuifuta historia.

Huwezi kusomesha historia ya uhuru wa Kenya bila kuwataja Wakikuyu na Mau Mau ukisema kufanya hivyo ni ukabila.

Chuo Cha CCM Kivukoni walijaribu na wakachapa kitabu amacho haya yote unayosoma kutoka kwangu hayapo.

Balaa laki ndilo hili leo wewe unasoma historia ya kweli unateseka,
Mkuu ni kina Nani ambao hawataki kuwataja waislam kama walichangia kupatikana Kwa Uhuru mbona kina Bibi Titi wanajulikana vizuri Tu? Lakini pia je ni faida gani inapatikana kama wakitajwa na hasara ipi inapatikana wasipotajwa waislam?

Na mwisho kabisa je ulitegemea uone wakristo wengi kwenye huo mchakato kama ulikuwa unafanyika pwani ya Dar es salaam tena kariakoo? Wote tunajua pwani zote zina wingi wa waumini wa Imani ya kiislam hivo kama mchakato huo ungefanyika kaskazini ni wazi ingekuwa ngumu kuona Muslims
 
Naona unamlilia sana sykes

Ova
Mrangi,
Mimi niliogopa nilipokabidhiwa Nyaraza za Sykes.
Nilikuwa nasoma hadi usiku wa manane na hii ni katika 1980s.

Najiuliza.
Hii ni kweli au naangalia Blockbuster ya Hollywood?

Sasa nikawa nachanganya na yale niliyokuwa nayaona udogoni nikajiambia mimi nina bahati kubwa kuzaliwa nyakati zile na watu wale.

Siku moja Ahmed Rashad Ali huyu alikuwa rafiki yake mkubwa Abdul Sykea ananieleza kuwa 1950 alimsindikia Abdul Sykes kuonana na Jomo Kenyatta kwenye mkutano wa siri Nairobi.

Ilikuwa wakati wa Kombe la Gossage na yeye alikuwa Captain wa timu ya Zanzibar na mashindano yalikuwa Nairobi.

Nimekaa mwili umekufa ganzi.
Abdul Sykes anakwenda kuonana na Kenyatta na kasindikizwa na Ahmed Rashad.

Abdul ana miaka 24.

Hii kweli au Mzee Rashad sasa anatunga stori?
Ahmed Rashad akiwa mwanafunzi India 1945 WWII imemalizika.

Abdul Sykes yuko Kalieni Camp nje kidogo ya Bombay, sasa Mumbai.
Askari wa Burma Infantry wanangoje ''repatriation,'' kurudishwa makwao.

Amekwenda kumtembelea rafiki yake Abdul Kambini.
Hapo Kalieni ndipo Abdul na wenzake walipoamua kuunda TANU.

Nilikuwa nimeingia katika dunia ambayo sikujua kama ipo.
Nikasema lazima nikamilishe hiki kitabu hii historia ije kusomwa.

Waliokataa kuiweka historia hii katika kitabu cha Histria ya TANU kilichoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni walijua wanachokifanya.

Huyu ndiye mimi na baba yangu Abdulwahid Sykes:

Sijui kama umepatapo kusoma habari hizi hapo chini:
Mohamed Said: TANGANYIKA POLITICAL INTELLIGENCE SUMMARY, MARCH 1952

"Tanganyika Political Intelligence
Summary, March 1952":

"...it is reported that the Secretary of the Association, Abdul Wahid Sykes has
dispatched letters to all branches asking members for suggestions under
the following heads for a memorandum to be prepared for the Royal
Commission..."

“...Abdul Wahid Kleist Sykes, Secretary of the African Association who, as
reported in last month's summary (paragraph 20) was going on safari up
country, visited Mwanza, where he met Paul Bomani, President of the
Bukoba African Association, and accompanied him to Bukoba. Sykes then
visited Kampala alone.....on 8th March, a secret meeting was held, attended
by leading members of the Mwanza Branch...”

(Hizi ni taarifa kutoka Rhodes House Library, Oxford kutoka majalada ya
kikachero ya Waingereza baada ya miaka 50 yanawekwa wazi kwa mtafiti
yeyote kuyasoma na kufanya nakala akipenda).

1622613485739.png


Mrangi,
Jiweke wewe kwenye nafasi yangu unasoma historia hii halafu unaambiwa kuwa TAA kilikuwa chama cha starehe na aliyeunda TANU ni Julius Nyerere.

Unafanyaje?
 
Mama Samia leo asubuhi aliamkia Soko la Karikaoo kuangalia biashara inavyokwenda na kuzumgumza na viongozi wa soko.

