Laiti Rais samia angeijua historia ya soko la Kariakoo katika kupigania uhuru wa Tanganyika

Wapigania uhuru wote huwa hawatajwi na huwa hawana umaarufu Sawa,ni kitu Cha kawaida,
Kuna vijana hata hawamjuhi Steve Biko,kwa kule SA,anayejurikana sana ni Nelson Mandela,lakini wapo waanzilishi wa ANC kabla ya Mandela hajajiunga,na wengi mchango wao huwa hautajwi sana,popote palipokuwa na mapambano ya kudai uhuru,
Tatizo we jamaa,muelekeo wako ni kuwa "waislam"ndio waliopigania uhuru wakati "wakristo"wakila bata na mkoloni,
So biased
 
Mimi ninachojua uislam wakati unaletwa na mwarabu uliwakuta wazee wetu.

Sasa ni kwanini hao wazee wako unawatambua zaidi kama wazee wa kiislam badala ya wazee wa Mzizima ?
 
Sitaabishwi na historia bali ni namna unavyoingiza maneno yenye malengo kuwa waislam walionewa.
Naona ni kama kuna kitu ungependa waislam wakidai. Ndipo ninapopata shaka na story nzima na kuhisi umeipindisha.
 
Juan...
Hii Steve Biko hajulikani umeitoa wapi?

Naijua vyema historia ya Afrika Kusini nimeisoma kidato cha kwanza 1967 tena nimesomeshwa na mwalimu Muingereza Mrs. Grant St. Joseph's Convent School.

Kitabu kilichoniathiri sana katika historia hii ni "Cry the Beloved Country," cha Alan Paton.

Nimefika Afrika Kusini mara mbili na nimetembelea Apartheid Museum na nimefika Soweto na nyumba ya Mandela ambayo sasa ni kumbukumbu yake.

Nimekisoma kitabu cha Mandela, "Long Walk to Freedom."

Nimeitembelea pia selo yake Roben Island.

Steve Biko ni mmoja wa mashujaa wa Afrika Kusini na hakuna asiyemjua.

Steve Biko ametengenezewa senema ya maisha yake.

Historia za mashujaa wao wote zipo hapo Apartheid Museum mpaka magari ya deraya yaliyokuwa yanatumika dhidi ya wananchi.

Afrika Kusini wamehifadhi historia yao.

Kabla ya kuandika ni vizuri kufanya utafiti.

Sanamu ya Mandela na selo yake Roben Island.



 
Sitaabishwi na historia bali ni namna unavyoingiza maneno yenye malengo kuwa waislam walionewa.
Naona ni kama kuna kitu ungependa waislam wakidai. Ndipo ninapopata shaka na story nzima na kuhisi umeipindisha.
Mafiningo,
Ni historia ndefu na inataka ujuzi si kitu kinachowezwa kujadiliwa na yeyote yule.

Kukusaidia kuelewa inabidi wewe mwenyewe kuisoma historia ya Tanganyika hadi kufikia uhuru mwaka wa 1961 na baada ya hapo.

Ukiwa ushasoma na kuelewa historia yote utakuwa katika hali ya kujua.

Anza hapa: mohamedsaidsalum.blogspot.com

Fanya search kwa matukio na majina.
 
Mimi ninachojua uislam wakati unaletwa na mwarabu uliwakuta wazee wetu.

Sasa ni kwanini hao wazee wako unawatambua zaidi kama wazee wa kiislam badala ya wazee wa Mzizima ?
Mkaruka,
Soma kwanza mjadala uelewe.
Utakuwa katika hali nzuri ya kujadili.
 
ni wapi naweza kusomewa dua hiyo leo hii....? nasikitika sana moja ya vitu tulivyo poteza ni asili yetu na hadi kufika mwaka 2045 apatokuwa na asili yoyote itakayokuwa inaeexit
 
ni wapi naweza kusomewa dua hiyo leo hii....? nasikitika sana moja ya vitu tulivyo poteza ni asili yetu na hadi kufika mwaka 2045 apatokuwa na asili yoyote itakayokuwa inaeexit
Prince...
Wakati natafiti kitabu cha Abdul Sykes nilipofika kwenye TANU imeshaundwa hii ni 1955 moto wa kudai uhuru unazidi kuongeza joto lake.