Allah ana rehma zake na hutukumbusha mengi kwa njia ambazo mtu huwezi kutegemea.

Hapo aliposimama kwenye gari Rais Mama yetu Samia Soko la Kariakoo alikoelekeza sura yake ni Mtaa wa Swahili na kona ya Tandamti na ameupa mgongo Mtaa wa Swahhili na Mkunguni.

Hapo mbele yake ndipo ilipokuwa Ofisi ya Market Master Abdulwahid Sykes miaka ya 1950 Tanganyika inaanza harakati za kupigania uhuru wake kutoka kwa Waingereza.

Soko la Kariakoo na ofisi hiyo palikuwa moja ya ngome za harakati dhidi ya ukoloni.
Bahati mbaya historia hii haifahamiki ila kwa wachache sana.

Sehemu nyingine ambako vijana wanaharakati walikuwa wakipita kwa hili au lile katika siasa za ukombozi ilikuwa Ilala Welfare Centre ofisi ya Hamza Mwapachu.

Vilevile wanaharati walikuwa wakikutana nyumbani kwa Dossa Aziz Mtaa wa Congo na Mbaruku na nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu na nyakati za jioni wakikutana Tanga Club Mtaa wa New Street na Mkunguni.

Ilikuwa hapo sokoni Kariakoo ndipo Julius Nyerere akija kumuona Abdul Sykes ofisini kwake kuanzia mwaka wa 1952 na ndipo alipojuana na wazee mashuhuri wa mji maarufu kupita wote ni Mshume Kiyate.

Mzee Mshume akaunga uhusiano na Nyerere uliopitiliza siasa za TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika akamfanya Nyerere mfano wa mwanae.

Kueleza mchango wa Mzee Mshume katika TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika kutarefusha hii makala.

Hapo sokoni ndipo Mwalimu Nyerere alipofahamiana na Shariff Abdallah Attas kwa karibu sana kiasi safari ya kwanza ya Nyerere UNO mwaka wa 1955 mkewe Shariff Attas, Bi. Chiku bint Said Kisusa alikuwa mmoja wa akina mama waliomsindikiza uwanja wa ndege pamoja na Bi. Titi Mohamed na Bi. Tatu bint Mzee.

Hawa ndiyo walikuwa wanawake pamoja na Bi. Hawa Maftah na Bi. Halima bint Salum kwa kuwataja wachache waliojenga msingi wa akina mama kuipa TANU nguvu za kutisha katika mikutano yake Viwanja Vya Mnazi Mmoja na katika sanduku la kura.

Hii ndiyo iliyokuwa Kariakoo ambayo ile ofisi ya Abdul Sykes pale Kariakoo ilimpa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Baba wa Taifa.

Itapendeza sana kama CCM itaweka ukumbusho pale sokoni kama kumbukumbu ya wazalendo hawa wake kwa waume.

Vinginevyo tutabaki kuwa taifa lisilo na historia inayoeleweka ya ukombozi wake.

Picha ya Soko la Kariakoo kama lilivyokuwa katika miaka ya 1950 Ofisi ya Market Master ni hilo jengo dogo mkono wa kulia.

Picha ya chini kabisa Mshume Kiyate na Julius Nyerere, 1964.

View attachment 1804842

View attachment 1804844

View attachment 1804850

Imekaa Njema Mkuu japo haujaeleza jinsi Mwalimu Nyerere alivyokutana na Mzee Mbowe au kwakuwa ni Mkristo hautaki kumuelezea kama mmoja waliomsupport Nyerere? Nadhani angekuwa Muislam ungeshamtaja.
Hata mimi nashangaa! Walikuwepo kama sikosei akina Mzee John Rupia.
 
Mrangi,
Mimi niliogopa nilipokabidhiwa Nyaraza za Sykes.
Nilikuwa nasoma hadi usiku wa manane na hii ni katika 1980s.

Najiuliza.
Hii ni kweli au naangalia Blockbuster ya Hollywood?

Sasa nikawa nachanganya na yale niliyokuwa nayaona udogoni nikajiambia mimi nina bahati kubwa kuzaliwa nyakati zile na watu wale.

Siku moja Ahmed Rashad Ali huyu alikuwa rafiki yake mkubwa Abdul Sykea ananieleza kuwa 1950 alimsindikia Abdul Sykes kuonana na Jomo Kenyatta kwenye mkutano wa siri Nairobi.

Ilikuwa wakati wa Kombe la Gossage na yeye alikuwa Captain wa timu ya Zanzibar na mashindano yalikuwa Nairobi.