Sheikh Hassan bin Ameir Mufti wa Tanganyika anauza kadi za TANU misikitini anakodarsisha.

Abdul Sykes anauza kadi za TANU sokoni Kariakoo.

Iko siku Town Clerk Mzungu akamvamia ofisini.

Ugomvi mkubwa ukatokea baina ya huyu Mwingereza na Abdul.

Ikawa wazi Abdul atafukuzwa kazi.

Mpashaji wangu alinieleza kwa yakini nini kilimfika yule Mzungu.

Mimi nilibakia kimya.

Abdul alibakia kazini na TANU ilizidi kupata nguvu.

Dua ya Rashid Ali Meli yeye alifungua sefu ya Dar-es-Salaam Municipal Council alikoajiriwa kama Bwana Fedha akatoa hela akampa Iddi Faiz Mafungo mratibu wa safari ajaze mfuko wa safari ya Nyerere ya kwanza UNO 1955 kisha hela zirudishwe haraka.

Siku ya pili wakaguzi wakaingia ofisini kwake.

Wanejuaje kuwa hela zimetoka?
Kisa kirefu.

Special Branch walikuwa na pandikizi lao ndani ya TANU.

Rashid Ali Meli akawaeleza viongozi wa juu wa TANU yaliyotokea ofisini kwake.

Bahati nzuri wakaguzi hawakugusa sefu siku ile.

Usiku ule ikapigwa dhikr nzito usiku kucha wanaomba Allah amnusuru ndugu yao Rashid Ali Meli.

Siku walipofungua sefu hela zote wamezikuta kamili.

Nimeinamisha kichwa nataka mpashaji wangu anieleze vipi fedha zilirudi kwenye sefu?

Hii ndiyo TANU iliyokuwa ikifungua mikutano yake kwa kusoma dua.

Yako mengi.

Mengine sikuweza kuyaandika kwani nilitaka ithibati ya taarifa.
 
Japo hukunielewa, sina ugomvi nawe kukumbuka zama zako hasa marhum mzee wako. Wote tunawapenda sana waliotutengeneza kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Pia hakuna sehemu yoyote nimegusia kuwafuta hao waislam wako. Kwani Kawawa, Karume, Kaluta, Bi Titi na wengine walikuwa matwahuti? Huwa mie si mtu wa udini hata kidogo. Wote mu watoto wangu.
 
Father,
Labda kama ikiwa ndiyo leo unanisoma mie kama wewe si mtu wa kuparurana.

Mimi sina Waislam wangu hao ni waja wa Allah aliyewaumba na kuwajaalia kuwa Uislam ndiyo dini yao.

Wala mie si mtu wa udini kama ulivyo wewe kwani ukiwa hivyo utawadhulumu wale ambao si wa dini yako na Allah kawaasa Waislam wasidhulumu na wasikubali kudhulumiwa.

Ndiyo maana kwa kufuata mafunzo hayo wazee wangu walimpokea Julius Nyerere Mkatoliki wakampa uongozi na wakamhami kwa kila hali.

Ikutoshe tu kuwa Abdul Sykes na Dossa Aziz ndiyo waliomfikisha kumjulisha kwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir.

Ilikuwa Abdul Sykes na Dossa Aziz ndiyo walikwenda Zanzibar na Nyerere kumtambulisha kwa Karume.

Ikutoshe pia ilikuwa Iddi Faiz Mafungo na Iddi Tosiri ndiyo waliompeleka Nyerere kumtambulisha kwa Sheikh Mohamed Ramiyya wa Bagamoyo.

Hapa ndipo niliposimama mie na kuandika kitabu kusahihisha historia ambayo haikuwa historia ya TANU.

Sihitaji kueleza upya kwa nini nimeikataa historia ya TANU ya Chuo Cha CCM Kivukoni.

Naikataa vilevile historia ya TANU kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Julius Nyerere.

Mimi sikudandia historia hii.