Nimekaa mwili umekufa ganzi.
Abdul Sykes anakwenda kuonana na Kenyatta na kasindikizwa na Ahmed Rashad.

Abdul ana miaka 24.

Hii kweli au Mzee Rashad sasa anatunga stori?
Ahmed Rashad akiwa mwanafunzi India 1945 WWII imemalizika.

Abdul Sykes yuko Kalieni Camp nje kidogo ya Bombay, sasa Mumbai.
Askari wa Burma Infantry wanangoje ''repatriation,'' kurudishwa makwao.

Amekwenda kumtembelea rafiki yake Abdul Kambini.
Hapo Kalieni ndipo Abdul na wenzake walipoamua kuunda TANU.

Nilikuwa nimeingia katika dunia ambayo sikujua kama ipo.
Nikasema lazima nikamilishe hiki kitabu hii historia ije kusomwa.

Waliokataa kuiweka historia hii katika kitabu cha Histria ya TANU kilichoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni walijua wanachokifanya.

Huyu ndiye mimi na baba yangu Abdulwahid Sykes:

Sijui kama umepatapo kusoma habari hizi hapo chini:
Mohamed Said: TANGANYIKA POLITICAL INTELLIGENCE SUMMARY, MARCH 1952

"Tanganyika Political Intelligence
Summary, March 1952":

"...it is reported that the Secretary of the Association, Abdul Wahid Sykes has
dispatched letters to all branches asking members for suggestions under
the following heads for a memorandum to be prepared for the Royal
Commission..."

“...Abdul Wahid Kleist Sykes, Secretary of the African Association who, as
reported in last month's summary (paragraph 20) was going on safari up
country, visited Mwanza, where he met Paul Bomani, President of the
Bukoba African Association, and accompanied him to Bukoba. Sykes then
visited Kampala alone.....on 8th March, a secret meeting was held, attended
by leading members of the Mwanza Branch...”

(Hizi ni taarifa kutoka Rhodes House Library, Oxford kutoka majalada ya
kikachero ya Waingereza baada ya miaka 50 yanawekwa wazi kwa mtafiti
yeyote kuyasoma na kufanya nakala akipenda).

View attachment 1805622

Mrangi,
Jiweke wewe kwenye nafasi yangu unasoma historia hii halafu unaambiwa kuwa TAA kilikuwa chama cha starehe na aliyeunda TANU ni Julius Nyerere.

Unafanyaje?
Basi historia imepindishwa

Ova
 
Mkuu ni kina Nani ambao hawataki kuwataja waislam kama walichangia kupatikana Kwa Uhuru mbona kina Bibi Titi wanajulikana vizuri Tu? Lakini pia je ni faida gani inapatikana kama wakitajwa na hasara ipi inapatikana wasipotajwa waislam?

Na mwisho kabisa je ulitegemea uone wakristo wengi kwenye huo mchakato kama ulikuwa unafanyika pwani ya Dar es salaam tena kariakoo? Wote tunajua pwani zote zina wingi wa waumini wa Imani ya kiislam hivo kama mchakato huo ungefanyika kaskazini ni wazi ingekuwa ngumu kuona Muslims
Ani...
Bahati mbaya wewe ndiyo leo unasikia haya.

Jitahidi usome kitabu cha Abdul Sykes kipo huu mwaka wa 23.

Kadi yake ya TANU ni no. 3 ya mdogo wake Ally no. 2 ya kitinda mimba wao Abbas no. 7 na African Association aliasisi baba yao 1929.

Kadi ya Julius Nyerere no. 1 na aliandikiwa na Ally Sykes na yeye huyo ndiye aliyechapa kadi 1000 za kwanza za TANU kutoka mfukoni kwake.

Ilipoandikwa historia ya TANU hawa wote wakafutwa.
 
Samahi kidogo waungwana.

Sipo kimsimamo wa dini yeyote.

Naomba kufahamishwa. Ni kwa nini inaonekana watu wenye majina ya kiislam na wenyeji wa mikoa ya pwani walikuwa mstari wa mbele sana katika harakati za uhuru wa hii Nchi.!???

Ni kwa kuwa harakati zilianzia dsm.?
Ni kwa kuwa ulikuwepo pia utawala wa waarabu!?
Au zamani hakukuwa na uhusiano wa mavazi na dini au majina na dini?
Au ni mimi tu kutoijua vizuri historia ??


Naomba kufahamu kidogo???
 