Hii historia mimi inanihusu kwa nasaba na ndiyo ikawa najua hadi vitu vidogo vidogo ambavyo wengi wanavisikia kwangu kwa mara ya kwanza.

Leo ile historia iliyofutwa sasa imehifadhiwa na atakae anaisoma.

Sasa kwangu mimi chochote utakachoandika liwe jina au jambo basi nitakuwa na historia yake.

Iwe umemtaja Bi. Titi au Karume au Nyerere mwenyewe.

Mimi nina miaka 69 sasa na ili mimi niwe umri wa kuwa mwanao wewe utakuwa mtu mzima sana.
 
Mbona kwenye uzi wako hujamtaja John Rupia ?
 
Kweli maana hajamtaja John Rupia !
 
huyu mzee anamaumivu ya ndani nafsi yake haijakubali kwanini waswahili (waislamu) hawakutambuliwa kama wapigania uhuru kitu ambacho sio kweli sana sema yeye hiyo line hakuwemo au waliona anadadisi sana wakamtema.
haya yalishapita ukombozi wa tanganyika haukuhusisha Dar es salaam tu bali nchi nzima ya Tanganyika sasa si kweli watu watafanana.
mwisho bado siku chache kwa kizazi kijacho hakitahitaji kujua yote haya bali yale yatakayosaidia wao kuondokana na umaskini na pia kuwa na nguvu ya kutawala Dunia
 
wewe nimtu mwema, umeeaelezea MATAGA vizuri maana wao wanalaumu na kuasifia tu
 
wewe nimtu mwema, umeeaelezea MATAGA vizuri maana wao wanalaumu na kuasifia tu
Jaji...
Hili neno MATAGA hulisoma kwingi lakini sijui maana yake na kwa kuwa sikuwa nona linanihusu sikutaabika kuuliza.

Nifahamishe maana ya neno hili tafadhali.
 
Jaji...
Hili neno MATAGA hulisoma kwingi lakini sijui maana yake na kwa kuwa sikuwa nona linanihusu sikutaabika kuuliza.

Nifahamishe maana ya neno hili tafadhali.

..mataga maana yake ni " make tanzania great again. "

..hili ni kundi mahususi la kumtukuza Magufuli na kumtetea kwa kila jambo.

..lengo lingine la mataga ni kutukana na kumdhalilisha yeyote asiyekubalina na Magufuli.

..kwa sasa hivi kundi la mataga limehamisha nguvu zake ktk kumkosoa, kumtukana, na kumdhalilisha, Rais Samia kwasababu wanaamini mafanikio yake yatamfunika mwendazake na kumfanya asahauliwe na Watanzania.
 
Chiwa,
Kwa kawaida inapoandikwa. ''Huyu Mzee,'' basi jua maneno yatakuwa kidogo makali.
Mwandishi anakuwa kaghadhibika kwani kama mtu anataka kuonyesha staha na heshima kwa mtu aliyemzidi umri hawezi kumwita, ''Huyu.''

Ataandika, ''Mzee Mohamed...''
Huyu ni karibu ya tusi.

Mimi sikuwemo katika kundi la kupigania uhuru ila babu yangu Salum Abdallah alikuwamo toka 1920s wanaanza African Association.

Baba yangu kaiona TANU inaasisiwa Dar es Salaam mwaka wa 1954 mimi ni mtoto wa miaka 2.

Kwa hiyo hayo yote uliyosema kuwa mimi nina uchungu sikupata cheo baada ya uhuru ni maneno hayana maana yeyote.

Hiyo picha hapo chini ni mimi wakati TANU inaasisiwa.

Aliyenipiga picha hii ni Mzee Shebe yeye alikuja kuwa mpiga picha wa TANU na kaacha hazina kubwa za kumbukumbu ya miaka ya mwanzo ya TANU.

Ninazo picha zake alizopiga miaka hiyo hadi uhuru na mbele yake katika Maktaba yangu.

 
Huyu mzee anajifanya anamjua Mwl Nyerere kuliko mama Maria Nyerere!!

Bahati nzuri ajenda zake watu wengi sasa wameishaanza kumstukia!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…