Mzee Mohamed bado wewe ni hazina/maktaba ya historia tukuka ya nchi hii hasa kipindi kuelekea kupigania uhuru, unajua mengi hasa kutoka kwa wazee wako. Historia ya nchi hii (kote Zanzibar na Tanganyika) imepindishwa sana, sasa ni wajibu wenu mnaoijua vizuri historia hii kuwafahamishe wale wasioijua, ndio maana nasisitiza tafuta namna basi ya kufikishia mama historia ya mahali pale aliposimama, sio kutamani tu kuwa kama angejua...hajui sasa! msaidie ajue!
 
Mzee Mohamed bado wewe ni hazina/maktaba ya historia tukuka ya nchi hii hasa kipindi kuelekea kupigania uhuru, unajua mengi hasa kutoka kwa wazee wako. Historia ya nchi hii (kote Zanzibar na Tanganyika) imepindishwa sana, sasa ni wajibu wenu mnaoijua vizuri historia hii kuwafahamishe wale wasioijua, ndio maana nasisitiza tafuta namna basi ya kufikishia mama historia ya mahali pale aliposimama, sio kutamani tu kuwa kama angejua...hajui sasa! msaidie ajue!
Kilembwe,
Nimeandika historia hiyo na wewe ulikuwa huijui sasa umeijua.

Historia hii si ngeni ipo ndani ya kitabu cha Abdul Sykes toka 1998.

Wajibu wangu unakomea hapo.
 
Naweza kuwa nalijua!
Maana hata historia ya mwafrika nayo ilipindishwa,
Nkirudi kwenye mada yetu,najiuliza kwanini
Historia ya TAA,TANU ilipindishwa,kwanini ukweli hawakutaka kuuweka


Ova
Mrangi,
Kisa kizima cha uandishi wa historia ya TANU nimekiandika hapa JF.

Rudi kwenye post za nyuma utakuta.
 
Mkuu ni kina Nani ambao hawataki kuwataja waislam kama walichangia kupatikana Kwa Uhuru mbona kina Bibi Titi wanajulikana vizuri Tu? Lakini pia je ni faida gani inapatikana kama wakitajwa na hasara ipi inapatikana wasipotajwa waislam?

Na mwisho kabisa je ulitegemea uone wakristo wengi kwenye huo mchakato kama ulikuwa unafanyika pwani ya Dar es salaam tena kariakoo? Wote tunajua pwani zote zina wingi wa waumini wa Imani ya kiislam hivo kama mchakato huo ungefanyika kaskazini ni wazi ingekuwa ngumu kuona Muslims
TATIZO KATIKA UTAFITI NA UANDISHI WA HISTORIA YA TANU1962

May 26
UTANGULIZI

Msomaji wangu jina lake Madagascar baada ya kusoma moja ya makala zangu niliyoeleza kuwa mradi wa kwanza wa kuandika historia ya TANU ulikuwa mwaka wa 1962 watafiti na waandishi wakiwa Abdul Sykes na Dr. Wilbert Klerruu, nilieleza kuwa Abdul Sykes alijitoa na Dr. Klerruu akabakia kukamilisha kazi, aliniandikia kutaka kujua sababu ya Abdul Sykes kujitoa.

Madagascar,
Kleruu alikuwa hana moja alijualo katika historia ya AA.

Abdul Sykes kwanza alikuwa na mswada wa kitabu alioandika baba yake.

Mswada huu ulikuwa kumbukumbu za baba yake akieleza historia ya vipi babu yake Sykes Mbuwane alikuja Germany Ostafrika kama askari mamluki chini ya Hermann Von Wissman.

Ndani ya mswada huu anaeleza maisha yake chini ya utawala wa Wajerumani hadi WW I akiwa askari ndani ya jeshi la Kamanda Von Lettow Vorbeck.

Anaendelea kueleza utawala wa Waingereza baada ya WW I 1918.

Anaeleza alivyounda African Association 1929 baada ya kukutana na Dr. Kweggiyr Aggrey 1924.

Anaendelea kueleza kilichomsukuma kuunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika 1933 kikiwa chama pembeni ya AA.

Hapa katika miaka ya 1930s anaeleza juhudi za Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika katika kujenga shule ili Waislam kama Wamishionari wawe na shule zao akiweka msisitizo wa Qur'an kusomeshwa kama somo katika shule.

Kleist anaeleza ushawishi wa Waislam katika taasisi hizi mbili AA na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na nguvu iliyozuka katika kukabiliana na ukoloni.

Abdul haya licha ya kuwa yameandikwa na baba yake lakini kazaliwa na kukua ndani ya historia hii na baada ya WWII na akiwa askari wa KAR ndani ya Burma Infantry akawa anaandika vipi vita hivi vilivyowasaidia Waafrika kujitambua na kuamua kudai uhuru wa Tanganyika.

Yeye binafsi alikuwa na mchango wake katika kuwakabiliaba na Waingereza kwanza kupitia Dockworkers Union kisha haada ya kuchukua uongozi wa TAA 1950 akiwa na Dr. Vedasto Kyaruzi.

Kipindi hiki ndicho kipindi muhimu sana katika historia ya TAA kwani vijana wengi kutoka Makerere College walijiunga na TAA mjini Dar-es-Salaam pale New Street.

Hiki ndicho kipindi cha bongo za kizazi kipya cha wakati ule akina Hamza Mwapachu na viongozi wengine kutoka Kanda ya Ziwa kama Ali Migeyo, Saadan Abdu Kandoro na Paul Bomani wakaanza kukusanya nguvu zao pamoja kumkabili Gavana Edward Francis Twining.

Abdul na Hamza Mwapachu wanaweka msingi wa kuunda TANU na kutafuta kiongozi mmoja kuongoza harakati za uhuru.

Abdul yeye alimtaka Chief David Kidaha Makwaia ndiye aje TAA waunde TANU.

Mwapachu yeye mtu wake alikuwa Julius Nyerere lakini mwaka wa 1950 Nyerere alikuwa hajulikani wakati Chief Kidaha alikuwa mjumbe wa LEGCO toka mwaka wa 1945.

Abdul Sykes 1950 tayari alikuwa kijana maarufu na kiongozi wa TAA na alikuwa mjumbe katika TAA Political Subcommitee pamoja na Mwapachu, Kyaruzi, Sheikh Hassan bin Ameir na Steven Mhando kwa kawataja wachache.

Huu ndiyo mwaka Abdul Sykes alikwenda Nairobi kufanya mazungumzo na Jomo Kenyatta.

Hii kamati ndani yake alikuwapo Mwanasheria Earle Seaton akitoa ushauri nyuma ya pazia.

Hii ndiyo kamati akiwemo Dossa Aziz na John Rupia iliyokuja kuunda chama cha TANU 1954.

Lakini muhimu alieleza mkutano nyumbani kwa Hamza Mwapachu, Nansio, Ukerewe alipokwenda kaongozana na Ali Mwinyi Tambwe agenda kuu ikiwa kupata kauli ya Mwapachu kuhusu kumtia Nyerere kwenye uongozi wa juu kabisa wa TAA.

Hamza alimshauri Abdul kuwa Nyerere asaidiwe ashinde uchaguzi wa 1953 awe President na 1954 TANU iundwe.

Haya ndiyo Abdul aliyoandika katika kueleza chimbuko la TANU na Abdul akaeleza vipi alikuja kujuana na Nyerere 1952.

Inasemekana kuwa Julius Nyerere hakupendezewa na historia hii.

Abdul akajitoa katika ule mradi akamwacha Dr. Kleruu.

Naweka kitabu cha Abubakar Ulotu, ‘‘Historia ya TANU,’’ kitabu kilichotokana na utafiti na uandishi wa Dr. Wilbert Klerruu.

Hiki kitabu cha Abubakar Ulotu ni kutoka mswada wa historia ya TANU kilichokuwa kinaandikwa pale TANU Office na Abdul Sykes na Dr. Wilbard Kleruu mwaka wa 1962 Nyerere akihusika.

Kama nilivyoeleza hapo juu Abdul Sykes alijitoa katika uandishi wa historia ya TANU.

Dr. Kleruu akaendelea na uandishi hadi ukakamilika lakini TANU hawakuweza kukichapa kitabu kile.

Abubakar Ulotu akachukua mswada ule kwa siri na bila idhini ya TANU akachapa kitabu baada ya kufanya mabadiliko kidogo akaweka jina lake kama mwandishi.

Hivi sasa kipo kitabu cha maisha ya Julius Nyerere.

Muhimu kujua nini kimeandikwa kuhusu uasisi wa TANU na mchango wa Nyerere.

Waandishi wa kitabu hiki walifanya mahojiano na mwandishi kama picha zinavyoonyesha na walimtunuku nakala kwa mchango wake huo.

Screenshot_20210602-122449_Facebook.jpg
 
Kilembwe,
Nimeandika historia hiyo na wewe ulikuwa huijui sasa umeijua.

Historia hii si ngeni ipo ndani ya kitabu cha Abdul Sykes toka 1998.

Wajibu wangu unakomea hapo.
Mzee Mohamed nimekuelewa...kuwa ni wajibu wake kusoma historia hiyo kama ilivyo wajibu wetu sisi!
 
Back
Top Bottom